True story: Babu yangu kama mshikaji wangu

True story: Babu yangu kama mshikaji wangu

...108
Nilishangaa yule mzee kunisema mi mchawi, nilijikaza na kumpuuza huku nikiingia ndani na kutoka na viti viwili vya mbao, niliviweka pale kivulini kisha nikafata vingine viwili, nilimkabidhi babu kiti kimoja na kingine nilikalia mwenyewe.

Ehe kijana wangu kwanza samahani kwa yote yametokea, alivunja ukimya mzee yule ambae mda si mrefu aliniita mchawi.

Sisi hapa ni wataalamu wa mambo ya jadi (waganga wa kienyeji) mimi na mwenzangu huyu, na huyo mzee mwingine ni mfiwa ambae amefiwa na mwanae wa kiume, lakini pia mke wake ni mgonjwa kitandani asiye jiweza, alisema mzee yule na kuendelea,

Kilichotufikisha hapa kwenu ni kutaka kujua ukweli, maana inaonekana kifo cha yule kijana kinatatanisha sana, na tumejaribu kufanya utaalam wetu ikaonekana kuna mchezo mchafu unachezwa ndani ya kijiji hiki.

Hatukufichi kwani unaonekana ni kijana uliepevuka sasa, hivyo hatutarajii tutakayo yaongea hapa utafungua mdomo na kumweleza mtu awae yote.

Tumepiga ramli ikaonekana mke wa huyu mzee ndo muhusika wa vifo viwili.
 
...109
Mke wa huyu mzee inaonekana amehusika na upotevu wa mjukuu wao na kifo cha kutatanisha cha kijana wao wa kiume.

Lakini dira zikaeleza sababu ya mama yule kumwua mwanae ni baada ya kijana yule kumwona mama yake akifanya kitendo cha kinyama kwa mjukuu wake ambae juzi alikamatwa na fisi mapema jioni, alieleza mzee yule na kuendelea,

Kilichotuleta hapa, dira yetu imekuona wewe ndo umesababisha ugonjwa wa huyu mama na mzee mwingine hapa kijijini kwa pigo ulilowapa, naam tunaomba utueleze bila kuficha chochote yale ambayo uliyaona mpaka kupelekea vita na wewe kuwaumiza hawa wau, alimaliza mzee yule.

Nashindwa hata nisemeje wazee wangu, yaani yote mloyaongea hapa hakuna hata moja nalolijua, nipo hapa leo siku ya 4 tu, na nimekuwa mtu wa kukaa hapa nyumbani bila kutoka, na kuhusu mambo ya nguvu za giza sijui hata dawa moja, nilijitetea kwa kujiamini.

Hapana mwanangu, tunaomba utusaidie ili tumsaidie kijana mwenzio ambae yupo katika hali mbaya na tunahitaji uthibisho wako kwa aliyosemani eti mamaye mchawi?
 
...109
Mke wa huyu mzee inaonekana amehusika na upotevu wa mjukuu wao na kifo cha kutatanisha cha kijana wao wa kiume.

Lakini dira zikaeleza sababu ya mama yule kumwua mwanae ni baada ya kijana yule kumwona mama yake akifanya kitendo cha kinyama kwa mjukuu wake ambae juzi alikamatwa na fisi mapema jioni, alieleza mzee yule na kuendelea,

Kilichotuleta hapa, dira yetu imekuona wewe ndo umesababisha ugonjwa wa huyu mama na mzee mwingine hapa kijijini kwa pigo ulilowapa, naam tunaomba utueleze bila kuficha chochote yale ambayo uliyaona mpaka kupelekea vita na wewe kuwaumiza hawa wau, alimaliza mzee yule.

Nashindwa hata nisemeje wazee wangu, yaani yote mloyaongea hapa hakuna hata moja nalolijua, nipo hapa leo siku ya 4 tu, na nimekuwa mtu wa kukaa hapa nyumbani bila kutoka, na kuhusu mambo ya nguvu za giza sijui hata dawa moja, nilijitetea kwa kujiamini.

Hapana mwanangu, tunaomba utusaidie ili tumsaidie kijana mwenzio ambae yupo katika hali mbaya na tunahitaji uthibisho wako kwa aliyosemani eti mamaye mchawi?
Kumekuchaa

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
...110
Alinisihi yule mzee ambae mke wake ndo yule mama mchawi aliekuwa akiyungumziwa pale.

Mdogo wangu kama kunakitu unakijua juu ya mambo haya nakuomba ueleze kila kitu, maana mimi nimewaleza hawa watu kwamba huna ulijualo kwenye ulimwengu wa giza, lakini wakanitaka nikukutanishe nao kwani ramli zao zinakuonesha wewe eti umesababisha balaa na kupelea wananzengo wawili kuwa hoi vitandani mpaka sasa, alinisihi babu.

