Toka kwa Wananchi: Kero na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea nchini vinavyotakiwa kufuatiliwa

Hadi kiasi cha rushwa wanachopokea kwa siku unajua.

Du!!!, uko vizuri kiuchunguzi.
 

wew kinachokuuma n nini
 
Kabisa hilo inabidi lifanyiwe kazi na wahusika.
 
Kero yangu ni katika barabara itokayo Zakhem Mbagala kwenda Mbagala Kuu ipitayo kibonde maji.

KERO: Kipande cha barabara kinachoanzia kibonde maji hadi Kichemchem hakijawekwa lami ina Mashimo Mashimo makubwa na mengi

MADHARA:-

-Magari yanaharibikaMara kwa Mara
- muda mwingi hupotea sana kukipita na kuvuka kipande hiki cha barabara
- Mvua ikinyesha Gari ndogo hazipiti kirahisi
- Daladala nzim hazipiti eneo hili kwa kuogopa kuharibika kwa hiyo route hii inatambulika kama ya Daladala mbovu.

Hoja zinazosikika mtaani zinasema kipande hiki kilirukwa hii barabara ilipokuwainajengwa lami sababu ya bomba la TAZAMA linalosafirisha mafuta kwenda Zambia.

Najiuliza mara kwa mara, kwamba ina maana hatuna utaalama wowote wa kuhakikisha lami inajengwa eneo hili bila kuathiri miundo mbinu ya Bomba la TAZAMA..!!!

Maana nakumbuka Bomba hili huko mbele limekatisha na kuvuka barabara itokayo Dar kwenda Tunduma..
Je? hapa inashindikana vipi.!



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ebu raisi wetu musimpe mzigo atatuwa kero za wananchi ngapi kwani viongozi wengine wanafanya nini au wanaunga mkono huku wao ni mkono kinywani tu ?
 
Wasalimie
 
Treni ya reli ya Kati DSM hadi mwanza, mabehewa ya second na first class hayatutoshi.
Mabehewa mawili ni machache. CEO TRL Ben Kadogosa tafadhali Kanda ya ziwa tuongezee mabehewa.
 
Ndugu viongozi wa ngazi mbalimbali katika Nchi yetu, nijuavyo mimi ni kwamba, WASALITI,WAHAINI na WAASI hawana nafasi ya kuendelea kuishi katika Nchi husika. Hata Malaika Mbinguni walipoasi tu Mungu aliwatimua,itakuwaje Binanadamu?
 

Hili swala liko kushoto kidogo, is this the official Robot or a hoax? As far as I know JF is already bought by a certain party, kulikoni?
 
Mheshimiwa Waziri wa Nishati, sisi wananchi wa Kijiji cha Ihowanza, Kata ya Ihowanza, Wilaya ya Mufindi, Mkoa wa Iringa, tunaomba utusaidie kutatua kero ya umeme. Umeme umekuwa ukikatika mara kwa mara bila utaratibu. Muda mwingine zinapita hadi Wiki mbili bila umeme kuwepo. Tuna mashaka na Mkandarasi aliyeleta umeme huku kwetu. Tunaomba msaada wako.
 
Ni wanufaika wa vyeo tenda mbalimbali kwenye kampuni zake binafsi na Serikalini hao kutwa kumsifia bila Aibu

April 11, 2020

ZITTO KABWE AICHAMBUA RIPOTI YA CAG 2018/19
Kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo, Mh. Zitto Kabwe (Mbunge Kigoma Mjini), akichambua ripoti ya CAG kwa mwaka 2018-19 na Ripoti za CAG kwa miaka 5 ya serikali ya awamu ya tano .
Hivyo uchambuzi huo unalenga ktk maeneo makubwa kumi muhimu :


Source: Mwanahalisi TV
  1. Kuporomoka kwa makusanyo ya kodi : hivyo serikali kushindwa kukidhi mahitaji ya bajeti na hivyo bajeti kukosa maana inayo kusudiwa ya uwiano wa makusanyo dhidi ya matumizi pia ufanisi wa kukusanya kodi.
  2. Deni la Taifa ktk awamu ya tano ya serikali ya CCM linakuwa kwa kasi kubwa yaani asilimia 12% kuliko kasi ya ukuaji wa uchumi wa nchi ulio ktk wastani wa asilimia. Serikali imeanza kushindwa kulipa madeni ya ndani mfano kulipia Hati Fungani yaani Government Bonds jambo lililo hatari maana yake wananchi na wanunuzi wengine wa hati fungani kukosa imani ya serikali kuweza kulipwa amana zao. Serikali inadaiwa kiwango kikubwa na watoa huduma ikiwemo wakandarasi, makampuni na watu binafsi. Wakala wa Barabara yaani TANROADS ni mdaiwa sugu mwenye deni kubwa yaani Bilioni 900. Serikali pia inaficha kipande cha madeni ya Hifadhi za Jamii yanayofikia trilioni 3 shilingi za kiTanzania na wastaafu kuwa ktk hatihati ya kushindwa kulipwa malipo yao.
  3. Ufisadi umerudi nchini kupitia transit goods kwenda nchi jirani umeongezeka sana kufuatana na taarifa ya CAG. Kiasi cha bilioni 300 ni kimepotea ktk awamu ya 5 huku awamu ya Jakaya Kikwete upotevu ulikuwa bilioni 45 tu.
  4. Kesi dhidi ya serikali yaani contingent liability kimefikia trilioni 1.8 za shilingi za kiTanzania kutokana na kutotii mikataba na wadai kukosa imani ya kulipwa.
  5. Manunuzi yasiyofuata sheria yafikia Shilingi Trilioni moja kwa unapproved suppliers.
  6. Serikali inaendelea kutumia fedha za umma bila kufuata katiba ibara ya 135 yaani kupitia mfuko Mkuu wa serikali yaani Consolidated fund bila idhini ya Controller and Auditor General.
  7. Ukaguzi wa Benki Kuu ya Tanzania umefanywa na GAG bila kutumia kampuni za Ukaguzi za binafsi Dillotte, KPMG n.k hivyo kukosa uwazi na uhuru wa kufanya ukaguzi huru unaoaminiwa na IMF, WORLD BANK na wabia wengine.
  8. Korosho zanunuliwa na fedha kutoka Benki Kuu na fedha hizi hazijarejeshwa Benki Kuu
  9. Ndege kununuliwa bila taratibu za kifedha zilizo wazi.
 
Tunahitaji katiba mpya ambayo hizo sauti zitapewa uzito
 
unyanyasaji wa waendesha pikipiki maarufu kama bodaboda umekithiri sana nchini kote, kila kituo cha polisi utakuta kimejaza pikipiki nje utadhani ni mojawapo ya mapambo ya vituo vya polisi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…