TRA yafafanua ongezeko la ushuru wa magari

TRA yafafanua ongezeko la ushuru wa magari

Pata picha sasa gari yako ndio iko kwny meli kuja Bongo unakutana na hio kodi ya Tsh. 31m,gari itaishia kupigwa mnada tu.
Kuna unyanyasaji sana ni kama hizo hela zipo , hivi hapa alaumiwe nani waziri wa fedha au hizi mamlaka, watuambie wametumia kigezo gani
 
Tuwakomalie wabunge wabadilishe hizi kodi za enzi za ujamaa kwenye magari. Japo unasema unalinda mazingira lakini kodi kubwa hivyo kwenye mtumba una viwanda vya magari?
Gari ni kitu kinachosaidia kukuza uchumi. Ingekuwa ni amri yangu ningeweka kodi karibu na sifuri. Kwenye magari ya kazi kama pickup na fuso watu wangenunua bila ushuru hata mia, ikiwezekana nawapa na hela ya asante[emoji3][emoji3]

Kulalamika haya mambo haitusaidii kitu. Inabidi wabunge, wanasheria nk walifanyie kazi.
Umesahau mkuu alishasema magari yamekua mengi anatafuta namna kulidhibiti hilo,
 
Yeah, wanaoumia ni walioagiza gari ambazo zipo kwenye meli kwa sasa. Ni mwendo wa maumivu tu no way. Either utafute hela u top up au gari ipigwe mnada, hasara kubwa hii. Tofauti ya 2-5mil tu inaweza kukufanya uliache gari bandarini hakyanani.
Hilo ongezeko ni pesa ya kununulia hata gari moja tena [emoji38][emoji38][emoji38]
 
Sio hajaelewa nini hata wewe nina uhakika hujaelewa, sasa kwanini waangalie gari imeingia kini wasiangalie gari imeagizwa lini???

Pia kwahiyo hilo ongezeke nmtokana na hiyo chat hapo ni ya december 2020 na January 2021 aisehh bado kuna mkanganyiko
Kinachoangaliwa hapo ni gari imeingia lini sio umeagiza lini!

Halafu kutokana na corona kutamalaki huko Asia, japan mizigo ilikuwa michache kuja huku, so wakawa wanajikusanya ili wajaze meli kwahiyo unakuta gari umeagiza toka October last year linaingia January hii[emoji848][emoji848]
 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imetolea ufafanuzi taarifa juu ya kupanda kwa gharama za kodi za magari yaliyotumika yanayoingia nchini.
Ufafanuzi huo umekuja wakati kukiwa na malalamiko ya wafanyabiashara ya magari wakidai kuwepo kwa ongezeko la kodi za magari ya mitumba.

Taarifa ya TRA iliyotolewa katika gazeti la Mwananchi leo Ijumaa Januari 8 imekuongezeka kwa ushuru wa baadhi ya magari kuanzia Januari mwaka huu kutokana na uthaminishaji uliozingatia bei halisi za magari hayo, huku pia magari mengine yakishuka bei.

“Kimsingi ongezeko hilo limetokana na bei halisi ya magari husika na hivyo haimaaishi kwamba TRA imeongeza ushuru wa magari,” imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

TRA imesema kuwa magari yaliyotumika hutozwa ushuru wa bidhaa kutokana na umri wa gari ambapo umri wa gari huhesabiwa kwa kufuata mwaka wakalenda.
Kwa upande wa magari madogo yenye umri wa maika minane hadi tisa pamoja na kodi nyingine hutozwa ushuru huo wa bidhaa kwa asilimia 15 na gari yeye umri zaidi ya huo hutozwa kwa asilimia 30.

“Hivyo ikiwa mwagizaji aliagiza gari binafsi lenye umri wa miaka tisa mwaka 2020 na likaingia nchini mwaka 2021 itatozwa ushuru wa bidhaa kwenye umri wa asilimia 30 badala ya asilimia 15 ambayo ingetozwa ikiwa gari yake ingewasili kabla ikiwa gari yake ingewasili kabla ya mwaka huu,” imesema TRA.

Mamlaka hiyo imefafanua kuwa kutokana na sababu hiyo waigizaji wa magari yenye umri huo waliagiza mwaka 2020 na kuingia mwaka 2021 ni wazi kuwa kodi kwenye gari aliloagiza itaongezaka hivyo wakasema hakuna kiwango cha kodi kilichoongezwa kwenye magari.

