TRA fanyeni kazi yenu kwa ufanisi! Watu hawaombi risiti na wenye maduka hawatoi risiti kikamilifu!

Utaratibu umebadilishwa ndugu ndo mana mapato yanapaa badala ya kushuka. Sasa hivi ni takribani trilion 1.9 kwa mwezi wakati kipindi cha jpm na marisit yake ilikuwa chuni ya hapo. Kupanga ni kuchagua we baki na marisiti yako ambayo haya add value.
Mimi sipo kubishana kuhusu makusanyo kwa mwezi! Maana hata SIASA inaweza kufanya kazi! Kama wanakusanya kiasi hicho tozo za nini? Mara uchumi umeshuka? Hao ni waongo tunataka wakusanye kodi waachane na tozo zisizo na kichwa wala miguu!
 
Jpm alichokifanya ilikuwa ni mechanical thinking isiyokuw na tija bali spending too much for nothing. Alijigamba eti amezui wizi kumbe amezui volume kubwa ya wezi tu na kuruhusu volume ndogo ya wizi ambayo ilikuwa inakimba haswaaa. Mfano watu kumi kila mmoja anaiba elfu 10 ambapo wizi ni sawa na 100,000,000 ikazuiwa/wakafujuzwa hivyo wakabaki watu wawili( pole pole na Bashiru au makonda) ambao kila mmoja anaiba 200,000,000 ambapo jumla ya wizi ni 400,000,000. Sasa hapo kazuia wizi au kazui wanufaika wasiwe wengi!!

Uchumi ni akiri tu. Mama samia anatumia akiri nyingi sana ndo mana mapato yanapaa bila marisiti au bila kelele wala utekaji
 
Mfumo wa TRA ni mbovu. Kipindi Wizara ya Fedha iliwahi shauriwa bidhaa zitambulike/zitozwe kodi toka kiwandani huko china. Lakini viongozi wetu wanapenda vitu vinavyowaongezea umaarufu kisiasa.
Hilo jambo halipo duniani na halitekelezeki. Ushindwe kukusanya kodi Kariakoo kwa watu ulionao ndio uje kuweza kwenye nchi za watu.
Na kama bidhaa hazitoki China hazitozwi. Kama bidhaa ni used hazitozwi. TRA wanafanya kazi Tanzania, nani ataenda fanya regulations kule China
 
Hapo kuna uongo mwingi sana usimusikilize msigwa! That is why miradi mingi inasuasua kama jana tulikuwa tunajadiri humu!
 
Tatizo lako unaleta ushaki wa kipuuzi soma jadili kwa hoja!
 
Yanini kudai risiti wakati hiyo kodi wakishainyaka wanaitumia kubambikia watu kesi, kuendesha kesi za kipumbavu na kupaa na ndege kila wiki?

Siwezi kuwa mzalendo kama viongozi wetu ndio hawa walafi
 
Mimi sipo kubishana kuhusu makusanyo kwa mwezi! Maana hata SIASA inaweza kufanya kazi! Kama wanakusanya kiasi hicho tozo za nini? Mara uchumi umeshuka? Hao ni waongo tunataka wakusanye kodi waachane na tozo zisizo na kichwa wala miguu!
HII HOJA IMEKUFICHUA, HUNA UCHUNGU NA NCHI YAKO UNACHOTAKA NI WACHACHE WABEBE MZIGO WA KODI KWA KIGEZO CHA BIASHARA.

Yaani unaona si sawa kulipa tozo ila unasikia uchungu mfanyabiashara akitaka kuuza bidhaa yake bila VAT.

Anayelipa VAT ni raia, huyo huyo aliyeambiwa lipa tozo....mfanyabiashara anaisaidia TRA kuikusanya bure tena akichelewa kutoa taarifa anapigwa faini.

Wanunuzi wengi hawataki kulipa VAT hivyo mfanyabiashara anabaki na chaguzi mbili, asiuze bidhaa au aiuze bila VAT asikupe risiti. Unadhani atachagua nn? STUPIDO MNYONGE

Unajua mfanyabiashara kalipa kodi ngapi mpaka hilo duka lipo hapo?
 
