Tuache porojo, hii ndiyo sababu ya kwanini Taifa Stars imepoteza. We're exactly where we belong

Tuache porojo, hii ndiyo sababu ya kwanini Taifa Stars imepoteza. We're exactly where we belong

Match fitness inaangaliwa baina ya wachezaji wanaocheza ligi linganifu.Mchezaji anaekaa bench Olympiacos (Greece league hii ni league kubwa nashangaa unaita ka league) ana fitness yakutosha kuliko mchezaji anaecheza mara kwa mara yanga au simba. Narudia tena hakuna kocha anaeweza kumuacha mkaa benchi everton, Brighton , CSk Moscow, Olympiacos au Getafe eti amchague anaecheza mara kwa mara simba au yanga, hayupo huyo kocha maana fitness anayopata akiwa kwenye training ni zaidi ya anaecheza mara kwa mara simba au yanga.
Ndio maana akina Elneny au Choup Moting wanaitwa timu zao za taifa Egypt na Cameroon pamoja na kukaa benchi kwenye vilabu vyao.

Pia ni sawa sawa na haiwezekani kupatikana timu bora ya taifa kwa wachezaji wanaocheza ligi isiyo bora hata kama wanajuana. Brazil au Argentina sio wajinga timu zao za taifa kuziunda kwa wachezaji asilimia kubwa kutoka ulaya.
Uko sahihi.Tujifunze kutanua wigo mpana wa wachezaji wetu kwenda mataifa mengine kuimarika.Ligi yetu leo tunaiona ina ushindani kati ya hivi vilabu vikubwa kwasababu ya uwepo wa wachezaji wakigeni ambao kimsingi tunaona uwezo wao ingawa nawenyewe bado hawana viwango vyakuitwa uko kwenye mataifa yao.Kwahiyo angalau nasisi badala yakulalamika tulipaswa kujenge uwezo wa wachezaji wetu wengi kwenda kutafuta changamoto nchi zingine ili tuwe na uwanja mpana wakupata timu ya taifa badala ya kuangaika kila siku na wachezaji wa yanga na simba ambao kimsingi nawao viwango vyao kwa sehemu kubwa vinabebwa na wachezaji wa kigeni.
 
Ulikuwa na idea nzuri ila mwisho ukaharibu ulivyoingiza ushabiki.

Issue kama hao wachezaji uliowataja wa Congo wapo kwenye ligi yetu wanawika, na wangeweza kuwepo kwenye kikosi cha timu yetu ya taifa kama ingewezekana, lakini pamoja na ubora wao hawapo kwenye timu yao ya taifa, hapa kama taifa tuna la kujifunza.

Kile kipigo tulikistahili kabisa. tena tuwashukuru wacongo kwa kutufunga 0-3 peke yake, wangeweza kutufunga hata 5.
 
Hivi baada ya kushinda World Cup 1966 England ilishashinda Kombe gani jingine ?

Kama kipimo ni ligi wachezaji wanazocheza basi England ingekuwa na Makombe ya Dunia sio mbali sana na Brazil na Germany na sio moja tu tena walilolipata wakiwa nyumbani kwao.... Na hio Euro ya 2020 ndio mara yao ya kwanza kufuki hata fainali...

Wakati kina Greece walishawahi kuchukua hilo Kombe.... Kwahio techincally na statistically huko unakosema wachezaji wengi wakicheza sio guarantee ya kufanya vizuri (unaweza ukawa na individuals with skills lakini team disintegrated au an average skill players lakini team working as a unit)....

Mkuu samahani Nimekupa Like 1000!
Uingereza ni 0 Kabisa!
Halafu eti kila siku sisi samahani mimi niondeo Watu wanaina Uingereza ndio mfano wa soka eti Tangu 1966 Walivyochukua world cup tena kwao hawajachukua Tena,Euro hivyo hivyo!
Mchezaji bora 1 tuu Keegan!
Sasa Angalia wenzao Italy,Spain,German France,Daa acha tuu,Sisi Tanzania Hatuna Tofauti na Uingereza Maneno meeengi.
Tuwekeze Kwwnye Riadha tuone vijana watafanya nini na Huko.
 
Acha kuchafua uzi wa mwenzako
Sasa anachafuaje Uzi wakati Uzi unahusu swala zima la mustakabali wa Soka letu ikiwemo wachezaji wa kigeni na makocha au kuna kitu kinafichwa hutaki tukijue kuhusu huyo Pablo?
 
Hapa mzee Baba alikuwa sahihi sana
,tunapaswa kuchukua wanajeshi

Mpira ni kipani ongeza na uwekezaji wa muda mrefu, tenga bajeti ya kutosha, jenga academy mpira ufundishwe huko, jenga shule za makocha, na usikariri hadi umalize form four ndio ucheze mpira yaani mtoto akichagua kucheza yeye atacheza kwa ufanisi akisomea kwa nguvu zote sio mara kile mara hiki, weka walimu wa aina za vyakula kwenye academy ili watoto miili yao ijengeke kimichezo, tafuta agents wa maana nchi mbalimbali ili vijana wakafanye trial za mara kwa mara uone kama utahitaji kusajili robo tatu ya timu za ligi ya ndani kutoka nje hapana, uwekezaji ukifanyika tutafika mbali lakini utegemee hamasa ya wanasiasa ndio ushinde haipo hivi tutapigwa kila kukicha
 
Tuwe waungwana. Kwa orodha ya timu zilizoingia kumi bora kombe la dunia Kanda ya afrika, Tanzania tungekuwemo ingekuwa kituko cha karne!
 
Back
Top Bottom