TRA fanyeni kazi yenu kwa ufanisi! Watu hawaombi risiti na wenye maduka hawatoi risiti kikamilifu!

Pengine kuja kwao iliitangaza nchi tukapata watalii ambao ndio wangeleta pesa za kumlipa huyo mwalimu kijijini.

Rwanda inatumia maelfu ya dola kutangaza utalii,hakuna kitu kinajishusha kama mvua.
 
Lini ilikuwa kiwango cha chini? Wewe hapo hufanyi selfishness kwa majirani zako?

Chuki za kijinga zinakusumbua,,kama haitumiki basi kila kitu huko mitaani watu wanajifanyia wenyewe kuanzia kujilinda,mashule yao, mahospital kila mtu yake,maji,umeme nk nk.
 
Kipindi Cha mwendazake Ile kamata kamata ya wasio toa risiti ilikuwa kubwa ,so wafanyabiashara wengi walikuwa wanatoa ...saiv wameacha kabisaa kutoa..

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Mimi sipo kubishana kuhusu makusanyo kwa mwezi! Maana hata SIASA inaweza kufanya kazi! Kama wanakusanya kiasi hicho tozo za nini? Mara uchumi umeshuka? Hao ni waongo tunataka wakusanye kodi waachane na tozo zisizo na kichwa wala miguu!
Naunga mkono hizi takwimu zinatia shaka mkuu... Kwanza wangetakiwa watupe monthly, quarterly and yearly targets mapema ili sasa waandishi wawe wa nafuatilia kama wamefikia target au laa.
 

Ule muamko wa matangazo tunaomba uendelee.
 
Kwa mtazamo wangu kuna matatizo ya msingi katika mifumo yetu ya kodi na sekta binafsi kiujumla yanayopelekea Hali hii ya kukwepa kutoa risiti.
1. Viwango vikubwa vya Kodi visivyoakisi uhalisia wa faida katika biashara. Kwa biashara ambazo sio kampuni ambazo ndio majority kwa hapa Tz, TRA wanakadiria kodi kwa kuangalia mauzo tu. Hawajali nature ya biashara. Iweje mtu anayeuza hardware akakadiriwa sawa sawa na mfanyabiashara wa nguo wakati profit margin zao hazifanani? Mfano Mfuko wa Cement unaouzwa 15000 utakuta faida yake haizidi 700. Ila Jeans la 15,000 faida inaweza kuwa 3000. Hivyo sio sahihi kuwatoza kiwango sawa cha kodi kisa mauzo ni 15,000. Hili linaweza kupelekea wenye biashara zenye faida ndogo kukwepa kutoa risiti. Maana anaweza kujikuta faida yote aliyopata inakuja kumezwa na kodi.

2. Sekta binafsi isiyo rasmi kwa kiwango kikubwa. Hili linaathiri sana upande wa VAT. Unakuta kwenye Supply chain yupo mtu/watu wenye kuuza bidhaa au kutoa huduma ambao sio VAT registered au hawako kabisa kwenye mfumo rasmi. Matokeo yake muuzaji wa mwisho hana uwezo wa ku-claim VAT yoyote kwenye huduma hizo za katikati na hii kupelekea sehemu ya faida yake kwenda TRA. Kwa style hio wengine ndo maana huamua kutotoa risiti.

So the bottom line is kunahitajika a thorough review of our Tax system. Naamini watu wengi wako tayari kuchangia maendeleo kupitia kodi. Ila ni muhimu upatikane mfumo sahihi wa ukadiriaji wa kodi.
 
Ni kweli mimi naamini watanzania walishazoea kukwepa kodi ma ikitokea mtu anafatilia kodi kikamirifu watamuona ni adui yao! Lakini wakumbuke tunakoomba misaada hawana utani kwenye kodi lakini huku tumachekeana!
Watu tunalipa Kodi lkn hatuoni maendeleo,acha wakwepe tu
 
Wewe kama unataka risiti chukua, me siipeleki risiti sehemu yoyote kudai fidia, sanasana nitaishia kuichana tu, so nikishachukua mzigo wangu nasepa, kwanini tutiane umasikini? Kwa serikali ipi hadi niipende sana nidai kikaratasi cha kuthibitisha nimenunua? Mali si naiona mkononi, karatasi la nini? Me namuambia mapema muuzaji mwana kibingwa niuzie bila kikaratasi nisepe, hata ya kubebea sitaki.

Wacha wanikate hela kwenye Payee tu maana sina namna ya kuwakwepa. Ukishaendesha nchi kwa ubabe na sisi tunatafuta ubabe kwingine kukukomesha.

Na ziwatoshe hizo kodi za kwenye tozo, kodi ya nyumba ya kwenye umeme, na nyinginizo.

Hata ninunue mali ya milioni 60, kikaratasi sitaki
 
Namba 1 siyo kweli sababu hata biashara binafsi ambazo siyo kampuni wapo wanaolipa kodi kutokana na faida. Angalia Kodi na Ushuru mbalimbali utaelewa nini nazungumzia.Kingine kodi haitozwi kulingana na aina ya biashara bali inatokana na mapato yako.

Namba 2 kama umenunua bidhaa kwa mtu ambaye hayupo kwenye mfumo rasmi au hajasajiliwa na VAT sioni sababu ya kudai marejesho kwani hujalipa VAT isipokuwa kama nawe umesajiliwa VAT ukiuza kuna asilimia 18% utakuwa umeiongeza ambayo ndiyo utaiwasilisha TRA.Kumbuka siyo faida yako bali wewe ni wakala tu wa kukusanya hiyo 18% ambayo utakuwa umeiongeza kwenye bidhaa au huduma.
 
Ni asilimia ngapi ya hao binafsi wanaolipa kwa kutumia faida? Most likely hao ni wale ambao ni VAT registered ambao sio majority. Na pia unaongelea kile kile nilichosemea mimi. Mimi nimetumia neno mauzo na wewe umetumia neno mapato which practically means the same thing. Na ndio maana nikatoa mfano wa bidhaa mbili tofauti zenye mapato sawa ila faida tofauti. Ila TRA wao watakadiria kutokana na mapato bila kujali kuwa faida haziliningani
 
Shida ni kwamba you are being theoretical rather than being pragmatic. . Hayo yote na mimi ninayafahamu. Vitu on the ground haviko simple kama unavyoongelea hapo.
 
Haya mambo aliyaweza Magufuli. Now enzi za jakaya zimerudi tuendelee kula bata. Si mlitaka maisha mepesi haya sasa yamerudi
 
Mjinga kweli wewe
 
Tozo za hovyo hovyo + kauli ya waziri wa fedha ya kuhamia Burundi + baadhi ya watumi kupewa posho kubwa isiyokuwa na makato ya kodi + wabunge kushutumiwa kutokulipa kodi. Je, mtu mpumbavu yupi atakayekataa ofa kama hiyo dukani? Unafikiri elimu ya uzalendo itaeleweka?
 
Uzalendo uanze na viongozi Kwanza,Kama wao ni bure na wananchi pia watakua ni bure tu...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…