Tofauti kati Mchawi na Mkristo

Tofauti kati Mchawi na Mkristo

Daah hii ukristo naona wengi ni jina tu na association ila nafsi zao kuna wachawi wa mchana na usiku
Tukisema hivi tutakuwa tunahukumiana.

Key words iwe;kila mmoja Mungu ndiye anayeijua imani yake kwake sasa ni huyo anayejiita Mkristo kuuishi Ukristo, toa sadaka kwa maskini ishi na watu kwa amani fariji wagonjwa na hakuna binadam asiye na uwezo wa kumsaidia mwenzake tunajitetea mimi siyo tajiri ila kila mmoja ajue kama leo hadi muda huu umeshakula umeshiba unataka kulala na mfukoni umebaki na Tsh 10,000/=.

Hiyo hela kuna mtu mahali ilikuwa umpe nae akale na familia yake tatizo ubinafsi umetuondolea macho ya kuwaona hao watu.
 
Kuwa mkristo ni kuamini unauwezo wa kuongea na kuvielekeza hata vitu visibyoongea na vikatii. Katika sayansi hiki kitu hakipo. Ikiwa unaamini Biblia na huamini haya, imani yako iko chini kuliko imani ya wachawi na majini kwa shetani wao.

Mchawi anaweza kumuamrisha Paka, Mbwa, Akaongea na ardhi, vumbi, miti na akaifanya ifanye anavyotaka.

Ikiwa unamuaminj Yesu alafu huamini kuwa hata mawe au nyumba au gari ukiongea nalo linakusikia. Watu wabaya wanaongea navyo vikudhuru wewe.

Ikiwa unaamini utakuwa na uwezo wa kugeuza na vikawa silaha zako za kumshindia shetani. Hata Moyo, figo, magonjwa wako unaweza kuongea nayo.

Ushahidi.
Yesu aliongea na upepo
Muda aliongea na mawe.
Yesu aliongea na homa.
Baalam aliongea na punda.
Ardhi ilimlilia kaini.
Nabii kijana aliongea na madhabau (Mawe kuni).
Biblia inasema anga linaongea. Latangaza utukufu wa Mungu .

Musa aligeuza vumbi likawa chawa.

Yesu hakutania aliposema.
Unaweza kuuambia Mlima, mkuyu ukafanya unavyotaka.

Hii ni siri kubwa. Hata magonjwa unaopoongea nayo, kama yameletwa na majini hayo majini yatapiga kelele na kuondoka. Mfano Juzi mama mmoja aliniambia anaumwa kisukari cha ghafla. Nikaanza kuongea na kisukari na kukiambia kitoke ghafla akaanza kupiga kelele. Kumbe ni tujini tumesurbotage insulin. Akawa mzima.

Ila hata kama ni cha kibaiolojia unaongea nacho. Acha watu wakuone umechizi ila Mungu anakuelewa. Kitatii na kuondoka ikiwa roho ataona vyema. Ila kumbuka wengi Mungu hatawaponya kwa sababu wanafanya kusudi kujiletea magonjwa hata kama waikipona mfumo wao wa maisha utayaleta tena. Hata usijisumbue. Wafundishe badala ya kuwachosha na maombi.

Kama umepata kitu sema amina.
 
Wakristo wengi wanadeal na vitu vya kuonekana kwa watu kama ulivyosema. Mchawi yuko kiroho zaidi
 
Trust me waganga weng wa kienyeji ....wanatumia Quran...bado cjaekewa kunauhusiano gani Kati ya uislam na uganga wa kienyeji....
 
Trust me waganga weng wa kienyeji ....wanatumia Quran...bado cjaekewa kunauhusiano gani Kati ya uislam na uganga wa kienyeji....
Hii ni kweli kabisa. Babu yangu alikuwa sheikh na alikuwa na uchawi wa kitabu
 
Trust me waganga weng wa kienyeji ....wanatumia Quran...bado cjaekewa kunauhusiano gani Kati ya uislam na uganga wa kienyeji....
ASALAAM ALEYKHUM WARAHMATULLAH WABARAKATU?NAAM BABUUUU👴🏿👴🏿👴🏿NI MASHINE YA KAZI HII YAPA🌳🌳🌳🐘🐘🐘CHINEMERA NEMBO/KINEMELA TEMBO NI SHIDAAAA👴🏿
1673405213890.jpg

