beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amesaini marekebisho ya Kanuni za Tozo za Miamala ya kutuma na kutoa Fedha na kupunguza viwango vya tozo kwa 30%

Pia Serikali imejadiliana na watoa huduma za simu ambao nao wameridhia kupunguza viwango vya tozo wanazotoza kati ya mtandao na mtandao mwingine kwa 10%

Viwango vilivyopunguzwa vitatangazwa rasmi Septemba 01, 2021

Taarifa Kamili:

 
Kwahio Punguzo hilo, litakuwa ni Ongezeko la Asilimia ngapi kutoka tulipokuwepo Awali....

Hii inanikumbusha story ya ukitaka kumchemsha chura ongeza moto kidogo kidogo..., ila huenda hapa ni kuweka moto mkali kuliko ili ukipunguza kidogo mtu aone ahueni ila kumbe bado ni moto mkali
 
Watanzania waliacha kutuma na kupokea fedha.
 
30% bado ndogo sana.. punguzo lilipaswa kuwa chini ya 50%.. kinachoendelea ni ujambazi wa mchana kweupe.
 
kumbe walikuwa wanafanya makusudi.

2025 kura yangu bora nimpe mwanangu chadema
 
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Agosti 31, 2021 ametia saini mabadiliko ya tozo za miamala ambapo serikali imepunguza 30% na makampuni ya simu Kupunguza 10% kutoka kwenye gharama za awali za ufanyaji wa miamala.
 
Naona kama kigongo cha wimbo wa Nay Wamitego al-maaruf Rais Wa kitaa! Kimesaidia kushusha presha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…