Ahsante sana kwa shule ya gesi
Meneja Wa Makampuni meneja wa makampuni,
Kuna hawa wachina wa Anric gas company CNG hapo awali waliingia mkataba na DIT( Dar Institute of Technology) kutengeneza na kufanya installation ya mifumo ya gesi ya CNG kweny magari, je, serikali haiwezi kutumia makampuni yake kufanya hizo installation na kusaidia kupunguza gharama za maisha kwa wananchi hata kwa magari ya serikali na umma?
Je, ile kampuni ya pan Africa energy pale ubungo maziwa ni ya nani inahusika na kujaza CNG?
Nimeona magari ya Dangote yamefungwa mifumo ya gesi CNG je anapata wapi gesi asilia? Anamiliki mitambo yake mwenyewe?
Kwanini vituo vya gesi ni kimoja tu kipo ubungo tu? Kwanini visiwepo sehemu nyingine mikoani n.k?
Je, miradi mikubwa kama hiyo kwa nini wasipewe taasisi Kama JWTZ kwa mikakati kutokana na credibility ya taasisi zetu?
Ukiacha EWURA na mamlaka zingine, idara yetu ya usalama wa Taifa ( TISS) ina nguvu gani au uelewa gani na mamlaka na uwezo wa kushauri mambo muhimu ya rasilimali Kama gesi? Je, kuna au tuna vijana wangapi mpaka sasa katika Taifa letu waliosoma ndani na nje ya nchi na kubobea kwenye taaluma ya gesi?
Serikali inakwama wapi kubadilisha mifumo yote ya mafuta na kuweka iwe ya gesi mpaka pikipiki Kama gharama za mafuta ni kubwa?
Kwanini gesi isitumike kuzalisha umeme kurahisisha kukua kwa uchumi wa viwanda?
Ahsante sana nitaendelea kuuliza na kijifunza hapa.