TRA yaweka Rekodi Mpya. Yakusanya Trilioni 7.79 kati ya Julai na Septemba 2024

TRA yaweka Rekodi Mpya. Yakusanya Trilioni 7.79 kati ya Julai na Septemba 2024

Hatuna haja ya hizo takwimu, tuna haja ya kuona maisha ya wananchi yanaboreshwa, watu wapate maji, umeme, barabara, huduma bora za afya, maslahi bora kwa watumishi, wananchi waweze kumudu gharama muhimu nk.
 
Waongo Hawa ,malengo yanavukwa ila wafanyakazi increments za 20,000 hawawezi TRA iache usaniiiii
 
Mi nacheka tu kupitia hasira Kali za nyumbu wa mbowe (haters wa mama Samia, The Mother of Modern Tanzania). Hujawa na hasira Kali mno Kila wasikiapo fanikio lolote la mama Samia. Kwakweli Wana Hali ngumu.
 
Hongereni ila sasa na matumizi nayo yangekua yapo sawa ningekua nawaelewa na hii rekodi yenu ila kwenye matumizi huko ndio mtihani tukisubiri taarifa ya CAG.
Na pia kwa hizi kodi kubwa za magari mtavunja rekodi mpaka mnaenda motoni.
 
Hatuna haja ya hizo takwimu, tuna haja ya kuona maisha ya wananchi yanaboreshwa, watu wapate maji, umeme, barabara, huduma bora za afya, maslahi bora kwa watumishi, wananchi waweze kumudu gharama muhimu nk.
Huduma za kijamii,ujenzi wa barabara,maslahi kwa watumishi wa umma kwa sasa bali ni nzuri sana.
 
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA), imesema imefanikiwa kukusanya kiasi cha Sh. Trilioni 7.79 ambayo ni sawa na ufanisi wa asilimia 105 ya lengo iliyokuwa imejiwekea ya kukusanya Sh. Trilioni 7.42 katika kipindi cha miezi mitatu (julai -Septemba) kwa mwaka wa fedha 2024/2025.

Kamishna Mkuu TRA Yusuph Mwenda amesema ufanisi huo umefanya kuvuka lengo la kila mwezi kwa miezi yote mitatu.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam jana Oktoba Mosi, 2024 Mwenda amesema katika kipindi cha mwezi Septemba mwaka wa fedha 2024/25, TRAi ilifanikiwa kukusanya kiasi cha Shilingi Trilioni 3.02, sawa na ufanisi wa asilimia 105 ya lengo la kukusanya Shilingi Trilioni 2.88.

"Makusanyo haya ni ya kiwango cha juu kabisa cha ukuaji wa asilimia 77.6 kuweza kukusanywa na TRA katika mwezi Septemba, ndani ya kipindi cha miaka mitano tangu mwaka 2020/21,"amesema Mwenda.

Ameongeza kuwa, ufanisi katika makusanyo yote umechangiwa na maagizo yaliyotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan, ya kuendelea kuhamasisha ulipaji kodi wa hiari nchini kwa kushirikiana na walipakodi, kuwasikiliza na kutatua changamoto zao pamoja na kukua kwa uchumi wa nchi na ongezeko la wawekezaji kutokana na uwepo na usimamizi wa sera nzuri za uwekezaji za serikali ya awamu ya sita.

Aidha amesema sababu nyingine ni kukua kwa ushirikiano na mahusiano kati ya TRA na walipakodi wote nchini kwa kuendelea kulipa kodi kwa hiari na ushirikiano mkubwa na mahusiano mazuri wanayoendelea kupokea kutoka kwa viongozi wa vyama vya wafanyabiashara wote nchini.

Amesema, Utendaji kazi mzuri, bidii na kujituma kwa watumishi ikiwemo kuwatembelea walipa katika sehemu zao za biashara siku za mapumziko (Jumamosi na Jumapili) na kutatua changamoto zilizopo kumesaidia katika zoezi hilo kwani ushirikiano huo wa umewezesha zoezi zima la ukusanyaji wa mapato ya Serikali.

Sambamba na hayo, kuendelea kuboresha mahusiano baina ya serikali na wafanyabiashara ikiwemo kutenga siku ya Alhamisi ya kila wiki kuwa ni siku maalum ya Kusikiliza Walipakodi' kupitia ofisi zote za TRA nchini kutaongeza hamasa ya walipa kodi kutimiza wajibu wao kwa hiari.

