True story: Nimeamua kumkataa mtoto rasmi

True story: Nimeamua kumkataa mtoto rasmi

mFuKuZa nDoTo

JF-Expert Member
Joined
Jan 17, 2021
Posts
492
Reaction score
639
Watu wa Jamii Forum Salaam, Naitwa Mfukuza Ndoto, Nina umri wa katikati ya ujana naishi mkoa fulani kanda ya kati. Basi bwana mnamo mwaka fulani nikiwa na 20+yrs nilitokea kumpenda binti fulani toka nyanda za juu kusini, binti huyo alikuwa mwanafunzi wakati huo katika chuo fulani hapa mjini. Namaanisha alikuja tu kwa ajili ya masomo.

Tukapendana, kwa kawaida huwa nikishaingia kwenye mahusiano huwa nadumu na kutulia ndio maana mpak sasa sina rekodi ya mtoto wa mtu niliyempotezea muda halafu nikamuacha, sina machozi ya mwanamke yeyote yanayoniandama zaidi wote hujutia na hicho ndio nilichokipanga kwenye maisha yangu mwanamke akitaka kupendwa atapendwa ashindwe yeye tu sipendi lawama.

Kabla yake nikiwa mwanafunzi miaka ya 2000's nilipoingia tu kidato cha kwanza nikapendwa na kabinti fulani(Na desturi yangu huheshimu sana hisia za mwanamke, yaani siingii kwenye mahusiano bila mwanamke mwenyewe kuonyesha interest na mimi nami nikiridhika nae anapitishwa.

Hapa nazungumzia mapenzi sio ngono kwa maana ya tamaa za mwili, nikitamani kuna sehemu zinajulikana na mabaharia hujipoza maisha yanaendelea
Kwahiyo kwenye maisha yangu nimepitia mahusiano yasiyozidi matatu, acha wale wa kushare nao tu shuka, tukiwataja tutajaza kurasa za Jf.

Kwahiyo baada ya kabinti kunipenda hiyo ni pre-form one mpaka tunaanza form one mpaka kidato cha nne tulikuwa wapenzi na shule nzima ilijua hilo lakini cha ajabu hatukuwahi kufanya mapenzi kabisa,
Ilitokea hivyo kwa sababu kuu mbili, kwanza tulikuwa wadogo sana nadhani nilikuwa na miaka 14(kwa mwanaume wakati huo nilikuwa mdogo sana) na yeye alikuwa mdogo zaidi, pili kwa wakati huo mpaka umvue nguo mwanamke ilikuwa shughuli, sio kama sasa katika umri huo kijana anazijua tayari na kama binti tayari anazijua P2.

Kuna wakati nilikuwa naazima mageto ya washkaji tunakutana huko na kabinti basi washkaji wanajua nimemaliza kazi kumbe nimegomewa na mimi ujanja sina sana[emoji1][emoji1] sababu ya tatu sitaitaja lakini ndio kubwa zaidi
Mimi na yule mwanadada tumekuja kuvunjana 'Upya' tukiwa tumeshamaliza form four tumefeli tuko mtaani, kwa kweli yeye na mimi wote tulikuwa wageni wa mambo kwahiyo tulifunguliana

Nayasema haya ionekane namna gani huwa siachi mwanamke nikishaingia nae kwenye mahusiano mpaka yeye aje kuharibu na ajilaumu mwenyewe na akishaharibu hata aje na Fiat (gari za zamani) huwa sibadili msimamo hata aroge vipi, kwa kuwa naamini ukishafanywa mpumbavu mara moja ukasamehe uwezekano wa kuonekana boya ni mkubwa na atakuumiza mara ya pili na zaidi
Kingine naamini wanawake ni wengi, shida ya nini kurudiana na mmoja aliyekuumiza? Sio kweli ile dhana ya kwamba umeandikiwa utaishi nae kumbuka binadamu wawili wawili kama uliandikiwa kuishi na huyo akizingua kuna aliyefanana tena na huyo huyo utampata, na ili tupeane masomo asijeenda kusumbua wengine unamgomea msamaha akienda kwa mwingine hatasumbua labda awe amepinda tu.

