TLS na Mwabukusi: Fungueni kesi dhidi ya serikali kwa ukiukwaji mkubwa wa haki na udhalilishaji wa utu wa binadamu katika mahabusu na magereza nchini

TLS na Mwabukusi: Fungueni kesi dhidi ya serikali kwa ukiukwaji mkubwa wa haki na udhalilishaji wa utu wa binadamu katika mahabusu na magereza nchini

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Kwako Mwabukusi, TLS na wadau wote wanaoguswa na ukiukwaji wa haki za binadamu na udhalilishaji wa utu (dignity) wa mwanadamu nchini.

Hali za mahabusu na magereza hapa nchini ni ambazo hazifai kwa binadamu kuwekwa. Ni jambo ambalo kila mtu anajua kwamba mfumo wa mahabusu na magereza zetu ni ule wa kikoloni, ambao ulilenga katika kuadhibu na kumdalilisha mwafrika, kumtoa utu. Wazungu waliojenga mfumo huu hawakupelekwa huko pale walipofanya kosa au uhalifu, kwa sababu waliojenga walijua hakufai mwanadamu kuwekwa huko.

Soma: Hali ya Magereza Mahabusu na Wafungwa

Na mbaya zaidi serikali yetu, ikitambua magereza na mahabusu zetu hazifai kuwekwa mwanadamu, wameamua kuweka vyumba maalumu kwa "vigogo" wanapokuwa mahabusu gerezani. Yaani serikali imeamua kuna tabaka la watu nchini ambalo halipaswi kupelekwa kule ambako mwananchi wa kawaida atapelekwa huko mahabusu au gerezani!

Miaka zaidi ya 60 baada ya uhuru bado tunafanya kitu kile kile huku tukiwalaani wakoloni kwa ukosefu mkubwa wa haki za binadamu na udhalilishaji wa mwafrika. Imefika sasa hili lipingwe mahakamani ili serikali ilazimishwe kubadili huu mfumo wenye kutojali utu wa Watanzania kama wanadamu wanaostahili heshima. Kwa mfano, kwa nini tuendelee kutumia mfumo wa kujisaidia ambao wakoloni waliutumia ili kutudhalilisha watu weusi?

Tuna mfumo wa mahabusu ambao kupelekwa huko ndio adhabu yako, mbali na kama ukifungwa. Tukumbuke huko mahabusu na magereza sio wote wanaopelekwa wanakuwa na hatia. Mhalifu adhabu yake inapaswwa kuwa kutengwa na jamii, sio kudhalilishwa na kuvuliwa utu wake kama mwanadamu.

Tungependa jambo hili lifikishwe mahakamani, ili hukumu rasmi itolewe kwamba mfumo wa mahabusu na magereza Tanzania upo kwa namna kubwa ya ukosefu wa haki za binadamu, kudhalilisha watu na kuwaondolea utu wao, iwe wana hatia au la.

Mwabukusi, tafadhali tusaidie katika hili.
 
Huyu mwamba namkubali.. Mwabukusi apewe nchi
 
Kweli ..pia mahabusu asifanyiwe kama mfungwa mpaka pale atapofungwa rasimi. Kuna mahabusu wanakaa mda mrefu hata miaka wakiwa magerezani na kuishi huko tayari ni adhabu..je ikitokea hatafungwa vipi hio adhabu? Maana ikitokea kafungwa inawezekana wakahesabia na ule mda aliosota mahabusu.
 
Huyu mwamba namkubali.. Mwabukusi apewe nchi
La kwanza atabadilisha Katiba. La pili ataondoa kinga ya kufikishwa mahakamani ya raisi, makamu wake, spika, waziri mkuu na mwanasheria mkuu. La tatu atapeleka mswaada bungeni kutungwa sheria ya mtu kushitakiwa kwa makosa aliyofanya wakati kuna kinga ya kushitakiwa. La nne kuna maraisi, maspika, nk watapelekwa gerezani!
 