Babu sijui lolote kabisa, na hapa nilipo hata dawa ya kichwa tu sijui, sasa uchawi nimeutowa wapi babu yangu, nilijitetea huku fedheha yakuonekana mchawi ikizonga na kupelekea mochozi yaanze kunitoka.

Hili jambo limekuwa zito sana, alisema mzee yule mwongeaji na kuendelea,
Vipi tunaweza ingia chumba anacholala huyu kijana tufanye ukaguzi kidogo? Aliuliza mzee yule huku akimwangalia babu.

Babu alinitazama kwa jicho la unasemaje mwana, nami nikatikisa kichwa kwamba hakuna ubaya.

Waliinuka wazee wale wawi ambao walionekana waganga wa kienyeji huku wakiongozana na babu mpaka getoni mwangu.
 
...111
Huku nje nilibaki na yule mzee mme wa yule mwanamke mchawi ambae ilisemekana yu hoi kitandani kutokana na pigo nililowapatia.

Mwanangu unanafasi ya kumsaidia kaka yako ambae ilikua azikwe jana, lakini kutokana na hali aliyokuwa nayo ya kutokwa damu puani, masikioni na mdomoni ingali akiwa amekufa ilitushtua na nikakata shauli asizikwe ili niite wataalam ambo walifika muda si mrefu na kufanya utaalam wao uliopelekea kijana wangu akarudiwa na pumzi...!

Babu na wale wazee wawili walitoka ndani mwangu huku wakionekana kukosa tumaini lolote.

Hakuna tulichokipata ndani ya nyumba ya huyu kijana, japo naamini kuna kitu anatuficha lakini hatuna namna zaidi ya kuondoka tukashuhulike na mgonjwa wetu, alisema mzee mwongeaji.

Wazee wenzangu, kijana wangu huyu katoka mjini juzi tu, hajui chochote huyu, alinitetea babu yangu.

Anaweza akawa hajui chochote lakini akapelekwa kwenda kuoneshwa mambo ya giza na anayejua kama ilivyotokea kwa huyu kijana ambae amenusurika kufa, alisema mzee mwongeaji huku wakiondoka.
 
...112
Waliondoka wakiongozana na babu huku nyuma nikibakiwa na maswali mengi kichani.

Inamaana jamaa amerudishiwa uhai wake ambao ilikuwa apokonywe na wachawi wale akiwemo na mama yake mzazi?

Kumbe pia jamaa yule baada ya kuzinduka aliwaeleza yote mpaka akawaambia ilionekana mtini alimokuwa amefichwa ili aone unyama wa mama yake hakuwa pekeyake, kulikuwa na mtu mwingine ambae baada ya yeye kushtuka na kudodoka chini, yule mtu alikimbia na wachawi wakagawanyika, wengine walimkamata yeye na wengine walishuhulika na aliyekimbia ambae ndo mimi.

Hii dunia inambo, niliingiwa na huruma juu ya yule jamaa alienusurika kuzikwa na pia mtoto wake kuliwa nyama japo mpaka muda huo sikujua yule mtoto alikuwa ameshaliwa ama bado.

Kwaupande mwingine nilijisifia kwa kuonesha msimamo na kutotetereka juu ya maswali yao, kwani nilikumbuka sharti la yunge mkubwa kuwa mbishi asiekubali kirahisi.

Japo nilishaanza kumchukia nilitamani atokee muda huo ili nimweleze yote yale.

Inamaana wameshindwa kabisa kumgundua yunge mkubwa?
 
...111
Huku nje nilibaki na yule mzee mme wa yule mwanamke mchawi ambae ilisemekana yu hoi kitandani kutokana na pigo nililowapatia.

Mwanangu unanafasi ya kumsaidia kaka yako ambae ilikua azikwe jana, lakini kutokana na hali aliyokuwa nayo ya kutokwa damu puani, masikioni na mdomoni ingali akiwa amekufa ilitushtua na nikakata shauli asizikwe ili niite wataalam ambo walifika muda si mrefu na kufanya utaalam wao uliopelekea kijana wangu akarudiwa na pumzi...!

Babu na wale wazee wawili walitoka ndani mwangu huku wakionekana kukosa tumaini lolote.

Hakuna tulichokipata ndani ya nyumba ya huyu kijana, japo naamini kuna kitu anatuficha lakini hatuna namna zaidi ya kuondoka tukashuhulike na mgonjwa wetu, alisema mzee mwongeaji.

Wazee wenzangu, kijana wangu huyu katoka mjini juzi tu, hajui chochote huyu, alinitetea babu yangu.