Kilichoniachanisha na huyu bikra mwenzangu nikiwa mtaani nimechoka sasa napigwa na maisha kotekote akanifuata jamaa mmoja, ni wale unakuta pale mjini ana sifa ya ukicheche(umalaya)
Zamani ilikuwa kama sifa, kila mji palikuwa na watu sifa yao ni hakuna demu anapindua kwao, na mara nyingi unakuta ni sababu ya maisha mazuri yake au ya familia yake, akishamudu kuwa na kageto na uwezo wa kubadili mavazi kidogo basi mademu wanapishana. Huyu jamaa akaniuliza kama huyo demu ni demu wangu(nafikiri aliambiwa kwa busara akaona asije kuingia anga zangu) basi mimi ile kujivunga eti nampima imani demu nikakataa ili kama atatongozwa akatae mwenyewe

Bwana wee sijakaa sawa demu ananipigia simu ananitukana kwa namba mpya sielewi sababu nini, huku akiwa na wifi zake(dada wa yule jamaa) kuja kufuatilia jamaa keshamtindua dah nikadata maana home kwetu walimjua mpaka dada zangu walimjua alikuwa anafika mpaka home, miaka zaidi ya minne ilikuwa lazima ajulikane. Na pia alipoanza kutoka na huyo jamaa dada zangu walijua ikawa fedheha sana, nikawaza, nikachanganyikiwa kwa aibu sio kwa sababu siwezi kupata mwingine.

Nikapiga moyo konde nikamove on, Mungu si athumani nikaotea kibarua kidogo, aliposikia akaanza kujirudisha.
Sikumtukana, sikumjibu vibaya nikamwangalia tu nikaachana nae mpaka leo ananiona tu mitandaoni.
Huyo ni mmoja kati ya hao watatu

Sasa tuendelee na huyu binti mwanafunzi wa chuo ngazi ya chini ya shahada...huyu nilikutana naye katika ofisi moja ya serikali ambapo alimsindikiza mwenzake na mimi ambaye mimi nilifahamiana nae, baada ya kusalimiana na kukaa wote kwenye benchi kwa muda mrefu tukisubiri huduma tukazoeana(na huyu binti mlengwa) tukabadilishana namba.
Nilipoondoka yule rafiki yake akanitanabaisha kwamba rafiki yake (Binti Mlengwa tumwite BM) anaonyesha namna fulani ya kunikubali/kunipenda/kunizimikia[emoji23][emoji23]sasa kama ilivyo desturi yangu huwa sidharau hisia za mwanamke awe amenipenda au ametamani kushare shuka tu na mimi lazima nimtimizie adhma yake.
Note: Haya hayatokei ikiwa nina mwanamke tayari ninayedumu nae, ni pale napokuwa 'Loose ball' na pia isitafsirike kwamba labda nina mvuto saana hapana hii hutokea kwa yeyote maana wanawake wana sababu nyingi za kupenda mwanaume kama ambavyo wanaume tuna sababu nyingi tu za kuvutiwa na mwanamke.

Tuendelee, nilipopata ujumbe ule nikajua cha kufanya hapa ni kuanza ukaribu tu mwanamke akishakupenda hawezi kukuanza lakini ukimsalimi siku ya kwanza, ukamchatisha bize siku mbili weekend inayofuata ukimtaka appointment atakuja tu hata kama atazuga kidogo, Basi, nikaweka mazingira na uhusiano ukaanza kwa namna hiyo

Mwanzo sikukapenda baadae nikakazoea basi nikakapenda, sijui kalinifanya nini nakiri ndio mwanamke nimewahi kumpenda haijatokea tenaaaaa

Visa vichache vilitokea wakati ule vilifaa kabisa kumuacha sikuviona leo hii ndio nayaona na kujiuliza hivi nilikuwa mimi kweli yule? Mfano kuna wakati nilifuma meseji kwenye simu yake ni dhahiri ilikuwa ya mwanaume na ana mahusiano naye nikafunika kombe mwanaharamu apite
Kuna wakati msanii mmoja alikuja kupiga show kwenye ukumbi fulani sikwenda lakini kuna jamaa akaropoka kwamba alimuona usiku huo huyo binti na kutoka chuoni mpaka mjini ni umbali ambao sio wa kurudi usiku, sasa alilala wapi hicho kiulizo kingine, lakini wakati naoambiwa huyo binti alikuwa club mimi nimeonge nae sana usiku mpaka kwenye saa tano au sita kwa akili yangu ndogo wakati ule sikumuamini jamaa nikafikiri nimemfananisha....maisha yakaendelea

