TISS Ikanushe tuhuma za uvamizi, utekaji, utesaji na mauaji!. Wasijadiliwe na Bunge kwa uwazi bali wachunguzwe, wakithibitika wafumuliwe!

Pasko kuwa Usalama wa Taifa basi Tunajua unapewaga briefing uzilete hapa na unafanya uandishi kama cover tu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Babe la mji , duh...!, yaani Pasco ni TISS!, uandishi ni kuzuga tuu!, kiukweli hii kali na kubwa kuliko!. Tiss anayeikosoa serikali yake mitandaoni!.

Kiukweli mimi najihesabu ni mtu mwenye bahati kuzaliwa familia ya TISS kwa baba na mama. Mzee Mayalla ndiye alikuwa RSO wa Mwanza ile 1976 wakati wa sekeseke ya Kesi ya Mauaji Mwanza.

Kwa vile kuna dhana ya mwana wa nyoka ni nyoka, na sisi kwetu tumezaliwa 8, we can't all be nyokas!. Ndugu zangu 5 wako serikalini na sisi watatu tuko sekta binafsi. Siwezi kuwasemea wengine, lakini mimi ningekuwa TISS nisingeweza kupandisha mabandiko kama hili? )

P
 
Mwandishi naomba nikupe hongera kwa bandiko hili. Linaweza kuwa na upungufu wake kiasi fulani, lakini kwa kweli zaidi ya asilimia 80 lina - uhalisia na ukweli.

Kwa machache nayo yafahamu, ni kweli Idara inahitaji kujisafisha au isafishwe....huo ndio ukweli wenyewe! Na tatizo kubwa ni ni kupoteza focus ktk kufanya recruitment ya maaofisa hao. Kuingia kwa suala la ukabila, Mtoto wa fulani, vimemo ndiyo yamesababisha kupata watu wasio na dira, uzalendo, uwajibika na kuelewa kazi inataka nini.

Naomba niishie hapo, na wahusika najua wapo humu na wanajua ukweli...ila kusema hawawezi.

Bravo Mwandishi.......
 
Mkuu pole kwa kudhhaniwa kuwa ndiye au siye.
TISS kwa kipindi cha awamu ya tano imedhalilika sana.
TISS na JWTZ ni taasisi ambazo moyoni wananchi tunaziamini sana.

Lakini awamu ya tano TISS imetumika vibaya, bila weledi(proffessionalism) na wakati mwingine kutenda vitendo ambavyo mbele ya umma ni outright hooliganism.
Utekwaji watu, na hata kuingilia Clouds wakiwa na uniform, ni vitendo vilivyo leta tahayari kwa watu ambao tunawaamini sana TISS kiutendaji.

Tunajua kuwa watendaji wakipewa amri ni kutekeleza bila kukiuka amri, lakini vitendo hivyo vimeumiza sana image ya TISS.

Awamu hii ya sita TISS ijinasibu na kurudisha heshima yake kiutendaji na huduma kwa Taifa.
 
Halafu kwa nini watekwaji wote ni wa kiume?!
Mashirika ya utetezi wa haki za kijinsia yalitazame hili.
 
Mkuu Mbogi, kila siku humu if, wanaingia madogo wapya, hivyo hawawezi kujua nani aliwahi kusema nini kuhusu wasiojulikana TISS Ikanushe tuhuma za uvamizi, utekaji, utesaji na mauaji!. Wasijadiliwe na Bunge kwa uwazi bali wachunguzwe, wakithibitika wafumuliwe!
Na ufafanuzi pekee wa kuondoa lawama hizi ni fanya uchunguzi wa kile kinacholalamikiwa ikiwa ni pamoja na mauaji/ majaribio ya mauaji ya watu yaliyotokea.

Wewe Pascal, lisaidie taifa letu kwa kusema ukweli.
Kwenye hili la wasiojulikana, nimejitolea hata kufanya uchunguzi





Mabandiko hayo ni uthibitisho wangu kulisaidia taifa kwenye hii issue ya wasiojulikana.

