True story: Babu yangu kama mshikaji wangu

True story: Babu yangu kama mshikaji wangu

...62
Sasa unahisi nani anaefanya mambo haya na kwafaida gani? Nilimwuliza yunge,
Mh! Watu wakijiji hiki wakiamua kukuchezea hawana cha sababu wala nini, alijibu.
Sasa inakuwaje wanakuja kufanya michezo yao hapa wakati inasemekana babu ni kiboko yawote na anaogopeka kwa ulozi?
Kwanza nikwambie tu, babu yako sio mchawi kama wanavyovumisha watu, kinachotokea ni kwamba, yeye babu katika kilimo chake anawekaga zindiko ambalo hakuna kati ya wanakijiji wote anaeweza kulitegua ili aweke chuma ulete, badala yake ukimwekea chuma ulete utakua unamwongezea mazao yako shambani mwake bila wewe kujua,
Hivyo kitendo hiki hupelekea babu yako kuvuna mazao ya uhakika kila mwaka na kupelekea chuki kwa wananzengo dhidi yako nahapo huanza kuvumisha ni mchawi! Alieleza yunge na kuendelea,
Kuhusu hii michezo ya mapaka na mabundi ni mtu wa karibu na familia hii ambae na ukitaka nitakuonesha ila uwe na kifua usije ukayamwaga kwenye kuku wengi, alifafanua kwa kirefu na kunitazama kungoja ruhusa yangu ili kama nnakifua anioneshe...!
Kimya mzeee
 
...63
Nioneshe mpenzi wangu, kuhusu usiri hilo usiwe na hofu kwani mimi sio kilopolopo, nilimsihi.
Alinitaka nimgonje kisha akatoka na kuelekea nyumbani kwao, hakukawia, akarudi ndani ya dakika 5 huku amepakata vitu kwapani akiwa amejitanda nguo.

Njoo hapa twende, alinambia na tukaelekea sebleni, aliitoa nguo alokua amejitanda na kutoa upembe mfupi mweusi uliozungushiwa vitambala vidogo vyeusi na manyoya matatu yaliyoonekana kuwa ya kuku.
Alinifuta kwa kiganja chake usoni na kunitaka nisifumbue macho, kisha nilihisi kautupa ule upembe mbele yangu ambapo nilihisi uliangukia hatua moja kutoka nilipo simama.
Haya piga hatua moja mbele kisha fumbua macho, alinipa maelekezo,
Nilipiga hatua moja kisha nikafumbua macho.
Lahaula! Niliona kichaka mbele yangu, niliangaza macho huku na kule ambapo kote vilionekana vichaka vitupu, angani hakukuwa na mbalamwezi ila maajabu niliweza kuona umbali wa mita kama 200 hivi,
Ajabu nilikuwa peke yangu nisimwone yunge.
Khiii! Nikishindo kilisikika kushoto kwangu, alitu yunge pale.
 
...64
Hapa ni wapi? Nilimwuliza.
Hutakiwi kuongea zaidi ya kujibu na kufata maelekezo yangu, alisema yunge akimaanisha nisimwulize jambo mpaka ruhusa yake.
Nimekuleta huku kwa sababu nakupenda na wewe ndie utakuwa mme wangu pekee, hivyo nimeamua nikuoneshe siri za kijiji hiki na watu wake ili ufahamu unaishi na watu wenye tabia ipi! Kingine nataka uijue vizuri familia uliyofikia ili ujue namna ya kuishi nao, alieleza yunge kwa kina .
Nimekuamini na ndomaana nimekupa usichana wangu ila kilichonifurahisha zaidi ni mimi kuwa msichana wako wa kwanza kumjua, aliongeza.
Sasa hapa utawaona watu mbalimbali ambao wengine hutoamini, na kwayote watakayokuwa wanayafanya naomba uwe na roho ya chuma ujikaze kwani ukiweza kujikaza mpaka mwisho nitakuamini mara mia nane, alieleza na kuendelea,
Sasa twende ikingali mapema ili uone mwanzo mwisho watu wanavyowasili eneo la shughuli.
Alitangulia nami nikamfata nyuma huku nikiwaza, huyu kumbe mchawi nae? Ila hawezi nidhuru.
Tulifika chini ya mti mkubwa.
Fumba macho na uruke juu!
 