Nilikapenda sana kale kabinti, kuna wakati nilitishia kukaacha kakalia usiku kucha, nikajisemea mwanamke si ndo huyu bwanaaa...nikadumu nae kwa miaka mitatu mpaka anamaliza, kilichonipa imani kwamba mke nimepata ni wakati alipomaliza shule, wanavyuo wengi wakimaliza na mapenzi wanaondoka nayo makwao lakini huyu BM aliendelea "ku-keep in touch" mpaka nikaanza kunenepa, huko huko aliko bado mawasiliano yalikuwa mazuri huku akija kunipikia kila alipopata nafasi
Hata wenzangu waliokuwa na wanawake pale chuoni ambao walishaachana na wapenzi wao waliamini nimependwa haswaaa na mimi ukinipenda nakupenda nataka nini kingine.

Ndio ikawa hivyo, akamaliza akaondoka, akaanza kudai ndoa, basi mi ndo kabisaa naona nimepata mke mwema, nikachukua likizo nikampeleka nyumbani kumtambulisha, kwanza nikaanza kwao kisha kwetu.
Nyumbani kwetu walimpenda sana, she was hard working na mrembo kiasi, tukiwa hapo nyumbani nafasi za ajira zikatoka akaajiriwa mkoa fulani kanda ya magharibi
Wakati nampeleka nyumbani ilikuwa mnamo August ya mwaka huo, kufika December ndio picha picha zilipoanza...


.....Wacha nichukue mapumziko....leo ndio nimeona ugumu wa kuandika...wale wazee wa itaendelea hawafanyi kwa makusudi inawalazimu kupumzika

Will Be Back!!!

Kuendelea bonyeza kiungo hapo chini

Sehemu ya pili
Sehemu ya tatu
Sehemu ya nne
Sehemu ya tano
Sehemu ya sita
Sehemu ya saba
Sehemu ya nane
Hitimisho
 
Watu wa Jamii Forum Salaam, Naitwa Mfukuza Ndoto, Nina umri wa katikati ya ujana naishi mkoa fulani kanda ya kati. Basi bwana mnamo mwaka fulani nikiwa na 20+yrs nilitokea kumpenda binti fulani toka nyanda za juu kusini, binti huyo alikuwa mwanafunzi wakati huo katika chuo fulani hapa mjini. Namaanisha alikuja tu kwa ajili ya masomo.
Tukapendana, kwa kawaida huwa nikishaingia kwenye mahusiano huwa nadumu na kutulia ndio maana mpak sasa sina rekodi ya mtoto wa mtu niliyempotezea muda halafu nikamuacha, sina machozi ya mwanamke yeyote yanayoniandama zaidi wote hujutia na hicho ndio nilichokipanga kwenye maisha yangu mwanamke akitaka kupendwa atapendwa ashindwe yeye tu sipendi lawama.
Kabla yake nikiwa mwanafunzi miaka ya 2000's nilipoingia tu kidato cha kwanza nikapendwa na kabinti fulani(Na desturi yangu huheshimu sana hisia za mwanamke, yaani siingii kwenye mahusiano bila mwanamke mwenyewe kuonyesha interest na mimi nami nikiridhika nae anapitishwa. Hapa nazungumzia mapenzi sio ngono kwa maana ya tamaa za mwili, nikitamani kuna sehemu zinajulikana na mabaharia hujipoza maisha yanaendelea
Kwahiyo kwenye maisha yangu nimepitia mahusiano yasiyozidi matatu, acha wale wa kushare nao tu shuka, tukiwataja tutajaza kurasa za Jf.
Kwahiyo baada ya kabinti kunipenda hiyo ni pre-form one mpaka tunaanza form one mpaka kidato cha nne tulikuwa wapenzi na shule nzima ilijua hilo lakini cha ajabu hatukuwahi kufanya mapenzi kabisa,
Ilitokea hivyo kwa sababu kuu mbili, kwanza tulikuwa wadogo sana nadhani nilikuwa na miaka 14(kwa mwanaume wakati huo nilikuwa mdogo sana) na yeye alikuwa mdogo zaidi, pili kwa wakati huo mpaka umvue nguo mwanamke ilikuwa shughuli, sio kama sasa katika umri huo kijana anazijua tayari na kama binti tayari anazijua P2.
Kuna wakati nilikuwa naazima mageto ya washkaji tunakutana huko na kabinti basi washkaji wanajua nimemaliza kazi kumbe nimegomewa na mimi ujanja sina sana[emoji1][emoji1] sababu ya tatu sitaitaja lakini ndio kubwa zaidi
Mimi na yule mwanadada tumekuja kuvunjana 'Upya' tukiwa tumeshamaliza form four tumefeli tuko mtaani, kwa kweli yeye na mimi wote tulikuwa wageni wa mambo kwahiyo tulifunguliana