NAAM NILIHAIDI KUTEREMSHA MASHINE YA KAZI KWENYE MITI BASI NDIO HII

PICHANI NI MTI MAALUFU UNAOJULIKANA KWA JINA LA CHINEMERA NEMBO AU KINEMELA TEMBO 🐘🐘🐘MTI AMBAO UNAVITUKO VINGI KWENYE TIBA ASILIA 👉JE UNAJUA KWA NINI UNAITWA CHINEMERA NEMBO?JE KUNA UHUSIANO GANI BAINA YA MTI HUU MNYAMA TEMBO?
👉BASI TULIA HAPA MJUKUU WANGU NIKUPE MAANA HALISI YA JINA HILI
👉NAAM KWANZA TAMBUA MTI HUU KIBABU BABU👴🏿👴🏿👴🏿 TUNAUITA CHUMA MWANA HAFUNYWA LUKOMBE,TUKIWA NA MAANA KUWA MTOTOTO HAFUNYWI NA KUCHA😀😀😀HIYO NDIO LUGA YA KIBABU BABU

👉SASA NAKUPA SIRI YA JINA HILI KWA TIBA ASILIA LIMEBEBA MAANA GANI👉KWANZA KABISA MTI HUU UMEPEWA JINA HILI KWA SABABU TEMBO NA UJANJA WAKE WOTE ,MABAVU YAKE YOTE HANA JEURI YA KUVUNJA MTI HUU

👉PIA UKIUKETA KWENYE KAZI YA TIBA NI NGUMU SANA KUSHINDWA KUFANYA ULILOKUSUDIA BIIDHIN LLAH ENDAPO UTAFATA TARATIBU ZAKE

👉1;MOJA YA FAIDA YA MTI HUU TENA ADHWIM NI KUFUNGA KESI👉KUMSHINDA ADUI YAKO 👉KUMSHINDA MCHAWI NA KILA AINA YA VITA BASI HUU NDIO KIBOKO YAKE
👉IKITOKEA SIKU UNAKESI MAHAKAMANI AU KUNA MTU UNAENDA KUSHINDANA NAE KWA JAMBO LOLOTE UNATAKA KUMSHINDA ,BASI NJOO KWENYE MTI HUU ASUBUHI SANA KABLA JUA KUCHOMOZA NA ITAPENDEZA IWE SIKU YA JUMANNE👉PIGA HODI ×7 KISHA UITE MTI HUU KWA JINA LA CHUMA MWANA HAFUNYWA LUKOMBE, NIMEKUJA KWAKO KUCHUKUA DAWA YA KUMSHINDA ADUI YANGU FULANI BIIN FULAN(JINA LAKE)WEWE HUSHINDWI NA CHOCHOTE ISIPOKUWA MUNGU,TEMBO KAKUSHINDWA WEWE NA UKUBWA WAKE WOTE BASI NA MIMI NATAKA KWENYE KESI YANGU NIMSHINDE FULANI KAMA WEWE ULIVYOMSHINDA TEMBO NATAKA MIMI NIKAIBUKE KIFUA MBELE👉NIKAMSHINDE KWA HOJA NA NGUVU

UKIMALIZA MWAGIA MWAGIA MCHELE SEMA HII NI SADAKA YA VIUMBE WOTE WATAKAOKULA HII SADAKA IKAWE KAFARA YA KUFANIKIWA JAMBO LANGU👉UKIMALIZA CHUMA HAYO MAJANI KINYUME NYUME LUDI NAYO NYUMBANI KISHA YAFIKICHE AU YATWANGE KISHA JIPAKE USONI ,KIFUANI NA MIKONONI NA MIGUUNI NENDA KWENYE HIYO KESI👉WALAHI , WABILAH,WATALAHI UTAONA MAAJABU HAKUNA UTAKACHOZUNGUMZA WEWE KIKAPINGWA SIKU HIYO👉NA UTAMSHINDA HUYO ADUI KWENYE HIYO KESI

👉PIA MAJANI HAYO UKIYACHUMA KWA WINGI NA UKAYAPINDA KWENYE KINU KISHA UKACHANGANYA NA MAKATA ORGINAL NA MAJI UKATUMIA KUOGA NA KUPAKA HUFUKUZA MIZIMU MICHAFU INAYOKUSUMBUA