TRA imesema katika taarifa hiyo kuwa uthaminishaji wa bidhaa hufanyika kwa mujibu wa kifungu cha sheria ya forodha ya Afrika Mashariki ya mwaka 2004 iliyorejewa mwaka 2019 kikisomwa pamoja na jedwali la nne la sheria hiyo.
Yaani nikisikia Hawa wahusika,wanahalalisha ongezeko la Kodi kwa kunukuu vifungu vya Sheria,Kana kwamba hizo Sheria ni vifungu vya bible au msahafu,huwa nashangaa sana,
 
Kuna mshikaji wangu kaagiza rav 4 kako kwenye meli huko aliko kama amepata taarifa hii, sijui itakuwaje.
Mjuze ajiandae kisakolojia kabla ya mzigo wake kufika, ajue anafanyaje
 
Na vile mi ndio nilimshawishi ye alitaka kwenda yadi, nitawaambia nini watu, ngoja niangalie kokokotoo tena

Hukujua nae hakujua ni mambo ya risk factor, cha msingi sangi wangewafanyia uwepesi wale walioagiza gari kabla ya mabadiliko maana ni uonezi
 
Kuna gari moja Zimbabwe jumla kodi waliikata kama one milion of TZS ila huku bongo gari ile kodi kwa wakati huo walikuwa wanachukua kama milioni 10 hivi.
Nenda hizi c center za be forward Japan au SBT kafanye utafiti juu ya hili
Nini kinatokea kwamba taifa linategemea kodi hii sana kuliko vyanzo vingine vya mapato
 
Tuwakomalie wabunge wabadilishe hizi kodi za enzi za ujamaa kwenye magari. Japo unasema unalinda mazingira lakini kodi kubwa hivyo kwenye mtumba una viwanda vya magari?
Gari ni kitu kinachosaidia kukuza uchumi. Ingekuwa ni amri yangu ningeweka kodi karibu na sifuri. Kwenye magari ya kazi kama pickup na fuso watu wangenunua bila ushuru hata mia, ikiwezekana nawapa na hela ya asante[emoji3][emoji3]

Kulalamika haya mambo haitusaidii kitu. Inabidi wabunge, wanasheria nk walifanyie kazi.
Wabunge hakuna awamu hii ni mkutano wa ccm .
 
Kinachoangaliwa hapo ni gari imeingia lini sio umeagiza lini!

Halafu kutokana na corona kutamalaki huko Asia, japan mizigo ilikuwa michache kuja huku, so wakawa wanajikusanya ili wajaze meli kwahiyo unakuta gari umeagiza toka October last year linaingia January hii[emoji848][emoji848]
Point yangu kubwa ni kwa haya mabadiliko yani ni vyema haya mabadiliko waangalie mtu alieagiza gari kabla ya haya mabadiliko waendelee tu na utaratibu wa awali, ili mabadiliko yaanze kwa watakao agiza gari kipindi hichi
 
Huko CCM kumesheheni wezi, walaghai, matapeli na wehu tupu.
 
Namhurumia staff mwenzangu kaagiza BMW X6

Watakachomfanya TRA hataamini, mi niko kwenye kikokotoo chao hapa namzooom[emoji134][emoji134]
... Itabidi aka-top up mkopo kupata fedha za kuwalipa TRA. Of course inategemea kama take-home yake bado inaruhusu otherwise kilio cha samaki.
 
Point yangu kubwa ni kwa haya mabadiliko yani ni vyema haya mabadiliko waangalie mtu alieagiza gari kabla ya haya mabadiliko waendelee tu na utaratibu mwingine, ili mabadiliko yaanze kwa watakao agiza gari kipindi hichi
... Mkuu style ya ufanyaji kazi ya TRA ni kuviziana; kushindwa kwa mlipa kodi ndio fahari yao. Na usikute wamelia timing makusudi kipindi hiki ili wanase wengi kwani kule Japan Novemba na Desemba ni kipindi wanaita BIG SALE.

Wana clear stock zao wanauza kwa bei chee so wabongo wengi wanavizia pia msimu huo. Kumbe monster mfilisi wananchi anawacheki tu kwa jicho baya la husda. Na atanasa wengi.
 
Tuwakomalie wabunge wabadilishe hizi kodi za enzi za ujamaa kwenye magari. Japo unasema unalinda mazingira lakini kodi kubwa hivyo kwenye mtumba una viwanda vya magari?
Gari ni kitu kinachosaidia kukuza uchumi. Ingekuwa ni amri yangu ningeweka kodi karibu na sifuri. Kwenye magari ya kazi kama pickup na fuso watu wangenunua bila ushuru hata mia, ikiwezekana nawapa na hela ya asante😀😀

Kulalamika haya mambo haitusaidii kitu. Inabidi wabunge, wanasheria nk walifanyie kazi.
Wabunge wa chama gani wafanye hiyo kazi, wakati Upinzani wote umefutiliwa mbali huko bungeni?
 
Back
Top Bottom