Timu ya wananchi kujenga uwanja kwa michango sio sawa

Timu ya wananchi kujenga uwanja kwa michango sio sawa

Kwa hiyo mmeanza kuhoji kabla hata fedha hazijachangwa na wala uwanja bado haujajengwa, ni wapi Simba/Mo pamoja na wanahisa wengine wametoa tamko kwamba mapato yatakayotokana uwanja yatawanufaisha wao wao pekee!?

Unapompa ndugu yako mtaji wa biashara kama msaada kisha akafanikiwa huko mbeleni kwa msaada uliompa utataka mgawane kila faida atakayopata!?


Mimi naomba niishie hapa maana mitazamo yetu imetofautiana tu na haimaanishi kwamba uko sahihi au umekosea, ndivyo hivyo na kwangu ilivyo.

Kama unaweza kuchanga, changa.
Kama hauwezi kuchanga kaa kimya hakuna atakekushitaki mahakamani kwamba hujachanga.

Ahsante.
Watu wanatumia uelewa mdogo wa watanzania kujinufaisha. Faida ya simba kwa miaka yote iliinufaisha kundi moja tu LA friends of simba
 
Bila kuwa Na makubaliano kuhusu namna ya kugawana mapato yatakayotokana Na uwanja uliojengwa Na wanachama Na mashabiki kwa michango yao ya mifukoni itakuja kutokea vurugu kubwa sana huko mbele ya safari.

Lazima mgawanyo wa faida itakayotokana Na uwanja kwa wanahisa ifahamike kabla watu hawajaanza kuchangia ujenzi wa uwanja. Iko siku mapato ya uwanja huo italiwa na MTU, familia, au kikundi kimoja tu cha watu. Ikitokea hivyo malalamiko yatazuka kwa wale wote waliochangia ujenzi wa uwanja huo.

Kulinda haki za watanzania serikali ihakikishe kuwa wananchi hawachangishwi ovyo bila kuwepo kwa andiko litakaloanzisha hiyo asset ya uwanja linaloonyesha umiliki Na mapato yatakwenda wapi.
Fact...maana kanjibhai mjanja mjanja sana yule b2 zake atataka agawane na timu 50/50 mapato[emoji3525][emoji3525][emoji3525]
 
mleta maada unashindana na malaymen utapatashida sana, inaonesha una elimu kubwa ya uwekezaji, nahisi una elimu ya kutosha probably uhasibu.
 
Hilo unalosema linawezekana kwenye kuchangia harusi Na perishables, sio kwenye asset kama uwanja ambao utaingiza pesa. Unataka kusema wanachama na wachangiaji watakubali mapato yooooote ya uwanja wao yaende kwa Barbara Na familia yake bila kuhoji?
Vipi kwani hakuna uwezekano wa mapato ya uwanja kwenda kwenye account ya club?
 
Vipi kwani hakuna uwezekano wa mapato ya uwanja kwenda kwenye account ya club?
Account IPI ya mwekezaji au ya walalahoi? Inayokaa kwenye account ya club ni hela ya uendeshaji sio faida, surplus. Faida lazima iende kwa wenye mali. Malengo ya kila mwekezaji ni kupata faida, ndio maana mo anasema anapata hasara simba. Sasa wewe unataka wanachama wawekeze kwenye uwanja bila kutarajia faida? Huo utakuwa wendawazimu.
 
Account IPI ya mwekezaji au ya walalahoi? Inayokaa kwenye account ya club ni hela ya uendeshaji sio faida, surplus. Faida lazima iende kwa wenye mali. Malengo ya kila mwekezaji ni kupata faida, ndio maana mo anasema anapata hasara simba. Sasa wewe unataka wanachama wawekeze kwenye uwanja bila kutarajia faida? Huo utakuwa wendawazimu.
Wanachama wakiwekeza kwenye uwanja inabidi wapewe hiyo faida,lakini hapa kinachofanyika watu wenye mapenzi na SSC wanadonate na sio investment

Mo hawezi claim ownership ya uwanja kama pesa imetoka mifukoni mwa watu wema,ndio maana nikasema bado kuna option pesa kuingizwa kwenye account za club
 
Yaani unataka wanachama wakubaliane kwanza jinsi watakavyokuwa wanagawana mapato? Nchi hii ngumu sana [emoji16][emoji16][emoji16]
[emoji23][emoji23][emoji23] nchi ngumu sana hii
 
Shida hapo sio kiwanja, bali hela za kiwanja nilichochanga kujenga anakula nani? Maguli Na Bashiru walipowanyang'anya watu ulaji wa mali za ccm si uliona mwenyewe malalamiko?
Kwani hela za kiingilio anakula nani?
 
