Tuache Unafiki: Bashe alichukua hatua sahihi kumaliza tatizo la sukari. Hongera Dr. Tulia kwa kumlinda na kulinda maslahi ya nchi

Tuache Unafiki: Bashe alichukua hatua sahihi kumaliza tatizo la sukari. Hongera Dr. Tulia kwa kumlinda na kulinda maslahi ya nchi

Mzalendo Mchwara.


Una akili kweli na inayofanya kazi??

Kilichokua kinahitajika, ndicho kilichoagizwa?? Kwann uagize Sukari nyingi kupita hitaji, maana yake Sukari yetu ya Ndani iloanzwa kuzalishwa mpaka mwezi 12 huko itakuaje ??.


MPINA anahoji, kwann uwape Tenda watu wasokua na SIFA?.. mfano, Itel, stationary,,, nikisema kwamba, hiyo Sukari ya ziada ni yahawa Mafisadi , na wao ndo walitoa Pesa kwenye vikampuni uchwara ili waagize Sukari kupitia vikampuni hivo ??.



Kwa uchache nirudie tu, hivi umetumia akili vizuri kweli???.
Typical JPM follower huna akili kabisa. Sasa nchi ina uhaba wa sukari, kilo ikauzwa mpaka elfu 8 eti mtu analeta Sukari hadi bei imeshuka watu bado mnalalamika.

Ingekua kosa kama angempa tender mtu mmoja pekee tungesema ni monopoly. Cha ajabu wameleta watu wengi na bei imeshuka sasa lawama za nini?

Je tulitaka sukari iuzwe kilo elfu 6 kisa wenye vibali hawaagizi? Hii nchi ina ujinga mwingi hatuwezi kuwa held hostage na watu wachache.

Kwa hili namuunga mkono Bashe,
 
Kwa hiyo kama makampuni ya kuzalisha sukari yalifanya uhuni wa kuficha sukari naye waziri akaamua kufanya uhuni kutoa vibali vya kuingiza sukari kihuni zaidi na kienyeji?
One wrong does not justify another.
Unatakiwa ujue taratibu za manunuzi serikalini zipo iwe emergence procurement au single source Waziri kaboronga kutoa vibali kwa kampuni zisizokuwa na sifa kwa maslai yake binafsi
Kwahiyo mfano siku DP world ikigoma kupakua mizigo basi nchi ikae bila huduma ya bandari kisa "taratibu" na "kanuni" za kumpata mwekezaji mpya "zinashughulikiwa"??

Hivi itakua nchi au kampuni binafsi?
 
Typical JPM follower huna akili kabisa. Sasa nchi ina uhaba wa sukari, kilo ikauzwa mpaka elfu 8 eti mtu analeta Sukari hadi bei imeshuka watu bado mnalalamika.

Ingekua kosa kama angempa tender mtu mmoja pekee tungesema ni monopoly. Cha ajabu wameleta watu wengi na bei imeshuka sasa lawama za nini?

Je tulitaka sukari iuzwe kilo elfu 6 kisa wenye vibali hawaagizi? Hii nchi ina ujinga mwingi hatuwezi kuwa held hostage na watu wachache.

Kwa hili namuunga mkono Bashe,
Naunga mkono hoja yako asilimia 100
 
Kwahiyo mfano siku DP world ikigoma kupakua mizigo basi nchi ikae bila huduma ya bandari kisa "taratibu" na "kanuni" za kumpata mwekezaji mpya "zinashughulikiwa"??

Hivi itakua nchi au kampuni binafsi?
Kosa moja halihalalishi kosa jingine.
Sheria na taratibu zipo zifuatwe sasa zinatungwa kwa nini?
Embu acha kujitoa ufahamu kutetea wizi
 
Hizi taratibu zinachelewesha maendeleo na haki ya walalahoi sana. Imagine aanze kufuatilia taratibu huku mwananchi anaendelea kuumia kwa miezi kadhaa!!


Sioni shida hata kama angepewa muuza mtumba akaleta hiyo sukari, na lengo la kuuziwa sukari bei ahueni tofauti na za hizo cartels za kipigaji za viwandani!!

