TRA yampiga faini ya 3,500,000 dereva kisa kapakia tenga 27 za nyanya

Unafahamu geti la mwisho la ushuru wa mazao unapotoka mkoani kuingia Dar????


Halafu faham kuna vitu vinaitwa Bahati wakati mwingine.
Kwa mfano kuna jamaa yangu karibia Mara tatu hajawahi kusimamishwa na TRA , na akawa anasema Hayo mambo ni uzushi na kutuambia sisi ni waongo. Lakini siku yalipomkuta alijifanya chizi Kwamba sukari yake inataka kushuka , alichoambiwa ikishuka tutakupeleka hospital na Hii Gari itakwenda yadi kwetu.
Kikubwa mkuu jipange unapokuwa road Hayo mambo ya kubishana kuhusu agizo la raisi Fanya ukiwa umebeba mahindi au maharagwe. Lakini Sio Mali kuoza..



Imagine unabishana na wakata ushuru kuhusu boksi 27 Kwamba hazikatiwi ushuru raisi Kasema coz hazizidi tani moja halafu ni Mali kuoza. Jitahidi kujiongeza unapokuwa msafiri.
 
Kuingia uchumi wa Kati lazima tujizatiti ili kusonga mbele, hivyo haya mengine tuvumiliane.
 
Tatizo lipo kwenye risiti ya usafiri kwa maana ya Kodi ya kile alicholipa mwenye mzigo kwa ajili yakusafishiwa mzigo wake. Risiti ya ushuru ni kitu kingine ndo maana fine imamhusu dereva maana yeye ndo angepaswa kuwasiliana na tajiri yake amtumie risiti hata kwa whatsup.
Watendaji wa vijijini siku hizi wana EFD machine?
Tangu lini?
Je ni Wote nchini au wa mijini tu?

Unajua nature ya kazi za dereva wa masafa marefu?

Je ni rahisi kwake kutafuta mtendaji wa kijiji alipo apatiwe risiti?
 
Huku kwetu watendaji wote wanazo mashine ukibeba mchanga, komoto, mawe, mbao na mazao ya biashara.
Watendaji wa vijijini siku hizi wana EFD machine?
Tangu lini?
Je ni Wote nchini au wa mijini tu?

Unajua nature ya kazi za dereva wa masafa marefu?

Je ni rahisi kwake kutafuta mtendaji wa kijiji alipo apatiwe risiti?
 

Kuna mabasi ya abiria kibao yanasafirisha abiria bila ticket, mbona hawafanyiwi hayo, niliwahi kutoa mfano wa mabasi ya Moro - Dar,
Kila nusu saa kuna bus linatoka stand Dar na Morogoro, hii ina maana kwa siku kuna mabasi 24 ya kampuni moja, kila bus linazidisha abiria 6 mpaka 8 bila ticket na nauli yao ni 8000, kwa maana hiyo 8000*8=64000 kwa route moja kwa bus, kisha zidisha mara idadi ya mabasi kwa siku ni kiasi gani kinakwepwa kulipiwa kodi kutokana na abiria kutopewa ticket?
 
Logic yako nini katika haya maelezo yako??
Maana naona Uko out of topic kabisa
 
Ndio sababu tunasema sheria kandamizi , hapo ni dereva amejiongeza kubeba mzigo wala tajiri hajui , lakini anaadhibiwa tajiri kwa kosa la mwajiriwa, ungetegemea apewe adhabu dereva kwenye Tin yake. Ili kila mtu awajibike kwa kosa lake .

Hzi faini zinapunguza Sana morale ya kufanya biashara ipo siku Tra watajikuta hawana mtu wa kumtoza kodi maana watu wataamua kuacha biashara kutokana na sheria kandamizi
 

Mwenye gari/mmiliki hamuruhusu dereva kubeba mizigo ya ziada. So ni kosa tyr anamponza mmiliki kumbuka anaelipa fine ni mmliki na sio dreva
 
Mwenye gari/mmiliki hamuruhusu dereva kubeba mizigo ya ziada. So ni kosa tyr anamponza mmiliki kumbuka anaelipa fine ni mmliki na sio dreva
Ndio sababu nikasema sheria ilitakiwa imbane mwenye kutenda kosa ,sio kumbebesha mmiliki mafaini amabayo hajui hata ilikuwaje
 
Ndio sababu nikasema sheria ilitakiwa imbane mwenye kutenda kosa ,sio kumbebesha mmiliki mafaini amabayo hajui hata ilikuwaje

Hivi mfano wewe ni baba na una mtoto, mtoto wako akikutwa na hatia nan atahusika??
 
Sasa mimi kama dereva nikiamua kumsaidia mzee wangu kumsafirishia tenga zake za nyanya pia nalazimika kutoa hizo risiti za efd?
 

Sasa hapo dereva ana biashara gani mpaka awe na mashine ya EFD? Kubeba hizo tenga alijiongeza tu kupunguza maumivu ya safari na ndiyo maisha yao madereva kwa mizigo midogomidogo kama hiyo akipakia anapata chochote
 
Hivi mfano wewe ni baba na una mtoto, mtoto wako akikutwa na hatia nan atahusika??
Mkuu kun mzazi amewahi kufungwa kwa kosa la mwanae?
Kinondoni na mwananyamala angebaki mzazi kwa mateja waliojazana pale?
Kosa la dereva lilitakiwa liwe la dereva na la tajiri kivyake
 
Wauza nyanya wana EFD? Hivi tukienda sokoni kununua nyanya tudai EFD? TRA waende wakawape wachuuzi wa sokoni wawe wanatukatia EFD receipts!!!!
 
Wauza nyanya wana EFD? Hivi tukienda sokoni kununua nyanya tudai EFD? TRA waende wakawape wachuuzi wa sokoni wawe wanatukatia EFD receipts!!!!
Jitahidi kusoma the whole thread Utapata majibu zaidi.


Inaonekana ni mvivu wa kusoma ngoja Nikusaidie Kidogo.
Mmiliki yeyote wa Gari ( Tandam, single ,mende ,kichanja. Etc) ni Lazima awe na EFD machine . narudia tena ni Lazima. Ambapo Huyo Dereva either anakuwa nayo hapo hiyo EFD machine au inakuwa kwa mwenye gari .
Kwa hiyo Dereva ni Lazima amkatie mteja wake receipt.
Na Wewe kama mfanyabiashara ukinunua mzigo kwa wachuuzi wadogo wadogo Unatakiwa wakupe receipt ya EFD machine . na hiyo receipt Unapata kwa watendaji wa vijiji ndo wanayo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…