Picha linaanza mnapofika ndani ya Gereza kabla ya kupelekwa kwenye selo,ni lazima wote mliopelekwa siku hiyo mvue nguo na ukaguzi ufanyike!

Kwa wanawake wanaingiziwa hadi Vidole kwenye Uke na Kwa wanaume mnainama huku vinyeo vikiwa juu kama ngiri!

Kwanini kusiwe na scanner kila Gereza?
 
Kweli ..pia mahabusu asifanyiwe kama mfungwa mpaka pale atapofungwa rasimi. Kuna mahabusu wanakaa mda mrefu hata miaka wakiwa magerezani na kuishi huko tayari ni adhabu..je ikitokea hatafungwa vipi hio adhabu? Maana ikitokea kafungwa inawezekana wakahesabia na ule mda aliosota mahabusu.
Unajua mtu kama raisi Samia wanaweza wakapuuza hili kwa sababu wanaona wao haliwahusu. Lakini Raisi Samia akumbuke kwamba mambo hubadilika, anaweza akakuta mpendwa wake Abdul anaishia mahabusu ambazo yeye aliona sio tatizo Watanzania wengine kuwekwa huko! Haiwezekani kwamba kama kuna makosa Raisi Samia amefanya na asishitakiwe kwa sababu ana kinga, hakuna namna ya kumfanya Abdul kuwa na yeye alihusika, na yeye hana kinga. Huo ndio ukweli. Raisi Samia anapaswa kubadili mahabusu na magereza zetu na mifumo yake kwa namna ambayo hata akisikia Abdul amewekwa ndani lisiwe ni jambo la kumnyima usingizi kwamba mwanangu sijui anaambiwa vua nguo, inama ufanyiwe body check au anajisaidiaje huko! What comes around goes around.
 
Picha linaanza mnapofika ndani ya Gereza kabla ya kupelekwa kwenye selo,ni lazima wote mliopelekwa siku hiyo mvue nguo na ukaguzi ufanyike!

Kwa wanawake wanaingiziwa hadi Vidole kwenye Uke na Kwa wanaume mnainama huku vinyeo vikiwa juu kama ngiri!

Kwanini kusiwe na scanner kila Gereza?
Haya yalifanywa na wakoloni kudhalilisha waafrika, sio kwa ajili ya usalama!
 
La kwanza atabadilisha Katiba. La pili ataondoa kinga ya kufikishwa mahakamani ya raisi, makamu wake, spika, waziri mkuu na mwanasheria mkuu. La tatu atapeleka mswaada bungeni kutungwa sheria ya mtu kushitakiwa kwa makosa aliyofanya wakati kuna kinga ya kushitakiwa. La nne kuna maraisi, maspika, nk watapelekwa gerezani!
Watu kama Tunawapoteza, uchawa na ushamba unasababisha tunakuwa viongozi wa ovyo..
Mwabukusi apewe nchi 2030
 
Huyu mwamba namkubali.. Mwabukusi apewe nchi
Mwabukusi akigombea uraisi dhidi ya Samia, na akaungwa mkono na vyama vyote vya upinzani, atapita kirahisi sana kuwa raisi. Hatapita ikiwa atagombea uraisi kupitia chama kimoja cha upinzani. Kampeni yake anaweza kuifanya kama uchaguzi wa kupiga kura kama referandum kuhusu bandari zetu, misitu yetu, ardhi yetu, madini yetu, mbuga zetu na Tanganyika yetu, ili kule visiwani wabaki na Zanzibar yao tuwe na muungano uliosawazika. Hapo Samia na CCM hawatafua dafu!

Hebu fikiria, unapiga kampeni unasema wale wote wanaoona bandari zetu, mbuga zetu, madini yetu, misitu yetu havipaswi kupewa waarabu wa nje wanipigie kura tuzuie hili! Wale wote wanaoona kwamba Tanganyika tunapaswa kuwa na serikali yetu ili tuamue mambo ya Tanganyika sisi wenyewe na Wazanzibar waamue mambo yao wenyewe wanipigie kura ili nibadilishe hili, make Tanganyika great again!!!!!!!i!
1730747393744.png
 
Kweli Mkuu yani mahabusu ni sehemu ambayo mtu anaweza kuingia akiwa mzima siku anatolewa tayari amesheheni magonjwa mengi ambukizi yaliyotokana na mazingira ya mle ndani.