Nayasema haya ionekane namna gani huwa siachi mwanamke nikishaingia nae kwenye mahusiano mpaka yeye aje kuharibu na ajilaumu mwenyewe na akishaharibu hata aje na Fiat (gari za zamani) huwa sibadili msimamo hata aroge vipi, kwa kuwa naamini ukishafanywa mpumbavu mara moja ukasamehe uwezekano wa kuonekana boya ni mkubwa na atakuumiza mara ya pili na zaidi
Kingine naamini wanawake ni wengi, shida ya nini kurudiana na mmoja aliyekuumiza? Sio kweli ile dhana ya kwamba umeandikiwa utaishi nae kumbuka binadamu wawili wawili kama uliandikiwa kuishi na huyo akizingua kuna aliyefanana tena na huyo huyo utampata, na ili tupeane masomo asijeenda kusumbua wengine unamgomea msamaha akienda kwa mwingine hatasumbua labda awe amepinda tu.

Kilichoniachanisha na huyu bikra mwenzangu nikiwa mtaani nimechoka sasa napigwa na maisha kotekote akanifuata jamaa mmoja, ni wale unakuta pale mjini ana sifa ya ukicheche(umalaya)
Zamani ilikuwa kama sifa, kila mji palikuwa na watu sifa yao ni hakuna demu anapindua kwao, na mara nyingi unakuta ni sababu ya maisha mazuri yake au ya familia yake, akishamudu kuwa na kageto na uwezo wa kubadili mavazi kidogo basi mademu wanapishana. Huyu jamaa akaniuliza kama huyo demu ni demu wangu(nafikiri aliambiwa kwa busara akaona asije kuingia anga zangu) basi mimi ile kujivunga eti nampima imani demu nikakataa ili kama atatongozwa akatae mwenyewe

Bwana wee sijakaa sawa demu ananipigia simu ananitukana kwa namba mpya sielewi sababu nini, huku akiwa na wifi zake(dada wa yule jamaa) kuja kufuatilia jamaa keshamtindua dah nikadata maana home kwetu walimjua mpaka dada zangu walimjua alikuwa anafika mpaka home, miaka zaidi ya minne ilikuwa lazima ajulikane. Na pia alipoanza kutoka na huyo jamaa dada zangu walijua ikawa fedheha sana, nikawaza, nikachanganyikiwa kwa aibu sio kwa sababu siwezi kupata mwingine.
Nikapiga moyo konde nikamove on, Mungu si athumani nikaotea kibarua kidogo, aliposikia akaanza kujirudisha.
Sikumtukana, sikumjibu vibaya nikamwangalia tu nikaachana nae mpaka leo ananiona tu mitandaoni.
Huyo ni mmoja kati ya hao watatu

