Castr
JF-Expert Member
- Apr 5, 2014
- 35,012
- 70,201
Ni usiku wa manane Ronnie Jr anasikia makelele baba na mama yake wanabishana. Anawafuata sebuleni anakuta damu zimesambaa sebule nzima, baba yake ameshikilia bunduki aina ya shotgun kumuelekea mama yake.
Baba, Ronnie Oneal, alipoona mwanae amefika pale akamuamrisha atembee kuzunguka sebule huku akiwa anasema 'Allah Akbar' vyanzo vinatofautiana, vingine vinasema muda huu Kenyatta alikimbilia kwenye chumba cha mwanae wa kike ambaye ni mlemavu na vyanzo vingine havisemi hili.
Ila vyote vinakubaliana kwamba muda huu ndiyo Mama, Kenyatta Barron, akapata nafasi ya kupiga namba ya dharura, 911.
Kenyatta enzi za uhai wake.
Katika tape iliyosikilizishwa mahakama anasikika Kenyatta akiongea:
'Nimepigwa risasi' sauti ni ndogo kama vile ananong'ona.
'Nisaidie tafadhalia nimepigwa risasi nisaidie tafadhali'
Hakimu anasema katika kesi alizowahi kushiriki hii ni ya kikatili kuliko zote. USA kesi za risasi ni kila siku hivyo inafanya ujiulize ni nini cha ziada kwenye hii kesi ya Kenyatta Barron.
Kwenye recording anasikika Oneal akiongea kwa kelele 'Allah Akbar' kisha anasikika akisema 'Njoo hapa umuue huyu malaya haraka'
Kenyatta anasikika akimwambia Oneal:
'Ronnie basi, nisamehe' anaendelea kuongea 'Nisamehe, nisaidie umenipiga risasi mkononi'
Baada ya muda kidogo inasikika sauti ya mwanaume (Ya Oneal) ikisema:
'Hauelewi'
'Ameniua huyu'
Kisha unasikika ukunga. Hakimu anasema 'Huu ni ukunga wa mtu anayejua leo ni siku yangu ya mwisho kua hai'
Kisha Oneal akamuamrisha mwanae aje ashiriki katika kumuua mama yake. Ronnie Jr mbele ya baba ambaye ameshakua mkali na ana bunduki hakua na jinsi, akaungana na baba yake.
Baba akamwambia Ronnie Jr waishike bunduki kwa pamoja na washoot kwa pamoja. Kwenye tape kinasikika kishindo lakini inaaminiwa siyo cha risasi. Hakiwezi kua cha risasi kwa kua shotgun iliishiwa risasi.
Oneal akamuamuru mwanane akalete kisu ili waje kummalizia Kenyatta.
Ronnie Jr akaenda kufuata kisu.
Huu muda wa kusubiri kisu Kenyatta akautumia kutoroka, akatoka nje ya nyumba akafika mpaka kwenye ngazi za jirani yao na hapo ndipo alipokamatiwa na Oneal. Oneal akatumia shotgun kumpiga nayo kichwani Kenyatta, alitumia nguvu kubwa kumpiga kwa hiyo shotgun mpaka ikavunjika vipande viwili na ikapinda.
Kisha akauburuza mwili kuurudisha ndani.
Ronnie Jr akiwa anatoa utetezi wake mahakamani anasema kisha baba akarudi na shoka akamfuata mdogo wake akamlaza kifudi fudi na kumkata kwa shoka nyuma ya kichwa.
Kutokana na hitlafu ya ubongo aliyonayo Ron'veya hata hakuleta upinzani. Kaka mtu anasema akashuhudia macho ya mdogo wake yakipinduka kurudi juu. Huo ukawa mwisho wa Ron'veya.
Ron'veya enzi za uhai wake.
Kisha baba, Oneal, akajaribu kuwachoma Ronnie Jr na Ron'veya ila hakufanikiwa, moto haukua mkubwa kama alivyotaka. Akachukua kisu na kumchoma Ronnie Jr.
Wapelelezi na majirani wanasema walidhani Ronnie Jr hatopona. Damu mwili mzima kiasi kwamba waliamini amechanwa matumbo.
Baada ya kumchoma kisu Ronnie na kuona amelala chini Oneal akatoka nje. Siyo ili atoroke, hapana, alitoka nje ili aichome nyumba nzima huku maiti za mkewe na wanae zikiwa ndani.
So akamwagia gasoline nyumba nzima na kuiwasha moto kisha sasa akatokomea.
Ronnie Jr, kwa ujasiri akajitahidi kujivuta mpaka nje. Akakutana na jirani yao ila akapoteza fahamu na akazindukia hospitali.
Kesi ikafunguliwa na Oneal akachagua kujiwakilisha mwenyewe, hakutaka wakili, katika ufunguzi Oneal anasema 'Mnaona kama nipo peke yangu ila Mungu mkuu yupo pamoja nami'
Oneal akiwa mahakamani.