Mahabusu chumba cha futi 8 kwa 9 mnaweza kuwekwa watu zaidi ya 20, usiku mzima mnalala wima.

Mazingira ya vyoo nayo ni mabaya, maji hamna.

Hata ikitolewa fungu kwa ajili ya kufanya ukarabati wa kituo sidhani kama wanakumbuka hata kutemga bajeti special kwa ajili ya mahabusu.
 
Kweli Mkuu yani mahabusu ni sehemu ambayo mtu anaweza kuingia akiwa mzima siku anatolewa tayari amesheheni magonjwa mengi ambukizi yaliyotokana na mazingira ya mle ndani.

Mahabusu chumba cha futi 8 kwa 9 mnaweza kuwekwa watu zaidi ya 20, usiku mzima mnalala wima.

Mazingira ya vyoo nayo ni mabaya, maji hamna.

Hata ikitolewa fungu kwa ajili ya kufanya ukarabati wa kituo sidhani kama wanakumbuka hata kutemga bajeti special kwa ajili ya mahabusu.
Ili kutoa hukumu itabidi majaji wapelekwe mahabusu wakajionee wenyewe kama mwanadamu mwenye utu na heshima anapaswa kuwekwa na kulazwa katika hali kama hiyo, hata kama amefanya kosa la kumpiga risasi raisi wa nchi na kumuua!
 
Kwako Mwabukusi, TLS na wadau wote wanaoguswa na ukiukwaji wa haki za binadamu na udhalilishaji wa utu (dignity) wa mwanadamu nchini.

Hali za mahabusu na magereza hapa nchini ni ambazo hazifai kwa binadamu kuwekwa. Ni jambo ambalo kila mtu anajua kwamba mfumo wa mahabusu na magereza zetu ni ule wa kikoloni, ambao ulilenga katika kuadhibu na kumdalilisha mwafrika, kumtoa utu. Wazungu waliojenga mfumo huu hawakupelekwa huko pale walipofanya kosa au uhalifu, kwa sababu waliojenga walijua hakufai mwanadamu kuwekwa huko.

Soma: Hali ya Magereza Mahabusu na Wafungwa

Na mbaya zaidi serikali yetu, ikitambua magereza na mahabusu zetu hazifai kuwekwa mwanadamu, wameamua kuweka vyumba maalumu kwa "vigogo" wanapokuwa mahabusu gerezani. Yaani serikali imeamua kuna tabaka la watu nchini ambalo halipaswi kupelekwa kule ambako mwananchi wa kawaida atapelekwa huko mahabusu au gerezani!

Miaka zaidi ya 60 baada ya uhuru bado tunafanya kitu kile kile huku tukiwalaani wakoloni kwa ukosefu mkubwa wa haki za binadamu na udhalilishaji wa mwafrika. Imefika sasa hili lipingwe mahakamani ili serikali ilazimishwe kubadili huu mfumo wenye kutojali utu wa Watanzania kama wanadamu wanaostahili heshima. Kwa mfano, kwa nini tuendelee kutumia mfumo wa kujisaidia ambao wakoloni waliutumia ili kutudhalilisha watu weusi?

Tuna mfumo wa mahabusu ambao kupelekwa huko ndio adhabu yako, mbali na kama ukifungwa. Tukumbuke huko mahabusu na magereza sio wote wanaopelekwa wanakuwa na hatia. Mhalifu adhabu yake inapaswwa kuwa kutengwa na jamii, sio kudhalilishwa na kuvuliwa utu wake kama mwanadamu.

Tungependa jambo hili lifikishwe mahakamani, ili hukumu rasmi itolewe kwamba mfumo wa mahabusu na magereza Tanzania upo kwa namna kubwa ya ukosefu wa haki za binadamu, kudhalilisha watu na kuwaondolea utu wao, iwe wana hatia au la.

