Trump: Achilieni mateka kabla sijaapishwa la sivyo mtabamizwa kwa kiwango hakijawahi kuonekana katika historia ya Marekani!"

Trump: Achilieni mateka kabla sijaapishwa la sivyo mtabamizwa kwa kiwango hakijawahi kuonekana katika historia ya Marekani!"

If you think Trump is going to stop with the terrorist, you've got another thing coming.
 
Sijui kama unajua unachosema. Israel ni kiini macho kilichotengenezwa na wazungu ili kuwatisha waarabu baada ya kugundua mafuta. Eti wanasema Mungu aliwapa hiyo ardhii. Ina maana Mungu hakujua kuwa hii nchi ni ya Wapalestina? Kama kweli Mungu aliumba dunia, inakuwaje asahau kuwa Palestina ni ya wapalestina na hivyo asinge'wapa' hawa majambazi?
Wewe kumbe hakuna kitu kabisa! Umetokea wapi wewe usiye na uelewa kiasi hiki!!

Wayahudi hawakupewa nchi na mtu yeyote, walichoomba mwaka 1947 ni kutambuliwa na kuwa mwanachama wa Umoja wa mataifa.

Soma historia ya Dunia, eneo lote ambalo wakoloni wa kirumi waliliita Palestine, ni eneo lililokuwa la Israel and Judah kingdoms. Kubadilisha jina hakubadilishi ardhi wala eneo. Ni sawa na hapa kwetu watu wakidai ardhi yao, ardhi iliyokuwemo ndani ya Tanganyika, huwezi kusema kuwa haipo eti kwasababu iliyokuwa inaitwa Tanganyika umeibadili jina na kuiita Tanzania.

Toka kale, Wayahudi ilikuwa ndiyo jamii kubwa ndani ya Judah na Israel kingdoms, japo ndani kulikuwa na jamii ndogo ndogo kama zile za waarabu, wasamaria, waajemi, n.k. Hakukuwa na jamii iliyoitwa wapalestina, hawa wanaojiita wapalestina leo, ni waarabu. Kama waarabu hawa waliishi ndani ya kingdoms hizi mbili wakati wa kale, hata leo wana haki hiyo pia, ila ni ukichaa wa hali ya juu, useme waarabu wanaoitwa wapalestina wana haki ya kuishi kwenye hilo eneo ambalo lilikuwa la kingdoms hizo 2, halafu useme kuwa wayahudi hawana haki.
 
Anaropoka tu..maisha hayajawahi kuwa rahisi na mepesi kiasi hicho...
Trump ni kama.mtoto wa kizungu tajiri aliyezoea kila kitu kwenda anavyotaka kwa kulia tu.

Analazimisha wenzake wacheze mpira anavyotaka yeye kwa sababu mpira ni wake na yeye anafadhili wachezaji wengi.

Lakini watu hawapendi alivyo na kiburi, wanaanza kujiondoa kwenye timu yake, wengine wanafuma mipira yao, wengine wanacheza vitenesi.

Mwishowe Trump atajikuta hana timu watu wote wamemkimbia amebaki yeye anacheza mpira na mbwa wake tu.
 
Ni kutumia akili, unaweza kusababisha vifo vingi, sio wameshindwa kuwaokoa, ni hiyo hofu, Trump huna hofu? Usiingie kichwa kichwa.
 
He is so bold and always speaks with great authority
Japo huwa anaogea kwa kejeli na madharau ila deep inside anaongea ukweli na hapendi kabisa kona kona,
Hana lolote huyu, kwanza ana maadui wengi ndani ya marekani kuliko huko mashariki ya kati. Waliotaka kumtungua bado wapo.

Mashariki ya kati ilikuwepo, ipo na itaendelea kuwepo. Yeye ana miaka 4 tu, halafu bye bye.
Lazima mjue huyu ni mfanya biashara, ni pesa tu anazohitaji.
 
Mimi ni muislam lakini hua najizuia sana kutazama hii vita kwa mtazamo wa kidini na nadhani hata sio vita vya kidini kwasababu ukiwaangalia Saudia, Egypt na nchi nyingine kubwa za kiislam, mateso ya Wapalestina hua kama hawana time nayo sanaaa!

Pia hua nakosa logical reasoning kwa Hamas kuteka wanawake na watoto, wanaweza vipi kuwa proud mpaka kuonesha video wanavyowachukua mateka wanawake na watoto? Au wanajua wangechukua wanaume tuu dunia isingepigana sana kumshinikiza Netanyahu kutafuta njia za amani za kuwarudisha kwasababu wanaume tunahesabika tuko expendable?

Lakini tukirudi kwa kauli ya Trump najiuliza atafanya kitu gani cha nguvu kuwarudisha mateka zaidi ya ambayo Netanyahu keshafanya.

Tatizo hao mateka kwasasa Hamas wanawafanya kama human shields, any move ya kumpiga aliewashikilia automatically inawaumiza na wao ndo maana Netanyahu alitumia nguvu sana akaua uongozi wote wa Hamas ila mwishowe ikabidi tuu atangaze dau $5m kwa yeyote atakaewezesha kuokolewa mateka hata mmoja.

Labda atie presha kwa Iran ili in return Iran nae awashinikize Hamas kuwaachia mateka lakini pia hii inagoma kwasababu wameuliwa pia karibu uongozi wote wa Hezbollah na hakuna mateka alieachiwa, sidhani kama hii inaweza kuwa solved kwa kutumia nguvu labda waamue hawahitaji tena kuokoa mateka wakiwa hai which again is pointless!!
Mie pia naona vita sio ya kidini ila israhell hana shida na mateka aliisha watoa sadaqa zamani sana
 
Hao israel inawashika sio mateka ni wafungwa waliofanya makosa sasa october 7 hamas walivamia israel wakawashika raia wasio na hatia hovyo hovyo tena wanawake na watoto, wakabaka, wakalawiti , wakaua kikatili embu tuambie dini yako ya uislamu mtume aliwaambia mshike mateka wanawake na watoto? Na mbake na kulawiti
Ondokeni kwenye ardhi za watu wazayuni hakuna dini dini munaleta nyie wazayuni wa jf ila wapalestina wanataka ardhi zao na siii Vinginevyo yaani
 
Sijui kama unajua unachosema. Israel ni kiini macho kilichotengenezwa na wazungu ili kuwatisha waarabu baada ya kugundua mafuta.
Sasa hizi ndo tunazoziita conspiracy theories. Tupe link inayothibitisha kauli hii.
 
Back
Top Bottom