Tozo ya kodi posta Tanzania unapoagiza bidhaa kutoka Aliexpress China

Tozo ya kodi posta Tanzania unapoagiza bidhaa kutoka Aliexpress China

Unaagiza nini?

Sijui customs wanatumia vigezo gani kuamua mizigo ipi ilipiwe ushuru na ipi ipite bila ushuru.

Kwa uzoefu wangu box likishakuwa kubwa customs wanalizuia. Ukienda ukawaonyesha bei uliyonunulia wanakupatia tax assessment kutokana na vitu ulivyonunua - ipo kisheria. Lazma uliwe kichwa.

Mi naona ukitaka usitozwe kodi agiza mizigo ije kwenye parcel ndogo ndogo au vimifuko hivi. Kitu kikishakuwa kwenye box hasa kubwa kikazuiwa na customs huna la kufanya inabidi ulipe utakachoambiwa maana unakutanishwa na maofisa wa TRA live na watataka kuona bei uliyonunulia.

Kitu kikija kwenye wrapping ndogo customs wanaruhusu kiingie nchini bila kulipiwa kodi - ndio pona yako.

Mfano kama unataka saa 10 badala ya kununua zote zije kama mzigo mmoja nunua zote independently zije moja moja. Box la saa 10 haliwezi kupona, ila saa moja moja inaweza kupita bila kuombwa ushuru.
Unafundisha watu kukwepa kodi ni kosa kisheria
 
Nimekuwa nikiagiza bidhaa nyingi kutoka aliexpress, na mara zote nimekuwa nikitozwa kodi kubwa na posta ninapoenda kuchukua mzigo zaidi ya bidhaa bei ninazoagiza.

Nataka kujua kwa wenzangu ambao mnaagiza kama nyie mnatozwa hivyo au mimi nakosea sehemu!

Mnielekeze nifanyaje ili kupunguza kodi.
Siku nyingine ukiagiza na ukatozwa tozo unayohisi ni kubwa:
1: Muone inchaji wa customs department akupe ufafanuzi, kipi kinachajiwa na kwa nini?
2: Muone mkuu wa posta unapochukulia vifurushi vyako akupe ufafanuzi.
Humu tutakujaza mafuta. Go to reliable source ( msisitizo)
 
Unaagiza nini?

Sijui customs wanatumia vigezo gani kuamua mizigo ipi ilipiwe ushuru na ipi ipite bila ushuru.

Kwa uzoefu wangu box likishakuwa kubwa customs wanalizuia. Ukienda ukawaonyesha bei uliyonunulia wanakupatia tax assessment kutokana na vitu ulivyonunua - ipo kisheria. Lazma uliwe kichwa.

Mi naona ukitaka usitozwe kodi agiza mizigo ije kwenye parcel ndogo ndogo au vimifuko hivi. Kitu kikishakuwa kwenye box hasa kubwa kikazuiwa na customs huna la kufanya inabidi ulipe utakachoambiwa maana unakutanishwa na maofisa wa TRA live na watataka kuona bei uliyonunulia.

Kitu kikija kwenye wrapping ndogo customs wanaruhusu kiingie nchini bila kulipiwa kodi - ndio pona yako.

Mfano kama unataka saa 10 badala ya kununua zote zije kama mzigo mmoja nunua zote independently zije moja moja. Box la saa 10 haliwezi kupona, ila saa moja moja inaweza kupita bila kuombwa ushuru.
Saa 10 zote unapeleka wapi?
Zawadi? Hapana ni biashara.
Kwa nini ukwepe kulipa kodi?
 
Asante kwa ufafanuzi mkuu.
Serikali hii ina mambo ya kinyonyaji sana kumbe bora kununua tu hkuhku bongo.
Mimi nitafurahi sana ukinunua hapa nchini:
1: Utampa fedha mtz mwenzio ambaye analipa tozo za serikali.
2:Mtz mwenzio atasonga mbele kiuchumi na mzunguko wa fedha utaongezeka na wewe au ndg yako atafaidika
 
Ongea na anayekuuzia andike bei ndogo hata kikija ni rahisi.ni shafanya sana
Mnaliibia Taifa. Wamo humu mtashangaa vifurushi vyenu vitakaguliwa.
Dunia ya sasa haiongopi. Ana google anajua bei.
Ukiona ulifaulu fahamu alikupotezea. Siku nyingine utashangaa.
 
