Top Secret: Nyaraka Namba 12333 kutoka Whitehouse

Top Secret: Nyaraka Namba 12333 kutoka Whitehouse

Status
Not open for further replies.
Umemaliza yote Ankal.

Kwanza naomba kudeclare interest kwamba mimi kigezo changu kikuu kwa mwanaume ni akili kubwa i.e mjuzi wa mambo.

Sasa The bold ni mjuzi mpaka kavuka kiwango kile nikitakacho mimi.
Ningeweza vipi kuchomoka kwa huyu kijana jamani?
Hakukuwa na namna kwa kweli,ndio maana nampenda namna hii...
Yessssssss
Nifah is in love,real love.
[emoji4] [emoji4] [emoji4]

Na hakuna bahati kubwa zaidi hapa duniani kama kuwa in love na mwanamke super beautiful alafu kichwani yuko njema..

# MyGirlIsTheBest # Nifah #TheBold's
 
Mkuu ni SAG walienda Iran wakachagua baadhi ya vijana wa Kiiran na kuwatrain..

Lakini kiongozi wa Operations wa SAG (CIA) aliyekuwepo Iran Bw. Donald Wilber alikuwa na kiasi fulani ana asili ya kiarabu (Wilber alikuwa kiongozi wa mission za kijeshi na Kermit Roosevelt alikuwa kiongozi upande wa Utawala (Senior Officer)). Pia Wilber alikuwa na ujuzi mkubwa wa lugha ya kiarabu na tamaduni zao. Hii ilitokana na ubobezi wake katika masuala akiolojia na historia ya kale ya Persia kama nilivyoeleza kwenye makala.

Hata muonekano wa Wilber na uvaaji wake ulikuwa wa kiarabu kabisa. Hii ilimsaidia 'kublend' kiurahisi katika jamii ya Wairan..

Nitapandisha picha yake hapa baada ya dakika kadhaa..
Hapo ndio hua nalikubali jeshi LA USA kwasababu ndani ya USA kuna askari Na watalaamu wenye asili ya nasaba zote duniani.

Wachina.
Wakorea
Wahindi
Waarabu
Wazungu
Waafrica
Ata jamii zingine zote
 
Nimesoma mpaka nimemaliza ndio nacheki na kugundua kuwa ndefu. Hongera sana mkuu kwa mada kali kama hizi. Nimependa pale kwa CIA-wazee wa fitinina duniani.
 
Na mimi uwe unanitag mkuu. Threads kama hizi ndizo zilinifanya niwe member wa kudumu JF sepecially jukwaa hili.
Mkuu kweli unapenda sana jukwaa hili.
Unakumbuka miaka miwili iliyopita mimi nawe tulikuwa hapa kujadili jamaa fulani Ustaadh aliyewapa tabu sana maadui zake kwenye mission zao za kumuua?
Ila alipoingia kwenye mambo ya ulevi na wanawake ndipo walipompata kiulaini kabisa.
Tena tukaenda mbali zaidi kujadili familia yake itakuwaje?
Nakumbuka uliniambia kuwa familia ya gaidi huwa inapotezwa,kuepusha kulipa kisasi baadae.

Natamani sana niuone ule uzi tena.
 
Wakati mwingine ukimya ni jibu zuri sn kwa yule ajionae mwelevu Na kuongea hovyo tu.....

Nimeona hiyo comment Yake huyo jamaa ikanichfua kabisa moyo lkn nikaona nikimjibu nitampa faida..... Bora kukaa kimya maana ukimya ni bora sn....
Kiukweli nimevumilia sana kutokumjibu huyo aliyeleta siasa katika hii thread.

Niliona kabisa tutauchafua huu uzi kwa siasa kama wale wafia dini walivyoumana ktk thread iliyopita.
[emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
nzuri japo fupi.story haijaisha nilipenda nijue ilikuwaje mpaka serikali ya iran iichukie marekani mpaka leo sawa ni kuipindua serikali halali lakini si waliweka mapandikizi yao iweje hayo mapandikizi yasiwe na uhusiano mzuri nao?
huyo waziri mkuu yupo mpaka sasa au alishafariki?kama kafariki kifo chake kilikuwaje ila hii nahisi itakuwa inatoka nje ya mada
 
MIAKA 26 BAADAE


Kwanza ni muhimu kufahamu baada ya Mosaddegh kuondolewa madarakani na Shah kurudishiwa mamlaka yake na Marekani kuanza kuhusika na uchimbaji wa mafuta Iran ikaanza kupata maendeleo ya kasi mno.