Mwabukusi, tafadhali tusaidie katika hili.
Tulimng'oa mkoloni ili kustawisha usultan nchini.

CCM ni mkoloni mamboleo. Haina habari na haki za raia
 
Kwako Mwabukusi, TLS na wadau wote wanaoguswa na ukiukwaji wa haki za binadamu na udhalilishaji wa utu (dignity) wa mwanadamu nchini.

Hali za mahabusu na magereza hapa nchini ni ambazo hazifai kwa binadamu kuwekwa. Ni jambo ambalo kila mtu anajua kwamba mfumo wa mahabusu na magereza zetu ni ule wa kikoloni, ambao ulilenga katika kuadhibu na kumdalilisha mwafrika, kumtoa utu. Wazungu waliojenga mfumo huu hawakupelekwa huko pale walipofanya kosa au uhalifu, kwa sababu waliojenga walijua hakufai mwanadamu kuwekwa huko.

Soma: Hali ya Magereza Mahabusu na Wafungwa

Na mbaya zaidi serikali yetu, ikitambua magereza na mahabusu zetu hazifai kuwekwa mwanadamu, wameamua kuweka vyumba maalumu kwa "vigogo" wanapokuwa mahabusu gerezani. Yaani serikali imeamua kuna tabaka la watu nchini ambalo halipaswi kupelekwa kule ambako mwananchi wa kawaida atapelekwa huko mahabusu au gerezani!

Miaka zaidi ya 60 baada ya uhuru bado tunafanya kitu kile kile huku tukiwalaani wakoloni kwa ukosefu mkubwa wa haki za binadamu na udhalilishaji wa mwafrika. Imefika sasa hili lipingwe mahakamani ili serikali ilazimishwe kubadili huu mfumo wenye kutojali utu wa Watanzania kama wanadamu wanaostahili heshima. Kwa mfano, kwa nini tuendelee kutumia mfumo wa kujisaidia ambao wakoloni waliutumia ili kutudhalilisha watu weusi?

Tuna mfumo wa mahabusu ambao kupelekwa huko ndio adhabu yako, mbali na kama ukifungwa. Tukumbuke huko mahabusu na magereza sio wote wanaopelekwa wanakuwa na hatia. Mhalifu adhabu yake inapaswwa kuwa kutengwa na jamii, sio kudhalilishwa na kuvuliwa utu wake kama mwanadamu.

Tungependa jambo hili lifikishwe mahakamani, ili hukumu rasmi itolewe kwamba mfumo wa mahabusu na magereza Tanzania upo kwa namna kubwa ya ukosefu wa haki za binadamu, kudhalilisha watu na kuwaondolea utu wao, iwe wana hatia au la.

Mwabukusi, tafadhali tusaidie katika hili.
Kwakweli serikali inatakiwa kuwajibika na hali za magereza mahabusu zetu zinanuka na zinatoa utu wa binaadamu, hii siyo sawa, nakubaliana tls ipiganie hili
 
Kwakweli serikali inatakiwa kuwajibika na hali za magereza mahabusu zetu zinanuka na zinatoa utu wa binaadamu, hii siyo sawa, nakubaliana tls ipiganie hili
Mie siku zote nimesema ile harufu ya mahabusu ina athari juu ya ubongo wa mtu. Uthibitisho ni jinsi Polisi wengi wanavyoonesha mapungufu makubwa kwenye uwezo wa kufikiri katika mambo mengi wanayofanya hadi watu wanadhani ni kwa sababu wanachukuliwa waliofeli shule. Utaona hata wale waliofaulu wakiingia polisi wanakuwa na akili ya ajabu sana. Lazima ni athari za ile harufu kwenye ubongo. Huwezi ukavuta ile harufu siku zote isiwe na athari kwenye ubongo wako. Mtu akitoka mahabusu kwa siku mbili au tatu hivi utaona kama hayuko sawa, baadae ndio anarudia hali ya kawaida.
 
Back
Top Bottom