Toka kwa Wananchi: Kero na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa

Toka kwa Wananchi: Kero na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa

Magu anaweza kuwa na nia na dhamira ila wana ccm ndo wanaomkwamisha mana hakuna aliye msafi jipu LA ufisadi wa wana ccm likitjmbuka then akaweka msingi wa katiba wa kuruhusu raisi aliyetoka madarakani kushitakiwa itakua poa. Katiba ya sasa iko kichama. Bila kumtumbua mkwere na sidhani kama anagusika
 
Lowasa na genge lake chini ya rostam azizi umelisahau
Wewe una uelewa mdogo kama Lowassa yumo mbona hatujasikia akikamatwa na yupo nje ya ccm? wewe unafikiri Lowassa angekuwa amefisadi kama alivyofanya Kikwete wangekuwa wamemwacha hadi leo? na kama amefisadi nchi basi wahusika wakubwa wapo ccm ndio maana wanashindwa kumkamata maana mambo yote yatakuwa hadharani
 
Kama ana nia ya dhati ya kumaliza ufisadi nchini afute Chama Cha Mapinduzi!
 
kupambana na ufisadi nchii hii ni ngumu sana. maana wahusika wakuu ni vigogo....
 
Nafikiri Magufuli apache kucheza zero sum game ya watumishi hewa aishughulikie ccm kwanza vingenevyo atastukia 2020 hii hapa hajafanya chochote
 
LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMIbLUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI LUGUMI
 
Kama ana nia ya dhati ya kumaliza ufisadi nchini afute Chama Cha Mapinduzi!
Chama cha mapinduzi hakina shida hata kidogo!
In fact hiki ni chama imara, bora na chenye misingi imara ya uongozi kuliko chama chochote nchini! Tazama mfumo wake wa uongozi!
Ila kuna shida ktk ccm kwa baadhi ya viongozi wake, kama Magufuli atachukua chama na kukifanya kama ilivyo serikali, then ccm itaimarika zaidi!
 
Chama cha mapinduzi hakina shida hata kidogo!
In fact hiki ni chama imara, bora na chenye misingi imara ya uongozi kuliko chama chochote nchini! Tazama mfumo wake wa uongozi!
Ila kuna shida ktk ccm kwa baadhi ya viongozi wake, kama Magufuli atachukua chama na kukifanya kama ilivyo serikali, then ccm itaimarika zaidi!

Kwa muktadha huo unaonaje ukamshauri msajili wa vyama vya siasa afute vyama vingine ibaki tu CCM?
 
Kwa muktadha huo unaonaje ukamshauri msajili wa vyama vya siasa afute vyama vingine ibaki tu CCM?
Sasa vyama vingine vifutwe kwa sababu zipi?
Uimara wa ccm unajengwa na changamoto zinazotokana na kuwepo kwa upinzani! Ni faida kwa watanzania wote, ukawa, ccm, vyama vingine na wasio na vyama pale unapotokea ushindani baina ya vyama au wagombea na pia kuongeza wigo mpana kwa watu kuchagua watendaji na vyama vyao, lkn pia wananchi kuchagua itikadi zitakazo ongoza dira ya maisha yao kupitia mlengo wa siasa!
 
Mimi ninadhani madini na wanyama ni rasilimali nyeti sana za nchi na ni mali ya watanzania wote.

Ninatamani kusikia kuhusu mikataba ya madini na mbugani sijui uwindaji ijadiliwe bungeni na wananchi tusikie na kujua madini yanayochimbwa ni kiasi gani yana thamani gani na nchi inapata kiasi gani kutokana na kiasi gani cha madini.

Na mikataba ya uwindaji wa wanyama kama ipo nayo iwekwe wazi bungeni na tutajiwe majina ya wamiliki wa kampuni za uwindaji si majina ya kampuni, bali majina ya watu!

Natamani kusikia viongozi wa juu wa nchi yetu wakilizungumzia hilila madini na ujangili.

Ninaamini nchi ikisimamia hizo sekta ( utalii na madini) tu vizuri sana na kuziba mianya ya wajanja wanaotafuna hizo sekta kweli hatuhitaji msaada wa kutoka nje.