As far bei ya sukari itashuka bei wapambana kushindana na products nyingine za huko duniani waache kulia lia tu hapa!!
Serikali yetu inajitabanaisha kama serikali inayofuata sheria.
Serikali inatumia fedha nyingi sana kugharamia utungaji wa sheria hizo sasa haikubaliki mtu avunje sheria tena waziri na alidanganye na bunge kwa sababu yeyote ile acheni wizi
 
Wakuu kwa sukari bashe mtamuonea tuu...
Ipo hivi mahitaji ya ndani ya sukari ni Tani 420,000...na uwezo wa viwanda vya ndani uzalishaji wake ni tan 280,000 hapa kuna ombwe la tani 140,000 za sukari ambayo itabidi iagizwe nje ili kukidhi mahitaji...

Mwaka jana kukawa na uhaba wa sukari sababu wazalishaji wa ndan au viwanda vya ndani kudai mashamba yalijaa maji...hii ilipelekea uhaba wa sukari hivyo sukari ikaanza panda bei...baadhi ya maeneo ilifika mpaka kilo sh 7,000...waziri bashe akatoa vibali kwa viwanda vya ndani kuagiza sukari nje ili kuzuia mfumuko wa bei ya sukari.,

Sasa wafanya biashara wa ndani kwa njama zao hawakutii agizo kupelekea sukari kupanda zaidi...Bashe alivyo ona agizo halijafanyika akawafutia vibali hivi viwanda vya ndani .,

Maamuzi aliyo chukua ni kuwapa vibali wafanya biashara wenye uwezo wa kuagiza sukari nje ili tu kuzuia mfumuko wa bei ya sukari na hapa ndio tunaona mpaka makampuni ya simu yalipewa tender ya kuagiza sukar nje na bei tuliona zilirudi mahali pake...ingawa ni nje ya utaratibu lakini ilitibu tatizo...

Kama wewe ungekuwa bashe ungefanyaje??? Binafsi nampa maua yake...sijajua tatizo lake na mpina lakini kwenye hili mnyonge mnyongeni haki yake apewe..
Mpina kaongwa hela na wenye viwanda
 
Typical JPM follower huna akili kabisa. Sasa nchi ina uhaba wa sukari, kilo ikauzwa mpaka elfu 8 eti mtu analeta Sukari hadi bei imeshuka watu bado mnalalamika.

Ingekua kosa kama angempa tender mtu mmoja pekee tungesema ni monopoly. Cha ajabu wameleta watu wengi na bei imeshuka sasa lawama za nini?

Je tulitaka sukari iuzwe kilo elfu 6 kisa wenye vibali hawaagizi? Hii nchi ina ujinga mwingi hatuwezi kuwa held hostage na watu wachache.

Kwa hili namuunga mkono Bashe,
Hivi mnatumiaga makalio kufikiria??.

Uhaba?? Nini ilikua kiini Cha uhaba huo wa Sukari?.

Je wazawa wetu wa Ndani wanaozalisha Sukari, waloshindwa ku anticipate mapema kua kutakua na uhaba??.

Na kama walijua Hilo, walitoa taarifa Kwa Bodi ya Sukari?.

Na kama Walitoa, walitoa muda gan?.


Je kama wazawa ambao Sheria inawapa Hali ya kuagiza Sukari, je BASHE aliwapa Kibali Baada ya muda gan Toka waandike Barua Yao??.


Kwa akili yako ndogo tu, unadhan Wazawa wetu Wamiliki wa Viwanda, wangeshindwa kuingia Sukari Ndani ya Nchi mapema kabisa, ikiwa Vibali wangewepa mapema??.


Kwamba Mtu ambaye shughuli zake zote ni Sukari, ashindwe kuingiza Sukari, badala yake mtu wa STATIONARY mwenye mtaji wa million Moja, Aweze kuleta Sukari Tani na matani??.


Kwamba kosa kama angempa mtu Mmoja?? Are you serious ?? Sheria zinataka Kibali Akina nani??

Je BASHE baada ya yeye kuona Wazawa wameshindwa , je alitangaza tenda hiyo kama Sheria zinavyotaka??.


Tukisema nyuma ya hizo kampuni uchwara, Kuna Fedha HARAMU za watu wachache , tutakua tumekosea?.


Yaan Bashe Atengeneze tatizo, aje na solution yake, alafu tumxhekee??.



Nia yake ni ipi?? Kuua Viwanda vya wazawa??? Kuua Ajira za watanzania? Kupunguza Kodi ?? Kuua Kilimo na kuua Wakulima??.


Hivi mna ukichaa????? .

Mnadhani Late JPM, alipoamua kufufua vya kwetu Hakua na akili??.

