MIAKA 26 BAADAE
Kwanza ni muhimu kufahamu baada ya Mosaddegh kuondolewa madarakani na Shah kurudishiwa mamlaka yake na Marekani kuanza kuhusika na uchimbaji wa mafuta Iran ikaanza kupata maendeleo ya kasi mno.
Huduma za kijamii zikaboreka sana na vipato vya wananchi vikakua maradufu.
Lakini Shah Mohammad Reza Pahlavi alifanya makosa haya makubwa;
1. Alikataa kuifanya Iran kuwa nchi ya Kiislamu tofauti na matamanio ya wananchi wengi.
Badala yake Shah Pahlavi akawa anaifanya Iran kuwa ya nchi ya kimagharibi zaidi kiutamaduni.
2. Aliishi maisha ya kifahari kupitiliza kiasi wananchi wakaanza kukwazika.
3. Akaingia kwenye mgogoro na Marekani kwa 'kusapoti' mkataba wa nchi za OPEC kuhusu kuongeza bei ya mafuta.
Makosa haya yakazaa yafuatayo;
=> likaanza vugu vugu la kiislamu la kudai Iran kuwa Jamuhuri ya kiislamu na kupinga umagharibi ndani ya Iran.
Vugu vugu hili liliongozwa na waislamu wa madhehebu ya Shia chini ya kiongozi wao Ayatollah Khomeini.
=> Marekani wakatangaza kuwa hawatakuwa bega kwa bega wala kuwauzia silaha nchi zisizo heshimu haki za binadamu.
=> Baada ya wapinzani wa kisiasa wa Shah kugundua uhusiano wa Shah na marekani umedorora nao wakaanzisha vugu vugu la kupinga Iran kutawaliwa na koo moja (Dynasty).
Baada ya mambo hayo kutokea, Shah Pahlavi akishikwa na kitete na kufanya makosa zaidi;
Mfano;
- akaamuru Ayatollah Khomeini akamatwe. Hii ikamlazimu Ayatollah khomeini kukimbia Iran na kwenda kuishi uhamishoni nchini Uingereza.
- Shah akasimamia kuuwawa kwa sumu kwa Mostafa Khomeini, mtoto mkubwa wa kiume wa Ayatollah Khomeini.
- Shah akasimamia pia kuuwawa kwa sumu kwa moja wa wanafalsafa nguli wa nchi hiyo aliyeitwa Ali Shariat ambaye kwa kipindi hicho alikuwa anaandika makala za kufikirisha mno lakini zikimpinga Shah na mawaziri wake.
- Shah akaamuri kuwekwa vizuizini na gerezani kwa wanasiasa wengi wa upinzani.
- Pia Shah akaanzisha mkakati wa kipumbavu kabisa, ambapo kupitia magazeti ya nchi hiyo zikawa zinaandikwa makala za kumkashifu Ayatollah Khomeini kuwa ni kibaraka wa Uingereza anayetumiwa kuivuruga Iran. Hii iliwaudhi wananchi wake ambao walikuwa wanamuheshimu sana Ayatollah na pia liliwaudhi mabwana wakubwa nchi za magharibi kwa kupewa tuhuma mbaya namna hiyo.
Mambo haya yote yakaifanya Iran kuwa katika 'tension' kubwa. Na hatimae mwaka 1977 waislamu wote wa madhehebu Shia nchi nzima wakaanzisha maandamano ya kupinga Shah Pahlavi na uongozi wake.
Mwishoni mwa mwaka huo pia kukatokea mdodororo wa kiuchumi na mfumuko wa bei kutokana na nchi za magharibi kugoma kununua mafuta ya Iran kutokana na kutoridhishwa na muonendo wa uongozi wa Shah Pahlavi.
Hii ikasababisha wafanyakazi wote kugoma nchi nzima na kuingia mitaani kuungana na wananchi wengine kumpinga Shah na uongozi wake.
Maandamano haya yalikuwa ni yale "maandamano yasiyo na kikomo" na yalifanyika nchi nzima.
Shughuli za kiuchumi zote zikasimama. Wananchi wote wako mitaani wanaandamana.
Shah Pahlavi alishindwa kulihusisha jeshi kwasababu alijua fika ingembidi kuuwa wananchi wote na ni wazi kama angeliamuru jeshi kufanya hivyo wangemgeuzia kibao na kumkataa.
Kwahiyo suluhisho aliloliona, mwezi Febeuary 1979 akaondoka kwa siri nchini Iran na kwenda uhamishoni.
Baadae mwezi machi Jeshi likatangaza kutokumuunga mkono Shah.
Taarifa za jeshi kuunga mkono juhudi za wananchi na kwamba Shah Pahlavi amekimbia Iran zikamfikia Ayatollah Khomeini aliyeko uhamishoni Uingereza.
Kwahiyo, mwezi April 1979 Ayatollah Khomeini akarejea Iran na kuchukua Uongozi wa nchi na kuitangaza Iran kuwa ni Jamuhuri ya Kiislamu na yeye Ayatollah akiwa kama "Supreme leader".
Huu ndio ukawa mwanzo wa historia ya Iran hii ya sasa tuliyonayo.
Nikipata wasaa huko mbeleni nitaweka Uzi kueleza kwa kina kuhusu Iran hii ya sasa ilivyanza.
nzuri japo fupi.story haijaisha nilipenda nijue ilikuwaje mpaka serikali ya iran iichukie marekani mpaka leo sawa ni kuipindua serikali halali lakini si waliweka mapandikizi yao iweje hayo mapandikizi yasiwe na uhusiano mzuri nao?
huyo waziri mkuu yupo mpaka sasa au alishafariki?kama kafariki kifo chake kilikuwaje ila hii nahisi itakuwa inatoka nje ya mada