TRC mnazua taharuki na madaraja yenu! Kwa hili mmetukosea sana wananchi

TRC mnazua taharuki na madaraja yenu! Kwa hili mmetukosea sana wananchi

Uzio huo hauna miaka 2 ngoja waturuki waondoke utakatwa wote.
Wao wangeweka matobo ya kupita watu chini ya reli ingesaidia kudumisha huo uzio
 
TRC - shirika la reli Tanzania kwakweli mmekuwa kero Kubwa sana kwasasa! Tunaheshim sana kazi mnayofanya lakini nyie hamtuheshimu WANANCHI wa Tanzania.

1. Mmeziba Barabara zoote za waenda kwa miguu, mkilazimisha watu wapite juu ya MADARAJA ambayo kiuhalisia bado hayajakamilika kujengwa. Hakuna alama ya wapita kwa miguu hakuna alama za barabarani! Hata fence juu ya MADARAJA hazijakamilika mnataka watu wadondoke wafe ndo akili iwakae sawa. Au mnataka ajali zitokee ndo mrekebishe.

2. Mmeziba Njia zoote za wapita kwa miguu mnawalazimisha wapite kwenye matobo ya chini kabisa! Huu si ubinadamu Wala ustarabu mmezingua kinoooma yaani apo.

3. Mmezingatia na watu wenye ulemavu au mnajifikiria nyie tu kuziba hizo njia, wajawazito je? Wazee je? Kwani nyie mnamatatizo gani mbona hamsomeki.

Solution: wekeni utaratibu mzuri toweni uzio huo woote, tengenezeni Railway cross nzuri.

Tuache hayo Mambo ya kizaman bhna hata Kama treni ni jipya haimaanishi mfanye mnavyotaka.

Maeneo: Majumba sita, Airport, mpaka gongo la mboto na maeneo mengine ambyo siyajui.

ASANTEN
Nchi nzima hata mijini na wilayani ipitayo reli kilio the same wamezuia watu kuvuka bila kuwawekea matobo chini ya reli
 
Ni ngumu kutoa uzio kwenye hii reli, mtazoea tuu kupanda na kushuka vivuko, ni safe zaidi kuliko kuiacha wazi
Wataingia gharama sana kurejeshea uzio kila mara pindi watu wakikata.
Mfano gongo la mboto wananchi walikata uzio wapite
 
Watanzania ni walalamishi tu. Reli imewekwa fence route nzima na wameacha sehemu maalum za kuvuka aidha juu au chini ya reli. Hawa waungwana wanataka wavuke popote pale halafu wakigongwa na hio treni watalaumu kama wanavyogongwa na mabasi ya mwendokasi.
Umbali wa vivuko sio rafiki kwa wakazi wa eneo husika
 
Wa kulaumiwa hapa ni mainjia wetu wao wanakaa masaki osterbay hawajui hadha wapatao wakazi wa huko.
Sijui walisomea wapi hivi unaziba vipi mji kwa wavu pande mbili bila kuweka vivuko vya miguu ili maisha ya wengine yaendelee.
Wanataka wapewe sifa na viongozi
 
Ana kitambi afu kalewa, dah sio poa.
Ukilewa hutoboi, maana Kwanza Kuna ka ngazi ka mchongo kushukia huko chini, halafu Kuna madimbwi pale lazima ukanyage mawe kadhaa kufika sehem kavu, then ubend kuelekea langoni, 😂😂😂😂 daah
 
Huo uzio walioweka TRC umepunguza mapato ya treni la mwakyembe ng'ambo ya pili wanashindwa kupanda tren kwa sababu ya fence ili apande treni anahitaji kupita vituo vitatu vya daladala ili akapate sehemu ya kupanda mwakyembe.
So kama TRC walimudu kubeba abiria elf 25 kwa siku Leo hata elf kumi hawafiki sababu ya fence hii imeathiri mapato yao kwa siku wapatayo toka kwa nauli ya mwakyembe.
Wanaweza kuwarudisha abiria hao 15 elf waliopotea kwa kuweka vipito salama yaani matobo au vipenyo chini ya reli kwenye mapitio asili ya watu.
Pale Ukonga wananchi wamezuiliwa haki ya msingi kumudu kupata hudumq za kijamii mfano nyumba za Ibada makanisa na misikiti ipo upande wa pili wa uzio.
 
Huo uzio walioweka TRC umepunguza mapato ya treni la mwakyembe ng'ambo ya pili wanashindwa kupanda tren kwa sababu ya fence ili apande treni anahitaji kupita vituo vitatu vya daladala ili akapate sehemu ya kupanda mwakyembe.
So kama TRC walimudu kubeba abiria elf 25 kwa siku Leo hata elf kumi hawafiki sababu ya fence hii imeathiri mapato yao kwa siku wapatayo toka kwa nauli ya mwakyembe.
Wanaweza kuwarudisha abiria hao 15 elf waliopotea kwa kuweka vipito salama yaani matobo au vipenyo chini ya reli kwenye mapitio asili ya watu.
Pale Ukonga wananchi wamezuiliwa haki ya msingi kumudu kupata hudumq za kijamii mfano nyumba za Ibada makanisa na misikiti ipo upande wa pili wa uzio.
Asante kwa kuliona Hilo na una maoni mazur san
 
Back
Top Bottom