Yaan Leo hii, turuhusu Viwanda kufa, Kilimo Cha miwa kufa, Ajira kufa, Umasikini kuongezeka kisa TUMEMILIKISHA BIASHARA YA SUKARI KWA MAJAMBAZI YASOPUNGUA 10 ??.


NI AKILI AU MATOPE??.
 
Kwa miaka nenda rudi genge la wazalishaji wa sukari wamekuwa wakilichezea soko letu ili kupiga super profit.

Wanatengeneza uhaba wa sukari, wanaacha ipande bei, kisha wanapata vibali vya kuagiza nje na kuuza kwa bei ya juu. Tena wakati mwingine wanabadili vifungashio ili ionekane imezalishwa nchini.

Sukari ya nchi za nje kama vile Brazil na Maritius ni bei poa mno, kwahiyo hawa mabwana walikuwa na kila motisha ya kutafuta namna ya kutengeneza uhaba wa sukari ili wapewe vibali vya kuagiza..

Alichokifanya waziri Bashe sio tu ni uamizi sahihi bali ni uamizi wa kizalendo, nchi haiwezi kuwa inashikwa mateka na genge la watu wachache.

Alichokisema Luhaga juu watu wachache kuhodhi sukari: Luhaga Mpina: Usambazaji wa sukari haukuwa ukifanywa na mfanyabiashara mmoja wa Mwanza pekee, Waziri Bashe alidanganya

Going foward hii ndio iwe dawa, tuendelee kulilinda soko la wazalishaji wa ndani lakini pale kunapotokea uhaba basi yeyote mwenye uwezo apewe kibali cha kuagiza sukari haraka iwezekanavyo.

Hongera Mh. Bashe kwa kufikiri nje ya box na kuthubutu. Kwenye hili Mpina amechemka, yaani nchi ikose bidhaa muhimu kwasababu tu kuna wapuuzi wanajivutavuta kuagiza sukari? Thubutu!

=====

Kupata ushahidi na ufafanuzi wa Luhaga juu ya Mpina juu ya sakata la uhaba wa sukari soma:

- Luhaga Mpina: Waziri Bashe na Mwigulu walitengeneza uhaba wa sukari nchini, zilikuwa njama za kuiba mapato ya nchi

- Luhaga Mpina amshukia Waziri Bashe, adai amelidanganya Bunge, awataja Magufuli, Rais Samia

- FULL TEXT: Maelezo ya Ushahidi wa Luhaga Mpina kwa Spika wa Bunge Dkt. Tulia Ackson juu ya Waziri Hussein Bashe kusema Uongo Bungeni kuhusu Sukari
Kumbe ni Mzalendo Uchwara????? 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣
 
Wewe nawe unaonekana huna unachokijua kwenye sekta ya sukari. Badala ya kujibu hoja za msingi unakuja na ngonjera. Huyo mtu hapo juu kakuuliza maswali ya msingi ngoja na mimi nikuongezee mengine japo najua huwezi kujibu!

1. Unajua jumla ya mahitaji ya sukari kwa nchi nzima ya Tanzania kwa mwaka?
2. Unajua capacity ya uzalishaji ya viwanda vyote vilivyopo Tanzania kwa mwaka?
3. Unaijua kwamba kuna capacity gap kati ya kinachozalishwa na kinachopungua?
4. Huo unaouita uhaba wa kutengenezwa, ni ndani ya ile gap au ni nje?
5. Unajua ni kwanini sukari ya nje inauzwa bei rahisi kuliko inayozalishwa Tanzania?
6. Kama sukati ya nje ni rahisi kuliko ya Tz, serikali inaporuhusu sukari ya nje i "flood the market" unataka nini kitokee kwa viwanda vyetu vya ndani?
7.
Nayajua majibu ya hayo maswali yote. Narudia tena, nimefanya kazi Kilombero sugar, Mtibwa sugar na Kagera Sugar. Wewe unasimuliwa hayo mambo, mimi nayajua kwa undani.

Uhaba wa sukari ulitengenezwa na wazalishaji wa sukari wenyewe wakitegemea ku exploit fursa ya wao kuwa waagizaji pekee wa sukari toka nje kwa ajili ya kufidia pengo lililopo kwenye uzalishaji.

Kwahiyo watu hao hawawezi kuwa part ya solution. Kuhusu nini kitatokea baada ya kujaza sukari ya bei nafuu kwenye soko ni hao wazalishaji kujifunza na kutorudia ujinga huo.