Sasa tuendelee na huyu binti mwanafunzi wa chuo ngazi ya chini ya shahada...huyu nilikutana naye katika ofisi moja ya serikali ambapo alimsindikiza mwenzake na mimi ambaye mimi nilifahamiana nae, baada ya kusalimiana na kukaa wote kwenye benchi kwa muda mrefu tukisubiri huduma tukazoeana(na huyu binti mlengwa) tukabadilishana namba.
Nilipoondoka yule rafiki yake akanitanabaisha kwamba rafiki yake (Binti Mlengwa tumwite BM) anaonyesha namna fulani ya kunikubali/kunipenda/kunizimikia[emoji23][emoji23]sasa kama ilivyo desturi yangu huwa sidharau hisia za mwanamke awe amenipenda au ametamani kushare shuka tu na mimi lazima nimtimizie adhma yake.
Note: Haya hayatokei ikiwa nina mwanamke tayari ninayedumu nae, ni pale napokuwa 'Loose ball' na pia isitafsirike kwamba labda nina mvuto saana hapana hii hutokea kwa yeyote maana wanawake wana sababu nyingi za kupenda mwanaume kama ambavyo wanaume tuna sababu nyingi tu za kuvutiwa na mwanamke.

Tuendelee, nilipopata ujumbe ule nikajua cha kufanya hapa ni kuanza ukaribu tu mwanamke akishakupenda hawezi kukuanza lakini ukimsalimi siku ya kwanza, ukamchatisha bize siku mbili weekend inayofuata ukimtaka appointment atakuja tu hata kama atazuga kidogo, Basi, nikaweka mazingira na uhusiano ukaanza kwa namna hiyo

Mwanzo sikukapenda baadae nikakazoea basi nikakapenda, sijui kalinifanya nini nakiri ndio mwanamke nimewahi kumpenda haijatokea tenaaaaa

Visa vichache vilitokea wakati ule vilifaa kabisa kumuacha sikuviona leo hii ndio nayaona na kujiuliza hivi nilikuwa mimi kweli yule? Mfano kuna wakati nilifuma meseji kwenye simu yake ni dhahiri ilikuwa ya mwanaume na ana mahusiano naye nikafunika kombe mwanaharamu apite
Kuna wakati msanii mmoja alikuja kupiga show kwenye ukumbi fulani sikwenda lakini kuna jamaa akaropoka kwamba alimuona usiku huo huyo binti na kutoka chuoni mpaka mjini ni umbali ambao sio wa kurudi usiku, sasa alilala wapi hicho kiulizo kingine, lakini wakati naoambiwa huyo binti alikuwa club mimi nimeonge nae sana usiku mpaka kwenye saa tano au sita kwa akili yangu ndogo wakati ule sikumuamini jamaa nikafikiri nimemfananisha....maisha yakaendelea

Nilikapenda sana kale kabinti, kuna wakati nilitishia kukaacha kakalia usiku kucha, nikajisemea mwanamke si ndo huyu bwanaaa...nikadumu nae kwa miaka mitatu mpaka anamaliza, kilichonipa imani kwamba mke nimepata ni wakati alipomaliza shule, wanavyuo wengi wakimaliza na mapenzi wanaondoka nayo makwao lakini huyu BM aliendelea "ku-keep in touch" mpaka nikaanza kunenepa, huko huko aliko bado mawasiliano yalikuwa mazuri huku akija kunipikia kila alipopata nafasi
Hata wenzangu waliokuwa na wanawake pale chuoni ambao walishaachana na wapenzi wao waliamini nimependwa haswaaa na mimi ukinipenda nakupenda nataka nini kingine.

Ndio ikawa hivyo, akamaliza akaondoka, akaanza kudai ndoa, basi mi ndo kabisaa naona nimepata mke mwema, nikachukua likizo nikampeleka nyumbani kumtambulisha, kwanza nikaanza kwao kisha kwetu.
Nyumbani kwetu walimpenda sana, she was hard working na mrembo kiasi, tukiwa hapo nyumbani nafasi za ajira zikatoka akaajiriwa mkoa fulani kanda ya magharibi
Wakati nampeleka nyumbani ilikuwa mnamo August ya mwaka huo, kufika December ndio picha picha zilipoanza...