Huduma za kijamii zikaboreka sana na vipato vya wananchi vikakua maradufu.

Lakini Shah Mohammad Reza Pahlavi alifanya makosa haya makubwa;

1. Alikataa kuifanya Iran kuwa nchi ya Kiislamu tofauti na matamanio ya wananchi wengi.
Badala yake Shah Pahlavi akawa anaifanya Iran kuwa ya nchi ya kimagharibi zaidi kiutamaduni.

2. Aliishi maisha ya kifahari kupitiliza kiasi wananchi wakaanza kukwazika.

3. Akaingia kwenye mgogoro na Marekani kwa 'kusapoti' mkataba wa nchi za OPEC kuhusu kuongeza bei ya mafuta.

Makosa haya yakazaa yafuatayo;

=> likaanza vugu vugu la kiislamu la kudai Iran kuwa Jamuhuri ya kiislamu na kupinga umagharibi ndani ya Iran.
Vugu vugu hili liliongozwa na waislamu wa madhehebu ya Shia chini ya kiongozi wao Ayatollah Khomeini.

=> Marekani wakatangaza kuwa hawatakuwa bega kwa bega wala kuwauzia silaha nchi zisizo heshimu haki za binadamu.

=> Baada ya wapinzani wa kisiasa wa Shah kugundua uhusiano wa Shah na marekani umedorora nao wakaanzisha vugu vugu la kupinga Iran kutawaliwa na koo moja (Dynasty).

Baada ya mambo hayo kutokea, Shah Pahlavi akishikwa na kitete na kufanya makosa zaidi;

Mfano;

- akaamuru Ayatollah Khomeini akamatwe. Hii ikamlazimu Ayatollah khomeini kukimbia Iran na kwenda kuishi uhamishoni nchini Uingereza.

- Shah akasimamia kuuwawa kwa sumu kwa Mostafa Khomeini, mtoto mkubwa wa kiume wa Ayatollah Khomeini.

- Shah akasimamia pia kuuwawa kwa sumu kwa moja wa wanafalsafa nguli wa nchi hiyo aliyeitwa Ali Shariat ambaye kwa kipindi hicho alikuwa anaandika makala za kufikirisha mno lakini zikimpinga Shah na mawaziri wake.

- Shah akaamuri kuwekwa vizuizini na gerezani kwa wanasiasa wengi wa upinzani.

- Pia Shah akaanzisha mkakati wa kipumbavu kabisa, ambapo kupitia magazeti ya nchi hiyo zikawa zinaandikwa makala za kumkashifu Ayatollah Khomeini kuwa ni kibaraka wa Uingereza anayetumiwa kuivuruga Iran. Hii iliwaudhi wananchi wake ambao walikuwa wanamuheshimu sana Ayatollah na pia liliwaudhi mabwana wakubwa nchi za magharibi kwa kupewa tuhuma mbaya namna hiyo.



Mambo haya yote yakaifanya Iran kuwa katika 'tension' kubwa. Na hatimae mwaka 1977 waislamu wote wa madhehebu Shia nchi nzima wakaanzisha maandamano ya kupinga Shah Pahlavi na uongozi wake.

Mwishoni mwa mwaka huo pia kukatokea mdodororo wa kiuchumi na mfumuko wa bei kutokana na nchi za magharibi kugoma kununua mafuta ya Iran kutokana na kutoridhishwa na muonendo wa uongozi wa Shah Pahlavi.

Hii ikasababisha wafanyakazi wote kugoma nchi nzima na kuingia mitaani kuungana na wananchi wengine kumpinga Shah na uongozi wake.

Maandamano haya yalikuwa ni yale "maandamano yasiyo na kikomo" na yalifanyika nchi nzima.

Shughuli za kiuchumi zote zikasimama. Wananchi wote wako mitaani wanaandamana.
Shah Pahlavi alishindwa kulihusisha jeshi kwasababu alijua fika ingembidi kuuwa wananchi wote na ni wazi kama angeliamuru jeshi kufanya hivyo wangemgeuzia kibao na kumkataa.

Kwahiyo suluhisho aliloliona, mwezi Febeuary 1979 akaondoka kwa siri nchini Iran na kwenda uhamishoni.

Baadae mwezi machi Jeshi likatangaza kutokumuunga mkono Shah.

Taarifa za jeshi kuunga mkono juhudi za wananchi na kwamba Shah Pahlavi amekimbia Iran zikamfikia Ayatollah Khomeini aliyeko uhamishoni Uingereza.

