Top Secret: Nyaraka Namba 12333 kutoka Whitehouse

Top Secret: Nyaraka Namba 12333 kutoka Whitehouse

Status
Not open for further replies.
Hahahah! Movie za james bond zina details nyingi sana pamoja na 'chumvi'..

MI6 na MI5 bado sijawahi kusikia kuweka hadharani mafaili ya siri nzito kuhusu shughulo zao ingawa siku za karibuni nimeona wameanza kuweka utaratibu wa kuwa na Kumbukumbu za Usalama wa Taifa (National Security Archives) lakini kadiri nilivyoangalia sijaona yale mambo mazito mazito yanayotia hamasa watu kufuatilia.

Nadhani hii pia inachangiwa na raia wa Uingereza kutokupenda "kudeka" sana kwa serikali yao. Unajua kingine kinachowaponza CIA na serikali ya marekank ni vile raia wake wanapenda sana "kudeka" ile kujifanya wanasimamia haki zao hata kama wanahatarisha siri za nchi. Ndio sababu hata ya kutungwa kwa "Freedom of Information Acy" ili kumaliza malalamiko ya wamarekanj kuhusu "haki" yao ya kujua "mwenendo" wa nchi yao..

Ila huko mbele tutegemee kuanza kuvuja au kuwekwa hadharani kisheria mafaili yahusuyo shughuli za MI6 na MI5.
Umedadavuwa vyema ukipata muda itapendeza ukituandalia makala ya Korea peninsula hasa ukiweza kuireview series ya Iris, hii series inaakisi mgogoro mzima wa Korea peninsula na unseen power na power within.

Ukiwatazama watu kama Baek san jinsi wanavyoweza kuigiza kiumahiri sasa vipi wakiwa kikazi kwenye reality?

Hili ni ombi maalum naomba uiliview IRIS na ukizingatia mtoa ombi ndio Ankal wa Nifah basi hili ni moja ya sharti katika mahari ya huyu Ankal wangu Nifah.
 
Umedadavuwa vyema ukipata muda itapendeza ukituandalia makala ya Korea peninsula hasa ukiweza kuireview series ya Iris, hii series inaakisi mgogoro mzima wa Korea peninsula na unseen power na power within.

Ukiwatazama watu kama Baek san jinsi wanavyoweza kuigiza kiumahiri sasa vipi wakiwa kikazi kwenye reality?

Hili ni ombi maalum naomba uiliview IRIS na ukizingatia mtoa ombi ndio Ankal wa Nifah basi hili ni moja ya sharti katika mahari ya huyu Ankal wangu Nifah.
Hilo sharti Ankali lazima litimizwe maana ma"ankali" wanakuwa wanoko kwa wapwa zao.The Bold tekeleza sharti la ankali wa Nifah ama sivyo ankali anaweza chukua maamuzi magumu.
 
Hilo sharti Ankali lazima litimizwe maana ma"ankali" wanakuwa wanoko kwa wapwa zao.The Bold tekeleza sharti la ankali wa Nifah ama sivyo ankali anaweza chukua maamuzi magumu.
Kabisa, bila sharti hili kutimizwa maamuzi magumu ni lazima, mjomba ndio kaka'ke Mama, bado nakumbuka pesa za visheti zilivyokuwa zinanitoka leo huwezi kujitwalia mrembo huyu kirahisirahisi tyuu.
 
Umedadavuwa vyema ukipata muda itapendeza ukituandalia makala ya Korea peninsula hasa ukiweza kuireview series ya Iris, hii series inaakisi mgogoro mzima wa Korea peninsula na unseen power na power within.

Ukiwatazama watu kama Baek san jinsi wanavyoweza kuigiza kiumahiri sasa vipi wakiwa kikazi kwenye reality?

Hili ni ombi maalum naomba uiliview IRIS na ukizingatia mtoa ombi ndio Ankal wa Nifah basi hili ni moja ya sharti katika mahari ya huyu Ankal wangu Nifah.
Hahahahaha!! Daaaaahh Ankal kwa sharti hilo naanza leo hii kulifanyia kazi ombi lako.. Maana sitaweza kuhimili kumkosa huyu mtoto Nifah..

Na mmejitahidi sana kumlea huyu binti aisee! Hongera Ankal na sista wako..