Ni makubaliano ya bei toka kiwandani. Yaani inakuwa hivi: TRA wanakuwa na bei za viwanda vyote huko China. Mtu akinunua mzigo inajulikana kabisa VAT iko kiasi fulani (kwa sasa TRA hawajui nani anamzigo kiasi gani na kodi kiasi gani).
 
Wewe ndo stupidi kwani wasio wafanya biashara hawalipi kodi! Mfano mwenye duka sianuza bidhaa ukiwa ameshajua faida yake kiasi fulani na ujue hiyo hela ya kodi iko ndani ya bidhaa hiyo anayouza! au unataka kusema wanagawa bidhaa bure? Usijifanye unajua hata mimi nafanya kazi zangu na kodi nalipa! Wewe kichwa chako unakijua mwenyewe umekibeba hakikusaidii! Mimi nasema walipe kodi sio waporwe bidhaa zao bado naonekana mbaya! Kwa mawazo yako tufute TRA! basi maana you are very stupid!
 
Sahihi hilo hata mimi nimelishuhudia jana posta kwenye duka moja la wachina, (jina nalihifadhi) Niliwenda nunua bidhaa kama mwezi umepita nikaambiwa bidhaa hizo ni out of stock kama sitojali nilipe advance bidhaa iagizwe kisha watanijulisha. Jana tarehe 02/10/2021 wakanipigia simu na kunijulisha kuwa bidhaa zimefika. Nikaenda kwa ajili ya kumalizia malipo na kuchukua bidhaa zangu. Ajabu wakasema bidhaa imepanda bei kila pcs wameongeza Tsh 10,000 wakidai gharama za usafiri zimepanda. Mimi nikakomaa kuwa sifanyi manunuzi upya nimekuja kuchukua bidhaa ambazo tayari nilishalipia. Wakakomaa kwamba hawauzi kwa hiyo bei la sivyo wanirejeshee pesa. Nikawaambia sitaki fedha nataka bidhaa la sivyo naondoka najua mtaleta bidhaa mpaka nyumbani kwa gharama zenu.
Nikaanza kuondoka natoka nje mdada mfanyakazi akaniita akaanza ongea nami bosi anasema hivi lipia kwa bei ile ya awali ila risiti itabidi aandike bei ya chini. Nikamwambia siwezi fanya kitu hicho kwa manufaa ya mgeni. Kwanza walikuwa wameniuzi sana maana walikuwa wanajibu kwa nyodo sana. Nikawaambia naondoka ila najua jumatatu mtaleta bidhaa hizo nyumbani kwangu na mtalipa na gharama usafiri pamoja kesi mahakamani.
Yule mdada akanisihi nirudi niongee na mchina. Wakateta pembeni baadaye wakasema lipia hiyo pesa. Wakanipa mzigo nikaondoka zangu.
Kama angelikuwa ni mtanzania ningeweza kuelewana naye maana hata kiasi anakwepa kodi, kitatumika humu mjini kuongeza ukwasi mtaani. Ila kwa mchina na mhindi siwezi fanya ujinga huo. Kwanza bei wanazoweka huwa hawapunguzi zaidi huwa wanapandishia kodi, unaweza dhani unapunguziwa kumbe unawanufaisha wao.
 
Unadhidi kudhihirisha you are stupid kwenye masuala ya Tax.

Ushajua kwann kuna bei ya risiti, bei bila risiti na bei nusu risiti? Ukishajua utaelewa anayekwepa kodi ni nani na anayemsaidia kukwepa ni nani na kwann.

Mfanyabiashara yeye analipa kodi kabla hata hiyo biashara hajaianza kwa njia ya makadirio. Kasheshe inakuja kwenye VAT ambayo yeye anaikusanya ili ampe TRA na kazi anaifanya bure.

Importation zote huwezi kwepa kuzilipia VAT wakati unaingiza mzigo. Kwa bidhaa za ndani pale kiwandani mizigo inachajiwa VAT.

Tatizo linakuja kwa nyinyi wanyonge wapenda mtelezo linapokuja suala la kulipa hiyo VAT. Hamtaki, mnataka mfanyabiashara ile kwake na mfanyabiashara hawezi kubali ile kwake.

