TRA yampiga faini ya 3,500,000 dereva kisa kapakia tenga 27 za nyanya

TRA yampiga faini ya 3,500,000 dereva kisa kapakia tenga 27 za nyanya

Huyo dereva aache kazi atafute namna nyingine tu ya kuishi, pia serikali itumie busara, jamani, sasa nyanya zinakuwa bei nafuu sababu ya kujiongeza katika usafirishaji, vinginevyo vyakula vitakuwa bei juu sana na wananchi watateseka, busara itumike
Zitaozea shambani.
Bongo michosho sana
 
Sio muumin wa Hii serikali ila ukweli Lazima usemwe.kwa hilo swala lako Dereva ana makosa kwasababu alitakiwa amkatie risiti ya EFD Huyo mteja wake ya huo mzigo.

Kwa hiyo Kosa hapa liko kwa dereva . Kwanini hakumkatia risiti ya EFD mashine Huyo mteja wake?
Wacha limkute
Mashine ni ya ofisi, sio ya dereva na dereva kajiongeza na huku kujiongeza ndio hufanya vyakula viwe bei nafuu hata wanyonge wanaweza kumudu kula, sasa tukikaza kila kona hadi kwenye vyakula tutaumiza wanyonge, busara iwe inatumika.
 
Imefika hatua waanze Kukata risiti. Ukipakia tenga moja kata risiti. Ujanja ujanja haupo tena. Hii ilipelekea wenye magari kuibiwa
 
Tenga 27 kwa bei ya juu kabisa ya mwezi uliopita ni 675,000 Tsh.

Faini inapigwa 3,500,000. Mfano angelipa kodi ilitakiwa iwe shilingi ngapi?

Kuna miongozo ya faini? Mfano thamani ya kipi inaangaliwa mpaka kuamua mzigo wa 675,000 faini iwe 3,500,000?
Mkuu iwe Tandam, singo au canter Dereva unapopakia mzigo ni Lazima umkatie risiti mteja wako na hayo magari ni lazima yawe na EFD mashine. Kwa mfano ukiwa unatoka mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Tabora, Singida na Manyara kuja Arusha na Moshi utakutana na TRA pale Makuyuni. Bila hiyo risiti hampiti hapo.

Na wewe kama mwenye mzigo pia unakaguliwa kama una risiti ya ushuru yenye jina lako pamoja na leseni ya biashara unayofanya. Bila hivyo vitu hupiti hapo.
 
Ushindwe na ulegee sana hadi mawazo haya mabaya yakutoke kichwani, kisha ujazwe mawazo mema kwa manufaa ya watanzania wote.
====
Na mpa pole huyo dereva. Hata hivyo, TRA wawe wanafanya kazi kwa kutoa elimu ya kutosha juu ya sheria zote zinazoboreshwa juu ya kodi na makato mengine. Si busara wwla hekima kuficha elimu ya sheria kwa wahusika ili uwavizie kuwatoza faini! Kuna na "mfuko mwingine wa masuala ya wafanyakazi wa viwandani", nao ulikiwa na mtindo wa namna hii lakini nadhani umeishajirekebisha.
Hao madereva wanajua kila kitu. Hapo huwa wana- gamble kama aliyebeba pembe za ndovu.
 
Rais alisema kama mzigo wako haijavuka tani moja usilipe kodi.
Na karudia rudia mara kibao.

Kwa hio sijaelewa.
Au yale yalikuwa maneno ya majukwaani???
Alisema kama una mzigo chini ya tani moja usilipe ushuru
 
Hili ni Kati ya masuala tata sana.
Kodi muhimu na kodi hii ipo kisheria.

Lakini upande wa pili wa shilingi kodi hizi kwenye usafiri wa mazao ya chakula utaongeza ugumu wa maisha na kushusha kipato cha wakulima wa mazao ya chakula, matunda na mboga mboga, maana madereva sasa hawatathubutu kubeba mizigo midogo kama hiyo njiani. Mazao yatawaharibikia na masokoni kutakuwa na upungufu wa bidhaa kisha bei zitapanda kama ilivyouzwa 1kg ya vitunguu kwa 10,000/- wakati wa Corona.

Lakini tujiulize, kama mwenye mgahawa anatakiwa atoe risiti ya EFD akiuza kitu cha chini ya 30,000 mfano kahawa cupuccino au juice au kuku nusu au Samosa(sambusa) kwanini mwenye kusafirisha mzigo na kutoza 70,000/- au 100,000/- asitoe risiti ya EFD?

Hapa madereva waongee na matajiri wao watembee na EFD na hii pesa ya mizigo ya juu kwa juu wapewe commission kubwa nje ya mishahara yao ili kuwaongezea kipato na kupunguza ugumu wa maisha.

Au
Njia ya pili ambayo mmiliki wa gari si lazima ahusishwe au ajue gari yake ilibeba mzigo wa juu kwa juu.

Kuwe na maafisa wa TRA ambao si wala rushwa wakikutana na mzigo kama huo wanakata kodi halali (yenye uwiano sahihi) kwa huo mzigo, wanatoa risiti ya EFD na gari inaendelea safari.

Kurahisisha zoezi hili na kuepuka udanganyifu wa madereva kuhusu bei walitoza kusafirisha mizigo inabidi TRA waweke vituo vidogo kama check-points au mfano wa vile vya maliasili barabarani kila Kijiji au umbali flani ambapo hapo wenye mizigo na madereva watapakilia hii mizigo na mbele ya hao afisa wa forodha.