Nakifanyia kazi ombi ASAP! [emoji1]
 
Hilo sharti Ankali lazima litimizwe maana ma"ankali" wanakuwa wanoko kwa wapwa zao.The Bold tekeleza sharti la ankali wa Nifah ama sivyo ankali anaweza chukua maamuzi magumu.
Mkuu hapo Ankal ameniweza walahi kuniwekea hilo sharti! Hahhahahah

Lazima nifanyie kazi hilo ombi aisee, nisije kumkosa mwali wao [emoji1] [emoji1]
 
Naam,nimemaliza sasa kuisoma makala hii ya aina yake.
Nami ngoja nihighlight sehemu zilizonivutia.

SAD
Hiki kitengo kimenitisha!Nimependa fitna zao,hakika wako vizuri sana.
Hasa tukio la kumng'oa madarakani Mohammed Mosaddegh limenisisimua sio kidogo.
Aling'olewa kitaalam kwelikweli.

Ila katika matukio yaliyonisisimua zaidi ktk kitengo hiki ni waliposhindwa kumng'oa madarakani Mzee mzima The Late Fidel Castro.

Tukio jingine lililoniacha na maswali lukuki ni mbinu gani waliitumia kumvusha Dalai Lama mpakani mwa China na kumpeleka India?
Nimetamani sana kujua walitumia mbinu gani.(Sadly umesema hakuna anayejua walitumia mbinu gani hadi leo hii)
Bila shaka ilikuwa mbinu hatari na wanaitumia hadi leo ndio maana hawajaianika kama hizi nyingine.

Katika matukio yaliyonichekesha sana ni matamanio ya Shah ya kwenda ulaya.
Mzee kagawa visima vya mafuta kisa tu akaoshe macho Hahahaaaaa

Yote kwa yote nimemkubali sana Mohammad Mosaddegh kwa harakati zake hadi aliposhinda.

Mwisho nina swali na ombi,nisijekuandika sana mwisho ikageuka makala ndani ya makala...lol

SWALI
Nimeona mwisho wa makala hii Waingereza walishinda 'vita' dhidi ya Mohammad Mosaddegh ambaye alikuwa kawabana mbavu katika dili la mafuta.
Na kiongozi aliyefuata alikuwa kibaraka wao aliyekuwa anafuata kila wamuambialo.
Je,Iran waliweza vipi kujikwamua kutoka katika utumwa huu dhidi ya Uingereza?
Ni nani aliyeongoza mapambano hayo ya kurejesha visima vyao vya mafuta?
Je alitumia mbinu gani?

OMBI
Naomba utuandikie makala kuhusu 'Simba aliyeshindikanika' Hayati Fidel Castro.
Nasikia huyu ndiye kiboko ya CIA.
Kama kumbukumbu zangu ziko sahihi ni kwamba wamewahi kumuwekea mitego mikali ya kumuua 21 lakini aliikwepa yote.
Hiyo mitego ilikuwaje? Aliikwepa vipi?
Naamini kupitia wewe nitakata kiu yangu ya kumfahamu Shujaa Fidel Castro kwa undani.

Asante kwa makala nzuri yenye mtiririko wa kusisimua,lugha na misemo ya lugha yetu adhimu ya kiswahili ni kivutio kingine katika makala zako.

Am proud of you my sweet darling
#TheBoldIsMine#
Hongera THE BOLD

Mkitaka kujua huyu jamaa yukoje kichwani angalieni jina lake, limesadifu yaliyomo na yasiyomo pia.

Nchi kama hii ya kwetu na huu utajiri tuliokuwa nao hawa jamaa hawachezi mbali kabisa hasa kutokana na uwepo wa jamaa wa wawili, china na russia katika maeneo nyeti ya gas na uranium.

Tatizo niuwezo wetu wakutambua japo viashiria vya mission nzito kama hizi bado upo chini mno, ndio hitajio lakuwa na vijana/ wazee kama THE BOLD linapokuja japo kuweza kubashiri hata kwa mbali kuwa kwa mwenendo huu hapa hatuko salama tuwe makini kidogo.

Hawatakiwi watu wanaowaza kesho nistaafu nipewe usemaji wa chama au ukuu w mkoa hapana, vinatakiwa vichwa makini sana na vinavyoweza kuunganisha dots za matikio mbalimbali na kupata mwanga kuwa inawezekana tusiwe salama.

Nchi ambazo nimeepukana na nakama za hawa jamaa au kupunguza kasi za hawa washkaji ni chache sana na nyingi hazipo Africa. Uroho wa madaraka na umasikini wakulazimishwa ni silaha nzito zinazoipiga Africa yetu na kuwafanya hawa watu wasiwe na mipango mikubws sana kwetu,

Vidume vichache sana Africa vilijaribu kuwatingisha wazungu na mwisho wao waliuliwa, Gaddafi ndie aliyekuwa na uchu hasa yakuwasomesha namba wazungu ila ndo hivyo tena walimkata koo.

Unaweza kubashiri pia lile vuguvugu la ubinafsishaji nanuuzwaji hovyo wa mali za umma na mashirika yake na kifo cha baba wa taifa hili.... Uwezekano wakumuwaisha mchonga ni mkubwa ili watu wajifanyie yao, haya yalishasemwa na ukiunga na hizi nondo za THE BOLD kitu imekolea
 
Dunia INA siri nyingi... Dah ila hawa wamarekani Mungu anawaona ..Asante Sana mkuu The Bold kwa Chakula cha Ubongo..
 
Hongera THE BOLD

Mkitaka kujua huyu jamaa yukoje kichwani angalieni jina lake, limesadifu yaliyomo na yasiyomo pia.

Nchi kama hii ya kwetu na huu utajiri tuliokuwa nao hawa jamaa hawachezi mbali kabisa hasa kutokana na uwepo wa jamaa wa wawili, china na russia katika maeneo nyeti ya gas na uranium.

Tatizo niuwezo wetu wakutambua japo viashiria vya mission nzito kama hizi bado upo chini mno, ndio hitajio lakuwa na vijana/ wazee kama THE BOLD linapokuja japo kuweza kubashiri hata kwa mbali kuwa kwa mwenendo huu hapa hatuko salama tuwe makini kidogo.

Hawatakiwi watu wanaowaza kesho nistaafu nipewe usemaji wa chama au ukuu w mkoa hapana, vinatakiwa vichwa makini sana na vinavyoweza kuunganisha dots za matikio mbalimbali na kupata mwanga kuwa inawezekana tusiwe salama.

Nchi ambazo nimeepukana na nakama za hawa jamaa au kupunguza kasi za hawa washkaji ni chache sana na nyingi hazipo Africa. Uroho wa madaraka na umasikini wakulazimishwa ni silaha nzito zinazoipiga Africa yetu na kuwafanya hawa watu wasiwe na mipango mikubws sana kwetu,

Vidume vichache sana Africa vilijaribu kuwatingisha wazungu na mwisho wao waliuliwa, Gaddafi ndie aliyekuwa na uchu hasa yakuwasomesha namba wazungu ila ndo hivyo tena walimkata koo.

Unaweza kubashiri pia lile vuguvugu la ubinafsishaji nanuuzwaji hovyo wa mali za umma na mashirika yake na kifo cha baba wa taifa hili.... Uwezekano wakumuwaisha mchonga ni mkubwa ili watu wajifanyie yao, haya yalishasemwa na ukiunga na hizi nondo za THE BOLD kitu imekolea

Mkuu umemaliza kila kitu,ila kubwa zaidi ya yote aya yako ya mwisho imenifumbua sana.

Wakati nasoma hii makala sikufikiria hilo, ila kwa tafakuri yako hii imenifanya nami nikaunga dot.
Dah ama kweli palipo na wengi kuna mengi.

Kuhusu The bold naungana nawe,Tanzania tunahitaji vijana wa aina yake.
Huyu mtu ana akili sana kiasi natamani akili hizi zitumike kwa manufaa ya Taifa na sio kuishia katika maandiko yake tata na ya kufikirisha.
 
Hahahahaha!! Daaaaahh Ankal kwa sharti hilo naanza leo hii kulifanyia kazi ombi lako.. Maana sitaweza kuhimili kumkosa huyu mtoto Nifah..

Na mmejitahidi sana kumlea huyu binti aisee! Hongera Ankal na sista wako..

Nakifanyia kazi ombi ASAP! [emoji1]

[emoji23] [emoji23] [emoji23] Ankal kakomaa...
Haya fanya baba umtimizie ombi lake asijeleta balaa.
Si unajua ni-hoi kwako?
Nami sitaweza kuhimili kukukosa.

So timiza ombi la Ankal for US.
 
Ume claim hati miliki.

Sijui kama unaweza kubeba simulizi la mtu mwingine, James Angleton, la matukio ya zaidi ya miaka 40 iliyopita, yaliyowekwa kwenye public records za national archives na kudai ni ya kwako.

Kwa nini, kwa sababu, awali ya yote, ndani ya simulizi hukuonyesha hukutofautisha kwa citation kipi umebeba cha mwenzio na kipi cha kwako, kama kipo.

