Toka amenitolea posa amebadilika sana

Toka amenitolea posa amebadilika sana

Nyamwi255

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2022
Posts
4,848
Reaction score
12,776
Hadi nastaajabu jinsi mume wangu mtarajiwa alivobadilika na kuonesha upendo ambao sijawahi kuupata kutoka kwa mtu mwingine isipokuwa wazazi.

Iko hivi, huyu kijana nimekutana naye nina kama mwezi na wiki, na hii ni baada ya kujitunza kwa muda mrefu. Lakini toka tumeingia kwenye mahusiano, hakuwahi kunipa hata hamsini mbovu na mimi sikuwahi kumuomba.

Nilikuwa najipa moyo nikasema labda ananipima, lakini mpaka unatimia mwezi sijaona akinipa chochote.

Sasa wiki moja iliyopita amenishangaza baada ya kunambia anataka kunioa. Binafsi sikuamini, nikajua labda ananitania, kumbe alikuwa serious na ameshajiandaa.

Basi nilipomuona yuko serious, nikampa muongozo ndani ya wiki hii akapeleka posa.

Sasa toka anipose amekuwa akinipa pesa na kunihudumia mpaka nashangaa, yaani naletewa zawadi kila siku na leo kanambia niseme nataka mahari Tsh ngapi. Madai yake anasema hataki mwezi wa saba uishe kabla hatujaoana.

Binafsi nafarijika sana na namuomba Mungu ndoa yetu ipite salama.

Kuna situation fulani ka raha sana nakapitia.

TBH, I am so excited nimeamua ni ka share na ninyi.

Mwanaume akiwa na malengo na wewe kumbe anakuhudumia hivi 🤔.
 
Hadi nastaajabu jinsi mume wangu mtarajiwa alivobadilika na kuonesha upendo ambao sjwahi kuupata kutoka kwa mtu mwingine ispokuwa wazazi.

Iko hivi huyu kijana nimekutana nae nina kama mwezi na wiki na hii ni baada ya kujitunza kwa muda mrefu, Lakini Toka tumeingia kwenye mahusiano hakuwahi kunipa hata hamsini mbovu na mimi skuwahi kumuomba.
Nilikuwa najipa moyo nikasema labda ananipima lakini mpaka unatimia mwezi sjaona akinipa chochote.

Sasa wiki Moja iliyopita amenishangaza baada ya kunambia anataka kunioa,.binafsi skuamini nikajua labda ananitania, kumbe alikuwa serious na ameshajiandaa.
Basi nilivomuona Yuko serious nikampa muongozo ndani ya wiki hii akapeleka POSA.

Sasa Toka anipose amekuwa akinipa pesa na kunihudumia mpaka nashangaa yani naletewa zawadi Kila siku na Leo kanambia niseme nataka mahari Tsh ngapi, madai yake anasema hataki mwezi WA Saba uishe kabla hatujaoana

Binafsi nafarijika sana na namuomba mungu ndoa yetu ipite salama.

Kuna situation Fulani ka raha sana nakapitia.
TBH am so excited nimeamua ni ka share na ninyi

Mwanaume akiwa na malengo na wewe kumbe anakuhudumia hivi🤔
Pimeni afya, hongera na kila la Kheri!
 
Hadi nastaajabu jinsi mume wangu mtarajiwa alivobadilika na kuonesha upendo ambao sjwahi kuupata kutoka kwa mtu mwingine ispokuwa wazazi.

Iko hivi huyu kijana nimekutana nae nina kama mwezi na wiki na hii ni baada ya kujitunza kwa muda mrefu, Lakini Toka tumeingia kwenye mahusiano hakuwahi kunipa hata hamsini mbovu na mimi skuwahi kumuomba.
Nilikuwa najipa moyo nikasema labda ananipima lakini mpaka unatimia mwezi sjaona akinipa chochote.

Sasa wiki Moja iliyopita amenishangaza baada ya kunambia anataka kunioa,.binafsi skuamini nikajua labda ananitania, kumbe alikuwa serious na ameshajiandaa.
Basi nilivomuona Yuko serious nikampa muongozo ndani ya wiki hii akapeleka POSA.

Sasa Toka anipose amekuwa akinipa pesa na kunihudumia mpaka nashangaa yani naletewa zawadi Kila siku na Leo kanambia niseme nataka mahari Tsh ngapi, madai yake anasema hataki mwezi WA Saba uishe kabla hatujaoana

Binafsi nafarijika sana na namuomba mungu ndoa yetu ipite salama.

Kuna situation Fulani ka raha sana nakapitia.
TBH am so excited nimeamua ni ka share na ninyi

Mwanaume akiwa na malengo na wewe kumbe anakuhudumia hivi🤔
Mwanamke anayeomba omba hela huwa simpendi.
Kila mwanamke ana mahitaji na ni lazima kumhudumia ila siyo yeye anavyotaka
 
Back
Top Bottom