.....Wacha nichukue mapumziko....leo ndio nimeona ugumu wa kuandika...wale wazee wa itaendelea hawafanyi kwa makusudi inawalazimu kupumzika

Will Be Back!!!
Hivi hii trend ya story fupi hata haifiki maneno 1500 unaanza mbwembwe kibao mizunguko were, unakatisha vijana mnamatatizo gani?
 
Fanya hima urudi...

Nimemiss kumcheka mie leo ,[emoji16][emoji16][emoji16]
 
SEHEMU YA PILI:

Kabla ya picha picha kuanza wakati nikiwa nae nyumbani haraka tukafunga ndoa ya bomani ili anapokwenda kuripoti kazini asajili cheti cha ndoa kusudi aanze haraka kufanya michakato ya kuhamia mahali alipo maisha yaendelee, akaenda zake.

Baada ya muda mfupi akaja kunitembelea nikafurahi sana kwamba bado anakumbuka kuna mtu amemuacha huku anayemhitaji na sasa maisha ya ajira yakawa yameanza kumkubali akanawiri akapendeza zaidi lakini kuna kitu kikanitia mashaka, hakuwa na pete ya ndoa[emoji848][emoji848][emoji848] nikamuuliza akajibu inambana nimnunulie nyingine, sasa hivi ndio najiuliza pengine aliposema inambana hakumaanisha nilivyoelewa, inawezekana alimaanisha inamzuia kufanya mambo yake...hilo nikamezea.

Akaondoka ndio hapo sasa ilipofika mwisho wa mwaka huo, kiufupi ni miezi isiyozidi minne tu tangu tule yamini pale bomani akaniambia ana ujauzito [emoji2307][emoji2307]kwa maana kwamba ni ujauzito alioupata alipokuja kunitembelea

Lakini uwasilishaji wake haukuwa wa furaha kabisa, wajua mimi nina uwezo wa kuhisi sana mambo, hata nikiongea na mtu tu kwa njia ya simu nahisi zile hisia zake halafu naunga dots haraka. Kwanza akawa jeuri jeuri hivi, baadae ndio akanijulisha juu ya ujauzito huo.

Mimi nikafurahi sana maana kwa umri huo wa katikati mwa 20's nilikuwa na moto hasa wa kupata mtoto, na sio mtoto tu bali mtoto na BM, Haraka nikamuuliza ana hakika ili niwajulishe nyumbani? Akajibu niwajulishe tu, basi sawa mimi nikawaambia home.

Tukaendelea na maisha lakini mimi nikawa na wasiwasi sana, wasiwasi nisioelewa ni wa nini, lakini kwa upande wake hakuwa sawa kuna vitu sikuviona sawa kabisa hasa kwa mtu uliyemzoea.

Mawasiliano yakawa hafifu kidogo plus majibu makavu makavu hivi baada ya mwezi au miezi miwili nilipokuwa najibebisha nikamuuliza kijacho wangu hajambo? Akanijibu kijacho gani?

Nikamwambia wewe si ndio ulisema una ujauzito mpaka home nimewajulisha?
Akanijibu nani ana mimba?

Nikiri wazi katika maisha yangu kuna kipindi nilipitia kudata kwa hali ya juu na kipindi chenyewe kilikuwa hicho.

Kumbe ule wasiwasi wangu Usio na sababu ulikuwa unani-alert na jambo fulani lijalo.

Baada ya majibu hayo makavu nikakaa chini nikajiuliza sasa nyumbani ntawaambia nini tena? Na nikiwaambia wataelewa nina mwanamke wa aina gani? Hii si aibu?
Yaani katika suala zima mimi kilichoniumiza ni aibu tu..sipendi aibu kuliko chochote.
Kuna kitu kimoja tu nilichoamini wakati huo kwamba huyu Mimba alikuwa nayo, sasa;
Inawezekana ni yangu lakini kwa sasa hanihitaji ndio maana siku za karibuni alipata mabadiliko ya tabia kwahiyo akatoa mimba JAMBO AMBALO NI BAYA NA LA AIBU mke kutoa mimba yako, Au inawezekana mimba haikuwa yangu akaona akiiacha atafanyaje na anaishi kwenye ndoa? Akaona bora anipe mimi lakini baadae akaona bora atoe tu JAMBO AMBALO NALO NI BAYA NA LA AIBU mke kupata mimba nje ya ndoa yake.