Katika tukio zima aliyepona ni mwanae wa kiume na akiwa kama shahidi Oneal akawa anamhoji maswali Ronnie Jr. Katika wapelelezi wa kwanza kufika kwenye tukio mmoja amemuasilia Ronnie Jr, jina la aliyemuasili halijawekwa wazi kwaajili ya usalama wa mtoto.
Mahojiano yao yalifanywa kwa kupitia screen, Ronnie Jr anasema amekaa na mbwa ili kumtia nguvu ya kuhojiwa na baba yake.
His own father.
Baba anamuuliza 'Unayaonaje maisha siku hizi?' kisha anamuuliza 'Uliona nikimshoot mama yako?' Ronnie Jr anajibu 'Hapana' anamuuliza tena 'Uliniona nikimuua mdogo ako?' Ronnie Jr anajibu 'Hapana'
Kisha anamuuliza 'Nimewahi kukuumiza?' Ronnie Jr anajibu 'Ndiyo, ulinichoma kisu'
Ronnie Jr kulia.
Kwa kusema hapana Ronnie Jr alikua ameenda kinyume na maelezo aliyotoa polisi. Ila katika saiokolojia ni kawaida ya oppressed kubadili maneno ikatokea anaulizwa mbele ya oppresser kwakua oppressed subconsciously huamini oppresser ana mamlaka juu yake.
Mbaya zaidi tukio zima halina sababu iliyo wazi ya kupelekea Oneal kufanya alichokifanya. Baba yake Oneal anasema mwanae aliwahi kumuambia anasumbuliwa na paranoia, kama unataka mfano halisi wa paranoia ni kama Deo Kisandu anavyoamini serikali ya Tanzania inacontrol maisha yake.
Oneal anasema alimuua Kenyatta kwa kua Kenyatta alikua anataka kuwaua watoto na yeye alimuua ili kuwatetew watoto. Ni utetezi wa ajabu kidogo ukiangalia mazingira na maelezo ya tukio.
Hapa JF tuassume Kenyatta alimuua Ron'veya na Oneal akaingilia kati na kumshoot mkononi Kenyatta.
Kulikua na haja gani kumuamrisha Ronnie Jr azunguke huku akisema 'Allah Akbar'?
Kulikua na haja gani ya kumchoma kisu Ronnie Jr?
Kulikua na haja ya kujaribu kumchoma moto Ronnie Jr na Ron'veya?
Kulikua na haja ya kuichoma nyumba moto?
Haya maswali mahakama haikupoteza muda kujiuliza. Wakili wa serikali alikua amedhamiria hukumu ya kumuangukia Oneal iwe kifo. Oneal, supporter mzuri wa 'Death penalty', alikwepa kikombe hicho na amefungwa kifungo cha maisha.
Baba, Ronnie Oneal, alipoona mwanae amefika pale akamuamrisha atembee kuzunguka sebule huku akiwa anasema 'Allah Akbar' vyanzo vinatofautiana, vingine vinasema muda huu Kenyatta alikimbilia kwenye chumba cha mwanae wa kike ambaye ni mlemavu na vyanzo vingine havisemi hili.
Ila vyote vinakubaliana kwamba muda huu ndiyo Mama, Kenyatta Barron, akapata nafasi ya kupiga namba ya dharura, 911.
Kenyatta enzi za uhai wake.
Katika tape iliyosikilizishwa mahakama anasikika Kenyatta akiongea:
'Nimepigwa risasi' sauti ni ndogo kama vile ananong'ona.
'Nisaidie tafadhalia nimepigwa risasi nisaidie tafadhali'
Hakimu anasema katika kesi alizowahi kushiriki hii ni ya kikatili kuliko zote. USA kesi za risasi ni kila siku hivyo inafanya ujiulize ni nini cha ziada kwenye hii kesi ya Kenyatta Barron.
Kwenye recording anasikika Oneal akiongea kwa kelele 'Allah Akbar' kisha anasikika akisema 'Njoo hapa umuue huyu malaya haraka'
Kenyatta anasikika akimwambia Oneal:
'Ronnie basi, nisamehe' anaendelea kuongea 'Nisamehe, nisaidie umenipiga risasi mkononi'
Baada ya muda kidogo inasikika sauti ya mwanaume (Ya Oneal) ikisema:
'Hauelewi'
'Ameniua huyu'
Kisha unasikika ukunga. Hakimu anasema 'Huu ni ukunga wa mtu anayejua leo ni siku yangu ya mwisho kua hai'
Kisha Oneal akamuamrisha mwanae aje ashiriki katika kumuua mama yake. Ronnie Jr mbele ya baba ambaye ameshakua mkali na ana bunduki hakua na jinsi, akaungana na baba yake.
Baba akamwambia Ronnie Jr waishike bunduki kwa pamoja na washoot kwa pamoja. Kwenye tape kinasikika kishindo lakini inaaminiwa siyo cha risasi. Hakiwezi kua cha risasi kwa kua shotgun iliishiwa risasi.
Oneal akamuamuru mwanane akalete kisu ili waje kummalizia Kenyatta.
