Trump aiambia Russia ichague mazungumzo na Ukraine au vikwazo zaidi hadi ifilisike kabisa

Putin ni lazima aachane na hii vita

zelensky kakubali kukaa meza ya mazungumzo, Putin anajifanya bado anakaza shingo

Putin akikaidi atanyooshwa tu
 
Kwa sasa Marekani anaweza kuweka vikwazo vip vitakavyo ifanya Urusi iogope?
Labda angesema kuwa ataivamia hapo kidogo maneno yange kuwa na uzito kidogo na sio hizo tumba za vikwazo.
Wabongo vituko tu yani upo zako tandahima unakula zako kiporo cha ugali unajikuta unaijua urusi kuliko trump anavyoijua
 
Urusi haiwezi kufilisika kutokana na kuwepo kwa vikwazo
 
Watu wenye uelewa na Geopolitics humu, hizi mada zingine muwaachie wanaojadili kwa hisia humu kuliko kubishana na watu wasiopenda kujifunza
 
fuatilia vizuri kuhusu namna gani Russia alijipanga na vita. acha kufatilia false news za vyombo vya vibaraka kama CNN, BBC & Al jazeera. mfollow ibrahim rahby pale mjini insta upate taarifa
 
Mkuu ile operation Urusi hakutegemea kufika huu mwaka wa 3 , anachopoteza anakijua, mtu mpaka anakwenda kuazima wanajeshi North Korea wewe unafikiri ni kawaida? Trump ni muungwana sana Kampa OFA ya kiutu uzima tusubiri tuone atapokea vip OFA
Wewe umejuaje kama Russia hawakua wanajua vita itachukua muda gani, kwa unataka kutuambia Russia na vita zote alizopigana na uwezo wake wote wa inteligensia hawakuwaza plan b kama vita ingechukua muda mrefu
 
fuatilia vizuri kuhusu namna gani Russia alijipanga na vita. acha kufatilia false news za vyombo vya vibaraka kama CNN, BBC & Al jazeera. mfollow ibrahim rahby pale mjini insta upate taarifa
Kila mtu anaona wala hakuna siri, hii vita sasa ni miaka 3 Urusi hakutarajia hili kutoka Ukraine
 
Wewe umejuaje kama Russia hawakua wanajua vita itachukua muda gani, kwa unataka kutuambia Russia na vita zote alizopigana na uwezo wake wote wa inteligensia hawakuwaza plan b kama vita ingechukua muda mrefu
Ile ilikuwa ni military operation ndio maana Target ilikuwa ni kuondoa unazi ambapo ni pamoja kumtoa mtawala wa hao wana ambaye ni Zelensky, majeshi ya Urusi yalifika mpaka nje ya KYIV baada ya kukutana na upinzani mkali wakakimbia na kubadilisha tena lengo la military operations wakasema sasa wanataka kuchukua Luhansk na Donetsk, akabadilisha gia angani Putin, hakutarajia aliyo kutana nayo Ukraine , Ndio unaona sasa kwasababu mambo yamekuwa magumu inabidi atafute namna ya kupambana sasa ndio akapiga mbio ndefu Korea kaskazini na Iran, tena Nakukumbusha wakati ananunua Drone kwa mara ya kwanza alimficha Iran kuwa anakwenda kupigana na Ukraine mpaka Iran wa watu anaanza kujitetea kuwa hakujua kama Urusi anaweza kutumia kwenye vita

 
Urusi kufilisika kwa vikwazo siyo kazi rahisi kama unavyofikiri. Urusi bado ni nchi kubwa sana yenye rasilimali nyingi sana.
Rasilimali nyingi sio hoja na ni kweli ni nchi inayoongoza duniani kwa hizo rasilimali lakini sasa hizo rasilimali zimeisaidia nini hadi wenyewe ndio wa kuwekewa vikwazo badala ya wenyewe ndio wangekuwa wanawawekea wengine vikwazo.

Sasa huoni kwamba kuwa na raslimali nyingi sio suluhisho kuna mengine zaidi ya rasilimali.
 

Ni kweli kabisa kwamba kuwa na rasilimali nyingi siyo suluhisho, lakini kumbuka kwamba Urusi ni nchi kubwa sana kwa eneo la kijiografia kuliko nchi zingine zote kabisa hapa duniani. Aidha, nchi ya Urusi pia imebarikiwa kuwa na Watu (Raia) wengi wenye akili nzuri sawa sawa kabisa ambao Kama Utawala wa nchi hiyo ungewatumia vizuri zaidi hao Watu Basi nchi hiyo ingeweza kuwa miongoni mwa nchi kumi za juu kabisa hapa duniani zenye uchumi mkubwa zaidi. Whether we like or not, Ukweli mchungu unabaki kuwa nchi ya Urusi ina uchumi ambao siyo mbaya sana ukilinganisha na nchi nyingi sana zilizopo katika ulimwengu huu.
Kinachoikwamisha Urusi aina ya Mfumo wa Utawala uliopo kwenye nchi hiyo, yaani Sera na Itikadi za Siasa za Kikomunisti/Ujamaa. Endapo kama Utawala wa nchi hiyo utabadili mtazamo wake na kuchukua mkondo tofauti juu ya Sera zake za Siasa za Kikomunisti/Ujamaa, Basi upo uwezekano mkubwa sana nchi hiyo ikapaa ghafla kiuchumi na kuweza kuzikaribia nchi za Marekani, China na Japan katika Uchumi wake.

China ina uchumi mkubwa sana na kuipiku Japan kutokana na ku-adopt Sera za Siasa Mseto za Itikadi za Kikomunisti, Ujamaa, Ubepari n.k. Utawala wa nchi hiyo ya China ulishituka mapema zaidi kwamba Sera ya Siasa za Kikomunisti/Ujamaa peke yake zisingeweza kuipaisha nchi hiyo kiuchumi kwa kasi ya haraka kama walivyokuwa wanataka, that's why wali-adopt Mfumo wa Ubepari na kuruhusu Mfumo wa Soko Huria.

NB:
Ni Mfumo wa Soko Huria siyo Mfumo wa Soko HOLELA!
 
Acheni ujinga, Trump ni mjinga kama wajinga wengine. Dunia sasahivi imebadilika sana. Vikwazo vimedunda ktk nchi ndogo kama North Korea na Iran ndio vije viweze kwenye taifa kubwa kama Russia?
Umesema vikwanzo vimedunda iran na north korea? Rudi kasome tena, huna idea nini inasema

Rais mpya wa iran alipoingia madarakani moja ya sera zake ni kuongoea na mataifa ya ulaya kulege,a vikwazo. Uchumi wao hauleweki sababu ya vikwazo

North korea ndio kabisa, is why bado wako nyuma sana kiuchumi, vikwazo

Shukuru Mungu uko bongo land hamna kitu kama hiko
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…