Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,506
- 16,003
DahIt's true, bakora za karma ni kama ufalme wa Mungu, kwa maana hamjui siku wala saa, na bakora zikitembea hakuna taarifa kuwa ndio bakora, ni majanga ya kawaida ya ugonjwa au ajali etc, the bottom line ni lazima upigike, madaraka, mamlaka au pesa, can't do a thing.
P.
Mkuu unaogopeshwa na nini katika hizo ramli unazoita chonganishi?Wanabodi,
Hili ni bandiko la wito wa Tuacheni Ramli Chonganishi Kuhusu Mhusika wa Shambulizi la Risasi kwa Mhe. Tundu Lissu, kupotea kwa mwana jf maarufu Ben Saanane, kupotea kwa mwanahabari Azory Gwanda, kuibuliwa kwa miili yenye majeraha kwenye viroba, au vitendo vingine vyovyote vya ukatili na umwagikaji damu kunalofanywa na watu wasiojulikana, hivyo kupelekea watu fulani fulani kuhisiwa kuhusika!, wito wangu ni "Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. Tuiachie "Karma" Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!".
Kwanza tuendelee kumuombea Lissu uponyaji wa haraka.
Nimenote katika baadhi ya mitandao ya kijamii, kumeibuka makundi ya watu kujenga nadharia mbalimbali kuhusu chanzo cha tukio hili, na hayo matukio mengine ya kupotea kwa Ben Saanane, Azori Gwanda na miili ya kwenye viroba, aliyepanga na aliyetekeleza, na wengine hadi kufikia kupiga ramli chonganishi kuwa aliyepanga mpango huo ni fulani, na kumtaji hadi majina!, mara ni fulani, mara ni fulani, alimradi kunyooshea watu vidole!, hili sio jambo jema hata kidogo!.
Kwa sisi wa imani ya Kikristu, dini yetu inatufundisha, "Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!". Tena kwenye ile kesi ya mwanamke kahaba aliyeshikwa ready handed, Bwana wetu Yesu Kristo akawaambia, "Na asiye na dhambi, awe wa kwanza kutupia jiwe!", hakuna aliyethubutu!.
Vivyo hivyo kwenye hili tukio la Lissu kupigwa risasi, na hayo mengine, maadam aliyelipanga ni binadamu, na watekelezaji ni wanadamu, tangu dunia hii kuumbwa, haijawa kutokea hata mara moja, uovu ukashinda wema, au uongo kuushinda ukweli, damu ya mwanadamu asiye na hatia, aliyeumbwa na Mungu, haiwezi ikamwagika bure bila kufidiwa, kila anayefanya uovu katika dunia hii, lazima atalipwa kwa uovu na malipo ni hapa hapa duniani, na kila anayetenda mema atalipwa mema.
Japo alichofanyiwa Lisu ni uovu mkubwa, mbaya na ukatili wa ajabu, na kwa hao wengine waliopotea, hakuna anayejua hatma yao ilikuwaje, you can just imagine!, lakini hakuna haja, wala sababu ya kuanza kunyoosheana vidole, tuviache vyombo husika kufanya uchunguzi na kutupatia majibu ya kina, kuhusu hao watu wasiojulikana, waliofanya ukatili huo, na endapo hivyo vyombo husika ndio wahusika na tukio hilo, bado kuna chombo kikubwa kuliko vyote kinachoitwa karma, ambacho ndicho pekee hutoa hukumu ya haki kwa kila kinachofanyika hapa duniani!.
Tumuombee Lissu to Get Well Soon, arejee nyumbani salama akiwa bukheri wa afya, tuombe muujiza wa Ben Saanae na Azori Gwanda, waibuke wakiwa hai toka huko mafichoni walikofichwa!.
Mungu yupo, kama alivyokusimamia Lissu hadi sasa bado uko hai, yeye ndiye pekee kupitia karma, atawahukumu watesi wako wako na watesi wa wengine hao!.
"The Power of 'Karma'- Ndio Hukumu Pekee ya Haki Kamili Hapa ...
Angalizo kwa Wana JF: Tuwaepuke "Prophets Of The Doom", kauli zao ...
Paskali
Ni ujinga kwa kweli.
Asante kwa uzi huu... Nina swali kidogo kuhusu Karma. Tumeelezwa kuwa Karma inatabia kama ya tukio la ' what goes around comes round' ...pia tumeelezwa kuwa karma ni sawa na sheria za Newton za Every action there is equal and opposite reaction. Swali lenyewe sasa....Mkuu, Ni wakati gani tunatambua kuwa Sasa Karma 'is going around' ama 'is coming around'....Na pia ni wakati gani tunaweza kusema sasa Karma is an ACTION na siyo REACTION?"Karma" Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!".
KaribuWe jamaa matakonini? Mbona watanzania wenzio wanapopotezwa unakaa kimya?, watu wanaotekwa hamjawahi kupaza sauti, watu wanapigwa risasi mpo kimya uzalendo ni kwenye mambo yanayomhusu magufuli pekee?? Uzalendo sio kutetea madege hayo uzalendo ni kusimamia misingi ya utawala bora, haki n.k nyie kwenu uzalendo ni kumsifia magu hata kwenye ujinga... Acha upuuzi Paskali umenikera
Si mafaili walisema yamefungwa ... Uchunguzi huo unafanywa na nani....!!?? Kuna jeshi jipya la polisi linalofanya uchunguzi tofauti na hili !!??Wanabodi,
Hili ni bandiko la wito wa Tuacheni Ramli Chonganishi Kuhusu Mhusika wa Shambulizi la Risasi kwa Mhe. Tundu Lissu, kupotea kwa mwana jf maarufu Ben Saanane, kupotea kwa mwanahabari Azory Gwanda, kuibuliwa kwa miili yenye majeraha kwenye viroba, au vitendo vingine vyovyote vya ukatili na umwagikaji damu kunalofanywa na watu wasiojulikana, hivyo kupelekea watu fulani fulani kuhisiwa kuhusika!, wito wangu ni "Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. Tuiachie "Karma" Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!".