👉2;MWANAMKE MWENYE CHANGO LA KUMWAGA BILA MAPUNZIKO YANI ANATOKA DAMU MFULULIZO AU HAPATI MIMBA CHUKUA MCHELE KATAMBIKE MWAGIA KISHA CHIMBA MIZIZI YAKE NENDA KAFUNGE NA USHANGA MWEUPE MCHEMSHIE KISHA MPE ANYWE KIKOMBE CHA CHAI 1×2 SIKU 7-15 UTAPATA JIBU KWANINI HUU NI CHUMA MWANA HAFUNYWA LUKOMBE,MTOTOTO HAFUNYWI NA KUCHA😀😀😀😀

👉3;NAAAM UKITAKA KINGA MUJARABU YA MWILI NA MJI TAFUTA PANGAA ZAKE ZIFUNGE NA KIPANDE CHA KANIKI KISHA KAALIKE KWENYE MKUNGWANILA (JALALA)SIKU 7 UKITOA PIGA MOTO USILA TUMIA KUCHANJIA AU KUZINDIKA MJI WAKO HATOKANYAGA KINYAGO WOWOTE HAPO

👉4;WENYE VIBAMIA LEGE LEGE MNATAKA VIKOMAE YANI MISURI IWE IMALA CHEMSHA MIZIZI TUMIA KUNYWA UJAZO WA KIKOMBE CHA CHAI 1×2 SIKU 7-15

👉5;UNA UCHAWI UNAKUSUMBUA MWILINI,UMEMALIZA MADAWA ,CHIMBA MIZIZI HII YA CHINEMELA NEMBO TENGENEZA USEMBE WAKE UTUMIE KWENYE UJI WA MTAMA SIKU 7-15 MWENYEZIMUNGU ATAKUSAIDIA INSHAALLAH

👉6;UNATAKA KUOGOPWA NA MAADUI ZAKO CHUKUA MCHELE KATAMBIKE KWENYE HUU MTI KISHA CHUMA MATUNDA YA HUU MTI NA UCHIMBE MZIZI MMOJA ULIONYOOKA UPANDE LINAPOTOKEA JUA KISHA KAUNGUZE KWENYE KINU UPATE USILA👉USILA HUO CHANGANYA NA MAFUTA YA NYANGUMI TUMIA KUCHANJIA UTAOGOPWA NA KILA MWENYE UBAYA NA WEWE
👉NAAM KWA UFUPI HUU NDIO CHINEMELA NEMBO🐘🐘🐘🐘🐘
👉NAAM KWA WALE AMBAO HAMJAPATA KITABU WASILIANA NAMI UTAKIPATA KWA HARD COPY NA KWA PDF HIVYO UNASHIDA NACHO UTAPIGA SIMU UTAPEWA MAELEZO WAPI UTAKIPATA ,SASA WEWE JIFANYE AMNAZO NIULIZE TENA KWENYE COMMENT UTAKIPATAJE IKIWA NIMESHATOA MAWASILIANO MAANA KUNA WATU WAGUMU KUELEWA

YALIYOMO KWENYE KITABU HIKI CHA MAKARAMA YA UGANGA WA AJABU KIBUYU CHA BABU
👉ELIMU NANE(8)ZA UGANGA
👉KUMTEGA MCHAWI NJIA PANDA
👉KUTEGA RADA ZA WACHAWI
👉DAWA YA KUUA UCHAWI KWENYE MJI
👉DAWA YA BIASHARA

👉KUTIBU KICHAA NA MALUELUE

👉KUMUADHIBU MWIZI

👉KUWAONA WACHAWI NA MAJINI

👉TUNGULI YA MVUTO WA AJABU

👉KIBERITI CHA MAPENZI

NAAM KAMA UNATAKA MIKWAJU YA KIBABUBABU ELIMU IPO HUMU



NAAM 👴🏿👴🏿👴🏿👑👑👑🔥🔥🔥🏃🏻‍♂️🏃🏻‍♂️🏃🏻‍♂️BY DOCTOR HURUMA.
 
Hii ni kweli kabisa. Babu yangu alikuwa sheikh na alikuwa na uchawi wa kitabu
Uyo babu yako alikua mchawi na ndo walivokua wazee wa zamani kuitumia elimu ya Qur-an kwa uchawi
Ila Mungu atuongoze
M nakuusia icho kitabu achana nacho na kadri unavompa mtu na ww unazidi kupata madhambi kwa Mola wako
Hakika ya Ushirikina una mwisho mbaya tu
Allah anasema kwenye Qur-an yake

( وَلَقَدْ أُوحِيَ إِلَيْكَ وَإِلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكَ لَئِنْ أَشْرَكْتَ لَيَحْبَطَنَّ عَمَلُكَ وَلَتَكُونَنَّ مِنَ الْخَاسِرِينَ )

الزمر (65) Az-Zumar

Na kwa yakini yamefunuliwa kwako na kwa walio kuwa kabla yako: Bila ya shaka ukimshirikisha Mwenyezi Mungu a'mali zako zitaanguka, na lazima utakuwa miongoni mwa wenye kukhasiri.

