Wanabodi
TISS ni idara nyeti, uadilifu wake unapaswa kuwa wa kiwango cha juu kabisa ambao haupaswi kutiliwa shaka yoyote, unapaswa kuwa ni uadilifu wa kiwango cha mke wa Kaisari, ile kutuhumiwa tuu ni kosa tosha hata bila kuthibitishwa, anahukumiwa!.
Hivyo ndivyo zilivyo tuhuma za TISS wetu, kuwa wale makirikiri wa Bashite ni TISS!, na yule mpuuzi wa Nape ni TISS!. Hivyo kama wale makirikiri wa Bashite waliovamia Clouds TV sio watu wao, TISS wasikae kimya wajitokeze na kukanusha!. Kama yule mpuuzi aliyemtishia Nape kwa bastola sio mtu wao, wajitokeze wakanushe. Huku kukaa kimya kunachukuliwa ni admission of guilt!.
Kama tuhuma dhidi ya TISS zimefika hadi kwenye Bunge letu Tukufu, na TISS iko chini ya Ikulu yetu, na Ikulu ni mahala patakatifu, tuhuma tuu kumhusu mke wa Kaisari zinatosha kumuondoa Ikulu asije akapanajisi patakatifu petu!. Hiyo TISS isikae kimya lazima ijitathimini na kujisafisha na uchafu wa makandokando haya!.
Huu mjadala unaoendelea kuhusu utekaji, utesaji na mauaji ambavyo vinahusishwa na idara yetu nyeti ya Usalama wa Taifa, TISS ni uthibitisho tosha kuwa TISS imechafuka inahitaji au kujisafisha au kusafishwa!.
Pamoja na Tanzania kuridhia mkakati wa Open Government Initiatives lakini kuna vitu huwezi kuvijadili openly lakini bado unaweza kuvichunguza na kuvifanyia kazi kimya kimya ila public ikaona matokeo na kurudisha imani.
Kuna watu wanadhani Usalama wa Taifa TISS wao ni malaika na hawawezi kabisa kufanya makosa kama madudu haya wanayotuhumiwa nayo sasa. No!, TISS sio malaika kwa sababu nayo inaongozwa na binadamu!.
Tiss huko nyuma iliwahi kufanya makosa ya utekaji, utesaji na hata uuaji, na ikafumuliwa!. Hivyo kwa vile tayari tunayo precedence ya vitendo viovu vya TISS huko nyuma, hivyo kwa kuutumia uthibitisho wa uovu huo, una justify kuwa kuna uwezekano ikawa ni kweli TISS is behind huu uovu na uchafu unaozungumziwa sasa Bungeni.
Lakini pia inawezekana sio TISS as TISS bali ni acts za individual members wa TISS wakifanya a "stand alone operations" bila kupokea command yoyote kutoka juu, hivyo vitendo vya wachache, vikaichafua TISS yetu collectively kwenye a collective responsibilities formula.
Pia inawezekana kabisa vitendo hivi vinafanywa na wahuni fulani, ambao wana pose as TISS just to make believe kuwa ni TISS kumbe sio TISS bali ni just impostors wanaochafua the good image ya TISS wetu waadilifu.
Whichever the case, TISS ijitokeze iwakane na kurudisha imani na TISS wetu
Hebu kwanza msikilizeni Tundu Lissu anasema nini kuhusu utekaji na utesaji wa TISS, hao anaowatetea ndio wenye bahati who could live to tell, hivyo ndio waliosalimika, only God knows kwa wale wasio na bahati hatima yao ilikuwaje because they couldn't live to tell!.
Kama tuhuma hii ni kweli, then serikali yetu ni serikali dhalimu! .
Hii sio mara ya kwanza kusikia serikali inafanya torture!. Hapa chini ni kisa cha kweli kabisa cha udhalimu wa TISS wa enzi hizo ambacho kilimhusu member wa familia yangu kujaribu kuwanusuru watuhumiwa wa torture na katika kufanya wema, wema wake ulimponza, RIP Mzee wangu Andrew Mayalla.
Kitendo kilichofanywa Clouds Media ni uthibitisho wa uhuni kama huu wa gross abuse of power na Nape alipotaka kufanya wema kuikingia kifua serikali yake isijinasibishe na uchafu huu, wema wake ulimponza.
Mwaka 1976 kule Mwanza kwenye eneo la Kigoto, watuhumiwa wa mauaji ya vikongwe walikuwa tortured na maofisa wa polisi.
Mzee wangu, Andrew Mayalla akiwa RSO wa Mwanza, akawanusuru watuhumiwa wawili, Masanja Makula Mazengenuka na Isaak Mwanamkoboko kutoka eneo la Kigoto baada ya mateso makubwa, wakiwa njiani wakamweza hawajala chochote kwa muda wa siku 3 za mateso ya usiku na mchana!.