Kwahiyo, mwezi April 1979 Ayatollah Khomeini akarejea Iran na kuchukua Uongozi wa nchi na kuitangaza Iran kuwa ni Jamuhuri ya Kiislamu na yeye Ayatollah akiwa kama "Supreme leader".


Huu ndio ukawa mwanzo wa historia ya Iran hii ya sasa tuliyonayo.

Nikipata wasaa huko mbeleni nitaweka Uzi kueleza kwa kina kuhusu Iran hii ya sasa ilivyanza.


nzuri japo fupi.story haijaisha nilipenda nijue ilikuwaje mpaka serikali ya iran iichukie marekani mpaka leo sawa ni kuipindua serikali halali lakini si waliweka mapandikizi yao iweje hayo mapandikizi yasiwe na uhusiano mzuri nao?
huyo waziri mkuu yupo mpaka sasa au alishafariki?kama kafariki kifo chake kilikuwaje ila hii nahisi itakuwa inatoka nje ya mada
 
Kiukweli nimevumilia sana kutokumjibu huyo aliyeleta siasa katika hii thread.

Niliona kabisa tutauchafua huu uzi kwa siasa kama wale wafia dini walivyoumana ktk thread iliyopita.
[emoji23] [emoji23] [emoji23]
Hahahahaaa

Nifah Na Mimi nilitekwa Na huo ufia dini ktk ule Uzi

[emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji39]
 
The bold mahala Fulani nimeona unasema JPM anajaribu kutuweka muguuni kutoka Kwa hawa jamaa.

Mimi sifikirii kua ni kz rahisi au ataweza kwasababu hawa jamaa sio rahisi kuwatoa hivi hivi. Hii makala kuhusu Iran inaonyesha ni namna gani walitumia kila njia Na mbinu zote kuhakikisha kua maslahi yao hayaharibiki Na yanabaki hapo hapo. Aliye weza ni Mugabe tu lkn Mugabe huyu anakoma Na vikwazo sn.... Utawala wake umekua Wa vikwazo maisha yote. Patrice Lumumba naye ndio hivyo walimmaliza, Laurant Kabila walimmaliza, Na sasa huyu kabila mtoto anawachokoza, genocide ya Rwanda wako nyuma hawa jamaa. King Cobra Michael Sata naye wamemmaliza. Huyu JPM ataweza kweli?

Unaweza kujikumbusha taarifa ya WeakLean ya Tz kutaka kuingia mikataba ya kijeshi Na USA wakati Tz iko Na mkataba Na China kitu kilitaka kuleta mgongano mpk mkuu Wa majeshi akastaafu. So sizani km mkulu ataweza kutuweka miguuni
 
The bold mahala Fulani nimeona unasema JPM anajaribu kutuweka muguuni kutoka Kwa hawa jamaa.

Mimi sifikirii kua ni kz rahisi au ataweza kwasababu hawa jamaa sio rahisi kuwatoa hivi hivi. Hii makala kuhusu Iran inaonyesha ni namna gani walitumia kila njia Na mbinu zote kuhakikisha kua maslahi yao hayaharibiki Na yanabaki hapo hapo. Aliye weza ni Mugabe tu lkn Mugabe huyu anakoma Na vikwazo sn.... Utawala wake umekua Wa vikwazo maisha yote. Patrice Lumumba naye ndio hivyo walimmaliza, Laurant Kabila walimmaliza, Na sasa huyu kabila mtoto anawachokoza, genocide ya Rwanda wako nyuma hawa jamaa. King Cobra Michael Sata naye wamemmaliza. Huyu JPM ataweza kweli?

Unaweza kujikumbusha taarifa ya WeakLean ya Tz kutaka kuingia mikataba ya kijeshi Na USA wakati Tz iko Na mkataba Na China kitu kilitaka kuleta mgongano mpk mkuu Wa majeshi akastaafu. So sizani km mkulu ataweza kutuweka miguuni
Aliyesema hayo ni Sikonge mkuu,sio The bold
 
The bold asante kwa makala nimejifunza mengi........nchi za magharibi hazitaki kuona nchi nyingine zikinufaika na rasilimali zao yaani unatengeneza hesabu za uongo usigawane faida na hali ni mali yake........aliyenacho anazidi kuongezewa............matajiri wanawadhulumu masikini ili waendele kuwa masikini wakisaidiwa na hao vibaraka
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom