Tottenham Hotspurs Thread

Tottenham Hotspurs Thread

Hili thread imekuwa tamu sana japo timu haifanyi vizuri. Mijadala inaenda deep. Ni hoja juu ya hoja.

Pongezi kwa wajumbe wote kwa kifikisha post 2000.

Labda sasa mods wataanza kufikiria kutupa heshima tunayostahili watuweke pale juu kwenye sticky threads.

Au watasubiri mpake tuchukue vikombe vyetu tulivyokatia hakimiliki msimu huu: Europa na Karaghabaho!

#COYS
Hahaa,, kwenye vikombe hapo... Sijui tufanyeje, lkn navyoona timu y mourinho naishiwaga nguvu kabisa! Uliona sanchez alivyokua anamkaba gundogan..[emoji2960]
Kama kweli mourinho anataka vikombe hvyo,, aanze kubadili game approach sasa, na kujua kwenye defence anaenda na wapi ambao nao tunatak tuone, consistency zao kwa hizi game zilozopo.

Sent from my Nokia 2.2 using JamiiForums mobile app
 
Kuna vitu viwili ambavyo ni muhimu sana kueleweka kuhusu SPURS.
1. Usajili na better scouting.
Naomba tukumbuke, ni lini spurs iliweza kusajili wachezaji wazuri. Wote tutakubaliana nami kwamba ni kipindi kabla Gareth Bale hajauzwa. Maake hela ya Bale pale tulibahatika tu kupata Eriksen wengine wote viwango vya kawaida mno(including Lamela). Miongon mwa wachezaji ambao waliletwa tangu hapo n pamoja na Roberto Soldado, Chiliches, hotberg, David sanchez, (ambao wote walikua ni typical Flopy players) atleast (Lamela, chadli, wanyama, ) wakali ni Son
#Kuna chief scouting nakumbuka alifukuzwa ambaye alikua fundi, na nakumbuka aliletaga watu kama (Dele Ali, Toby, Jan, n.k)#
Ili team ifanye vizur ni muhimu sana kuwa na sajili zenye manufaa, kuna kipindi hapo tumekwama sana kwenye hili

2. Game tactics.
Game tactics ya mourinho ni Defensing,,
KWANINI MBINU HIZO HIZO ZA KUJILINDA ALIFANIKIWA NAZO, CHELSEA NA TEAM ZINGINE HUKO NYUMA LKN SIO MAN U, SPURS NA MADRID??
1, Aina ya wachezaji aliokua nao. Huwezi ukafanikiwa na hii mbinu kama hauna wachezaji wazuri kwenye ulinzi na kufanya mashambulizi ya kushitukiza. Je, kwa spurs ya sasa anamlinzi gn anayeweza akalinda kweli?? (Kama kipind yuko na akina John Telly, Essein, Obi, na Cole pale chelsea) wakati huo huo ana team yenye washambuliaji makini pia, wakifika golini ni Goli,,.
2. Huwezi ukalinda,, kwa kila muda kukaba tu,, the whole team.
Wachezaji wanatumia nguvu nyingi sana, wanachoka,, huku wasipate matokeo mazuri.
Mpira wa sasa, ili ujilinde ni lazima either uwe unashambulia, au umiliki mpira. Vinginevyo ndo hizo individual errors zisizo koma na sasa technologia tukiwa na VAR.

NINI KIFANYIKE.
Kuna haja kubwa sana ya, kuwa na
1.scouting team nzuri.. sio kuleta wachezaji hata hawana msaada kwenye team,, eti kisa wana uzoefu au ni bei nafuu.
Kumbuka: msimu mwakajuzi tuliofika nusu fainali UEFA hatukisajili lkn team wachezaji wengi walikua wako kwenye peak nzuri. Na angepatikana mmoja tu (Dyabala)kama wataalamu wanavyosema,, labda tungebebaga ile ndoo.
2. Kocha anaye endana na mpira wa sasa.
Mourinho kwa sasa,, kaishiwa mbinu team zishamjua na hanaga mbinu nyingind yeyote ya ziada.
Better tukapata kocho mwingine,, ataye ruhusu team ifanye plessing kama spurs iliyozoeleka machon pa watu.
As currently neither we enjoy playing footbal or Results.
3. Scoud update,,
Team ili ifanye vzr lazima tubadili kikosi mara kw mara.

MAONO YANGU NI HAYO.

Sent from my Nokia 2.2 using JamiiForums mobile app
Nachoelewa Mafanikio ya kocha ni vikombe alivyovipata katika timu husika.
Uyu mwamba katika msimu wake wa kwanza united aliwapa vikombe vitatu Europa,,,Carabao cup na ile ngap ya jamii. Akiwa real madrid nako aliwapa vikombe vitatu kikiwemo LaLiga Santander title kwa pointi 100 na magoli 121.
KWA iyo uyu jamaa kote alikopita hakuna ambapo hajafanikiwa Mana kuna makocha timu zao zinapiga pasi 900 katika mechi ola kwenye kabati hakuna kombe hata moja.
Hakuna mpira mzuri husiokuwa na kombe.
 
Hahaa,, kwenye vikombe hapo... Sijui tufanyeje, lkn navyoona timu y mourinho naishiwaga nguvu kabisa! Uliona sanchez alivyokua anamkaba gundogan..[emoji2960]
Kama kweli mourinho anataka vikombe hvyo,, aanze kubadili game approach sasa, na kujua kwenye defence anaenda na wapi ambao nao tunatak tuone, consistency zao kwa hizi game zilozopo.

Sent from my Nokia 2.2 using JamiiForums mobile app
Nilipenda sana namna D Sanchez alivyojaribu kumkaba Gundogan. Alizidiwa uwezo ila alionesha determination ya hali ya juu sana. Hicho ni kitu nakipenda kutoka kwa Jose; kumfanya mchezaji anayejitambua kucheza to the fullest bila kujalisha level ya kiwango chake. Mchezaji anajituma kama yuko vitani vile.

Ila namshauri Levy ampe Mourinho anachotaka dirisha lijalo. Aache mambo ya kutafuta cheap bargains kwenye zama hizi za soka. Kwa defense hii ya Spurs naamini angekuwa kocha mwingine hasa hao wanaocheza attacking football, timu ingekuwa inasubiri kuona ratiba ya mechi zake za Championship msimu ujao.

Imagine mechi kama ile ya City tungekuwa na kocha kama Bielsa wa Leeds ambaye angetaka kushambulia tu. Ndiyo zile mechi City anashindaga goli 9.
 
Nilipenda sana namna D Sanchez alivyojaribu kumkaba Gundogan. Alizidiwa uwezo ila alionesha determination ya hali ya juu sana. Hicho ni kitu nakipenda kutoka kwa Jose; kumfanya mchezaji anayejitambua kucheza to the fullest bila kujalisha level ya kiwango chake. Mchezaji anajituma kama yuko vitani vile.

Ila namshauri Levy ampe Mourinho anachotaka dirisha lijalo. Aache mambo ya kutafuta cheap bargains kwenye zama hizi za soka. Kwa defense hii ya Spurs naamini angekuwa kocha mwingine hasa hao wanaocheza attacking football, timu ingekuwa inasubiri kuona ratiba ya mechi zake za Championship msimu ujao.

Imagine mechi kama ile ya City tungekuwa na kocha kama Bielsa wa Leeds ambaye angetaka kushambulia tu. Ndiyo zile mechi City anashindaga goli 9.
Kiukweli sikufurahia Mou kuja kuifundisha Spurs, Mourinho ni winner by nature, ukimletea wachezaji anaowataka andaa kabati la kujaza vikombe.
Levy ana deals ngumu na za ubahili, timu haina uwezo wa kupigania mchezaji yoyote mkubwa. Hivyo hii timu kushinda kombe ni kocha atumie akili zote kichwani ndio atoboe, kutokana na hilo mafanikio yake ni amsha amsha tu uwanjani ili ifaulu UEFA, hakuna cha zaidi.
Mpaka sasa unasikia club kama Chelsea, Man au Liver tayari wanafuatilia kwa ukaribu wachezaji wa msimu ujao( tena zile big guns kwa Ulaya.
Levy kanunua wachezaji wa mafungu na wengine kwa mkopo(tena wakiwa wameflop kwenye timu zao) kakaa kakunja nne anataka kunyanyua kwapa kwa kuchukua makombe. Hii biashara huenda isilipe.
 
#COYS

Leo tumewapiga hawa wakulima Wolfsberger FC.

FT: 1 - 4

Kizuri ni kuwa Bale, Dele Alli, Lamela, Moura, Winks, Vinicious na flops wengine wameosha nyota leo kwa magoli na assists.

Pia tuliua mchezo kipindi cha kwanza hivyo kutoa nafasi kwa Sonny kupumzishwa. Ikumbukwe kwamba Sonny alikimbia km zaidi ya 28 kwa kila mechi, dhidi ya Everton na dhidi ya City. Hivyo ilikuwa muhimu leo acheze dk chache tu. Mwenzake Kane kapumzika mapema mara tu baada ya game ya City. Kapewa off duty siku hizi mbili tatu.

Kibaya ni kwamba bila wachezaji wetu kufungisha mechi haijaisha. Sissoko kamwangusha mtu kwenye box wakapata goli.

Siyo mbaya. Next stop Jumapili vs Burnley. Mechi yetu ya marudiano Europa itakuwa Jumatano badala ya Alhamisi. Sijui kwa nini.

#COYS
 
#COYS

Leo tumewapiga hawa wakulima Wolfsberger FC.

FT: 1 - 4

Kizuri ni kuwa Bale, Dele Alli, Lamela, Moura, Winks, Vinicious na flops wengine wameosha nyota leo kwa magoli na assists.

Pia tuliua mchezo kipindi cha kwanza hivyo kutoa nafasi kwa Sonny kupumzishwa. Ikumbukwe kwamba Sonny alikimbia km zaidi ya 28 kwa kila mechi, dhidi ya Everton na dhidi ya City. Hivyo ilikuwa muhimu leo acheze dk chache tu. Mwenzake Kane kapumzika mapema mara tu baada ya game ya City. Kapewa off duty siku hizi mbili tatu.

Kibaya ni kwamba bila wachezaji wetu kufungisha mechi haijaisha. Sissoko kamwangusha mtu kwenye box wakapata goli.

Siyo mbaya. Next stop Jumapili vs Burnley. Mechi yetu ya marudiano Europa itakuwa Jumatano badala ya Alhamisi. Sijui kwa nini.

#COYS
Jumapili ni Tottenham vs Westham, Burnley ndio game ya ligi itafuta baada ya hiyo ya Jumapili. Kwa game hizi naamini Mou atapata matokeo.
 




Bale is getting back people. Kwa hii display ya game iliyopita huenda leo akaanza. Ni aibu kuwa na tatizo la RW wakati tunaye Bale kikosini. Aoneshe ukomavu wake kwa kushusha performance nzuri match in match out.

My prediction vs West Ham; 4 2 3 1

Hugo, Doherty, Davies, Dier, Toby, Hojbjerg, Sissoko, Son, Ndombele, Bale, Kane.
 
Leo ni pointi 3 bila maelezo.
Screenshot_20210221-145053.jpg
 
Watetezi wa Mourinho mko wapi tajiri anajiandaa kumtimua huyo kinyago wenu na kumchukua Brendon Rodgers wa Leicester City
 
Respect mkuu. Mimi naomba nijaribu kujibu swali lako kuhusu Leicester. Nitakutajia nafasi mbili tu. Hizo nyingine ukafuatilie wewe mwenyewe ili usije kusema namtetea sana Jose.