( وَإِذْ قَالَ لُقْمَانُ لِابْنِهِ وَهُوَ يَعِظُهُ يَا بُنَيَّ لَا تُشْرِكْ بِاللَّهِ ۖ إِنَّ الشِّرْكَ لَظُلْمٌ عَظِيمٌ )

لقمان (13) Luqman

Na Luqman alipo mwambia mwanawe kwa kumpa mawaidha: Ewe mwanangu! Usimshirikishe Mwenyezi Mungu. Kwani hakika ushirikina bila ya shaka ni dhulma iliyo kubwa.

Nimekunasihi ndugu yangu ima ufuate au uache ni jukumu lako
 
Trust me waganga weng wa kienyeji ....wanatumia Quran...bado cjaekewa kunauhusiano gani Kati ya uislam na uganga wa

Uchawi wa vitabu

Kwa wale wasomi wengi wa Lugha ya Kiarabu watakuwa tayari wameishajua nini ninataka kuongelea.Uchawi mwingi ambao upo hapa kwetu unaoitwa uchawi wa vitabu na hutumiwa sana na baadhi ya watu kuumiza wenzao na kuwagombanisha au kuwaachanisha kati ya mke na mume, kuwagombanisha ndugu, kuwatupia majini watu, kuwapa nuksi na mengine mfano wa hayo.
Kuna watu huwa Mungu kawajaalia kuwa na akili mashuleni ila inapofikia kipindi cha Mitihani hufeli vibaya sana na wanakuwa wanaishia mitaani, katika hawa huingia mambo ya madawa ya kulevya, uvutaji bangi , ujambazi na unyang’anyi na mengine mengi ya ajabu na aibu.Mengi katika haya hutokana na uchawi wa kijini na uchawi unaotumia vitabu au uchafu.
Suali letu , uchawi huu wa vitabu asili yake ni wapi?
Ukitizama sana vitabu hivi vingi vimeandikwa kwa Lugha ya Kiarabu, na hivyo kimakosa wengi wanaweza kufikiri ni Kuruani.La hasha, vingi katika vitabu hivi si Kuruani ila maandiko ya makuhani wa Kigiriki(wayunani), makuhani wa Kiyahudi , makuhani wa Kihindi(Kihindu) na pia Makuhani wa Kisuriyani waliowahi kuishi miji ya Nineve na Babiloni(miji hii imetajwa katika Kura’ani na bibilia )
Swali letu la msingi bado linaendelea, mbona basi vipo katika Kiarabu?
Kwanza ieleweke , Kiarabu kinahusishwa sana na Uisilamu, hivyo wengi wameingia makosani kusema kuwa uchawi huu ni uchawi wa Kuruani au uchawi wa Kiarabu.Kamwe huu si uchawi wa Kuruwani, kwani Kuruani inakataza matendo ya Kishirikina ikiwemo kumshirikisha Mungu na kiumbe chochote na mfano utaona Kuruani inaongelea suala la majini walivyoanza kufundisha uchawi katika miji ya Babiloni na Mungu akawapa watu wa Babiloni watu wenye sifa za Kimalaika walioitwa Haruti na Marut ili kuwafundisha hao watu hiyo elimu ila wakawaonya watu kuwa tunakufundisheni elimu hii lakini sisi hatujamuasi Mungu.Kwa nini hawa malaika walianza kufundisha watu uchawi ikiwa basi Kuruani inakataza uchawi?Walifanya hivyo ili kuwaweka watu sawa kuwa majini si Miungu wala hawana nguvu za Kimungu au muujiza na hizo nguvu hazikuwa nguvu za Kimungu au muujiza ila nguvu za Giza au mauzauza na hivyo kila mtu anaweza kufanya huo uchawi na hivyo kuwapa tahadhari wanadamu kuwacha kuwaabudu Mashetani kwa kuwaonyesha mazingaombwe yao ili wapate ukubwa wa Ki-Mungu.
Baada ya matukio haya ya Babiloni, watu wakaanza kuandika uchawi katika vitabu na kufundishana.Lugha kubwa iliyokuwa ikitumika kuandika vitabu hivi ni Ki-Suriani ambayo hivi sasa ni lugha ambayo imetoweka ila bado wapo watu hususan wenye kufuata mafundisho ya Kikiristo huko maeneo ya Mashariki ya kati huitumia lugha hii kwa ibada zao. http://www.syriac.talktalk.net/syriac_history.html
Baada ya ujio wa Mitume wengine wa Mungu katika taifa la Israel lugha hii iliendelea kuwa Lugha ya mawasiliano na Lugha ya Kimaombi na elimu ya vitabu vya uchawi na uganga viliandikwa katika lugha hii.
Baadae watu wa Israeli nao wakaanza kuandika elimu hii na wakaishjihisha kuwa ni moja katika elimu za dini ya Kiyahudi na wakaiita Kaballah au Qaballah.Wakachanganya elimu za Mungu na elimu za Makuhani wakuu toka Iqipti(Egypt) mara baada ya kukombolewa na Nabii Musa toka Misr.
Maingiliano ya Warumi ,Wa-Iqipt, watu wa Babiloni, Nineve, Wayahudi, Wa-ajemi(Persian) ukazaa mabadilishano ya elimu hizi za uchawi , maarifa ya kimaisha na ujuzi , mila na ustaarabu,, elimu za kitabibu na elimu nyingine nyingi ambazo hapa si mahala pake pa kujadili.
Warumi walikuwa wameathirika sana na Wagiriki ambao walibobea katika elimu za Nyota, elimu za tiba, elimu za majini(mizimu), elimu za Falsafa na kadhalika
Ancient Greek Philosophy | Internet Encyclopedia of Philosophy