Akaamua kuwapeleka Bugando, on their way akasimama mahali kuwanunulia soda na kitafunio, soda waliweza kunywa, kutafuna walishindwa.
Bugando akawakabidhi kwa Dr. Nkulila. The next day they were both dead, mtuhumiwa wa kwanza ni aliyewaleta!.
Hizo ni enzi za Nyerere, tulikuwa tukiishi Isamilo ya chini, next door ni RPC alikuwa akiitwa Mkwawa, nyumba ya tatu ni DSO. Just imagine majirani watatu wanaishi nyumba zinazofuatana wanapokutwa na kisanga.
Baada ya Taarifa kumfikia Nyerere, kuanzia Waziri wa Mambo ya Ndani, Ali Hassan Mwinyi alipoteza uwaziri, IGP wa wakati huo Pundugu alipoteza kazi, Mkurugenzi wa Tiss, Mzena, alipoteza kazi, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Peter Kisumo, alipoteza kazi,
Mzee wangu, Mzee Mayalla, RSO, RPC, DSO na OCD wa Mwanza wote walistaafishwa kwa manufaa ya umma, tulihamishwa usiku usiku na kurudishwa kijijini (detention fulani za Nyerere).
Wakati yote haya yakifanyika, mimi nilikuwa mdogo sana, sikujua hili wala lile, hadi ilipoanza kuunguruma, Kesi ya Mauaji Mwanza, ndipo niligundua dingi alikuwa nani!, na thanks God, mtu pekee aliyenasuka ni Mzee Andrew Mayalla (RIP) kufuatia kazi kubwa iliyofanywa na wakili Murtaza Lakha.
Kwa wale tuliofuatilia ile kesi ya Uhaini ya mwaka 1982 tulisoma jinsi TISS wanavyoteka, wanavyo tesa na wanavyo ua yakiwemo mauaji ya Martin Tamimu. Utekaji wa Hatty Magee, kule jijini Nairobi, etc.
Mahakama ndio Mhimili pekee wa haki ndani ya katiba yetu, kwenye kesi hiyo ya uhaini, tumeshuhudia watuhumiwa wakitoa ushuhuda jinsi walivyoteswa na TISS kwenye torture chambers zao na kulazimishwa kukiri, hivyo kupelekwa kwa Walinzi wa Amani kukiri kuhusika kwao halafu walipofika mahakamani wakavikana viapo vyao kwa Walinzi wa Amani na kusema waliteswa ndio maana wakakiri.
Japo torture ni kinyume cha sheria, polisi na TISS zote duniani wanatumia mbinu hizo kuhoji ambazo nyingine ni halali na nyingine ni haramu.
Marekani ndio inayoongoza kwa kutumia torture na kuihalalisha ila kwa vile ni kinyume cha sheria za nchi hiyo, wanalitumia gereza la Guantanamo Bay lililoko kwenye kisiwa cha Cuba ambako sio ardhi ya Marekani kufanya ushenzi huo.
Hivyo kama tuhuma hizi za Lisu ni kweli, hii sio mara ya kwanza kwa TISS kuhusishwa na makando kando ya ajabu!. Ya Ulimboka tuliyasoma Mwanahalisi, hadi yakamuibua msemaji wa Tiss ya wakati huo Jack Zoka.
Ya Kibanda nilishikwa sikio na mtu tete a tete ila hii nilielezwa ni wale vijana wa Kijitonyama ila it was a personal social issue!.
Yaliyotokea Clouds TV wote tumeyashuhudia kupitia CCTV, na yale makirikiri tumeyaona, na ya Nape Mnauye tumeyashuhudia live mubashara kwenye TV huku huyo mpuuzi akionekana wazi hadi sura watu wanamjua.
Naunga mkono TISS isijadiliwe na Kamati ya Bunge kwa uwazi kama ambavyo bajeti yao na ile ya defence hazijadiliwi, lakini bado wanaweza kuchunguzwa, na Sheria ya Usalama wa Taifa, sheria namba 15 ya mwaka 1996 ina mapungufu makubwa, imepitwa na wakati na kila siku sio tu inavunjwa na TISS wenyewe, bali pia inatumiwa vibaya na wanasiasa kuanzia Mkuu mwenyewe kuitumia kama bakora ya kuwachapia wapinzani!.
Just imagine, Mkuu wa nchi mwenyewe, anatamka hadharani kuwa simu za watu zinadukuliwa, bila wanaharakati kupiga kelele wakati inafahamika wazi kabisa, udukuzi kwa simu za wanasiasa ni kosa kisheria!, kwa mujibu wa Kifungu cha 5(2) cha sheria ya usalama wa Taifa kinaizuia TISS kumfuatilia mtu yeyote wala kumpekua pekua au kumfanyia ujasusi kwa sababu ya msimamo wake kisiasa au Uhuru wake wa kuipinga Serikali. TISS inavunja sheria kila wakati kwenye eneo hili, rais anatangaza wanadukua simu za watu, by implication, waelewa wote, walielewa aliyedukuliwa!, kisha rais akasema kwa hasira, wasaliti wa aina hii, hawawezi kuachwa hivi hivi na kutolea mfano wa kinachowapata wasaliti wa jeshini, then mara mtajwa, yanamkuta ya kumkuta!, hata mtoto mdogo lazima atadhania ya kudhania!.