P
 
Kweli mkuu Mayalla uliona mbali Leo TL anathibitisha tuhuma ambazo uliziandika miaka kadhaa nyuma🤔
 
Tumechoka hatuwezi kuvumilia tena. Sasa utatueleza vizurii kwa nini taasisi yetu ifumuliwe. Nimewatuma Vijana wangu wawili Rama ma Frenki wanakufuata wape ushirikiano.
 
Tulijuwa tunawanyooshea vidole hawa jamaa kuhusika na wasiojulikana, kumbe wasiojulikana ni miongoni mwetu sisi wengine na kumbe kuna wenzetu miongoni mwao, wanawajua lakini wamekula kobisi!.


Jee tutafika?.
P
 
🤣🤣🤣Pascal
 
Kwa hiyo Pascal Ulivyoitwa kule bungeni kuhojiwa ulienda kukutana na Workmates wenzako🤣🤣
 
Mkuu Evarist Chahali, kwanza nikuombe radhi kwa ku super impose hii hoja. Kweli wewe ni sauti adimu kuhusu mageuzi sekta ya usalama wa taifa, na hoja ya kiufumua hii idara, ila you could be the only one and not the only one.

You are the only one as the only Tiss anayefahamika na ku expose na kuzungumza publicly uozo wa Tiss na madudu yake!, but you are not the only one kuizungumzia Tiss ifanyiwe mabadiliko na maboresho.

Bandiko hili ni uthibitisho.

P
 
K
Kijana jiangalie sana
 
Jamani kwanini mtu akihoji yawa kama katukana watu? Au kakosea? Au labda kuna ukweli ndani yake?
Binadamu unapomkataza kujadili kitu ndipo hapo atang’ang’ania, that is if ana akili timamu. Tujadili watu watoe maoni kama hupendi basi usiingie kwenye thread. Haya ni mawazo tu. Unless kuna walengwa wanaona watakosa chakula!
 
Paschal Mayala,wewe ni mtu wa idara ya usalama wa Taifa na ccm wamekupandikiza kwa makusudi humu mitandaoni kwaajili ya kuvuruga movements za Watanzania za kuing'oa ccm na kudai katiba mpya
Mkuu monde arabe, du...!.
Naheshimu freedom of thinking and freedom of expression yako,
Hivyo inawezekana hata siku ile pale Ikulu ni Idara ndiyo ilinituma kumuuliza swali hili Hongera sana Pascal Mayalla, Ndio Mwandishi Pekee Uliyemuuliza Swali Rais Magufuli bosi wangu?.

Na katika kuisafisha Idara, huyu ni ofisa wa Idara amekuja humu kuisaidia kuisafisha idara TISS Ikanushe tuhuma za uvamizi, utekaji, utesaji na mauaji!. Wasijadiliwe na Bunge kwa uwazi bali wachunguzwe, wakithibitika wafumuliwe!

Na ili kulisafisha Bunge letu, itakuwa ofisa kipenyo huyu alishauriwa kuandika kuhusu Bunge kujipendekeza kwa serukali kisha ikamtuma dodoma Pascal Mayalla ahojiwa na kamati ya Bunge

Na kulipotokea tishio la usalama kwa taifa letu, afisa kipenyo huyu ali copy and paste ripoti ya ofisini na kuimwaga humu jf Security alert kwa Serikali yetu: Tuwe makini sana na Marekani, kuna kitu kinapangwa halafu wajifanye walionya kabla. Je, wanapanga kutu-Libya?

Then kiukweli tutakuwa na TISS ya ajabu sana!.
Kama kila watoto wanaozaliwa na wazazi wote baba na mama ambao ni Tiss na watoto wao ni Tiss then TISS itakuwa na watu wengi sana!, sisi tumezaliwa 8!.
P
 
Kwa hiyo miaka yote tangu ianzishwe, ndio leo mnatuambia kazi yao ndio hiyo!? Mbona malalamiko juu yake ni siku hizi na sio tangu!?
TISS enzi zile za giza nene ilikuwa ikitesa, kuteka na kuua watu kupitia KAKIKUNDI KANAITWA VIJANA WAZALENDO TZ.... kakikundi haka kaovu kalipatikana pale makumbusho kakiongozwa na MSIGWA GRAYSON
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…