TTCL fiber na Voda Supakasi ipi yafaa kwa matumizi ya home intaneti?

TTCL fiber na Voda Supakasi ipi yafaa kwa matumizi ya home intaneti?

ni hivi mimi natumia VODACOM SUPAKAS internet since last July, na napata 10mbps kwa gharama ya 115,000 (its unlimited).

kwa mimi nililipa security fee (2month) na unapewa router free na wanakuja kukufungia antena. Mnaweza tumia hata watu 10 na speed yake is good honestly unaweza download hata movies au kustream.

Payment yao ni post paid.

sijawahi tumia TTCL fibre but nitajariubu kuulizia pia hiyo supakasi simcard nione inakuwaje
Router wanayotoa inakubali kuunganisha kwa waya (Ethernet)? Model gani?
 
Kwa uzoefu wangu leo umetimia mwez mzima tukiwa na mradi wa fibre ya ttcl ikiwa kwa ofisi ,package inayolipiwa ni ya laki hio speed n nzur ila kuna ka tabia ka kuminya sometimes so vpn inatatua ila sio mara kuna mda adi video za resolution ya 1444 kama sijakosea ile zaidi ya 1080 zinakua zina ganda ganda
 
Kwa uzoefu wangu leo umetimia mwez mzima tukiwa na mradi wa fibre ya ttcl ikiwa kwa ofisi ,package inayolipiwa ni ya laki hio speed n nzur ila kuna ka tabia ka kuminya sometimes so vpn inatatua ila sio mara kuna mda adi video za resolution ya 1444 kama sijakosea ile zaidi ya 1080 zinakua zina ganda ganda
Ofisi mnatumia wengi mkuu? Unaweza kuibia muda hakuna watu ofisini kama unapata full speed? 100mbps?
 
Voda ipo mzee sisi tunatumia ofisini huu unaenda MWAKA 2
kuna kipindi huduma ilisuasua
ila kuanzia mwaka jana katikati mwanzo mwisho inakimbiza hata router walitupa kubwa ya HUAWEI awali tulikuwa tunatumia Mi-fi za ALCATEL

KWA makadilio ya matumizi kwa miezi 3 tangu novemba mpk leo milivoangalia tushatumia zaidibya terabyte 2 za data(2tb)
ambazo tumelipia kama laki 3 na 45 kwa maana ya laki na 15 kwa mwezi
hvyo tunaweza sema tumenunua gb 700 kwa laki tu na 15 kila mwezi
na mm ndio natumia sana 7bu ndio pekee nadownload mafile makubwa makubwa kwa siku 1 naweza downloda hata gb 20 ni movie tu au APPS

hyo ndugu namshauri achukue VODA
ttcl ni kichomi hutakuja kujuta baadae

VODA unlimited ni REALY sio blahblaha

ila tu vigezo mashart kuzingatiwa hapo ndio kipengele
Hiyo ni fibre au unapewa tu moderm?

Manake hata mtu akiwa kibaha ambapo hakuna fibre anaweza unganishwa na hii huduma?
 
Kwa uzoefu wangu leo umetimia mwez mzima tukiwa na mradi wa fibre ya ttcl ikiwa kwa ofisi ,package inayolipiwa ni ya laki hio speed n nzur ila kuna ka tabia ka kuminya sometimes so vpn inatatua ila sio mara kuna mda adi video za resolution ya 1444 kama sijakosea ile zaidi ya 1080 zinakua zina ganda ganda
Asee bongo nyoso, wateja si wachache wa fibre inakuaje wanaminya.

Je, wanaminya kwa muda gani? Siku? Masaa? Wiki?
 
Asee bongo nyoso, wateja si wachache wa fibre inakuaje wanaminya.

Je, wanaminya kwa muda gani? Siku? Masaa? Wiki?
Inategemea. Ofisi yetu haina watu wengi tuko ,13super user ni mimi na baadhi hata smartphone hawatumii .kiufup ni wapuuz yaani youtube kuna mda 720 haiplay na mradi umekata pesa ndefu zaidi ya km3 mzee kuweka kila kitu sio mchezo
 
Wakuu mbona hatudiscuss kabisa kuhusu halotel fibre?
Au huku hakuna watumiaji wake?
Wana mtandao wa fibre Tanzania nzima mjini hadi vijijini

images.jpeg


img_20190105_220739_3371105139275.jpg

CY_77FUWcAAtPlT.png
 
mimi nmeambiwa kuvuta fiber cable ttcl mpka hapa nlipo nikaribia milioni 4 alafu umbali na fiber ya ttcl ilipo ni chini ya 1km sasa sjui izi charges ni kweli au vipi

Inawezekana ni kweli mkuu maana nilisikia ni ghari sana hii fiber
 
Ni unlimited? Gharama zikoje?

Na mpaka wana advertise router ya simcard hio si fiber
Mm ninajua wametandaza fibre Tanzania nzima ndo mana nasema hivyo niliwahi kwenda ofisini kwao kipindi nipo morogoro wakaniambia bei mpaka waje kufanya survey
Hapa nilipo luna fibre 3 zimepita halotel. Voda na Ttcl
 
Mm ninajua wametandaza fibre Tanzania nzima ndo mana nasema hivyo niliwahi kwenda ofisini kwao kipindi nipo morogoro wakaniambia bei mpaka waje kufanya survey
Hapa nilipo luna fibre 3 zimepita halotel. Voda na Ttcl
Hizo ni fiber za minara mkuu, kuunganisha mnara mmoja na mwengine, halafu mtu wa kawaida unapata Internet toka kwenye mnara ndio maana unahitaji line.

Fiber yenyewe unakuja waya kama waya huhitaji line, na kama mtaani upo mwenyewe unaetaka fiber ndo hapo unasikia wanakwambia kuileta itacost milioni kadhaa.
 
Hizo ni fiber za minara mkuu, kuunganisha mnara mmoja na mwengine, halafu mtu wa kawaida unapata Internet toka kwenye mnara ndio maana unahitaji line.

Fiber yenyewe unakuja waya kama waya huhitaji line, na kama mtaani upo mwenyewe unaetaka fiber ndo hapo unasikia wanakwambia kuileta itacost milioni kadhaa.
Ndio hizo hizo wameniambia laki 7.5 20mbps omg
 
Back
Top Bottom