...65
Nilifumba na kuruka juu kwa nguvu, ajabu tayari nilikuwa juu ya ule mti nikiwa nimeshikilia tawi la ule mti ambao sikupata kuujua jina mpaka leo.
Nakuacha hapa, naomba ukaze moyo kwa utakachokiona, vinginevyo wakikuona utakuwa kitoweo, alitahadharisha.
Sasa nilianza kuogopa hata kabla sijaona nini nimekuja kuoneshwa, yaani mimi niwe kitoweo? Ngoja tuone, niwaza.
Chukua upembe huu, usogeze karibu na sikio lako, nitakuwa nakupa maelekezo ya nini ufanye kupitia upembe huu, alimaliza yunge kisha akanivika miwani iliyotengenezwa kwa manyoya, miwani hii haikuwa na galasi kwenye mboni ilikuwa ya fremu pekee.
Kwaheri, alisema na kupotea pale kitendo kilichonifanya niogope na kuanza kuangaza juu yamti.
Nilitupa macho mbele ya ule mti kama mita 80 hivi ambapo niliona moto mkubwa unawaka.
Nilishangaa kumwona pale yunge huku akiwa kajifunga nguo nyeusi kusitiri matiti na nyeti zake tu.
Ghafla niliona vumbi kwa zito linatimka kwa mbali ambapo nikaza macho nione nini kile.
Nilimwona bibi juu ya fisi mkubwa mno.
Mh?
 
...66
Fisi huyo alifika pale alipokuwa yunge, aliendelea kutimua vumbi huku akiuzunguka moto ule mkubwa mara kadhaa kisha akashuka huku pia akiwa kavaa kwa mtindo wa kusitiri matiti na nyeti zake tu.
Bibi ni mchawi? Nilijiuliza,
Ghafla fisi wengine kama 7 walokuwa wamebeba watu walitokeza pale na mwendo ukawa uleule kuuzunguka moto kwa mikwara huku vumbi zito likitimka, kisha walishuka juu ya fisi huku yale mafisi wakiyafunga kwenye miti iliyokuwa pembeni! Mara vilisikika vishindo kama vinne hivi,
Puuh!
Puuh!
Puuh!
Puuh!
Lilitimka vumbi baada ya vishindo vile kisha mda kidogo vumbi lilipotea na wakaonekana watu wanne wanaume wote.
Mhh! Mbona kama yule namjua? Nilipigwa butwaa kumwona jamaa mmoja ambae alikuwepo kiwanjani jioni akifanya mazoezi, jamaa huyu alikuwa striker tegemezi pale kijini na ilisemekana alikuwa hatari akilisogelea lango la timu pinzani, nikiwa bado nashangaa pale juu ya mti, nilimwona pia mzee aliekuwepo pale kiwanjani jioni na alinisifia kwa moyo wangu wa kujitoa.
Nahuyu mzee ni mchawi!!
 
...65
Nilifumba na kuruka juu kwa nguvu, ajabu tayari nilikuwa juu ya ule mti nikiwa nimeshikilia tawi la ule mti ambao sikupata kuujua jina mpaka leo.
Nakuacha hapa, naomba ukaze moyo kwa utakachokiona, vinginevyo wakikuona utakuwa kitoweo, alitahadharisha.
Sasa nilianza kuogopa hata kabla sijaona nini nimekuja kuoneshwa, yaani mimi niwe kitoweo? Ngoja tuone, niwaza.
Chukua upembe huu, usogeze karibu na sikio lako, nitakuwa nakupa maelekezo ya nini ufanye kupitia upembe huu, alimaliza yunge kisha akanivika miwani iliyotengenezwa kwa manyoya, miwani hii haikuwa na galasi kwenye mboni ilikuwa ya fremu pekee.
Kwaheri, alisema na kupotea pale kitendo kilichonifanya niogope na kuanza kuangaza juu yamti.
Nilitupa macho mbele ya ule mti kama mita 80 hivi ambapo niliona moto mkubwa unawaka.
Nilishangaa kumwona pale yunge huku akiwa kajifunga nguo nyeusi kusitiri matiti na nyeti zake tu.
Ghafla niliona vumbi kwa zito linatimka kwa mbali ambapo nikaza macho nione nini kile.
Nilimwona bibi juu ya fisi mkubwa mno.
Mh?
Pita mwana fuba ali ku mbiti...
 
