Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 53,857
- 121,995
- Thread starter
-
- #501
Wanabodi
Declaration of Interest
Tunapojadili jambo nyeti kama hili, ni vizuri ku declare interest ili kwanza kujenga imani kwenu wasomaji wangu kuwa mwandishi wa makala hii ni mtu wa kuaminika, hizi data kwenye bandiko hili ni data za kuaminika authentic, bonafide genuine from trusted sources na sio data za kuokoteza, data za kubuni, kuzua, au kuunga unga, hivyo ni vyema mimi nikajitambulisha kidogo kwenu, pia kwa sababu mtu unapotoa data nyeti from time to time katika mabandiko yako, huchelewi kunyooshewa kidole kuwa huyu jamaa ni TISS, hivyo na mimi kudhaniwa ni TISS, hivyo bandiko kama hili, litawafungua macho wengi humu kuwa huyu mtoa mada atakuwa ni TISS wa ajabu sana kuilaumu ofisi yake mitandaoni!.
Mimi Pascal Mayalla ni mwandishi wa habari wa kujitegemea mwenye uwezo wa kuandika Investigative Stories, (IJ), ila pia nimepata bahati ya kuzaliwa na kukulia katika familia ya TISS kwa wazazi wangu wote wawili, baba na mama. Baba Mzee Andrew Mayalla (RIP) ameishatangulia mbele ya haki, na mama bado yuko hai, hivyo baadhi ya hoja zangu za kiitelijensia, sio kwasababu mwana wa nyoka ni nyoka, bali mtoto ukizaliwa kwa wazazi wote wawili ni wana inteligensia wa TISS, unazaliwa na natural intelligence ambayo ni tool muhimu sana kuweza kuwa Investigative Journalist.
Mkuu Phillipo Bukililo, mtu wa kitengo, angeweza kuleta bandiko kama hili TISS Ikanushe tuhuma za uvamizi, utekaji, utesaji na mauaji!. Wasijadiliwe na Bunge kwa uwazi bali wachunguzwe, wakithibitika wafumuliwe!Kaka Pascal Umenitisha sana mzee wa kitengo pale Saint Peters.
Au hili Security alert kwa Serikali yetu: Tuwe makini sana na Marekani, kuna kitu kinapangwa halafu wajifanye walionya kabla. Je, wanapanga kutu-Libya? kwanini nilete humu nisipeleke ofisini?.
Mkuu wa TISS ni CinC, ningekuwa kule, baada ya kuona maisha ya CinC yako hatarini, kwanini nisiripoti kitengo, na badala yake nikaja kuripoti humu?, US/EU Walimtoa Saadam, Ghadafi na Mugabe? Je, wanapanga kumtoa Rais Magufuli madarakani? Watanzania wazalendo tutakubali? mwisho wa siku you know what happened!, kwanini sikusaidia?.
Kinachofanya watu humu kunidhania, ni kufuatia wazazi wangu wote wawili, baba na mama both ni watu wa huko, hivyo watu kudhani mwana wa nyoka ni nyoka!, sisi tumezaliwa 8!, kama watoto wote wa kitengo wanaajiriwa kitengo, hicho kitengo kina watu wangapi?. Kati ya sisi 8, mwenye watoto wachache ni 6!, mimi ninao 10 wa home!, hicho kitengo kitakuwa na watu wangapi?.
P