Walikuwa hawatozi zamani... ila sasa hivi kila mzigo wanatoza 5000
 
Asante kwa ufafanuzi mkuu.
Serikali hii ina mambo ya kinyonyaji sana kumbe bora kununua tu hkuhku bongo.
Mkuu, kulipa Kodi sio unyonyaji bali ni wajibu wa kila mtu. Kwa hiyo unapoagiza kitu kutoka nje, ni lazima ulipie Kodi. Ikitokea ni bidhaa ambayo ina msamaha wa Kodi hutalipia.
Lipa Kodi kwa maendeleo ya nchi.
 
Mnaliibia Taifa. Wamo humu mtashangaa vifurushi vyenu vitakaguliwa.
Dunia ya sasa haiongopi.Ana google anajua bei .
Ukiona ulifaulu fahamu alikupotezea. Siku nyingine utashangaa.
Upo sahihi mkuu. Sidhani Kama wadau wanalijua hili. Kibaya zaidi wanajadili jinsi ya kukwepa Kodi humu mitandaoni Bila kujua kwamba humu humu Kuna wahusika wa TRA. Hii ni mbaya Sana na nikinyume na sheria za nchi.

Kama umeagiza bidhaa lazima Kodi ilipwe, ikitokea hujaambiwa ulipe Kodi basi mshukuru Mungu.
 
Walikuwa hawatozi zamani... ila sasa ivi kila mzigo wanatoza 5000
Hii inawezekana isiwe Kodi, bali gharama za posta za usafirishaji wa percel yako kutoka makao makuu Dar mpaka ulipo. Wakati mwingine unaweza lipa vyote,Kodi jumlisha gharama za posta.
 
Wakuu swali lingine naweza agiza mzigo domestic toka bongo posta wakafikisha nilipo?au wao wanapokea tu toka nje? Kama wanatuma gharama zao vp let say 5kg kamzigo tu maybe vibambala.
 
Upo sahihi mkuu. Sidhani Kama wadau wanalijua hili. Kibaya zaidi wanajadili jinsi ya kukwepa Kodi humu mitandaoni Bila kujua kwamba humu humu Kuna wahusika wa TRA. Hii ni mbaya Sana na nikinyume na sheria za nchi.

Kama umeagiza bidhaa lazima Kodi ilipwe, ikitokea hujaambiwa ulipe Kodi basi mshukuru Mungu.
Nasi tunajadili tufanyeje ili tusiambiwe kulipa kodi
 
Utatunguliwa yafuatayo:-
1. Custom Processing Fee = 0.6%
2. Railway Dev Levy = 1.5%, na
3. VAT = 18%.

Sasa assume simununua kwa TZS 500,000

0.6% ya TZS 500K = TZS 3000...... i
1.5% ya TZS 500K = TZS 7500..... ii

Now, thamani ya simu itayotakiwa kukatwa kodi ni 3000 + 7500 + 500,000 = 510,500

VAT 18% ya 510,500 = TZS 91,890 -- Hiyo ndo utawaachia TRA!

Itoshe tu kwamba, ukiagiza bidhaa kwa bei ya kukurupuka, halafu ukaingia kwenye mikono ya TRA, unaweza kujikuta unalipia bidhaa husika kwa pesa ya juu zaidi kuliko kama ungenunua TZ!
Mkuu TRA wanajumuisha pesa ya usafiri kwenye kukata hyo 18% au hamna
 
Siku nyingine ukiagiza na ukatozwa tozo unayohisi ni kubwa:
1: Muone inchaji wa customs department akupe ufafanuzi, kipi kinachajiwa na kwa nini?
2: Muone mkuu wa posta unapochukulia vifurushi vyako akupe ufafanuzi.
Humu tutakujaza mafuta. Go to reliable source ( msisitizo)
Ndugu nataka niwe naagiza mali china unaweza nisaidie
 
Hivi ukiagiza mzigo kwa kutumia Aliexpress na tracking ikikuonesha kuwa mzigo tayari umeshafika Tz, vipi ndio niwahi posta kwenda kufata mzigo wangu?!
 
Hivi ukiagiza mzigo kwa kutumia Aliexpress na tracking ikikuonesha kuwa mzigo tayari umeshafika Tz, vipi ndio niwahi posta kwenda kufata mzigo wangu?!
Samahani wakulungwa.... hivi kuagiza mzigo kwa njia ya POSTA ni lazima nifungue SANDUKU la posta???
Au naweza muagiza bila hata ya kuwa na sanduku laleo posta,?? Na mzigo ukafika ??
 
Back
Top Bottom