147
Nilishtuliwa usiku sana na kelele za mafisi, yalikuwa yanatoa sauti mbaya mno, baadae niligundua kumbe yalikuwa mbali na pale nyumbani hivyo hofu ilipungua, nilipitiwa usingizi tena mpaka asubuhi.
Hodi, ilikuwa sauti ya yunge akigonga dirishani.
Nakuja, nilimjibu huku nikinyanyuka kitandani, nilivaa nguo na kwenda kufungua mlango, nilimwona yunge akiwa na jembe moja kuashiria alikuwa tayari kwenda mbugani.
Oooh! Bibi umempitia mchumba wako kwenda majarubani? Samahani sana mwenzio hayupo sawa, nitakujulisha akipona sawa mwanangu? alisema babu hata kabla hatujaongea neno lolote na yunge.
Sawa babu, shkamoo, alikubali yunge na kusalimia.
Marahaba, hatakiwi kutoka nje baridi kali hili, hivyo mwache alale, alikomalia yunge ambae alinisalimia na kuniuliza kwa sauti ya chini, umepatwa nini jamani?
Tutaongea tukipata muda, niache nipumzike kwani nahisi baridi kali sana, nilimdanganya akanipa pole na kuaga yeye anakwenda mbugani kuvuruga na mchana angepita kunijulia hali.
Tule haraka tunakazi nzto ya kufanya.