Tuache kudanganyana, Ajira zina afadhali zaidi kuliko kujiajiri, watu wengi waliojiajiri ndio wapo kwenye utumwa

Tuache kudanganyana, Ajira zina afadhali zaidi kuliko kujiajiri, watu wengi waliojiajiri ndio wapo kwenye utumwa

Kila kitu ni mentality na aina ya kazi uliyo jiajiri nayo.
Amna raha kama kazi ya kujiajiri kikubwa tu upende hiyo kazi.....
Uweze kuifanya vizuri hiyo kazi ikue.....
Uwe na time table nzuri ya kazi na mpangilio wa muda kwenye kazi yako.
Hakika ukizingatia huwezi kuwa mtumwa na pesa lazima upate.
 
Jamaa yangu mmoja alipata mtaji na mafanikio ya biashara akiwa muajiliwa akaona muajiliwa kuna mnyima mda wa kufanya mambo yake, akaacha kazi akaenda jiajiri rasmi bwana wee

Uko akakutana na misingi ya kujiajiri, kusanya sana tumia kidogo, fitna, ushirikina, ujanja, jamaa akapambana navyo at the end kabaki jina tu kashindwa mapambano ya mtani

MY TAKE
Ukiwa umeajiriwa na umejiajiri heshimu sana ajira yako kwani mafanikio ya kujiajiri kwako yanabustiwa na ajira yako
 
Shida ya kuajiriwa Kwanza unapoteza mda wako mwingi kumtumikia mtu na wengi tunawaona mtaani wakishaacha kazi wanakuwa Wana maisha magumu Sana na hata wakipewa pensheni hazikai mwisho wa siku anakuwa omba omba maisha halisia ni kujiajiri na unakutana na changamoto nyingi za maisha na mwisho wa siku unazizoea

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Kujiajiri hupelekea kila siku unaumiza kichwa na kupata pressure za ajabu ajabu juu ya biashara yako. Ndo maana wengi wao huzeeka mapema.

Hali kadhalika mawazo na hofu juu ya mwenendo na maendeleo ya biashara yako.

Kujiajiri kumesababisha watu wengi sana kuwa wachawi kwa ajili ya kuboresha vipato vyao.

Kujiajiri ni safari ya kupanda na kushuka, na pia haieleweki na hata Maendeleo ya watu wake hayaeleweki pia.
Na kikukweli wengi waliojiri ndio watumwa wa biashara zao.
Hili lina ukwel kabisaaa..nimeingia kwenye mapambano ya kujiajiri..aisee ni frustrations za kufa mtuuu...ila siachi..i believe this is a real experience of life...
 
Kiinua mgomgo chako kwa kazi yako utakacho lipwa. Ndio namiliki Bank.
Tofauti n PESA iliyoko kwenye mzunguko w bzness yangu.
Asante mungu kwa kunifanya niwe entrepreneur.
Jamani raha kuona PESA zako ziko ongezeka kidogo kidogo BANK mpk kua sw n kiinua mgomgo cha mtu.
Pia fresh money ni raha mnoooo. Pia likizo unajipangia uende wapi.
HII NI KWA NIA NJEMA TU
Kila mtu ashinde mechi zake.
Ndio advantage ya biashara ulipo...ikisha kaa stable una enjoy ila before hapo unahenyeka na kumenyeka mpaka unatamani kukufuru
 
Najua kwa haraka haraka mtafikiria kunijibu kwamba "Mwajiri hawezi fikia mafanikio ya Mo ai Bakhresa" ....vuta pumzi tulia!! Hao kina Mo watoe akilini mwako maana wapo kundi tofauti kabisa ni wafanyabiashara waliofikia mafanikio ya biashara zao kujiendesha hata wakiwa wamelala.

Mtu mwenye ajira hapa bongo serikalini ana nafuu zaidi maana mwisho wa mwezi mwajiriwa ana uhakika ila aliejiajiri ni juhudi zake, akipoteza mda imekula kwake.

Mwajiriwa hata akifiwa, akiumwa, akioa/kuolewa, anapewa kalikizo.. hapo kila jumamosi na jumapili yupo free, bado ana likizo ya mwezi moja kila mwaka, sherehe za serikali na za dini haendi kazini, Ana muda mwingi wa kuweza kupumzika na familia na kufanya shughuli za kijamii.