Huu ndio wakati serekali ingebidi nayo iweke mkono wake kwa nguvu zote ili angalao tuwe na viwanja vyenye hadhi ya kimataifa ili ifikie siku tu compete kuandaa Afcon
 
Bila kuwa Na makubaliano kuhusu namna ya kugawana mapato yatakayotokana Na uwanja uliojengwa Na wanachama Na mashabiki kwa michango yao ya mifukoni itakuja kutokea vurugu kubwa sana huko mbele ya safari.

Lazima mgawanyo wa faida itakayotokana Na uwanja kwa wanahisa ifahamike kabla watu hawajaanza kuchangia ujenzi wa uwanja. Iko siku mapato ya uwanja huo italiwa na MTU, familia, au kikundi kimoja tu cha watu. Ikitokea hivyo malalamiko yatazuka kwa wale wote waliochangia ujenzi wa uwanja huo.

Kulinda haki za watanzania serikali ihakikishe kuwa wananchi hawachangishwi ovyo bila kuwepo kwa andiko litakaloanzisha hiyo asset ya uwanja linaloonyesha umiliki Na mapato yatakwenda wapi.
Kwahiyo Mimi niliechangia 50k nitapaswa kupata mgao wa faida? Akili zingine Ni kinyero kabisa.
Sisi km mashabik tunataka uwanja Basi Mambo ya mapato watajua viongoz na timu ,kama watapasuka faida wao kwa wao fresh tu kikubwa tunataka uwanja uonekane kwanza na timu iendelee kuwa Bora wachezaji wapate mshahara kwa wakat na sorting nzur ya wachezaj bac.

Mimi siwez kuendesha familia yangu kwa kutegemea mpato ya uwaja wa Simba et kisa nilichangia 50k ,ntakua fala wa mwisho kuamini Hilo ,kwangu Ni burudani tu na kuona Simba ikimilik uwanja bac mengine hayanihusu .
 
Zile ni fedha ambazo zililipa mishahara, nauli, chakula Na posho (utilities) Na kwisaha kabisa. Hii ni tofauti Na kujenga uwanja utakaodumu miaka 100 ukiingiza pesa. Haiwezekani ni change Mimi lakini pesa ule we we? Je, kama timu ikifa uwanja unabaki kwa nani? Je kama uwanja utafanya faida pesa zitamnufaisha nani Na nani?
Bado akili yako Ni ya kindez Sana .Haya ngoja nikupe wanufaika hapa .
Bonus kwa wachezaji
Posho kwa viongoz wa pande zote mbili wale wa upande wa more na upande wa wanachama.
Kuboresha miundo mbinu ya uwanja kadri itakavyotakiwa.
Kulipa walinz wa uwanja.
Kulipa wafanya usafi wa uwanja.
Kuongeza kibubu na kutunisha account kwa ajili ya kusort wachezaj wa Bei ya juu Zaid .
Sasa unataka kila mwanachama apewe faida kisa alichangia? Wakila viongozi na wachezaj inatosha wanwakilisha wengi.
Ukweli upo hapo ,chukua mfano wa wabunge wawakilishi wa wananchi maisha wanayoishi na wanaowaongoza huo ndio mfano real kabisa hutak kunya boga.
 
Si umeona hapo, siku ccm ikishindwa uchaguzi viwanja vyooote hivi vitarudi kwa wananchi, maana vilijengwa Na wananchi. Lakini kama ccm itajenga kiwanja kipya sasa hicho kitakuwa ni cha ccm hata kama kitashindwa uchaguzi
Nan kakudanganya kuwa vitarud kwa wananchi? Bora ungesema Vita chukuliwa na ruling party kidogo ungeeleweka kidogo ,una mawazo finyu sabab ya wivu tu
 
Wanachama wakiwekeza kwenye uwanja inabidi wapewe hiyo faida,lakini hapa kinachofanyika watu wenye mapenzi na SSC wanadonate na sio investment

Mo hawezi claim ownership ya uwanja kama pesa imetoka mifukoni mwa watu wema,ndio maana nikasema bado kuna option pesa kuingizwa kwenye account za club
Je, watu wanafahamu hivyo kuwa wanatoa sadaka? Ni nani amewaambia kuwa itakuwa ni sadaka?
Maajabu ni kwamba ramani ya uwanja hakuna alafu wanakwambia uwanja kujenga ni 30 bil.

