TISS walibariki UJENZI wa GHOROFA linalotazama IKULU

TISS walibariki UJENZI wa GHOROFA linalotazama IKULU

Kwani TISS ndo wanatoa vibali vya ujenzi? acheni jamani kuleta propaganda kwenye mambo ya msingi.

Hivi leo ukiitwa zuzu kwa mujibu wa ulichokiandika hapa utakataa? Nani ana wajibu wa kulinda ikulu? Hata kama si wajibu wao kutoa vibali vya majengo kwa hiyo tukubali kuwa mwehu yeyote akitoa kibali cha ujenzi ambao ujenzi wake utahatayarisha usalama wa ikulu tumwachie tu???????
 
Nashangaa sana Mkuu. Hivi kwenye mchakato wa kutoa vibali vya ujenzi, TISS inahusika?

Wenyewe tulikuwa tme-relax, ziara ya Obama ndo imeleta hizi chokochoko, nasikia CIA wakiwa kwenye maaandalizi ya ziara ya Obama Nchini ndio walihoji inakuwaje serikali imeruhusu jengo hilo refu lijengwe mita chache kutoka ikulu na kwamba hiyo ni hatari kwa usalama wa Ikulu.

Sekeseke lilianza pale CIA waliuliza kama usalama wa taifa wanajua uwepo wa jengo hilo.

haya bongo na movie kama kawaida kama bongo movie!!
 
tiss ni wakandarasi? mbona mnadanganyana danganyana kihuni huni ivi? tiss wanaoingiaje kwenye tender na kubariki ujenzi.

sure Mkuu, huyu Mkurugenzi wa TBA atakuwa aliingizwa chaka. sidhani kama hata huyo Othman aliwahi kuonana naye ana kwa ana labda kwenye picha tu

Nashangaa sana Mkuu. Hivi kwenye mchakato wa kutoa vibali vya ujenzi, TISS inahusika?

tiss haikamati haishtaki wala haipo kwenye utendaji wa shughuli za ujenzi

hawa ndio waandishi makanjanja wanaotakiwa kutungiwa sheria zenye adhabu kali kabisa, kazi kuandika uongo na uzushi

mbaazi ikikosa maua lazima isingizie jua, hawa wahuni wamevunja sheria za nchi kwa kujenga jengo kinyume cha sheria wanaanza kutafuta mchawi, hilo jengo libomolewe na wahusika wafikishwe mahakamani

Nyie msiwe mambumbumbu wa kuandika upuuzi kala mara kwa hali halisi ya ujenzi wa jengo lile TISS lazima wahusike kwani lipo mazingira ya Ikulu isitoshe katika maelezo ni hao hao TISS walioomba wapewe ofisi katika floor ya mwisho(18) na hii inaonyesha jinsi hii taasisi ya Usalama wa Taifa katika nchi yetu walivyo mbumbumbu kwani kwa kuomba ofisi floor ya mwisho wao ndio waliona watakuwa wanacontrol vizuri ulinzi wa Ikulu. Swali la msingi napenda kuwauliza nyie wakurupukaji ghorofa hili limejengwa hadi limekamilika ilikuwaje Serikali haikugundua mapema tatizo la kiusalama juu ya jengo hilo hadi pale FBI katika ujio wa Obama walipowashtua ndipo songombingo zote zilipoanza?
 
Hii mada ilikuwa inaendelea vizuri ikitafuta kiini cha tatizo. Sema kuna pandikizi humu ndani wanatutoa kwenye mstari.
Haya turudi kwenye mada, hadi sasa tunafahamu yafuatayo

1. TISS wanahusika na hili swala kwasababu ni sehemu ya kazi yao. ( kama unabisha anzisha Uzi mwingine ujadili kazi za TISS)

2. Inawezekana kuwa mmiliki wa hili jengo ni mtu mwenye nguvu sana.

Naomba wachangiaji turudi kwenye mada je huyu mtu ni nani kiasi hadi TISS wamekaa kimya?
 
wana bodi, nianze na mshangao kwanza, watu wanasoma habari imetoka mahakamani washindwa kuielewa!! mbona watu wamekuwa wagumu kuelewa? hawa ndo ma GT wa JF?

Tiss, wametajwa kuhusika maana ki usalama, walipaswa kushirikishwa, na kwa maelezo ya mtuhumiwa Mkurugenzi wa TBA walishirikishwa!! TBA ni idara ya serikali ina bodi ambayo ndo inapitisha miradi mikubwa kama huo. Bodi inateuliwa na raisi wa nchi, msimamizi ni wizara ya ujenzi. mawaziri wawili kwa nyakati tofauti wameusifia na kuutolea maelezo mradi huo. Magufuli na kawambwa, sasa mradi umechukua zaidi ya miaka 3 kukamilika, leo umekamilika mkurugenzi anashitakiwa.