Kwenye RB

Leicester wana Pereira na Timothy Castign. Spurs tuna Matt Doherty na Serge Aurier.
Kama unajua mpira utaona ipi iko vizuri zaidi.

Kwenye namba 10 (CAM)

Sisi tuna Dele Alli na Le Celso (pancha). Leicester wanaye Madisson. Again kama unajua mpira utaona nani ana advantage.

Pia ujue kwamba kuwa na mchanganiko wa nyota kadhaa na magarassa kadhaa kwenye first eleven kama Spurs kunaifanya kuwa na kikosi dhaifu kuliko timu yenye wachezaji average lakini hawana garassa hata moja.

Kama unadhani Lamela au Moura kwenye RW wana ubora kuliko Gray basi ujue nakutakia mafanikio katika maombi yako ya kutaka Jose afukuzwe. Ila ujue Levy ni genius na anajua Mourinho atampa nini.
Levy kasema anasubili msimu uishe afanye maamuzi ya kumtimua au hapana.Leo tena West Ham wamejinyolea mwendawazimu
 
Ukiangalia hata mechi tulizopoteza, Mou anaingia na approach sahihi ila makosa binafsi ndio yanaicost team. Lakini hata hivyo, Tott karibia kamaliza zile fixtures ngumu zote. Naamini game zijazo timu itatulia na vita ya top four itaanza upya. Ila msimu ujao beki na ushambuliaji ni lazima vifanyiwe kazi ili kupata timu ya mashindano.
Mtafutieni Mou timu ya kufundisha spurs anachukua kocha mwingine la sivyo anarudi kucheza na dog wake home
 
Mtafutieni Mou timu ya kufundisha spurs anachukua kocha mwingine la sivyo anarudi kucheza na dog wake home
yaani nawaambia kila leo na sitaacha kuwaambia kwa mpira wa kisasa Mou kaishiwa hana tena jipya makocha wengi wameshamjulia yani akijilinda anapigwa,akifunguka anapigwa hajui hata afanyeje.bado yule mwenzake wa LA LIGA kashaanza kudondosha point akikutwa na kupitwa wala sitashangaa maana wote wana mipira ya hovyohovyo tu.......NB. furaha yangu ni kuona Mourinho anafungwa kila leo.
 
yaani nawaambia kila leo na sitaacha kuwaambia kwa mpira wa kisasa Mou kaishiwa hana tena jipya makocha wengi wameshamjulia yani akijilinda anapigwa,akifunguka anapigwa hajui hata afanyeje.bado yule mwenzake wa LA LIGA kashaanza kudondosha point akikutwa na kupitwa wala sitashangaa maana wote wana mipira ya hovyohovyo tu.......NB. furaha yangu ni kuona Mourinho anafungwa kila leo.
Ivi mpira wa kisasa upoje tuelewashane kwanza hapo?
Afu timu ngapi zinacheza mpira wa kisasa zitaje?
 
yaani nawaambia kila leo na sitaacha kuwaambia kwa mpira wa kisasa Mou kaishiwa hana tena jipya makocha wengi wameshamjulia yani akijilinda anapigwa,akifunguka anapigwa hajui hata afanyeje.bado yule mwenzake wa LA LIGA kashaanza kudondosha point akikutwa na kupitwa wala sitashangaa maana wote wana mipira ya hovyohovyo tu.......NB. furaha yangu ni kuona Mourinho anafungwa kila leo.
Furaha yako itakamilika mwishoni mwa msimu. Pale Mourinho atakapokuwa na kikombe (Europa/EFL). Wewe utakuwa na modern football aka attacking football but trophyless.
 
Watani mna hali ngumu kiukweli. Kinachoniuma ni kwamba sioni timu ikijiandaa
 
Back
Top Bottom