Huu si uchizi, itengenezwe kwanza ramani alafu ziandaliwe makisio ya gharama zinazohitajika kwa ajili ya ujenzi ndio gharama ifahamike.

Hii timu sasa ni SIMBA QUEENS FC a.k.a Barbara FC a.k.a Lialia FC a.k.a Upatu FC
Wajinga hawaishi, wataendelea kuwepo tu milele. Mo arena kwa lipi?
 
Maamuzi ya hasira tusubiri huko mbeleni mda uta amua
Ni jambo jema kwa timu kubwa kuwa Na uwanja wake, hata hivyo isiwe kwa mihemko ya MTU mmoja aliyetaka kulazimisha na watoto wake wawe VVIP kwa TFF, waswahili wanasema "ukijamba kwa hasira utajinyea" uwanja uje lakini kwa utaratibu rasmi Na kuratibiwa vizuri.
 
Zile ni fedha ambazo zililipa mishahara, nauli, chakula Na posho (utilities) Na kwisaha kabisa. Hii ni tofauti Na kujenga uwanja utakaodumu miaka 100 ukiingiza pesa. Haiwezekani ni change Mimi lakini pesa ule we we? Je, kama timu ikifa uwanja unabaki kwa nani? Je kama uwanja utafanya faida pesa zitamnufaisha nani Na nani?



Naamini ushawah sikia kitu kinaitwa board of trustee... kazi yao ni kulinda mali za taasisi.. sheria haitambui club ya mpira kupitia wachezaji na viongoz ila inatambua club ya mpira kama
taasisi kupitia katiba na miongozo iliosajiliwa so kiuhalisia club haitakufa bali inaweza ikasitisha kufanya shughuli zake za kimichezo

lakini mali za club bado zitakuwa mali za club hakuna cha kusema mali zinakwenda kwa nani

kwa msaada zaidi rejea Pan Africa na Nyota nyekundu.. Pan Africa hawana team ila wana jengo kariakoo na kila mwaka wanakutana na kila miaka minne wanafanya uchaguzi wa viongoz.. ingawa hawazidi hata watu 30..

ni kweli watu wanaweza kutumia jengo kupangisha na kula pesa ila watakula hizo pesa kupitia jina la club kwa maana ya kuwa lazima huyo mtu awe ametambulika kisheria kuwa ni kiongoz wa club husika na ana mamlaka ya kuingia mikataba kwa niaba ya club..

so kwa namna hiyo tunaweza kusema kuwa majengo ya Pan Africa pale
kariakoo kuna watu wanakula pesa badala ya kuwekeza kufufua club.. ila kwa mfano huo huo hata sasa hivu kuna viongoz wa hizi club za ligi kuu wanakula pesa za club kupitia mgongo wa club so hawana tofauti na viongoz wa team iliojifia ya Pan Africa

ila wote hawawezi kuuza mali za club sababu zinalindwa kisheria

NB: Jiulize mchakato wa Simba kwa nn ulichukua mda mrefu wakiwa wanapigizana kelele na Mzee Hamisi.. sababu ni kuwa Ilibidi Simba wawe na docz zote za kuonyesha mali zao so Mzee Hamisi akiwa kama mjumbe wa bodi ya wadhamin akawa anagoma kutoa docs..

kitu ambacho kitawakuta yanga pia wakifika kwenye uhakiki wa mali za club sababu docz zimetapakaa kila mzee wa zaman ana yake huyu ana ya kiwanja huyu ana sijui ya jengo
 
Kiongozi mchango wa hiari siku zote huwa hauna return, mtu anachanga alichonacho kama ameguswa, sio lazima.

Hakuna atakayekushikia panga uchangie.

[emoji1787][emoji1787][emoji1787]paragraph ya mwisho inachekesha sana
 
Back
Top Bottom