Dunia ikawa imezama katika giza la upotofu na ukweli, elimu za Ki-Mungu zikachanganyika na elimu za kishetani.Ikumbukwe kuwa elimu hizi ziliendelea kuandika kwenye vitabu na watu waliendelea kufundishana elimu hizi kwa simulizi na kujifunza maneno ambayo yalikuwa yanaminika yana nguvu kuita majini au viumbe vingine visivyoonekana.Bado elimu hizi ziliendelea kuandikwa katika lugha za Kisuriani , Kiyunani, Kiyahudi , Ki-Ajemi, kwa herufi za Ki-iqipt(Hieroglyph) na hata kwa lugha za Kihindi , Nabatean, Aramaik na maandishi mengi zaidi yalikuwa ya Kigiriki.
Jewish Magic and Superstition: Appendix I. The Formation of Magical Names

Mbona elimu hii ya uchawi iko katika maandishi ya Kiarabu?
Ni kweli tunaona hivi hii leo maandishi mengi ya elimu za uchawi na Matalasimu yako katika lugha za Kiarabu, kwa nini na tunaambiwa uchawi ni haramu katika Kuraani?
Baada ya kufa Mtume Muhammad (s.a.w) kulikuwa kuna tawala nyingi za ki-Khalifa na elimu hii ilikuwa haramu mtu kuwa nayo.Na watu wengi walikuwa wakiuwawa(ndio Hukm ya Kiisilamu juu ya mchawi) mpaka ilipofikia U-Khalifa wa Abbasia(Abbasid Khalifate) katika mwaka 832 AD, Khalifa Harun Rashid aliona kuna haja ya kuanzisha idara ya kutafsiri elimu toka katika lugha kuu zingine zilizokuwa zikitumika ktika elimu za Kitiba na maarifa mengine , ni wakati huu ndipo ilipoanzishwa Bayt al Hikma huko Baghdad na walikusanywa wataalamu wa elimu hizi na elimu nyingine wakiwemo kinaThabit Ibn Quraa ambaye hakuwa Musuilamu
bali mfuasi wa dini ya Sabian na maandishi yao yalikuwa katika lugha ya Kigiriki.Hawa wanaitikadi kuwa wanamfuata Nabii Idris(Enoch).Huyu Thabit ndio muandishi na mtunzi wa kitabu cha kiganga kinaitwa Ghayat al Hakim ambacho kilitafsiriwa na kasisi wa kikatoliki Marsilio Ficino na kukiita De Imaginibus na kitabu hiki kilikuwa kikipatikana sana nchi za ulaya na kujulikana kwa jina jingine kama Picatrix
http://www.renaissanceastrology.com/picatrix.html
http://www.renaissanceastrology.com/thabit.html
Ukuwaji wa Baitu al Hikma ilisaidiwa sana baada ya china kugundua na kuanza kutengeneza karatasi na kusambaza Baghdad na Andalusia(Spain, kusini mwa Italy/Sicily, Ureno na baadhi ya maeneo ya Ufaransa mpaka Al-Hambra.