Wafanyabiashara wengi nawajua tangu nimepata akili za kuijua dunia mpaka leo hii wao siku ya kupumzika ni christmas tu, wenye nafuu huwa wanapumzika jumapili pekee, siku zingine hizo ni bampa to bampa wanaondoka alfajiri wanarudi usiku, yani hata muda wa kuspend na watoto hawana,

Ukiwa kwenye ajira unaweza kujiajiri pia

Nani mtumwa hapo
Mawazo ya kufilisika
 
Kama kujiajri kwenyewe ndio huku kwa kuendesha boda boda,kibanda Cha mpesa,duka la reja reja,ufugaji wa kuku,kuendesha Tex,kuuza genge,
Huko kote ni stress sana,
Kujiajiri kwenye nafuu ni kwa wale wanaomiriki makampuni,Tena wameajiri watu kadhaa,hata akilala nyumbani,pesa inaingia,hiyo ni level nyingine,lakini una duka la tv,na cm kariakoo,useme hiyo ajira inakupa ahueni,aaah wapi.
Hizi ajira zetu za kujiajiri ni low key,kule Kenya zinaitwa "side hustle"zinakusaidia vijipesa tu,
Ila hako ka side hustle ukikalea kakakua,unaweza ukafika hatua,unalala mambo yanaenda unakuwa umewaweka wakulungwa wengine wakufanyie kazi
 
Kiinua mgomgo chako kwa kazi yako utakacho lipwa. Ndio namiliki Bank.
Tofauti n PESA iliyoko kwenye mzunguko w bzness yangu.
Asante mungu kwa kunifanya niwe entrepreneur.
Jamani raha kuona PESA zako ziko ongezeka kidogo kidogo BANK mpk kua sw n kiinua mgomgo cha mtu.
Pia fresh money ni raha mnoooo. Pia likizo unajipangia uende wapi.
HII NI KWA NIA NJEMA TU
Kila mtu ashinde mechi zake.
Wa hivi ni wachache Bwashee usijitoe ufahanu, majority are toiling
 
Najua kwa haraka haraka mtafikiria kunijibu kwamba "Mwajiri hawezi fikia mafanikio ya Mo ai Bakhresa" ....vuta pumzi tulia!! Hao kina Mo watoe akilini mwako maana wapo kundi tofauti kabisa ni wafanyabiashara waliofikia mafanikio ya biashara zao kujiendesha hata wakiwa wamelala.

Mtu mwenye ajira hapa bongo serikalini ana nafuu zaidi maana mwisho wa mwezi mwajiriwa ana uhakika ila aliejiajiri ni juhudi zake, akipoteza mda imekula kwake.

Mwajiriwa hata akifiwa, akiumwa, akioa/kuolewa, anapewa kalikizo.. hapo kila jumamosi na jumapili yupo free, bado ana likizo ya mwezi moja kila mwaka, sherehe za serikali na za dini haendi kazini, Ana muda mwingi wa kuweza kupumzika na familia na kufanya shughuli za kijamii.

Wafanyabiashara wengi nawajua tangu nimepata akili za kuijua dunia mpaka leo hii wao siku ya kupumzika ni christmas tu, wenye nafuu huwa wanapumzika jumapili pekee, siku zingine hizo ni bampa to bampa wanaondoka alfajiri wanarudi usiku, yani hata muda wa kuspend na watoto hawana,

Ukiwa kwenye ajira unaweza kujiajiri pia

Nani mtumwa hapo
.
 
Jiulize swali kwanini wenye mshahara wa 700k hawana uwezo wa kuwa na akiba ya 100k Kwa mwezi.mshahara hauwezi kukuta 10k ya mshahara mwingine .Kiufupi ukiwa kwenye ajira na unalipwa chini ya million tofauti yako na mama siwema anayechoma vitumbua vya miatano miatano ni ndogo sana ,utamzidi kuvaa ,madeni , kukopa kwenye vikundi na saccos.
Acha uongo salary ya 700k Kwa mtu mwenye nidhamu ya pesa anasevu 200k-300k na sio pungufu ya hapo..

Kumbuka Kuna watu wanaishi Kwa salary za 300-400 na wanakomaa.
 
Back
Top Bottom