Ronnie Jr akaenda kufuata kisu.
Huu muda wa kusubiri kisu Kenyatta akautumia kutoroka, akatoka nje ya nyumba akafika mpaka kwenye ngazi za jirani yao na hapo ndipo alipokamatiwa na Oneal. Oneal akatumia shotgun kumpiga nayo kichwani Kenyatta, alitumia nguvu kubwa kumpiga kwa hiyo shotgun mpaka ikavunjika vipande viwili na ikapinda.
Kisha akauburuza mwili kuurudisha ndani.
Ronnie Jr akiwa anatoa utetezi wake mahakamani anasema kisha baba akarudi na shoka akamfuata mdogo wake akamlaza kifudi fudi na kumkata kwa shoka nyuma ya kichwa.
Kutokana na hitlafu ya ubongo aliyonayo Ron'veya hata hakuleta upinzani. Kaka mtu anasema akashuhudia macho ya mdogo wake yakipinduka kurudi juu. Huo ukawa mwisho wa Ron'veya.
Ron'veya enzi za uhai wake.
Kisha baba, Oneal, akajaribu kuwachoma Ronnie Jr na Ron'veya ila hakufanikiwa, moto haukua mkubwa kama alivyotaka. Akachukua kisu na kumchoma Ronnie Jr.
Wapelelezi na majirani wanasema walidhani Ronnie Jr hatopona. Damu mwili mzima kiasi kwamba waliamini amechanwa matumbo.
Baada ya kumchoma kisu Ronnie na kuona amelala chini Oneal akatoka nje. Siyo ili atoroke, hapana, alitoka nje ili aichome nyumba nzima huku maiti za mkewe na wanae zikiwa ndani.
So akamwagia gasoline nyumba nzima na kuiwasha moto kisha sasa akatokomea.
Ronnie Jr, kwa ujasiri akajitahidi kujivuta mpaka nje. Akakutana na jirani yao ila akapoteza fahamu na akazindukia hospitali.
Kesi ikafunguliwa na Oneal akachagua kujiwakilisha mwenyewe, hakutaka wakili, katika ufunguzi Oneal anasema 'Mnaona kama nipo peke yangu ila Mungu mkuu yupo pamoja nami'
Oneal akiwa mahakamani.
Katika tukio zima aliyepona ni mwanae wa kiume na akiwa kama shahidi Oneal akawa anamhoji maswali Ronnie Jr. Katika wapelelezi wa kwanza kufika kwenye tukio mmoja amemuasilia Ronnie Jr, jina la aliyemuasili halijawekwa wazi kwaajili ya usalama wa mtoto.
Mahojiano yao yalifanywa kwa kupitia screen, Ronnie Jr anasema amekaa na mbwa ili kumtia nguvu ya kuhojiwa na baba yake.
His own father.
Baba anamuuliza 'Unayaonaje maisha siku hizi?' kisha anamuuliza 'Uliona nikimshoot mama yako?' Ronnie Jr anajibu 'Hapana' anamuuliza tena 'Uliniona nikimuua mdogo ako?' Ronnie Jr anajibu 'Hapana'
Kisha anamuuliza 'Nimewahi kukuumiza?' Ronnie Jr anajibu 'Ndiyo, ulinichoma kisu'
Ronnie Jr kulia.
Kwa kusema hapana Ronnie Jr alikua ameenda kinyume na maelezo aliyotoa polisi. Ila katika saiokolojia ni kawaida ya oppressed kubadili maneno ikatokea anaulizwa mbele ya oppresser kwakua oppressed subconsciously huamini oppresser ana mamlaka juu yake.
Mbaya zaidi tukio zima halina sababu iliyo wazi ya kupelekea Oneal kufanya alichokifanya. Baba yake Oneal anasema mwanae aliwahi kumuambia anasumbuliwa na paranoia, kama unataka mfano halisi wa paranoia ni kama Deo Kisandu anavyoamini serikali ya Tanzania inacontrol maisha yake.
Oneal anasema alimuua Kenyatta kwa kua Kenyatta alikua anataka kuwaua watoto na yeye alimuua ili kuwatetew watoto. Ni utetezi wa ajabu kidogo ukiangalia mazingira na maelezo ya tukio.
Hapa JF tuassume Kenyatta alimuua Ron'veya na Oneal akaingilia kati na kumshoot mkononi Kenyatta.
Kulikua na haja gani kumuamrisha Ronnie Jr azunguke huku akisema 'Allah Akbar'?
Kulikua na haja gani ya kumchoma kisu Ronnie Jr?
Kulikua na haja ya kujaribu kumchoma moto Ronnie Jr na Ron'veya?
Kulikua na haja ya kuichoma nyumba moto?
Haya maswali mahakama haikupoteza muda kujiuliza. Wakili wa serikali alikua amedhamiria hukumu ya kumuangukia Oneal iwe kifo. Oneal, supporter mzuri wa 'Death penalty', alikwepa kikombe hicho na amefungwa kifungo cha maisha.