TTCL hoi kwenye soko la mawasiliano nchini

TTCL is a hopeless company.
Nina namba yao. Nina mpango wa kuitupa.Nilikuwa na ki-modem chao, nimeshakitupilia mbali huko.
 
Biashara ya simu za mkononi ni nyanya sana kwa TTCL, ndiye anayewawezeshea mawasiliano karibia wote uliowataja, Tanzania mpaka nchi jirani!
Sent using Jamii Forums mobile app
 
TTCL iko vizuri mkuu, hiyo internet unayotumia kupost hapa iwe ni unatumia Vodacom, tigo, smart, Zantel au airtel jua tiari ushawalipa TTCL, unapoona wanatoa gawio usidhani ni hadithi.
We huwajui...
1. Market share 1% utasemaje wapo vizuri..??

2. Zamani backbone sites za makampuni mengine ilikuwa ni kupitia towers za TTCL... MFANO..pale Mkutanga AIRTEL walikuwa wanapitisha mawasiliano yao pale yakielelea Mtwara Lindi, Masasi na Tinduru. Mnara wa mkuranga ukizima tu, inamaanisha huko kote hawana mawasiliano... sasa kumpata mhandisi wa TTCL aje atatue tatizo, nayo ni down time nyingine... gari analo dereva..mafuta anasaini mtu wa logistic, then atafutwe mhandisi aliko apelekwe kutatua tatizo. Na usiombe iwe Wekend ndo balaa.... UKIRITIMBA... WENZAO MAGARI WALIKUWA NAYO WAHANDISI MAJUMBANI.. IKITOKEA ISHU ANACHOMOLA STRAIGHT KWENDA ENEO LA TUKIO

Hali hii ilipelekea wengine kuamua kuhama.. wakajenga towers zao na TTCL inakosa mapato makubwa yaliyotokana na wengine kutumia sites zao... ISHU NI UIKITIRIMBA.. kuanzia huko uhandisini mpaka malipo ya suppliers wao
 
Tatizo la TTCL hakuna business plan, wanalamisha watumishi wa umma watumie laini zao ila mtaani siwaoni wakitafuta wateja

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna watu wanasema soko la kuanzisha kampuni ya simu ni gumu lakini mimi napinga. TTCL kama wangekuwa na uongozi wenye maono na juhudi wangewagagaza hawa kina Vodacom, Tigo etc vibaya sana. Nyingi za kampuni za simu tulizonazo zinaendesha huduma zake bila kujali malalamiko lukuki ya wateja. Inahitaji kampuni itakayokuwa inajali wateja na kuwapunguzia bei tu na hao wengine watalimia meno. Ila si ajabu ukakuta hata uongozi wa TTCL uko kwenye payroll ya haya makampuni mengine ili wasiifanye TTCL iinuke.
 
Mkuu, kwema?
 
Ttcl inauawa na watendaji wake wenyewe. Imekaa kama shamba la bibi pamoja na juhudi zote za kubebwa na serikali bado inataka kudekezwa kama yatima hakuna ubunifu wala malengo kibaya zaidi HAWAJALI WATEJA WAO!! WALISHAJIONA NI GIANT'S WANAOJITOSHELEZA!!!
Walipokuja na slogan Rudi nyumbani kumenoga waliaminisha wateja kwamba kweli nyumbani kumenoga mwisho wa siku NYUMBANI KUMEDODA!!
 
TTCL iko vizuri mkuu, hiyo internet unayotumia kupost hapa iwe ni unatumia Vodacom, tigo, smart, Zantel au airtel jua tiari ushawalipa TTCL, unapoona wanatoa gawio usidhani ni hadithi.
Mkuu huo ni mkongo wa taifa (NICTBB) TTCL ni msimamizi tu kama ilivyo konda na mwenye bus!! Ila cha ajabu TTCL bei zao za kuunga internet hususan fiber ziko juu kuliko hao "wateja wao!!!"
KUNA TATIZO MAHALA FULANI...
 
Kisha mtu anataka akuaminishe kwamba wao ndio wanaouza jumla kwa wengine ina maana WANAJIHUJUMU MAKUSUDI AU?
 
W Naomba niseme kwa kunong'ona "tatizo ni c....c...emu!!"
 
Siku zote serikali haiwezagi kufanya biashara

Ova
 
Chama kinahusikaje sasa?
Wala hilo lisikushangaze Mkuu. Ila mimi nilinong'ona tu sikupaza sauti ila kwa sababu umeisikia nitakuuliza kijiswali ili twende sambamba; hivi kwani mbia mwenye hisa kubwa TTCL ni nani? Je usimamizi mkuu ama ruzuku hutoka wapi? Ukipata jawabu hapo utafahamu hoja yangu ilipo.
Kwa nyongeza "kwa nini TTCL yenye miundombinu kila kona ya nchi hii ishindwe kutandaa ilhali hao walioanza juzi 1998+ wameenea kila kona ya nchi? Je kwanini washindani (wateja wa ttcl) wanaosambaza mkongo wa taifa kwa wateja wao gharama zao ni chini na vifurushi vyao vina kasi kuliko msambazaji mama? Kwa mfano; ukitazama ukubwa wa njia wanayotumia ttcl kwenda kwa wateja ukafananisha na vijikampuni vingine waweza amini ukubwa ule unamaanisha ubora wa huduma lakini wapi ni changamoto tupu!! Ipo haja ya ttcl kujitathmini na kujiamini vinginevyo haitatofautiana na mashirika mengine ya umma yaliyokufa au yanayochechemea.
 
TTCL iko vizuri mkuu, hiyo internet unayotumia kupost hapa iwe ni unatumia Vodacom, tigo, smart, Zantel au airtel jua tiari ushawalipa TTCL, unapoona wanatoa gawio usidhani ni hadithi.
Sio kweli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…