TISS inatakiwa kubadilika na kuunda kitengo madhubuti cha ujasusi wa kiuchumi, mfano, tuna Balozi zetu katika nchi zote zinazochenjua Mchanga wa makinikia, TISS wangekuwa wa maana, by now tungeisha jua hao Acacia wanapata nini kwenye Mchanga wetu, gharama za uchenjuaji container la Mchanga ni kiasi gani na kila kinachopatikana!, lakini wao wamekalia kudukua tuu simu, badala ya kudeal na serious issues za kiuchumi!. Kiukweli ile bili ya trilioni 190 ya TRA sio realistic, rais wetu ataonekana mjinga, Waziri Kabudi ataonekana mjinga, na nchi nzima tutaonekana ni taifa la wajinga, wakati ukweli utakapobainika, kitu ambacho TISS makini ingeweza kuzuia!.
Serikali yetu lazima ifanye damage control kwa msemaji wa TISS kuibuka na kumkana yule mpuuzi aliyemtisha Nape Bastola na kuwakana wale makirikiri wa Bashite!.
Huu ukimya wa Mwigulu, na serikali ni uthibitisho kuwa serikali has a hand kwenye hayo!. Ili kuonyesha kuwa serikali haihusiki na uhuni,upuuzi na ushenzi huu, rais Magufuli lazima akasirike kama Nyerere alivyo kasirika idara ya TISS inapochafuliwa, aliifumua mwanzo mwisho bila huruma.
Ukiondoa hizo torture za TISS zilizoibuliwa mahakamani, torture za jeshi la polisi ndio isiseme kabisa, innocent (until proven guilt) people have been tortured to death, hakuna kesi and nobody cares as if polisi are doing the right thing!.
Tukio la mwisho ni gunning down waendesha bodaboda wawili na abiria wao wawili kisa wamesimamishwa pale daraja la Mkapa wakapitiliza!. Polisi wakawaripoti hivyo walipofika next check point walimiminiwa tuu na kumaliza kazi hapo hapo, hawakukutwa na silaha yoyote!.
Haya ya polisi tumeisha yapigia sana kelele humu jukwaani.
IGP Mwema, Please, Please, Please, Stop This Police Brutality!. Utampeleka JK The Hague-Part II!
Vifo vya Mahabusu Mwanza, IGP Mangu, Usikubali Kudanganywa!, Polisi Wako Ni Wauaji!. P'se Stop This
Police Brutality in Tanzania: The World has a Right to know!
Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na kupandishwa vyeo limekaaje?
Na kwa wale wenye interest na TISS kuijua zaidi, tembelea
Namna ya kujiunga na usalama wa Taifa | JamiiForums | The Home of
Kujiunga na Chuo cha Usalama wa Taifa kilichopo Mbweni, Bunju
Afisa usalama wa taifa "shushushu" ni nani? Anafanya shughuli gani
Shushushu (Afisa Usalama wa Taifa) ni mtu wa aina gani .
Natafuta Kazi Usalama Wa taifa | JamiiForums | The Home of Great .
Nadharia ya Usalama wa Taifa (TISS) ibadilike kuanzia sasa ...
Dr. Hassy Kitine, aliyekuwa Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa .
Usalama wa Taifa waibana polisi; NI KUHUSU TUHUMA ZA MKE ...
Paskali
Update
Mkuu
Mchambuzi
thanks very much for this, its very objective naona kama umemaliza kila kitu!.
It's true kuna lots of details nime avoid kutokana na uzalendo, pia nimemtaja Mzee wangu tuu kwa sababu alihusika direct, lakini sikumtaja mama yangu ambaye she is still alive and retired (hawaritayi kabisa) wala sikusema kuwa hata mimi nilipomaliza shule na kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria, nilipomaliza JKT, nilijiunga JWTZ straight japo niliacha Jeshi. Ukiwa ni mtoto wa hawa jamaa, both parents, born and breed Tiss, then mimi nami ni almanusura sana!. Anyway haya tuyaache.
Although mhusika mkuu hataisoma kutokana na lingua uliyotumia, wahusika wenyewe wamesoma, na wamesikia labda waendelee tuu kutia pamba masikioni kwa sababu kujadili jambo lolote kuhusu TISS was considered a taboo hivyo bandiko hili kwa TISS ni kama abomination!.
Thanks again.
Paskali