Some people can only learn the hard way. Walitegemea super profit sasa wanakwenda kula hasara. Hawatarudia ujinga huo next time. Na waziri kawaambia waziwazi, warudie waone.

Huyo Mpina hawezi kuwasidia. Waache konakona wafanye wajibu wao, kama umewashinda basi waachie hivyo viwanda wapewe wengine wenye uwezo wa kuendesha.
 
Bashe yupo sahihi sukari imeagizwa na kuletwa, imesambazwa wananchi wamepata unafuu. Swala la kiwango kuwa kikubwa ametolea ufafanuzi kuwa ni kutokana na hali ya hewa, mvua kuwa nyingi mwaka huu miundo mbinu ya uingiaji mashambani kuwa mgumu na hali hiyo itapelekea viwanda vyetu kuchelewa kuanza uzalishaji kwa muda mrefu, hivyo ili kuondokana na tatizo la upungufu wa sukali Wizara ikaagiza kiwango kikubwa. Kuhusu nani amepewa kibali wakati sukari imeletwa sioni kasoro, wangeshindwa au kuleta kwa bei kubwa hapo tatizo lingekuwepo. Mpina Msukuma na anasukumwa na wajanja waliobanwa maslahi yao
 
Ukiondoa kodi na ushuru mwingine kwenye sukari, kilo moja ya sukari itauzwa chini ya shilingi 1,000. Sasa hapo ndio utajua anaemuumiza mwananchi ni nani.

Kwa hoja hii tuache kupambana na waagiza sukari, tupambane na serikali iondoe kodi kandamizi kwa wazalishaji ili bei iwe nafuu kwa mlaji.

Na siyo kupambana na anayeingiza sukari nchini then tunaacha kile kinachosababisha maisha yetu kuwa duni.

Wenzetu Kenya wanaelewa umuhimu wa sheria zinazopitishwa namna zitakavyokandamiza wananchi.

Hata leo hii Bashe angefuata sheria bado hizi cartels za wazalishaji wa sukari wangefanya kila namna sukari iadimike ili wapige faida ndefu zaidi.
 
Serikali yetu inajitabanaisha kama serikali inayofuata sheria.
Serikali inatumia fedha nyingi sana kugharamia utungaji wa sheria hizo sasa haikubaliki mtu avunje sheria tena waziri na alidanganye na bunge kwa sababu yeyote ile acheni wizi

Kwa hiyo sheria ifuatwe tu hata kama inaonyesha kuwa na mapungufu!! Hili nakataaa kuwatetea hawa wenye viwanda.

Hoja ya Mpina ukiingalia kwa jicho la tatu imejikita kutengeneza monopoly ya viwanda vya ndani kuumiza wananchi!! Kuwatengenezea nafasi ya kutoshindana ili kuumiza wananchi!! Wakubaliane na hali washindane na wazalishaji wa viwanda vya nje.

Sisi tunachotaka walaji ni sukari ishuke bei, hizi nyingine ni bla, bla bla tu,
 
Je wazawa wetu wa Ndani wanaozalisha Sukari, waloshindwa ku anticipate mapema kua kutakua na uhaba??.
Walijua uhaba unakuja ila ni faida kwao maana supply ikiwa ndogo demand inapanda na ndio maana bei ikafika elfu 8 kwa kilo na kuna maeneo ilikua haipatikani kabisa.

Wazalishaji wa ndani hawawezi anticipate maana scarcity ndio huwanufaisha.
 
Kinachohitajika ni sukari ipatikane kwa bei nafuu.hayo ya nani mzalishaji au muingizaji wala hayana umuhimu kwa mwanachi wa kawaida kwasababu hayo yanakuja kutokana na usimamizi na uwajibikaji mbovu.
 
Kwamba Mtu ambaye shughuli zake zote ni Sukari, ashindwe kuingiza Sukari, badala yake mtu wa STATIONARY mwenye mtaji wa million Moja, Aweze kuleta Sukari Tani na matani??.
Acha kukariri tokea enzi za JPM hata Bakwata wana kibali cha kuagiza sukari kwani Bakwata wana kiwanda cha sukari? Kuna mambo kama hujui uliza.

Kampuni huwa zinafanya multiple business, ndio maana hata NMB licha ya kwamba ni benki ila imeshinda tender ya kutengeneza vitambulisho vya JAMII NUMBER!! Let alone inafanya biashara ya data hosting.

Jitahidi kutafuta exposure sio kuleta ujuaji kwenye mambo yaliyokuzidi uwezo
 
Back
Top Bottom