Swali: Nini hapo umekibuni wewe, umeongeza ya kwako ya kichwani, kiasi cha kukupa hati miliki ya ubunifu juu ya simulizi hili?
Hilo tu ndo umeliona???hayo magazeti yanabeba mawazo yetu humu na hata haya tu aknowledge,this is not an academic work,hapa ni baraza tunapeana stori kama kule kitaa
 
Unastahiki pongezi mkuu, The bold.
Umesababisha nitazame tena historia ya taifa la Iran.
Toka kusimama kwa dola ya (SAFAVID EMPIRE 1502-1785 A.D) kuanzia kwa watawala wao kina;

1. Shah Ismail Al Haadi As Safavi huyu alitawala kwa miaka 22 kuanzia mwaka 1502-1524 A.D katika vioja na viroja vya bwana huyu aliwaamrisha wafuasi wake wamsujudie na wakafanya hivyo ni watu wa jamii ya [Kizilbas] hili ni kabila lenye nguvu nchini Iran, asili yao ni Uturuki ni muunganiko wa makabila 9, na walikuwa askari watiifu kwa dola ya Safavi.



2. Shah Tahmasp huyu alitawala baada ya kifo cha baba yake kwa miaka 52 kuanzia mwaka 1524-1576 A.D

3. Shah Ismail wa pili huyu alitawala kwa muda mfupi tu mwaka 1 tu kuanzia 1576-1577 A.D, wafuasi wake walimuekea sumu baada ya kumuona amebadilika katika msimamo wa mambo ya dini

4. Shah Mohammed Khodabandeh huyu alitawala kwa kipindi cha miaka 10 kuanzia mwaka 1577-1587 A.D

5. Shah Abbas maarufu kama; The Great huyu alitawala kwa miaka 42 kuanzia mwaka 1587-1629 A.D

6. Shah Safi wa kwanza huyu alikuwa ni mjukuu wa Shah Abbas ambaye alifahamika kama The Great naye huyu mjukuu wa The Great alitawala kwa muda wa miaka 13, kuanzia mwaka 1629-1642 A.D

7. Shah Abbas wa pili huyu alitawala kwa muda wa miaka 25 kuanzia 1642-1667 A.D

8. Shah Suleiman Safi wa pili huyu alitawala kwa miaka 27 kuanzia mwaka 1667-1694 A.D

9. Shah Sultan Hussein huyu alitawala kwa muda wa miaka 28 kuanzia mwaka 1694-1722 A.D

10. Shah Tahmasp wa pili huyu alitawala kwa miaka 10 kuanzia mwaka 1722-1732 A.D

11. Shah Abbas wa tatu huyu alitawala kwa miaka 4 tu kuanzia 1732-1736 A.D.

Kama ilivyo ada ya watawala basi yalipita matukio makubwa makubwa ya kutisha na ya uvamizi vituko na vitakuro vingi vilitokea kwa mfano uvamizi wa mji wa Tabriz ambao kwa sasa ni makao makuu ya Mkoa wa Azerbaijan ya mashariki nchini Iran na ni mji wa nne kwa ukubwa nchini Iran baada ya Tehran, Mashhad na Isfahan na uvamizi pia katika mji wa Shirvan huu ni mji uliopo Mkoa wa Khorasan nchini Iran pia mji huu unaitwa [Sharvan, Shirwan, Shervan, Sherwan na Servan. Basi zikapita nyingi dahari, miaka kwa mikaka ndio wakaja hawa wanamapinduzi kina Khomein.
 
Katika matukio yaliyonichekesha sana ni matamanio ya Shah ya kwenda ulaya.
Mzee kagawa visima vya mafuta kisa tu akaoshe macho Hahahaaaaa

Mkuu,

Haya ndio yaliyotokea huku kwetu pia. Wakoloni walitumia "udhaifu wa matamanio" ya wazee katika kufanikisha "mipango yao ovu" dhidi yetu.

Kaka ...
 
Hilo tu ndo umeliona???hayo magazeti yanabeba mawazo yetu humu na hata haya tu aknowledge,this is not an academic work,hapa ni baraza tunapeana stori kama kule kitaa
Kaka ile ishu ya jana uliyonistua kwenye fb nimekutumia ujumbe, tafadhali njoo kwa email tuongee au nibip nikutwangie unipe mwanga kidogo ''kaka fursa hiyo usiiache''
 
Hilo tu ndo umeliona???hayo magazeti yanabeba mawazo yetu humu na hata haya tu aknowledge,this is not an academic work,hapa ni baraza tunapeana stori kama kule kitaa

Sasa kama sio academic work bali ni stori tu kama za kitaa kwa nini mnamaindi wadau wakisambaziana story? Kwamba isitumike bila ruhusa, yeye mwenyewe kapakua bure sehemu... hana haki miliki
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom