TLS pamoja na Mwabukusi waziombe radhi Simba na Yanga hadharani kwa kuzitolea kauli za hovyo

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Nimeona Rais wa TLS akiwa anahojiwa na chombo cha habari akiwatusi watanzania kwamba wanafuata mambo ya hovyo na yasiyo ya maana, na akatoa mfano wa watanzania kuwa na mapenzi na simba na yanga kiasi kwamba wanaweza kutembea uchi

Hii ni dharau kubwa kwa klabu hizo ambazo zimejijenga kwa miaka mingi katika mioyo ya watanzania. Kama wao wanathamini demokrasia, kwa nini wanadharau machaguo ya watanzania na kuwapangia maisha?.

Pia mashabiki wa timu hizo ni watu wazima kiumri, kusema kwamba wanaweza kutembea uchi ni dharau kubwa nyingine kwa watu wa umri wa wazazi wake

Nani kawazuio wasiimarishe vyama vyao ili wananchi wavipende? Yaani watu hata harusini, mpirani, disco wasiende?

Nalaani sana kauli ya TLS kwa kuwa iko chini ya kiwango na inapaswa kulaaniwa na kila mzalendo, mwanamichezo wa nchi hii.

N. B:
Hata Mwabukusi hakuandamana, ila alitaka wengine waandamane, chichi dodo
 
Ukweli mara nyingi Huwa unauma
 
Kasema ukweli kabisa kuwa watanzania wanapenda sana Simba na yanga lakini hawapendi kuchukua hatua pale haki zao zinapokiukwa na hii serikali ovu ya mama Yao wanayemwita hangaya.mfano kwenye maandamano wamewasaliti wazalendo wa chadema waliotaka watanzania wote wapate haki sawa na kuyamaliza mambo ya kutekwa hadharani yanayofanywa na chiefu hangaya.Ingekuwa ni Simba na yanga wangejaa uwanja mzima.
 
TLS sio chama cha siasa kuanza kusimanga watu!
 
Mimi shahidi zama zile simba Vs yanga mmojawapo akishinda basi kutoka uwanja wa Taifa hadi msimbazi/jangwani ….chi nje nje; kweli wewe mshamba
 
Kwani Mwabukusi nini alichoongea ambacho siyo sahihi?

Watanzania "wamelogwa" Kwa ushabiki wa Yanga na Simba.
Full Stop
 
Kila mtu apende anachopenda. Wengine tumechagua kupenda Simba na Yanga, na nyie pendeni kuandamana na kufoka foka.
 
Uk
Ukweli mchungu
 
Inawezekana wewe ni mmoja kati ya wale wanaoshinda kwenye redio kutwa nzima wakisikiliza uchambuzi wa mpira usioisha, ila huo ndio ukweli.
 
Watanzania tunatumika kupumbazwa na simba na yanga...kweli kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…