Anaweza akawa hajui chochote lakini akapelekwa kwenda kuoneshwa mambo ya giza na anayejua kama ilivyotokea kwa huyu kijana ambae amenusurika kufa, alisema mzee mwongeaji huku wakiondoka.
Dah umewapatia pigo la haja

Hlf hujui hta dawa ya kichwa

Hhhhhhh
 
...112
Huyu binti ni kiboko yao, sasa kama upembe tu umewalaza vitandani wale wachawi wawili, je akiamua kunigeuza bundi si itakuwa kufumba na kufumbua tu? Niliwaza sana.

Nilijikuta nammis sana yunge mkubwa, kitendo cha kuwajeruhi washirika wake kisa wasiniguse mimi kilinipa kichwa na kujiona kweli mzee mzima napendwa.

Hisia nzuri za kimapenzi juu yake ziliniijia kichwani na kujikuta natabasamu mwenyewe.

Kupendwa raha jamani, yaani mtu anakuwa tayari kuumiza wengine kwa ajili ya ampendae tu, hapa niliamini maneno alonambia kwamba hakuna mtu atakugusa nzehe.

Mbona unatabasamu mwenyewe huku umetizama juu, kuna malaika unaongea nae nini, ilikuwa ni sauti ya yunge mdogo akishangazwa na ninavyotabasamu mfululizo bila uwepo wa mtu mwingine.

Basi tu! Nilijibu.
Vipi umemmisi bi mkubwa nini? Aliuliza yunge mdogo.

Kiukweli nimemmisi yunge mkubwa, nimemmisi sana, natamani nimkumbatie, nahisi ananipenda sana yule msichana, hata mimi nampenda pia, ndio nampenda mno, niliongea mfululizo kwa hisia kali sana.
 
...112
Huyu binti ni kiboko yao, sasa kama upembe tu umewalaza vitandani wale wachawi wawili, je akiamua kunigeuza bundi si itakuwa kufumba na kufumbua tu? Niliwaza sana.

Nilijikuta nammis sana yunge mkubwa, kitendo cha kuwajeruhi washirika wake kisa wasiniguse mimi kilinipa kichwa na kujiona kweli mzee mzima napendwa.

Hisia nzuri za kimapenzi juu yake ziliniijia kichwani na kujikuta natabasamu mwenyewe.

Kupendwa raha jamani, yaani mtu anakuwa tayari kuumiza wengine kwa ajili ya ampendae tu, hapa niliamini maneno alonambia kwamba hakuna mtu atakugusa nzehe.

Mbona unatabasamu mwenyewe huku umetizama juu, kuna malaika unaongea nae nini, ilikuwa ni sauti ya yunge mdogo akishangazwa na ninavyotabasamu mfululizo bila uwepo wa mtu mwingine.

Basi tu! Nilijibu.
Vipi umemmisi bi mkubwa nini? Aliuliza yunge mdogo.

Kiukweli nimemmisi yunge mkubwa, nimemmisi sana, natamani nimkumbatie, nahisi ananipenda sana yule msichana, hata mimi nampenda pia, ndio nampenda mno, niliongea mfululizo kwa hisia kali sana.
Yunge mdogo atakuwa anataka kupasuka baada ya kusikia haya maneno
 
113
Maneno yangu yale yalimkosesha amani yunge mdogo, alinywea kabisa na kuonekana kama mtu mwenye homa kali.

Basi sawa ngoja mie nirudi nisije haribu ndoa za watu, alisema kwa unyonge yunge mdogo.

Hapana huwezi haribu chochote kwa kuja kunitembelea tu, wewe ni jirani yetu, kwahio tunaweza kutembeleana na kupiga stori bila shida yoyote, nilimtuliza yunge mdogo huku sasa nikiwa nimeshasahow kumwuliza juu ya ndoto yangu ya kupaa ilihali yeye akisema ilikuwa live.

Lakini si ulinambia na kunihakikishia kwamba unanipenda sana na yunge mkubwa humtaki tena, kumbe ulitaka kumaliza haja zako tu? Aliuliza yunge mdogo ambae alionekana kutokuwa na raha hata tone.

Naomba uniwie radhi ndugu yangu, kiukweli mwenzio alikuwahi kwakweli, alionesha kunipenda mara baada ya kunitia machoni kwa mara ya kwanza, tofauti na wewe ambae ulionesha kunichukia sana, pia kubwa kuliko ni zawadi aliyonipa.

Alinipa zawadi ya usichana wake na kuniahidi mambo mengi mazuri, kiukweli nampenda mwenzio, nilimchana live bila chenga.

Sawa bwana
 
Back
Top Bottom