Chief Sanze
JF-Expert Member
- Jun 13, 2014
- 1,668
- 3,736
Amecomment kama mtu aliyetoka usingizini au yuko ndani ya pipa hajui chochote kinachoendelea ni bora angekaa kimya kuliko kucomment utumboUwezo wako wa kuchanganua mambo ni mdogo sana samahani kwa kukuambia hivyo.
UmesikiaaaaaWale mbwa hata ikibidi kunyongwa ni sawa tu hawana utu kabisa wamemdharirisha sana yule binti.
Inasemekana polisi wameshampata binti kwa mahojiano ili watuhumiwa wapatikane ila nimesikia kuna dada yake kwa uchungu amekunywa sumu hata hivyo wasamaria wema wamemkimbiza hospital.
Jeshi halijawahi na halitakaloshindweIla nimeshtuka sana nilipoona polisi imetoa namba za simu kuomba isaidiwe kuwapata. Jeshi lenye kila aina ya nyenzo linaombaje kusaidiwa na raia kuwakamata washenzi kama wale? Wakija wahalifu wakubwa kama kina Carlos jeshi litafanyaje?
Ni kosa kisheria kumpiga mtu kipara alafu ukajorekodi na ukasambaza so hata kama hawakumlazimisha hiyo bado ni kesi, kimsingi hapo kuna kesi zaidi ya moja hao majamaa hawana pakutokea, mfano yule alosema atamla jokeri nae asishitakiwe ? Eti me nikiingia nakula mavi, nakula jokeri daaah 😂😂😂Swali kwako, wewe umethibitisha vipi kwamba binti amelazimishwa?
Vipi kwa mfano mahakama ikaja kusema labda hakubakwa, yalikua makubaliano yao wenyewe, (sisemi kwamba hawatahukumiwa kwa makosa mengine mf kujirekodi), ila kosa mama linalowafanya mshipaze shingo. Ikaonekana jamaa hawana hatia itakuaje?
Kwa hiyo kuliko kupiga makelele ni bora tukae kimya tuvipe muda vyombo vyetu vya usalama vichunguze, halafu majibu yakija ndio tuchague kushupaza shingo au
Kwa haraka haraka pana kesi tatuNi kosa kisheria kumpiga mtu kipara alafu ukajorekodi na ukasambaza so hata kama hawakumlazimisha hiyo bado ni kesi, kimsingi hapo kuna kesi zaidi ya moja hao majamaa hawana pakutokea, mfano yule alosema atamla jokeri nae asishitakiwe ? Eti me nikiingia nakula mavi, nakula jokeri daaah 😂😂😂
Sawa mtetezi wa haki za binadamuUmesikiaaaaa
Anyway
wale si mbwa na ni watu wanahaki zao.
Wanapaswa kupelekwa mahakaman nao wasikilizwe ili mahakama itende haki
Sizan kama ni kazi yaoNi jambo jema kwa TLS kufanya hivyo.
Lakini tunakuomba Bwana Advocate Mwabukusi na TLS unayoiongoza kwamba ianzishe Mpango Maalumu kabisa wa kuliangazia janga kubwa sana na baya kabisa lililoibuka kwa kasi miaka ya hivi karibuni, janga la Wananchi kutekwa na Watu wasiojulikana (Forced disappearence)
Unarukaruka kijana, huku upo kule upo.Na ndio nilikua naandika kile ninachoona ni sahihi kwangu.
Ni miongoni mwa masuala ambayo yapo ndani ya kazi zao, ni suala la kisheria linalohusu Haki za binadamu.Sizan kama ni kazi yao
Shule,shule hakuna.Video hii imesikitisha watu wengi sana, narudia tena kama wale vijana ni wanajeshi kweli basi CDF aangalie sana nidhamu za vijana wake.
Kama kweli ni wajeda wale unaanzaje kuwapeleka front line askari wasio na discipline?
Kuna shida kwa wanajeshi wengi kujiona wako juu ya sheria na kufanya lolote lile.
Jeshi la polisi limepewe mamlaka Kwa kushirikiana na MP's kudeal na askari wote wasio na nidhamu uraiani kuu.
Shule,shule hakuna.
Wanajiita majeshi kunoga,wao hutumia nguvu badala ya akili,nimesikia mwenye mme ni kapteni nimeshangaa afisa wa jeshi kuwa mjinga namna ile.Nakubaliana na wewe kabisa, wale unakuta ni form 4 graduates kabisa, halafu ndio wanatabia zile.
Lakini kwa upande mwingine huenda yawezekana hao waliofanya hivyo walikuwa wapo sahihi, kwa sababu nasikia kwamba hao ni Askari, na walifanya kitendo hicho baada ya kupewa amri na Kamanda wao mwenye cheo Cha Kapteni. Sijui taarifa hii Ina ukweli gani, lakini kama taarifa hizi zitakuwa zina ukweli maana yake ni kwamba hao wahusika walikuwa wanatekeleza 'amri halali kutoka kwa Kamanda wao.' Tukumbuke kwamba utendaji katikà Jeshi huongozwa na AMRI kutoka kwa Mkubwa wako aliye juu, kupinga kutekeleza amri kutoka kwa Kamanda wako aliyekuzidi Cheo inahesabika Kama kosa baya Sana la insurbonation au Uhaini.Mimi nilivyosikia tu mtoto mmoja wa ndugu yangu mmoja wa mbali katakiwa pesa Ili aingie jeshini na aliyemuambia hivyo ni polisi tena yeye aliingia na almost milioni mbili kasoro nikaona kabisa hapa hatuna wanajeshi tena, si JWTZ, PT na wengineo almost ni watu wasiojitambua vizuri, sitashangaa kama nchi tukifeli vibaya kiusalama, kiuwajibikaji baada ya miaka Ishirini ijayo maana wazee wa connection ndiyo watakuwa wapo kwenye vyeo vya juu.
Ipo haja ya viongozi wa jeshi wa Sasa hivi kufanya namna ya kutibu hili tatizo, tunajua na nyinyi mna maslahi yenu lakini sio Kwa hichi kinachoendelea, yaani mtu wa usalama ndo wa kufanya mambo kama hayo kweli?.
Lakini kwa upande mwingine huenda yawezekana hao waliofanya hivyo walikuwa wapo sahihi, kwa sababu nasikia kwamba hao ni Askari, na walifanya kitendo hicho baada ya kupewa amri na Kamanda wao mwenye cheo Cha Kapteni. Sijui taarifa hii Ina ukweli gani, lakini kama taarifa hizi zitakuwa zina ukweli maana yake ni kwamba hao wahusika walikuwa wanatekeleza 'amri halali kutoka kwa Kamanda wao.' Tukumbuke kwamba utendaji katikà Jeshi huongozwa na AMRI kutoka kwa Mkubwa wako aliye juu, kupinga kutekeleza amri kutoka kwa Kamanda wako aliyekuzidi Cheo inahesabika Kama kosa baya Sana la insurbonation au Uhaini.
Laanaa inatutafuna jamanChama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kimelaani vikali kitendo cha udhalilishaji na ukatili wa kijinsia kilichooneshwa kwenye video inayosambaa mitandaoni, ikimuonesha mwanamke akifanyiwa vitendo hivyo na kundi la wanaume zaidi ya wanne. TLS imelitaka Jeshi la Polisi kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wahusika na kuhakikisha haki inatendeka. Chama hicho pia kimetoa wito kwa jamii kusimama pamoja kupinga udhalilishaji na ukatili wa kijinsia. TLS pia imeahidi kushirikiana na vyombo vya usalama na haki jinai katika kufuatilia suala hili kwa karibu na kuhakikisha wahalifu wanafikishwa Mahakamani.
Tamko hilo linasomeka.
“Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kimepata taarifa kupitia mitandao ya kijamii na taarifa maalum kwa Umma kutoka kwa Jeshi la Polisi Tanzania juu ya video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonesha mwanamke anayesemekana anaishi eneo la Yombo Dovya Jijini Dar es Salaam akifanyiwa vitendo vya udhalilishaji na ukatili wa kijinsia na kundi la Wanaume huku wakirekodi video ya vitendo vile viovu. Tukio hilo sio tu ni kinyume na sheria za nchi yetu lakini pia ni kinyume na maadili na utamaduni wetu kama Watanzania.
Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), kinalaani kitendo hiki kiovu na tunalitaka Jeshi la Polisi kuchukua hatua stahiki za kisheria na kuhakikisha wahalifu wote walio tenda kitendo kile na waliowezesha kutendwa kwa kitendo kile kiovu wanakamatwa na kufikishwa Mahakamani mara moja ili haki iweze kutendeka. Aidha TLS inapinga vitendo vyote vya kikatili na udhalilishaji dhidi ya wanawake na iko tayari kushirikiana na vyombo vyote vya usalama na haki jinai katika kuhakikisha wahalifu hao wanafikishwa katika mamlaka sahihi za haki ili kujibu mashitaka yao. TLS pia kupitia kifungu cha 4 (e) cha Sheria iliyounda TLS (Tanganyika Law Society Act, Cap. 307 R.E. 2002) inaendelea kufuatilia mwenendo wa suala hili kwa ukaribu zaidi kwa kushirikiana na vyombo vya usalama na vinavyosimamia haki jinai ili kuhakikisha hatua stahiki kwa waliohusika zinachukuliwa kwa wakati na kwa mujibu wa Sheria.
Kila binadamu anastahili heshima, haki na usawa katika jamii yetu. TLS inatoa wito kwa jamii kusimama pamoja kupinga udhalilishaji, unyanyasaji na ukatili wa kijinsia wa aina yoyote ile ikiwemo kuacha mara moja kusambaza video zinazohusu tukio hili ili kulinda haki ya mhanga.
Tanzania bila udhalilishaji, unyanyasaji na ukatili wa kijinsia inawezekana!
Imetolewa na Baraza la Uongozi la Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS)
Boniface A.K Mwabukusi - Rais”
Soma pia: Polisi yaanza kufuatilia tukio la Binti aliyebakwa mande na wanaume watatu
Mie niko tofauti kidogo.
Kwani huyu binti kasema nini mpaka saizi?
Jamaa waliokamatwa je wao wamesema vipi?
Hili jambo linahitaji utulivu, watu wanalipapatikia kihisia sana na hili ndio tatizo la kulelewa na singo mama, wana judge mambo kwa feelings kuliko kufikiri hata kidogo.
Vipi kama ikija kujulikana wote kwa pamoja(majamaa na mdada)waliamua kurekodi video kwa hiyari yao, ila wakaamua kuigiza kama binti anashurutishwa??? Labda kwa lengo fulani kama kutafuta Kiki???
Siungi mkono matendo ya namna hiyo lakini tusubiri kidogo uchunguzi ndio tuongee.
Watu wamelipokea hili tukio kwa hisia sana(singo mama product) hivyo kila mtu anatoa matamko tu kana kwamba imethibitika ni ukweli.
Mara ngapi tunaonaga video za x unakuta mwanamke anashurutishwa kweli kweli lakini mwisho wa siku unaona ni maigizo tu.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Ni kosa kisheria kumpiga mtu kipara alafu ukajorekodi na ukasambaza so hata kama hawakumlazimisha hiyo bado ni kesi, kimsingi hapo kuna kesi zaidi ya moja hao majamaa hawana pakutokea, mfano yule alosema atamla jokeri nae asishitakiwe ? Eti me nikiingia nakula mavi, nakula jokeri daaah [emoji23][emoji23][emoji23]