TRA: Usajili wa TIN kwa mwananchi umri kuanzia miaka 18 siyo kwa ajili ya biashara bali ni kwa utambuzi

TRA: Usajili wa TIN kwa mwananchi umri kuanzia miaka 18 siyo kwa ajili ya biashara bali ni kwa utambuzi

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema hadi kufikia Desemba 31, mwaka huu kila mtu mzima nchini anatakiwa kuwa na Namba ya Mlipa Kodi (TIN).

Hayo yameelezwa na Ofisa Mkuu wa Usimamizi wa Kodi (TRA), Hamadi Mteri wakati wa ufunguzi wa semina kwa wanachama wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Dar es Salaam (DCPC).

Alisema wa mujibu wa mabadiliko ya sheria, kila Mtanzania mwenye umri wa miaka 18 anapaswa kuwa na TIN ifikapo Desemba 31 mwaka huu, la sivyo litakuwa ni kosa kwa mujibu wa sheria.

Akifungua semina hiyo, Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi (TRA), Richard Kayombo alisema Juni 30, tarehe ya mwisho wa mwaka fedha 2022/23 watakuwa wamekusanya Sh23.1 trilioni, mafanikio aliyosema yametokana na utoaji wa huduma za kidijitali na mifumo rafiki.

“Kwa sasa TRA imerahisisha mfumo kwa wafanyabiashara, hususani kwenye suala la namba ya utambulisho ya mlipa kodi (TIN), ulipaji wa kodi na mfumo wa forodha ambapo mteja anaweza kufanya vyote hivi kwa kurahisisha kazi zake," alisema Kayombo.

CHANZO: MWANANCHI


UPDATES…

Alipoulizwa kuhusu madai ya kosa la jinai kwa ambaye mtu ambaye hatakuwa na namba ya TIN kama ambavyo Ofisa Mkuu wa Usimamizi wa Kodi (TRA), Hamadi Mteri alivyonukuliwa, Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo amesema “Naomba usininukuu chochote, press release ndio tamko letu.

“Ukitaka kuzungumza kitu chochote ambacho kipo nje ya press release yetu maana yake unachokonoa kitu kingine ambacho hakipo, naomba jikite kwenye press release yetu.

“Ufafanuzi wote upo kwenye press release, na ndicho wananchi wanachohitaji kukijua, hata huyo aliyeandika alijitungia, sitaki kuzungumzia hayo, ndio maana tumetoa press release ili mtu asije kuandika nje ya tulichokiandika.

“Sitafafanua chochote zaidi ya kilichoandikwa kwenye press release.”

TRA.jpg

Taarifa ya TRA
 
Kwahiyo mpaka mtoto wa high school anafunguliwa tin si ndio?

Halafu ikae tu kabatini kumngoja miaka ya mbeleni atakapoajiriwa ama kujiajiri?
 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema hadi kufikia Desemba 31, mwaka huu kila mtu mzima nchini anatakiwa kuwa na Namba ya Mlipa Kodi (TIN).

Hayo yameelezwa na Ofisa Mkuu wa Usimamizi wa Kodi (TRA), Hamadi Mteri wakati wa ufunguzi wa semina kwa wanachama wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoa wa Dar es Salaam (DCPC).

Alisema wa mujibu wa mabadiliko ya sheria, kila Mtanzania mwenye umri wa miaka 18 anapaswa kuwa na TIN ifikapo Desemba 31 mwaka huu, la sivyo litakuwa ni kosa kwa mujibu wa sheria.

Akifungua semina hiyo, Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi (TRA), Richard Kayombo alisema Juni 30, tarehe ya mwisho wa mwaka fedha 2022/23 watakuwa wamekusanya Sh23.1 trilioni, mafanikio aliyosema yametokana na utoaji wa huduma za kidijitali na mifumo rafiki.

“Kwa sasa TRA imerahisisha mfumo kwa wafanyabiashara, hususani kwenye suala la namba ya utambulisho ya mlipa kodi (TIN), ulipaji wa kodi na mfumo wa forodha ambapo mteja anaweza kufanya vyote hivi kwa kurahisisha kazi zake," alisema Kayombo.

CHANZO: MWANANCHI
Sidhani kama ni kweli maana nimeona tangazo na sheria nimechukua hakuna kitu kama hiki.Mbona TRA wametoa ufafanuzi wa hili
TRA.jpeg
LAW.jpeg
 
Alisema wa mujibu wa mabadiliko ya sheria, kila Mtanzania mwenye umri wa miaka 18 anapaswa kuwa na TIN ifikapo Desemba 31 mwaka huu, la sivyo litakuwa ni kosa kwa mujibu wa sheria.
Upuuzi huu sasa!
 
Mamlaka ya Mapato Tanzania imetoa ufafanuzi kuhusu wanaostahili kuwa na TIN na namna gani takwa hilo kisheria limesemwa. Ni kuwa ukiwa na miaka 18 unastahili kuwa na TIN na haimaanishi kuwa utalipishwa kodi sababu inaweza kuwa huna biashara au hujaajiriwa na hata kama unabishara pengine hujafika kiwango cha kulipa kodi.
TRA.jpeg
 
Waje wanikamate nipo Namtumbo Sina TIN wala NIDA.
 
Back
Top Bottom