True story: Babu yangu kama mshikaji wangu

True story: Babu yangu kama mshikaji wangu

...24
Niliondoka kuelekea kisimani kuchota maji kukiwa kumeanza kupambazuka sasa na ukungu unaelekea kuisha! Nmetembea kama dakika 4 hivi, nikaona waschana wawili kwambele wanatoka kisimani wamebeba ndoo vichwani! Wanaelekea niliko mimi yaani uso kwa uso nakutana nao!
Ng'wangaluka yunge (habari ya asbuhi yunge) nilimsalimia yunge mdogo ambae alisimama ghafla na kunikata jicho, umelijuaje jina langu? Usinizoee sawa? Alinikoromea yunge mdogo huku akizichapa hatua na kuondoka, nilimtizama kwa nyuma, dah! Kweli nilikiri yale aloniambia yunge mkubwa, niyule binti alie nikamatia jogoo ndani mwao, ambae nilimkuta amepauka anaanua maharagwe, leo namwona asbuhi hii akiwa safi kabisa! Kweli alikua msichana mzuri sana ika aliniudhi kwa dharau alonionesha, nikawaza ntakuonesha pimbi wewe! Nilienda kuchota maji pale kisimani ambapo kulikuwa na kina mama na wasichana kadhaa waliokuwa wamepanga foreni kungoja zamu ya kukinga maji kwenye bomba lile, nikawasalimia kwa heshma na wakaniitikia freshi tu, mama mmoja aliniuliza!
Hukujiuliza Babu kukumbuka miaka yenu
 
....25
U mgeni hapa baba?
Ee mimi mgeni, nmekuja kumtembelea babu yangu mzee bhuhabi, nilijibu!
Wewe ni mtoto wa faida?
Aliuliza mwanamke mwingine aliekua ananyongo bomba la maji,
Ndo mimi mama,
Nilijibu!
Wewe mtoto ulikua na vituko sana, uliwahi kumwaibisha mama yako msibani kwa mzee manyanda, mbele ya umati wa kina mama, ulituacha hoi kwakweli, sasa umekua mwanaume mtu mzima, ama kweli siku hazigandi,
Alibwabwaja mwanamke yule ambae baadae nilikuja gundua kuwa mzee wangu alikua anamnyandua enzi za ujana wao,
Utakuja nyumbani utusalimie mwanangu, faida tumesoma nae darasa 1,
Aliongeza mama yule aliejaaliwa mzigo wa maana huko nyuma,
Ntakuja mama yangu wala usjali! Nilijibu!
Walichota maji mpaka ikafika zamu yangu! Nilianza kuchota maji, wakati nmeja dumu zangu nilishuka kutoka pale juu ya bomba, mara nikasikia sauti kutokea nyuma,
Nisaidie na mimi mwanangu kusukuma bomba, alikua ajuza alieoneka kula chumvi lundo,
Sawa bibi, lete ndoo nikuchotee, nilimwomba!
Nilimchotea maji, akashukuru na kusema!
 
...26
Umekuja jana ukiwa mwepesi kama karatasi, ila leo tu umekua mzito kama tembo! Babu yako yu makini sana, ndo nachompendea huyu mzee! Alitangu na kuondoka, huku nikivuta kumbukumbu kama jana nilionana na kikongwe huyu, sikukumbuka, halafu kuwa mwepesi jana na leo mzito kiasi kikubwa hicho, je nimenenepa kwa usiku mmo tu?
Sikutilia maanani sana nikabeba dumu zangu na kuanza kuuchapa mwendo, nmetembea kidogo nikakutana kikundi cha wasichana kama 8 hivi, niliwapa hi baadhi yao kwani niligundua wengine waliniacha pale kisimani, hivyo nilikua nmesalimiana nao, tulipishana, kisha nikazichapa hatua kama 20 hivi, kisha nikatua madumu haraka na kugeuka nyuma, hamadi!!
Wale wasichana wote walikua wamesimama na kuniangalia, walishtuka na kugeuka haraka na kuendelea na safari yao kuelekea kisimani, nilicheka, nikajisemea ntawajaza mimba wote, nilibeba madumu nikatembea mpaka nyumbani pale! Niliweka maji jikoni ambamo nilimkuta bibi anachemsha chai, nilimpa hi na utani wa hapa na pale, nikamwuliza bab wapi?
Humuoni?
 