Ndugu ma-GT, tujiulize mambo kiasi, jengo lilipo 75% ya mawaziri wanaliona jengo daily, viongozi wengi wanakaa masaki, mikocheni mbezi nk njia yao kuu ni ocean road jengo linaonekana, mh Rais na waziri mkuu, ofisi zao ziko mita chache kutoka lilipo jengo hilo. je nani alipaswa kulisimamisha?

Labda swali jingine je kesi ni kutoa kibali cha ujenzi au kujenga jengo linalokiuka taratibu za ujenzi wa eneo husika? Pengine tusogee mbele hatua moja tena, mkurugenzi wa TBA naye anaomba kibali cha ujenzi kwenye mamlaka husika, yaani wizara, JIJI na wilaya, je huko walitoa vibali gani? walijua ujenzi huo? moja zaidi je nani anawajibu wa kuzuia/kusimamisha ujenzi endapo mwekezaji amekiuka maelekezo?

Mwisho kwa mtazamo wangu, hapo hamna kesi, jamaa watatoka hapo na kesi itaisha, na hao pia watamwanga mboga/ maana TAKUKURU wamemwaga ugali. Tegemea kusikia majina makubwa TISS tayari wametajwa na leo wanakalia ghorofa tatu za juu. Mawaziri ni wapangaji, mengine mengi yanakuja.
SP
 
ikulu.JPG

Yeah, tumeliona!Wote hao viongozi wa serikali ni wahuni! Jengo linajengwa mpaka linafikia hapo Ikulu na TISS hawakuliona? Ndiyo maana akina Kenyatta, Kagame na Mseveni wanatenga Kikwete! He is not serious!!
 
Kuondoa shida zote Serikali ilinunue jengo hili lifanywe ofisi za usalama wa Taifa au wizara ya ulinzi.
 
Jengo lipo karibu na ikulu thats why wanahusishwa na TISS na kama sikosei wana ishi maeneo hayo.......
 
Jengo lipo karibu na ikulu thats why wanahusishwa TISS na kama sikosei wana ishi maeneo hayo.......
 
Kwa mtazamo wangu, hilo ghorofa ni la kubomolewa kutokea juu floor ya 18 hadi ya 6! Ishu ya kuwa floor za juu kabisa wakae TISS haina nguvu sana kwa mtazamo wangu, kwani haiwezekani afisa wa TISS mmoja kurubunika ili aamue (kuwa sniper) kumuua rais akiwa anafanya mazoezi au matembezi katika viunga vya ikulu?!

Marais wengi wamewahi kuuwawa na walinzi wao wanaotokana na idara zao za usalama, hapa siongelei inside job, bali afisa mmoja au zaidi kutumiwa kumuondoa rais aliyepo kwa manufaa ya kundi fulani ndani au nje ya system.
 
nchi ya jk swafiii kabisa

Binafsi ningekuwa rais, nisingekubali kukaa ikulu na hilo jengo libakie kuwa hapo hapo lilipo sasa. Kwa ukimya huu, inawezekana kabisa wakubwa wanahusika nalo!
 
tatizo ajira na teuzi zake hazi zingati vigezo, matokeo yake mtu anapelekewa ramani ya hili jengo anashindwa kuona asicho kiona mbele ya uso wake bila kupiga mahesabu ya angle nk.
 
Kwanini Serikali
1)Isijenge IKULU ya kisasa, na ya ulinzi wa kutosha kuliko kuendelea kung'ang'ania jengo liloachwa na wakoloni?
2) Jengo hilo liachwe na liwe kama makumbusho tu ya taifa
 
TISS wanahusika tu, kwa sababu wenyewe ndio wanaolinda ikulu na maeneo yanayozunguka sasa kitendo tu chakujenga hilo jengo pale TISS lazima wangegoma kama waliona halistahiri kujengwa......
 
Hii mada ilikuwa inaendelea vizuri ikitafuta kiini cha tatizo. Sema kuna pandikizi humu ndani wanatutoa kwenye mstari.
Haya turudi kwenye mada, hadi sasa tunafahamu yafuatayo

1. TISS wanahusika na hili swala kwasababu ni sehemu ya kazi yao. ( kama unabisha anzisha Uzi mwingine ujadili kazi za TISS)

2. Inawezekana kuwa mmiliki wa hili jengo ni mtu mwenye nguvu sana.

Naomba wachangiaji turudi kwenye mada je huyu mtu ni nani kiasi hadi TISS wamekaa kimya?

Nakubaliana na wewe kwa hiyo nyekundu. Kwanza kwa nini hatajwi? Unaweza kukuta ni mtu katibu mkuu fulana kwa kishirikiana na jamaa wa nje
 
Back
Top Bottom