Kama kweli unaipenda nchi yako ungependekeza wafanyabiashara wasikusanye VAT bali ziingizwe kama indirect tax na usingeponda TOZO.
 
Umesomeka mzalendo,
 
Yaani hao wachina siku hizi hanaichezea sana nchi hii! Wako kila koma na mambo yao ni magumashi kuanzia vibali vya kuishi mpaka mambo yao!
 
Wewe naona unajua sana hiyo mashine a EFD ina kazi gani? Si ndo inakuja kufanya checkup ya mauzo yote
 
Wewe naona unajua sana hiyo mashine a EFD ina kazi gani? Si ndo inakuja kufanya checkup ya mauzo yote

Upo sawa, ila ngoja nikupe mfano ili tuelewane...

Umekuja kwangu kupangisha nyumba nakutoza kodi ya pango halafu nakwambia kila mteja anayekuja kununua bidhaa yako nataka kwenye kila bidhaa unikusanyie elfu moja.

Ukishindwa kunipa taaarifa za mauzo kwa wakati nakupiga adhabu na riba.

Wewe unakubali, unalipa kodi ya pango awamu ya kwanza unaenda kununua mzigo uje kuuza dukani kwako.

Anayekuuzia mzigo naye kapanga kwangu na maelekezo nimempa yale yale.

Unanunua mzigo kwa mpangaji mwenzako na kulipia kila bidhaa elfu moja.

Unakuja dukani kuuza mzigo anakuja raia hataki kulipia elfu moja ila atanunua bidhaa kama ww utanidanganya kuwa hujauza.

Unadanganya ili mzigo usikudodee.

Ukinidanganya mda mrefu imekula kwako maana mm najua wapangaji wangu wote na mlivyouziana mizigo. Kuna siku tu ntakupata na kukutoza faini na interest na hiyo kodi utailipa pia maana utakuwa huna mzigo ila huna mauzo pia na mm mwenye nyumba najua ulinunua mzigo kwa wapangaji wangu kadhaa sasa ukowapi? Umeuza bila kunipa elfu zangu. Zilipe sasa hivi zote na nakuchaji adhabu halafu nakuchaji riba kwa muda wooote uliokaa na hizo fedha.

Sasa umeshapata picha wanachopitia wafanyabiashara? Wanalipa kodi yao, wanafanya kazi ya kukusanya kodi na pia hiyo kodi inaathiri utokaaji wa bidhaa. Hapo hujaongelea kodi za huduma, wafanyakazi, manispaa, mabango, mishahara, sdl, Wcf n.k n.k n.k

Ni kweli Mashine ya Efd kazi yake ni kuonyesha mauzo ili kuhakiki kama VAT ilikusanywa kihalali na kwa ufasaha na mfanyabiashara hajadanganya ukubwa wa biashara yake ili akadiriwe kodi kidogo.

Kwa wafanyabiashara wengi Tatizo si kutoa risiti au kulipa kodi yao halali ya 30% ya faida, tatizo ni utayari wa mnunuzi kulipia VAT, mfanyabiashara abaki na faida yake halafu ampelekee VAT TRA.

Wengi hawataki kununua bidhaa bei kubwa. Sasa muuzaji anabaki na choice mbili, abaki na mzigo kwa sababu ya kumkusanyia TRA VAT au auze bila VAT. Akiuza bila VAT kabisa inabidi asitoe risiti kabisa maana ataulizwa VAT ikowapi?

Hata na hivyo mwishoni kama mzigo aliulipia wote VAT bado anakuwa kwenye matatizo akifanyiwa audit kwa makosa ya mnunuzi asiyetaka kuuziwa bei juu maana stock closing balance haitaendana na sales.

WAFANYABIASHARA WANATESEKA NA KODI HAMJUI TU MAANA WAO WANAFANYA KAZI MBILI NGUMU, KUKUSANYA KODI NA KUILIPA KWA TRA KWA WAKATI NA KUFANYA BIASHARA.
 
Wewe utakuwa kapumbavu! Mbona tumevuka lengo la makusanyo kwa mwezi September? Wacha tu watu waendelee hivyo hivyo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…