...27
Humuoni? Aliuliza bibi,
Sijamwona, nilimwacha anaota moto pale nje, nimerudi sijamwona, nilijibu,
Unazeeka vibaya mume wangu, humwoni babu yako? Aliuliza tena bibi,
Hahaaa! Macho yako bado hayafumbuka, yatafumbuka tu! Alisema babu ambae nilimwona ghafla baada ya kuangua kicheko,
Nilistuka sana, alikua amekaa hatua mbili kulia kwangu palepale jikoni! Nilishangaa ametoka wapi wakati niepita pale wakati namimina ya le maji mtungini?
Huyu mzee ni mchawi kweli? Hata kama nimchawi, ndo ananifanyia na mimi mjukuu wake? Niliwaza nikiwa nimekodoa jicho mlangoni nisijue ninacho kitazama?
Mume utamzoea tu babu yako, tena nakwambia hutotamani kurudi kwenu tena! Alisema bibi!
Niligeuka kumwangalia babu, nilishangaa kumwona bibi amekaa alipokua amekaa babu, Haraka niligeuza shingo kutizama alipokua amekaa bibi, nilishangaa kumwona babu ndo anageuza kipolo cha wali pale juu ya mafiga!
Mh? Wamebadilishana viti muda gani?
 
...28
Nawa tule, alisema bibi ambae alikua amerudi pale kwenye siti yake bila mimi kuelewa, yani kitendo chakuhamisha macho kutoka hapa kwenda pale, unakuta mambo yamebadilika!
Niligeuka kumtazama babu ambae tulikutanisha macho,
Vipi mdogo wangu, unataka kukimbia? Sasa ukikimbia kwako utakua mwanaume gani? Inabidi uzoee tu, kwani mambo kama haya yatakutokea sana hapa kijijini, lakini hakuna atakae kugusa mwanangu,
Alisema babu akiwa ananawa!
Tule haraka nataka niende kwa mzee maganga nikamfariji, nikweli mjukuu wake aliliwa na fisi na hawakubahatika kupata hata masalia ya mwili wa mtoto yule, aliongeza babu,
Jiukweli nilikula nikiwa sijielewi kabisa, mambo walionifanyia hawa wazee ndani ya dakika 2 yalinitisha sana! ile nyama ya kuku haikunoga tena!
Kula babu usiniogope, bibi yako amekwambia utanipenda sana, tena utawasahow baba na mama yako, alisema babu,
Tulikunywa chai ile kisha babu na mke wake wakaaga na kuondoka huku wakinitaka nisitoke pale nyumbani,
Nilingia ndani mwangu na kujilaz.

******Hodi!
 
...29
Nilichungulia nje na kumwona yule msichana wa pale jirani,
Karibu, niliitikia huku nikitoka ndani! Karibu, niliendelea kumkaribisha yunge mdogo!
Bibi yupo? Aliuliza,
Hayupo, wamekwenda kumfariji mzee aliepatwa tukio la mtoto kuliwa na fisi! Nilimjibu,
Nilipita kumwomba nichume kisamvu pale shambani alisema kwa kujiamini!
Ndo hivyo ameondoka si muda mrefu,
Nilimjibu huku nikigeuza kuingia ndani kujilaza, sikutaka kuendelea kuongea nae kwani dharau alonionesha asbuhi ilinikera sana,
Nilifika chumbani, ila kabla sijalala niliona nimchungulie yunge mdogo pale nje, nilisogea dirishani na kuchungulia, alikua amesimama palepale nilipo mwacha! Alionekana kuzama katka fikra, hapo nilipata kumchunguza vizuri sasa, alikua ni msichana mwenye mwonekano maridadi sana! Binti alivutia sana ila nilimchukia kwa dharau zake,
Aliondoka kinyonge, nilipata kumwona tena kwa nyuma, jamani mali ilikuepo si haba, nilijilaza kitandani kabla usingizi haujanichukua,
Nilikuja kustuka mtu yupo kifuani kwangu,
Hah? Yunge umekuja?
 
Back
Top Bottom