Wewe naona unajua sana hiyo mashine a EFD ina kazi gani? Si ndo inakuja kufanya checkup ya mauzo yote
Upo sawa, ila ngoja nikupe mfano ili tuelewane...
Umekuja kwangu kupangisha nyumba nakutoza kodi ya pango halafu nakwambia kila mteja anayekuja kununua bidhaa yako nataka kwenye kila bidhaa unikusanyie elfu moja.
Ukishindwa kunipa taaarifa za mauzo kwa wakati nakupiga adhabu na riba.
Wewe unakubali, unalipa kodi ya pango awamu ya kwanza unaenda kununua mzigo uje kuuza dukani kwako.
Anayekuuzia mzigo naye kapanga kwangu na maelekezo nimempa yale yale.
Unanunua mzigo kwa mpangaji mwenzako na kulipia kila bidhaa elfu moja.
Unakuja dukani kuuza mzigo anakuja raia hataki kulipia elfu moja ila atanunua bidhaa kama ww utanidanganya kuwa hujauza.
Unadanganya ili mzigo usikudodee.
Ukinidanganya mda mrefu imekula kwako maana mm najua wapangaji wangu wote na mlivyouziana mizigo. Kuna siku tu ntakupata na kukutoza faini na interest na hiyo kodi utailipa pia maana utakuwa huna mzigo ila huna mauzo pia na mm mwenye nyumba najua ulinunua mzigo kwa wapangaji wangu kadhaa sasa ukowapi? Umeuza bila kunipa elfu zangu. Zilipe sasa hivi zote na nakuchaji adhabu halafu nakuchaji riba kwa muda wooote uliokaa na hizo fedha.
Sasa umeshapata picha wanachopitia wafanyabiashara? Wanalipa kodi yao, wanafanya kazi ya kukusanya kodi na pia hiyo kodi inaathiri utokaaji wa bidhaa. Hapo hujaongelea kodi za huduma, wafanyakazi, manispaa, mabango, mishahara, sdl, Wcf n.k n.k n.k
Ni kweli Mashine ya Efd kazi yake ni kuonyesha mauzo ili kuhakiki kama VAT ilikusanywa kihalali na kwa ufasaha na mfanyabiashara hajadanganya ukubwa wa biashara yake ili akadiriwe kodi kidogo.
Kwa wafanyabiashara wengi Tatizo si kutoa risiti au kulipa kodi yao halali ya 30% ya faida, tatizo ni utayari wa mnunuzi kulipia VAT, mfanyabiashara abaki na faida yake halafu ampelekee VAT TRA.
Wengi hawataki kununua bidhaa bei kubwa. Sasa muuzaji anabaki na choice mbili, abaki na mzigo kwa sababu ya kumkusanyia TRA VAT au auze bila VAT. Akiuza bila VAT kabisa inabidi asitoe risiti kabisa maana ataulizwa VAT ikowapi?
Hata na hivyo mwishoni kama mzigo aliulipia wote VAT bado anakuwa kwenye matatizo akifanyiwa audit kwa makosa ya mnunuzi asiyetaka kuuziwa bei juu maana stock closing balance haitaendana na sales.
WAFANYABIASHARA WANATESEKA NA KODI HAMJUI TU MAANA WAO WANAFANYA KAZI MBILI NGUMU, KUKUSANYA KODI NA KUILIPA KWA TRA KWA WAKATI NA KUFANYA BIASHARA.