TRA: Ukinunua bidhaa na usipodai risiti utapigwa faini ya kati ya Tsh. 30,000 na Tsh. 1,500,000

TRA: Ukinunua bidhaa na usipodai risiti utapigwa faini ya kati ya Tsh. 30,000 na Tsh. 1,500,000

2Kwa hiyo anayepinga mamlaka inayotawala ana pinga chombo kilichowekwa na Mungu; na watu wanaoasi watajiletea hukumu.
3 Kwa maana watawala hawatishi watu wanaotenda mema bali wale wanaotenda maovu. Kama hupendi kuishi kwa kumwogopa mwenye mamlaka, basi tenda mema naye atakusifu.
Mema ya mamlaka mbovu unayajua? mfano wake ni kusifia uovu, ukijaribu kuyaonya kwa kuyapinga uovu wanaofanya utaishia kuokotwa kwenye kiroba Coco Beach.

Kusifiwa na huyo mwenye mamlaka ni sawa na kusifiwa na shetani.
 
Maada hapa ni kulipa kodi sio kuua.
Weka maada ya kuua ijadiliwe
Hope umeshaona ilivyo ngumu kuheshimu mamlaka za ulimwengu, vingine vigumu huwezi kuvitetea.
 
Uko sahihi kwa maandiko lakini sio vitendo
Mungu hakushindwa kuzuia lolote

"Kila mtu hana budi kutii serikali inayotawala. Kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na serikali zote zilizopo zimewekwa na Mungu."


"Enyi mlioamini Mtiini Allah, na mtiini Rasuli (Wake Muhammad) na Wale waliopewa mamlaka kutoka miongoni mwenu, ...... (Qur'ani, 4:59)
 

Warumi13​

1 Kila mtu hana budi kutii serikali inayotawala. Kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na serikali zote zilizopo zimewekwa na Mungu.
2 Kwa hiyo anayepinga mamlaka inayotawala ana pinga chombo kilichowekwa na Mungu; na watu wanaoasi watajiletea hukumu.
3 Kwa maana watawala hawatishi watu wanaotenda mema bali wale wanaotenda maovu. Kama hupendi kuishi kwa kumwogopa mwenye mamlaka, basi tenda mema naye atakusifu.
4 Maana mwenye mamlaka ni mtumishi wa Mungu kwa manufaa yako. Lakini kama ukitenda maovu, basi ogopa kwa maana hatembei na silaha bure. Yeye ni mtumishi wa Mungu anayetekeleza adhabu ya Mungu juu ya watenda maovu.
5 Kwa hiyo ni lazima kutii wenye mamlaka, si kwa sababu ya kuogopa adhabu tu bali pia kwa ajili ya dhamiri.

6 Kwa sababu hiyo hiyo mnalipa kodi, kwa maana watawala ni watumishi wa Mungu ambao hutumia muda wao wote kutawala.
7 Wal ipeni wote haki zao; mtu wakodi mlipe kodi; na mtoza ushuru mli pe ushuru; astahilie kunyenyekewa, mnyenyekee; astahiliye hesh ima, mheshimu.




Qur'ani
"Enyi mlioamini Mtiini Allah, na mtiini Rasuli (Wake Muhammad) na Wale waliopewa mamlaka kutoka miongoni mwenu, ......" (Qur'ani, 4:59)
Aliyeandika Biblia alikuwa mtu mwenye akili sana alijua haya yote na kwa maslahi ya utawala
 
Mamlaka ya mapato Tanzania ( TRA) imetoa mwongozo wa kisheria kwa wananchi wote kwamba endapo utanunua bidhaa au Huduma ni lazima udai risiti.

Endapo utakamatwa umenunua bidhaa au Huduma na hauna risiti basi utapigwa faini ya kati tsh 30,000 na 1,500,000 kwa mujibu wa kanuni za sheria ya kodi.

Kumbuka kudai risiti kila wakati.

Maendeleo hayana vyama!
Bwashee, wale machinga mnao watoza elfu 20 za vitambulisho nao wanatoa risiti au kwa kauli hii mnatuambia tusinunue bidhaa zao?
 
Mema ya mamlaka mbovu unayajua? mfano wake ni kusifia uovu, ukijaribu kuyaonya kwa kuyapinga uovu wanaofanya utaishia kuokotwa kwenye kiroba Coco Beach.

Kusifiwa na huyo mwenye mamlaka ni sawa na kusifiwa na shetani.
Mungu atabaki kuwa Mungu tuu hata pale ambapo mapenzi yetu hayatimii bado ni Mungu.

Kama unaamini Mungu yupo ongea nae kwa kila kitu
 
Anayepaswa kupigwa faini ni mtoaji risiti na si mteja! Tunakoelekea tutakuwa tunaviziana!
 
Mungu hakushindwa kuzuia lolote

"Kila mtu hana budi kutii serikali inayotawala. Kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na serikali zote zilizopo zimewekwa na Mungu."


"Enyi mlioamini Mtiini Allah, na mtiini Rasuli (Wake Muhammad) na Wale waliopewa mamlaka kutoka miongoni mwenu, ...... (Qur'ani, 4:59)
A Bible is an Opium for the People by .....philosopher mmoja makini!!!
 
Sipendi mtu anayejidai kunukuu nukuu vifungu vya maandiko ya dini kwenye sehemu ambazo hata hakungekuwa na ulazima/haja ya kufanya hivyo
 
Sijaelewa kidogo...
Kwamba mwanzo ilikuwa kuhamasisha (optional) ila sasahivi imekuwa kuamrisha (obligatory)
 
Back
Top Bottom