TRA inaweza kuweka hata mawakala kwenye vituo hivi kupunguza gharama za kuajiri watu wengi.
Hakuna haja ya ku- centralize kila kitu.

Hivi vituo pia vinaweza kuwa kama vile masoko ya madini Kila wilaya.
Mkulima kazi yako kutoa mzigo wa mazao shamba na gari ndogo kisha kufikisha kwenye vituo hivi. Iwepo na miundombinu ya kusaidia baadhi ya mazao haya yasiharibike yakisubiria usafiri.

Serikali isihusike kabisa kupanga bei ya usafiri wa hii mizigo, hiyo iwe mapatano ya mwenye mzigo na dereva.

Nafikiri haya ndiyo mawazo yangu ambayo si lazima niwe sahihi.
 
Rais alisema kama mzigo wako haijavuka tani moja usilipe kodi.
Na karudia rudia mara kibao.

Kwa hio sijaelewa.
Au yale yalikuwa maneno ya majukwaani???
Lile ni tamko tu, ila halibadilishi nguvu ya sheria waliyonayo hao jamaa
 
2345690.jpg
 
Siku chache zilizopita niliandika kueleza ugandamizwaji unaofanywa na TRA uliomuhusu dereva mmoja wa semi ambae alipigwa faini ya 3,000,000/= kisa kapakia tenga 20 za parachichi na alipoulizwa risiti ya transport hakuwa nayo kwani mzigo ule haukuhusu ofisi,ilikuwa ile kawaida ya madereva kujiongezea kipato kwa vimizigo vya njiani ambacho kilimponza akapoteza ajira.

Sasa huyu ni muendelezo wa vitimbi vingine kwani dereva mwingine amepigwa faini ya 3,500,000/= kisa kapakia tenga 27 za nyanya na alipoulizwa risiti ya transport hakuwa nayo. Dereva huyu analazimika kukatwa hii pesa na ofisi kwenye mshara mpaka deni litakapoisha.

Kwakweli kama hizi ndio sheria zilizotungwa kwa ajili ya kutetea wanyonge basi hiki ni kituko.

Hivi mshahara wa raisi ni sh ngapi,mawaziri pesa ngapi,wabunge je?Hawa hawatusikii kwakuwa wao wanalipwa pesa ndefu,hivi dereva mwenye mshahara wa laki tatu kwa mwezi atakatwa hilo deni mpaka lini?

Ushauri wa bure ni kwamba;hii miradi mikubwa ilioanzishwa nchini inasababisha mateso kwa raia,ni bora tukarudi kwenye mgao wa umeme kuliko haya maisha ya karaha tunayoishi sasa.

Kwakweli nachuma dhambi ila kama Mungu anasikia vilio vyetu basi.
Uchumi wa Kati. Hamsomi washamba mnapiga makofi bila kujuwa mnapigia nini.
 
Mashine ni ya ofisi, sio ya dereva, na dereva kajiongeza, na huku kujiongeza ndio hufanya vyakula viwe bei nafuu hata wanyonge wanaweza kumudu kula, sasa tukikaza kila kona hadi kwenye vyakula tutaumiza wanyonge, busara iwe inatumika
Ni kweli Dereva kajiongeza sahihi kabisa ila ndio kakutana na sheria sasa
 
Wakulima nao Wana EFD?.
Mzigo unatoka shamba efd inatoka wapi?
Sio muumin wa Hii serikali ila ukweli Lazima usemwe.kwa hilo swala lako Dereva ana makosa kwasababu alitakiwa amkatie risiti ya EFD Huyo mteja wake ya huo mzigo.

Kwa hiyo Kosa hapa liko kwa dereva . Kwanini hakumkatia risiti ya EFD mashine Huyo mteja wake?
Wacha limkute
 
Side effects ya hili jambo wafanyabiashara kutokuweka pesa benki, hatimaye benki kuyumba kiuchumi!

Ndio maana wahindi na Wachina hawaweki pesa benki, pindi akipata pesa ananunua dola anaficha ndani.
Hata Mimi siweki pesa benki.
Unaweka laki benki yaani sehemu ya usalama. Ukienda kuicheki baada ya miezi kadhaa unakuta imekatwa umebakiziwa 78,000.
Sasa hiyo benki Ni sehemu salama ya kuhifadhi pesa au utopolo??
 
Ushindwe na ulegee sana hadi mawazo haya mabaya yakutoke kichwani, kisha ujazwe mawazo mema kwa manufaa ya watanzania wote.
====
Na mpa pole huyo dereva. Hata hivyo, TRA wawe wanafanya kazi kwa kutoa elimu ya kutosha juu ya sheria zote zinazoboreshwa juu ya kodi na makato mengine. Si busara wwla hekima kuficha elimu ya sheria kwa wahusika ili uwavizie kuwatoza faini! Kuna na "mfuko mwingine wa masuala ya wafanyakazi wa viwandani", nao ulikiwa na mtindo wa namna hii lakini nadhani umeishajirekebisha.
Naungana nawe, watoe elimu, watoe matangazo, watu waelewe!
Siyo watumie mianya ya wao kujielemisha bila kuelimisha walipa kodi, kuwakomesha walipa kodi!

Everyday is Saturday................................😎
 
Back
Top Bottom