Timu inayochukua Kombe la Dunia ni lazima iwe na wachezaji hawa

Timu inayochukua Kombe la Dunia ni lazima iwe na wachezaji hawa

Kombe la dunia limefikia tamati.

Ilikuwa rahisi kukisia matokeo ya mechi nyingi na kuona timu ambazo hazitafika mbali. Ili timu yoyote ibebe kombe la dunia ni lazima wachezaji hawa wawepo:

1. Mchezaji anayeweza kubadilisha matokeo wakati wowote

2022 Argentina - Messi
2018 France - Mbappe
2014 Germany - Muller
2010 Spain - Villa
2006 Italy - Pirlo
2002 Brazil - de Lima
1998- France - Zidane

2. Mchezaji mgumu na muhuni anayetawala dimba la katikati

2022 Argentina - de Paul
2018 France - Kante
2014 Germany - Bastian
2010 Spain - Xavi
2006 Italy - Gatusso
2002 Brazil - Gilberto
1998- France - Deschamps

3. Beki mkatili sana anayeweza kuzuia hatari wakati wowote

2022 Argentina - Otamendi
2018 France - Varane
2014 Germany - Hummels
2010 Spain - Puyol
2006 Italy - Cannavaro
2002 Brazil - Lucio
1998- France - Thuram

4. Golikipa anayeweza kuokoa jahazi pale mabeki wanapozidiwa mbinu.

2022 Argentina - Martinez
2018 France - Lloris
2014 Germany - Neuer
2010 Spain - Casilas
2006 Italy - Buffon
2002 Brazil - Marcos
1998- France - Barthez

Sasa ukiangalia Spain na Germany walikuwa dhaifu karibu maeneo yote maana walileta watoto, ubelgiji walileta wazee waliochoka, Brazil wakajaza wavivu na mabishoo. Portugal hawakuwa na bahati kama ilivyo kwa waingereza wanaochezea mpira mdomoni.

Croatia na Morocco walikuwa na safu butu za ushambuliaji huku waholanzi wao kama kawaida hawana bahati. Japan walipambana na udhaifu wao kwenye penati ukawaangusha huku Korea kusini wao walikosa kocha ambaye ni tactical. Uswisi walipoteana kwa kukosa nidhamu siku walipocheza na ureno.

Tukutane 2026 panapo majaliwa.
Good analysis...
 
sikufurahishwa namna kocha alivyomtoa Di Maria ili Messi aoenekane, madhara yake wakayaona
Kocha amekuwa na makosa mara nyingi alipofanya sub hata mechi ya uholanzi na Australia ilikuwa hivyo hivyo.

Tatizo la di Maria ni kwamba hakabi ndio maana alimuingiza acuna ili akakabe maana walikuwa wanaongoza kwa 2 bila. Sidhani kama lengo ilikuwa kumfanya Messi aonekane.
 
Unaweza kuwa na wachaezaji wote hao uliowataja, lakini refa akaamua nani ashinde.
Kwa mfano refa alivyowasidia makolo aka sembe fc kumfunga geita gold goli tano za mchongo
Sikuangalia mechi ya simba ila kwenye kombe la dunia hakuna hayo maana var ipo.
 
Jana nimeona Ottamendi kacheza kistaarabu Sana Mana hata ile move ya koloumuane kamzuia kisoka ilikuwa amlambe bunda la kuvunja ugoko na hii ndio michezo yake na kulizua ni KAWAIDA Sana kwake.
Angemgusa kidogo tu refa angefunika mkwaju wa penati.
 
Kombe la dunia limefikia tamati.

Ilikuwa rahisi kukisia matokeo ya mechi nyingi na kuona timu ambazo hazitafika mbali. Ili timu yoyote ibebe kombe la dunia ni lazima wachezaji hawa wawepo:

1. Mchezaji anayeweza kubadilisha matokeo wakati wowote

2022 Argentina - Messi
2018 France - Mbappe
2014 Germany - Muller
2010 Spain - Villa
2006 Italy - Pirlo
2002 Brazil - de Lima
1998- France - Zidane

2. Mchezaji mgumu na muhuni anayetawala dimba la katikati

2022 Argentina - de Paul
2018 France - Kante
2014 Germany - Bastian
2010 Spain - Xavi
2006 Italy - Gatusso
2002 Brazil - Gilberto
1998- France - Deschamps

3. Beki mkatili sana anayeweza kuzuia hatari wakati wowote

2022 Argentina - Otamendi
2018 France - Varane
2014 Germany - Hummels
2010 Spain - Puyol
2006 Italy - Cannavaro
2002 Brazil - Lucio
1998- France - Thuram

4. Golikipa anayeweza kuokoa jahazi pale mabeki wanapozidiwa mbinu.

2022 Argentina - Martinez
2018 France - Lloris
2014 Germany - Neuer
2010 Spain - Casilas
2006 Italy - Buffon
2002 Brazil - Marcos
1998- France - Barthez

Sasa ukiangalia Spain na Germany walikuwa dhaifu karibu maeneo yote maana walileta watoto, ubelgiji walileta wazee waliochoka, Brazil wakajaza wavivu na mabishoo. Portugal hawakuwa na bahati kama ilivyo kwa waingereza wanaochezea mpira mdomoni.

Croatia na Morocco walikuwa na safu butu za ushambuliaji huku waholanzi wao kama kawaida hawana bahati. Japan walipambana na udhaifu wao kwenye penati ukawaangusha huku Korea kusini wao walikosa kocha ambaye ni tactical. Uswisi walipoteana kwa kukosa nidhamu siku walipocheza na ureno.

Tukutane 2026 panapo majaliwa.
Bro sio laxima wote tuwe wachambuzi🤣🤣🤣🤣
 
Lloris kwenye penalty ni kivuli
2018 wangeenda penalty wasingechukua

Kwenye midfildi
De paul na gattuso ndio wahuni
Hao wengine hawana uhuni zaidi ya kucheza soka safi
 
Rodrigo De Paul🙌🙌🙌.Huyu Mwamba mda wote anachakarika!
Bila kumsahau Leandro Peredes.
 
Dah miaka minne ni mingi sana wapunguze miaka. Nitalimis sana kombe la dunia mpaka nahisi kuumwa. Hongera sana Messi na Argentina mmepigana vita vikali mmestahili. Mbappe nakupenda sana ingawa leo nilitaka Argentina nao waonje raha ya ubingwa maana wewe ulishaonja 2018. Kikosi kizima cha ufaransa nawapenda sana nasubiria 2026 mchukue kombe lenu chini ya captain Mbappe inshaallah
huko kusubiri muda mrefu ndio kunalifanya liwe tamu.
 
Dah miaka minne ni mingi sana wapunguze miaka. Nitalimis sana kombe la dunia mpaka nahisi kuumwa. Hongera sana Messi na Argentina mmepigana vita vikali mmestahili. Mbappe nakupenda sana ingawa leo nilitaka Argentina nao waonje raha ya ubingwa maana wewe ulishaonja 2018. Kikosi kizima cha ufaransa nawapenda sana nasubiria 2026 mchukue kombe lenu chini ya captain Mbappe inshaallah
France wapo vizuri, lakini 2026 hatujui nchi zingine zitakuja kivipi; tunaweza kushangazwa pale France na Argentina watakapotolewa kabla ya Nusu Fainali.

Wajerumani walichofanyiwa 2018 na 2022 imetufundisha kwamba World Cup haihitaji mazoea.
 
Back
Top Bottom