Timu ya uchunguzi wa Makosa makubwa kutoka ofisi ya DCI yatumwa kuchunguza Mauaji ya Ali Kibao wa CHADEMA

Timu ya uchunguzi wa Makosa makubwa kutoka ofisi ya DCI yatumwa kuchunguza Mauaji ya Ali Kibao wa CHADEMA

Niliwahi kuandika , tume ya haki jinai nayo ikaona,

Na narudia tena, ipo haja ya kuwa na taasisi inayojitegemea ya upelelezi wa makosa ya jinai.
Yaani ndani ya polisi au nje ya Polisi .
Je waweza kutolea mfano wa Nchi nyingine yenye kitengo kama hicho.
Mimi ninafikiri njia zetu za ukamataji , zibadilike, zisiwe za kimabavu, kama vile polisi wetu ni watakatifu na raia ni waovu.
Hivyo njia ya kwanza ni kumpa MTU wito WA kufika kituoni, asipofika ndio afuatwe, na ki kawaida polisi atapita kwenye serikali zetu WA MTA au watachukua Jirani wakashuhudie ukamataji.
Ni katika matukio machache utaratibu huo unaweza kupindishwa, kwenye matukio makubwa kama ujambazi au fujo za papo Kwa papo .
 
Mhe. Rais kwa unyenyekevu Mkubwa na Mapenzi Makubwa niliyonayo kwako, Kwa Nchi yangu na Chama changu CCM.
Naomba kama utaona Comment yangu hii, wafuatao washauriwe kujiuzulu ili kuendelea kulinda Heshma yao na Mchango wao Mkubwa kwa Taifa letu! na endapo watasita kujiuzulu basi usisite kuwatumbua wafuatao ndani ya wiki hii.

1. Mh. Waziri wa Mambo ya Ndani
2. IGP
3. Mkurugenzi Mkuu wa Usalama wa Taifa.

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Mbariki Rais wetu na watu wake.

Naomba kuwasilisha.
Kwani wao ndio. Walio tenda au walikuwa na uwezo wa kulizuia
 
mkuu hivi upo serious na ulichoandika..? unazijua hatari za kuita wapelelezi toka nchi nyengine..?😂
hii siafiki tumalizane humuhumu mbona tunatoshana watafahamika tu.
Kweli bosi, sijui kabisa maana mi ntu wa Ntwara huku Tandahimba sijui kitu kabisa. Basi tutumie wa kwetu naafiki
 
Nchi za wenzetu waloendelea waziamini sana CCTV kwamba ndo suluhisho pekee katika kufanya uchunguzi wowote kuhusiana na uhalifu wa aina yoyote.

Kwasababu katika uchunguzi hatua ya kwanza kabisa ni kukusanya ushahidi kazi ambayo ni ngumu.

Tena siku hizi polisi (detectives) hutumia masaa mengi kupitia footage za matukio yoyote kupitia CCTV, DashCam kutoka kwa raia wema ambao wana vifaa hivyo katika magari na smartphones ambazo raia wamechukua picha na video.

Kwa hapa tulipofikia nchi yetu kwa sasa wananchi wapaswa kuzinduka na kuwa alerted kwa kila jambo khasa hili la utekaji.
Najiuliza hayo maeneo ya kibo complex hakuna hata camera za kwenye majengo na za barabarani zilizofanikiwa kunasa hili tukio?
 
Kweli bosi, sijui kabisa maana mi ntu wa Ntwara huku Tandahimba sijui kitu kabisa. Basi tutumie wa kwetu naafiki
umekubali kirahisi sana i atakiwa mpk mti atoke damu hapa!
 
Mimi mbumbumbu ningeambiwa niorodheshe kwanza washukiwa angalao kumi tu.

Ambao ningewaorodhesha hapa, najisikia kutetemeka kuendelea kuandika.

Na katika washukiwa watatu wa juu kwa umuhimu kufanyiwa kazi kuna mmoja ikidhihirika ndiye mhusika, hakuna hata haja ya kuanza huo uchunguzi.

Sababu, akitangazwa anahusika nani atamchukulia hatua. Na ni nani atathubutu kumtaja.

Kwahakika, tukio lile ni kizungumkuti ambacho wahusika au mhusika, wakipewa nafasi nyingine hawawezi lifanya kwa namna ile, ni fedheha kwa macho ya wanadamu. Kwa Mungu hata sijui ni nini, sina hayo mamlaka.
 

Timu ya uchunguzi wa matukio makubwa toka Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai toka Makao Makuu imetumwa kuongeza nguvu ili kuhakikisha waliofanya mauaji ya Ali Kibao Kada wa CHADEMA wanakamatwa na kufikishwa mahakamani.

Jana Septemba 7, 2024 Jeshi la Polisi lilitoa taarifa juu ya Ally Mohamed Kibao kuhusishwa kutoka kwenye basi la Tashrif na kuchukuliwa na watu ambao hawakuweza kutambuliwa na kwamba uchunguzi ulianza baada ya kupokelewa taarifa hiyo.

Baada ya kutolewa taarifa za kuonekana mwili wa mtu mwanaume ambaye hakuweza kutambuliwa kwa wakati huo ni mwili wa nani huko Ununio Jijini Dar es Salaam, utambulisho umefanyika kwa mujibu wa taratibu na kubainika ni mwili wa Ally Mohamed Kibao.

Soma Pia:
Aidha, uchunguzi wa mwili wa marehemu (postmortem) umefanywa leo tarehe 08/09/2024 na Madaktari bingwa kwa kushirikisha familia.

Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hili la kusikitisha na timu ya uchunguzi wa matukio makubwa toka Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai toka Makao Makuu imetumwa kuongeza nguvu kwenye timu ya awali ili kuhakikisha waliofanya mauaji haya wanakamatwa na kufikishwa mahakamani.
Vipi kuhusu Matokeo yatokanayo na Uchunguzi wa timu hii ya wachunguzi?
 
Utapeli mtupu.
IMG-20240905-WA0000.jpg
 
Back
Top Bottom