Natamani kuiona Tanzania ikiwa nchi tajiri, na hilo linawezekana ufisadi ukizimwa kila ofisi nchi nzima, sasa nina miaka 40 wimbo ni mmoja tu Tanzania ni nchi masikini!

Mimi binafsi nimechoka mno kusikia wimbo huu!

Na sioni kama kunayo sababu gani ya kuifanya mikataba kama ya madini kuwa ni ya siri hasa ukizingatia ya kwamba hakuna ushindani maana hatuna nchi washundani ktk sekta kama ya madini kwa sababu ikiwa tunayo tanzanite jirani yetu hana na ikiwa tunayo dhahabu pia jirani yetu hana dhahabu ya kuitosheleza dunia ili tuseme ya kuwa tunaogopa tukiiweka mikataba yetu hadharani wanaweza kutupiku na hata baadaye wakawachukua wawekezaji wetu ambao tumezianika siri zao

zaidi ya hapo mimi naona mikataba kama hii inafichwa kwa ajili ya maslahi ya wachache

hivyo naungana na mtoa kero mikataba kama hii ipelekwe bungeni ijadiliwe na wabunge kwa faida ya wananchi wa tanzania
 
Habari,

Majipu yapo mengi ila kuna hili la madini nadhani nalo ni la muhimu kama walivyotangulia kusema wengine.

Nasema hivi kwa kuwa nina wasiwasi wachache ndio wanaonufaika. Kama unasafiri mara kwa mara kutokea Mwanza kwenda Dar au Arusha hapo katikati utakutana na Malori si chini ya 30(nimeshawahi kuhesabu) either yakitoka nchini au yakiingia kuchukua Udongo wetu kuupeleka huko nje, watu wamekwisha hoji sana lakini hakuna kinachofanyika.

Hali hii ni ya kutumbua, haiwezekani mtu atumie nguvu nyingi kusafirisha udongo usionathamani kubwa zaidi alafu yule mwananchi wa maeneo husika hana maji wala umeme, kama mzalendo nadhani hili ni jipu sugu.
 
Wafanyakazi wa kitengo cha mipango miji Halmashauri ya Kinondoni wanatakiwa watumbiliwe haraka iwezekanavyo.

Hawa wafanyakazi hasa cartographers ambao wengi wao ni wakina mama wa makamo wakiongozwa na mama mmoja wa kipare wanakalia kazi walizoambiwa warekebishe na wizara ili kuwawezesha wananchi wapewe hati zao.

Hati nyingi hazijakamilika kule wizarani kwasasababu "VIZIDUO" vilivyoambatanishwa toka wizarani havijafanyiwa kazi na wahusika wanaomba rushwa mpaka ya shs.700,000 mpaka shs 800,000 ili wawakamilishie wahusika vizuduo vyao na kuvipeleka wizarani!!

Kuna umuhimu wa kuwamulika vizuri hawa cartographers ambao ni watu wazima na heshima zao lakini wanawasumbua wananchi kwa kutotimiza wajibu wao na kuomba rushwa.

Mimi ni muhanga wa tatizo hili na natarajia kwenda kumuona mkurugenzi wa halmashauri nione nae atalishuhulikia vipi kwani ninafuatilia hati yangu toka mwaka 2010 NA SIKO TAYARI KUHONGA!!!

Hawa cartographers hawajui kuwa kwa ufisadi wao huo wanaikosesha serikali mapato kutokana na land rent ambayo hailipwi kwani wananchi hawajapewa hati zao!!
Ninaunga mkono hoja.

Mimi faili langu limepotea inabidi nianze upya. Huyo mama wa kipare nilifika ofisini kwake akaonyesha jeuri ya hali ya juu. Watu wanalipwa mshahara kwa kodi yetu ili watutumikie lakini bado wanataka tuwape hela watufanyie kazi ambayo ni haki yetu. Angalau wangefanya hiyo kazi wakapewa shukurani baadaye.

Hili jipu kama halitatumbuliwa basi itakuwa ni shida sana kupata haki yako hapo Halmashauri ya Kinondoni.
 
Back
Top Bottom