"Kuongezeka kwa usimamizi wa wafanyakazi kwa kukemea vitendo vya uvunjifu wa maadili ikiwemo kukemea vikali vitendo vya rushwa na kuchukua hatua kwa wanaopatikana na kuthibitika kuhusika katika vitendo hivi, kufuatilia na kuchukua hatua za haraka za kutatua changamoto za walipakodi wanazowasilisha moja kwa moja kwenye ofisi ya Kamishna Mkuu kupitia TRA SIKIKA APP iliyozinduliwa mwezi Agosti 2024," amesema Mwenda

Pia Mwenda amesema kuendelea kuimarisha mazingira ya ufanyaji biashara na uwekezaji nchini kwa kuhakikisha marejesho ya madai ya kodi yanafanyika kwa wakati ili kufanikisha fedha hizo kurejeshwa kwenye mzunguko wa shughuli za kiuchumi nchini kumesaidia ongezeko kubwa.

"Kuendelea kutekeleza kwa vitendo maelekezo yaliyotolewa na Serikali ikiwemo la utengenezaji wa mfumo wa kurahisisha ugomboaji wa mizigo inayoingia kwa utaratibu wa ufungishaji wa mizigo (consolidation).Kuendelea kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara nchini kwa kusimamia kikamilifu bidhaa nane ambazo zimewekewa bei elekezi (vitenge, mashati, nguo zingine, vipodozi, vito vya thamani, nguo za ndani, leso na vesti) na ni sababu iliyochangia,"amesema Mwenda.

 
najiuliza tu hivi hizi taarifa sijui ni ripoti haziwezi kukamilika bila kumtaja kiumbe anayeitwa raisi? kwani yeye ndio anafnya kila kitu? nilishawahi kusema ukiona kiumbe mmoj tena wakike anatajwatajwa mara nyingi kuliko Mwenyezi Mungu ujue hiyo nchi ina shida tena kubwa sanasana.
Ndio haziwezi kukamilika Kwa sababu Watendaji wanatekeleza sheria na maono ya Rais.

Yeye ndio aliwaambia sitaki Kodi za dhuluma na mara kadhaa wakigoma Huwa unaona viongozi wanaleta Maelekezo ya Rais.

Sasa wewe akitajwa unaumia wapi? Mbona mkiandamana Huwa mnamshutumu Rais ila kwenye mafanikio hamtaki atajwe?

Punguza chuki na upuuzi
 
Bila kutoa mchanganuo wa Hilo ongezeko inakuwa vigumu mtu kuona matokeo hata chanya au hasi yametokana na nini.
Kuongezeka kwa mapato, au kupungua kwa thamani ya shilingi , kuongezeka kwa vyanzo vya kodi, au idadi ya walipa kodi.
Kupungua Kwa thamani ya Shilingi kunaongeza vipi makusanyo ya serikali?

Kwamba hujui kilichosababisha Mapato kuongezeka? Hujasoma taarifa ya TRA?

Kuna ufanisi yaani kukaba mianya ya wakwepa Kodi

Kuna ongezeko la ulipaji Kodi Kwa hiari na

Kuna ongezeko la shughuli za kiuchumi kuanzia Utalii,Usafirishaji, biashara,Ajira ,Kilimo ,viwanda nk vyote hivi vinaongeza Mapato ya Serikali.
 
Hongereni ila sasa na matumizi nayo yangekua yapo sawa ningekua nawaelewa na hii rekodi yenu ila kwenye matumizi huko ndio mtihani tukisubiri taarifa ya CAG.
Na pia kwa hizi kodi kubwa za magari mtavunja rekodi mpaka mnaenda motoni.
Onyesha huo mtihani kwenye matumizi na Mimi nikuonyeshe matokeo ya ongezeko la Kodi.
 
Kupungua Kwa thamani ya Shilingi kunaongeza vipi makusanyo ya serikali?

Kwamba hujui kilichosababisha Mapato kuongezeka? Hujasoma taarifa ya TRA?

Kuna ufanisi yaani kukaba mianya ya wakwepa Kodi

Kuna ongezeko la ulipaji Kodi Kwa hiari na

Kuna ongezeko la shughuli za kiuchumi kuanzia Utalii,Usafirishaji, biashara,Ajira ,Kilimo ,viwanda nk vyote hivi vinaongeza Mapato ya Serikali.
Mfano Kodi za kuingiza bidhaa iwe mafuta ya kupikia au ya kuendeshea mitambo. Kwa hiyo wewe Ndio hujui vyanzo vya mapato na matokeo ya pesa kukosa thamani dhidi ya Fedha za kigeni
 
Jamani !
Umenikumbusha Maneno ya Zito Kabwe enzi za uongozi wa JPM 😀😅
Siku hizi Zito Kabwe anaona mambo yanaenda Sawa sawa au vipi?!

Salamu zimfikie popote alipo.

Kwamba ako ana-observe table manners 😆😆😆
Zito yupo kwa sasa chama chake ni tawi la CCM
 
Back
Top Bottom