...66
Basi nilistaajabu sana, sasa nikawa natumbua macho kwa makini kuona kila fisi atakefika kama babu nayeye atakuwepo, waliendelea kuwasili pale watu wale kila mtu kwa mtindo wake, kuna waliotokeza ghafla wakiwa wamepiga goti moja na mkono mmoja kushika chini! Wengine walikuja wanapaa kama ndege, kiujumla uwasiliji wawatu wale ulikuwa burudani iliyoogopesha.
Ghafla nilisikia sauti pale chini ikiamrisha fumba macho na uruke juu,
Nilitaka kutazama chini nione kuna nini, lakini kabla sijafanya hivyo nilisikia sauti ya yunge kupitia upembe ule akinitaka nisijishughulishe na wale kwani kuwatazama tu, watasisimkwa miili hivyo kuhisi uwepo wa mtu pale.
Mara kidogo nikasikia sauti ileile ikitowa maelekezo kwa mtu yuleyule kwamba ajikaze ili aone kitu ambacho huwa anaambiwa na yeye kutoamini, wakati huu sauti ilisikika usawa wangu juu ya mti upande wangu wa kulia, nikajua pale tupo wawili sasa ambao tumeletwa kila mmoja kwa mpango wake.
Kule kilingeni kwa wachawi kulianza kuchangamka na watu walikuwa wengi sasa.!
 
...66
Basi nilistaajabu sana, sasa nikawa natumbua macho kwa makini kuona kila fisi atakefika kama babu nayeye atakuwepo, waliendelea kuwasili pale watu wale kila mtu kwa mtindo wake, kuna waliotokeza ghafla wakiwa wamepiga goti moja na mkono mmoja kushika chini! Wengine walikuja wanapaa kama ndege, kiujumla uwasiliji wawatu wale ulikuwa burudani iliyoogopesha.
Ghafla nilisikia sauti pale chini ikiamrisha fumba macho na uruke juu,
Nilitaka kutazama chini nione kuna nini, lakini kabla sijafanya hivyo nilisikia sauti ya yunge kupitia upembe ule akinitaka nisijishughulishe na wale kwani kuwatazama tu, watasisimkwa miili hivyo kuhisi uwepo wa mtu pale.
Mara kidogo nikasikia sauti ileile ikitowa maelekezo kwa mtu yuleyule kwamba ajikaze ili aone kitu ambacho huwa anaambiwa na yeye kutoamini, wakati huu sauti ilisikika usawa wangu juu ya mti upande wangu wa kulia, nikajua pale tupo wawili sasa ambao tumeletwa kila mmoja kwa mpango wake.
Kule kilingeni kwa wachawi kulianza kuchangamka na watu walikuwa wengi sasa.!
Ohoooooo kumekuchaaa

Ila wachawi m siwakubali ata kidogo yni na nikishakujua tu napunguza na kuacha mazoea na ww
 
...66
Lakini kilichonishangaza ni bibi kuwa na wasiwasi huku akiangaza macho huku na kule na tangu afike pale hakuonekana kuchangamka kama wenzie, nikiwa bado namtazama bibi na hali yake nilisikia sauti ya yunge akinipa maelekezo kupitia upembe,
Ukitaka kusikia maongezi ya mtu yeyote fumba jicho moja na jingine umkazie kumtazama mtu unayetaka usikie maongezi yake kwani sasa mkutano haujaanza ndo maana sauti husikii, ila mkutano ukianza utasikia kila kitu, ilisikika sauti ya yunge kupitia upembe.
Basi nilfanya majaribio kwa bibi ambae alionekana kutotulia kama kunajambo amelihisi!
Nilimwona akimfata yunge na kumvuta pembeni, hapohapo nilifumba jicho moja kisha nikawakazia jicho moja bibi na yunge, nilisikia kwenye ule upembe sauti ya bibi akimwambia yunge,
Mbona moyo wangu unawasiwasi hivi? Najihisi kutokuwa huru tangu nimefika hapa na mwili unanisisimka, sijui kuna shida gani, aliuliza bibi.
Nikawaida tu bibi utakaa sawa, huwenda wakati wa kuja mmepita njia mbaya,
Alijibu.
Aliondoka pale.
Mara ghafla...!
 
Back
Top Bottom