Elimu hii ikaanza kuingizwa kwenye lugha ya Kiarabu na vitabu vingi vikawa vinachapwa kwa lugha ya Kiarabu ila matamshi yaliwachwa vilevile mfano Adonai Asw-bahut al Ushudaya(ambacho ni Kiyahudi) na matamshi kama Ashmakhin Namushalakhin Aqshamshqin ambayo ni lugha ya Kisirianiyah.
Pia kuna maombi mengi toka lugha hizi ambayo yapo kwenye vitabu hivi ambayo si maombi ya Kiarabu wala mafundisho ya Kiisilamu mfano kuna maombi yanaitwa Barhatiyah ambayo yasemwa ni Lugha ya Kisuriani na lugha hii kwa mujibu wa vitabu inasemwa ilitumika wakati wa Nabii Adam.Vilevile kuna maombi yanaitwa Lahutiyah na Mahutiyah , haya pia si maombi kwa lugha ya Kiarabu ila herufi zake zimewekwa katika lugha ya Kiarabu na matamshi haya yako kwenye lugha ya Kisuriani na Kiyahudi na mafundisho mengine ya Kipagani.
Katika vitabu hivi maneno ya kigeni, yaani maneno ambayo siyo ya Kiarabu hufanyiwa tarjumani au tafsiri kwa lugha ya Kiarabu ili msomaji awe anaelewa nini anasoma.Mfano ni majina haya ya Kiyahudi na haya ya Kisuriani
Mfano neon Ahujin hutafsiriwa sawa na Al-Ahad yaani Mungu ni mmoja
Katika majina haya inaandikwa kuwa yana nguvu za kufanya jambo lolote zuri au baya ikiwa utafuatiliza masharti yake ipasavyo, mfano kufuata mwendo wa saa kwa kutmia , matumizi ya mafusho sahihi na kufuatiliza mwendo wa mwezi.
Katika vitabu hivi, ulifikia wakati wa dola za Kiisilamu kuvichoma moto na kuwauwa wale waliokuwa wakivitumia au kuviandika na kuvisambaza.mpaka pale lilipotokea kundi la watu ambao leo hii wanafanana na Free Mason(Masunia) likijulikana kama Ikhwan al Safwaa ambao walikuwa wakifuata Uisilamu wa Kishia mrengo wa Ismailia. Wao ndio walianza kuvihifadhi vitabu hivi na walikuwa na fikra ya kusema kuwa Mungu anayeombwa ni mmoja awe anatajwa kwa Lugha ya Kiyahudi au Kihebrania ,Kigiriki, Kisuriani au lugha yoyote maadam ni Mungu huyohuyo Mmoja wa Kweli na Haki basi na afuatwe.Ndio maana katika vitabu hivyo utakuta maneno kama Iluuhim(Elohim) Aswbahuwt(Asvaht) Ahya sharahiya na mengine mfano huo kutoka katika dini ya Kiyahudi.Hawa Ismailia walikuwa wanaitikadi ya Perenialism(walichanganya dini zote za kimila na dini za kimapokeo kuwa sawa)
Hawa Ismailia walipata nguvu baada ya kushika mamlaka na kuanzisha ukhalifa wao wa Fatimia na wakawa makao makuu yao nchini Misr.
Unaweza kusoma zaidi kuhusu Ikhwan al Safa hapa Ikhwan al-Safa’ | Internet Encyclopedia of Philosophy
Elimu hii ya vitabu kama inavyofahamika imekuwepo kwa karne nyingi hata kabla ya kuja kwa Mtume Muhammad SA.W kama tulivyoona katika makala yetu imeingizwa katika lugha ya Kiarabu na wengi wenye kujua kusoma Kiarabu vitabu hivi kwao inakuwa rahisi kuvipata na kuvielewa ila ni vyema watu wakajifunza zaidi elimu za Kiroho(Tazkiyah na Tasawuf) na kutegemea maandishi ya kiroho zaidi kuliko kuingia katika elimu hizi kwani zina mashaka mazito na mitihani mikubwa mno. Mungu akitujaalia tutaendelea kukuleteeni makala majini ni viumbe wa namna gani?Uchawi ni kitu gani?jinsi ya kujikinga na majini na uchawi , kwa nini watu wanajihusisha na uchawi?Masuunia ni nani na wanafanya nini?
Hakkam Mzee
 
Back
Top Bottom