Kwa haya yaliyoanza kuizonga akili yangu taratibu nikaanza kubadilika/kuvurugika
Watu wangu wa karibu walishtukia tu nimeshakuwa mlevi wa kupindukia lakini siri hii mpaka kesho ninayo mimi tu juu ya nini kilinivuruga, nashukuru Mungu nilikipita kile kipindi kigumu baada ya miaka kama miwili ya kupitishwa katika tanuru la moto halafu nikaibuka kuwa imara ajabu.

Basi bwana, hilo suala nikiwaza kukaa kimya haiwezekani, nikifikiria kuwajulisha nyumbani kichwa kinapata moto[emoji27][emoji27][emoji27]hali inaniacha dilemma, nachanganyikiwa, nadhoofu, nawaza, nazidi kuwa mlevi tu[emoji24][emoji24]

Mpaka hapo mimi nilishaanza kujua BM wangu ameshaanza kuzuzuka baada ya kuanza kupendeza na ajira, ndio kilichoanza kuzunguka akilini mwangu, basi siku moja nikajivisha mabomu nikamwambia mama kwamba ujauzito wa mkwe wao umeharibika

Sikutumwa kusema hivi, yaani kwa jinsi nilivyompenda nikapanga kumlinda wasijekuniambia niachane nae, ni jambo ambalo sikutaka kusikia hivyo nikadanganya imeharibika

Lakini mama ni mtu mzima aliguna tu, hili likapita kidogo pakatulia.
Baadae kidogo kuna binti nilikuwa nafahamiana nae alipata kutembelea mkoa anaofanya kazi BM, akaniambia nimekutana na mkeo ila huu mkoa haumpendi ni kama amepungua kidogo

Mimi nikaunga matukio, alipokuja kwangu alinawiri, na sasa naambiwa kapungua, huyu katoa mimba, iwe yangu au ya mwingine yote ni mabaya. Dah!!

Baada ya miezi kama mitatu tukiwa tumeshavuka mwaka, yaani ni mwezi wa tatu wa mwaka uliofuata dada yake aliyekuwa mkoa niliopo (Ambaye ndiye alimtafutia kile chuo) aliugua ikabidi BM aje kumtazama, huyo dada yake anafanya kazi vijijini ni mtandaji huko. Basi BM akaniita twende wote kwa dada yake niliyemheshimu kama mkwe, nikafurahi sana, wajua ukipenda halafu ukaona penzi linapotea unaumia sana halafu umpendaye akionyesha kitu kama cha kuonyesha uzito wa penzi bado upo unaona kama amekutua mzigo fulani moyoni mwako.

Tukaenda kwa dada yake, tulikaa huko siku tatu mimi nikaondoka kurudi kazini maana niliomba ruhusa ndogo tu, cha ajabu wakati tunaagana akawa anaaga kana kwamba akitoka hapo anarudi kazini kwake mkoani kwake mbali kabisa, yaani hatujaonana muda mrefu, tumekutana juu kwa juu anarudia huko huko[emoji15][emoji15][emoji15] nikamsema akaona aibu ndio baada ya siku mbili akaja kwangu, ieleweke kwamba mimi na dada yake tunaishi mkoa mmoja wilaya tofauti
Kwahiyo akaja kama kawaida pete hanaga tena, akakaa siku moja akaondoka

Alipofika kazini kwake baada ya mwezi akaniambia ana ujauzito, akimaanisha alipokuja alipata ujauzito dah, sifahamu mahesabu ya siku za hedhi lakini nakumbuka tukiwa kwa dada yake alienda kwenye siku zake sijui zilikata lini, baada ya siku kama mbili au tatu akaja kwangu wajuzi wataniambia siku za hatari ni ngapi baada ya kukata hedhi.

Kwahiyo tumefikia hapo nilipoambiwa ana ujauzito, mimi kama kawaida nikafurahi na nikawajuza nyumbani....


Will Be Back...
 
Namtaleta Sana story zenu..mzee mwitore kawafungua akili [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Back
Top Bottom