Kwanza tuendelee kumuombea Lissu uponyaji wa haraka.
Nimenote katika baadhi ya mitandao ya kijamii, kumeibuka makundi ya watu kujenga nadharia mbalimbali kuhusu chanzo cha tukio hili, na hayo matukio mengine ya kupotea kwa Ben Saanane, Azori Gwanda na miili ya kwenye viroba, aliyepanga na aliyetekeleza, na wengine hadi kufikia kupiga ramli chonganishi kuwa aliyepanga mpango huo ni fulani, na kumtaji hadi majina!, mara ni fulani, mara ni fulani, alimradi kunyooshea watu vidole!, hili sio jambo jema hata kidogo!.
Kwa sisi wa imani ya Kikristu, dini yetu inatufundisha, "Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!". Tena kwenye ile kesi ya mwanamke kahaba aliyeshikwa ready handed, Bwana wetu Yesu Kristo akawaambia, "Na asiye na dhambi, awe wa kwanza kutupia jiwe!", hakuna aliyethubutu!.
Vivyo hivyo kwenye hili tukio la Lissu kupigwa risasi, na hayo mengine, maadam aliyelipanga ni binadamu, na watekelezaji ni wanadamu, tangu dunia hii kuumbwa, haijawa kutokea hata mara moja, uovu ukashinda wema, au uongo kuushinda ukweli, damu ya mwanadamu asiye na hatia, aliyeumbwa na Mungu, haiwezi ikamwagika bure bila kufidiwa, kila anayefanya uovu katika dunia hii, lazima atalipwa kwa uovu na malipo ni hapa hapa duniani, na kila anayetenda mema atalipwa mema.
Japo alichofanyiwa Lisu ni uovu mkubwa, mbaya na ukatili wa ajabu, na kwa hao wengine waliopotea, hakuna anayejua hatma yao ilikuwaje, you can just imagine!, lakini hakuna haja, wala sababu ya kuanza kunyoosheana vidole, tuviache vyombo husika kufanya uchunguzi na kutupatia majibu ya kina, kuhusu hao watu wasiojulikana, waliofanya ukatili huo, na endapo hivyo vyombo husika ndio wahusika na tukio hilo, bado kuna chombo kikubwa kuliko vyote kinachoitwa karma, ambacho ndicho pekee hutoa hukumu ya haki kwa kila kinachofanyika hapa duniani!.
Tumuombee Lissu to Get Well Soon, arejee nyumbani salama akiwa bukheri wa afya, tuombe muujiza wa Ben Saanae na Azori Gwanda, waibuke wakiwa hai toka huko mafichoni walikofichwa!.
Mungu yupo, kama alivyokusimamia Lissu hadi sasa bado uko hai, yeye ndiye pekee kupitia karma, atawahukumu watesi wako wako na watesi wa wengine hao!.
"The Power of 'Karma'- Ndio Hukumu Pekee ya Haki Kamili Hapa ...
Angalizo kwa Wana JF: Tuwaepuke "Prophets Of The Doom", kauli zao ...
Paskali
Karma iliyowajaa nikuamua kumuua Lissu? Mtakufa tu na mafunza watawatafuna vizur.Naam Paskali nimependa hii hoja ya kuachia Karma... Japo wapo baadhi husuasan ambao nafsi zao zinawasuta watakutukana.
Heshima kwako
Mkuu Kaka Mkubwa Wakudadavua, usemayo ni kweli, na nimeanza kuziona dalili za karma kufanya jambo.Naam Paskali nimependa hii hoja ya kuachia Karma... Japo wapo baadhi husuasan ambao nafsi zao zinawasuta watakutukana.
Heshima kwako
Mkuu Pascal Mayalla nakumbuka ulijibu swali langu hili hapa chini. Lakini majibu yako siyaoni jamvini na kwenye uzi huu. Uliyafuta majibu yale!?Mkuu Kaka Mkubwa Wakudadavua, usemayo ni kweli, na nimeanza kuziona dalili za karma kufanya jambo.
P
Asante kwa uzi huu... Nina swali kidogo kuhusu Karma. Tumeelezwa kuwa Karma inatabia kama ya tukio la ' what goes around comes round' ...pia tumeelezwa kuwa karma ni sawa na sheria za Newton za Every action there is equal and opposite reaction. Swali lenyewe sasa....Mkuu, Ni wakati gani tunatambua kuwa Sasa Karma 'is going around' ama 'is coming around'....Na pia ni wakati gani tunaweza kusema sasa Karma is an ACTION na siyo REACTION?
Kwa kifupi, ni wakati gani ama ni vigezo vipi tunatumia kutambua kuwa sasa Karma inaanzisha duara na ama sasa KArma inafunga duara?
===
Kwa haraka haraka ninajua kabisa umelielewa swali langu barabara. Nasubiri majibu Mkuu.
Mkuu Superbug, hii ni ramli chonganishi!.Tunaweza kwa uchungu kukaa kimya juu ya Azory gwanda kwasababu kidogo aligusa usalama wa nchi kule mkiru lakini Ben sanane alikosa Nini? Hivi mtu akiniambia Mimi ninaelimu ya la Saba wakati c kweli inampasa kupotezwa?
Ila asubuhi asubuhi unataka kutibua watu nyongo. Mtu akipotea mwenye wajibu wa kwanza kumtafuta ni mke/mume, kisha familia maana yaweza kuwa sio kupotea ila kuchepuka. Baada ya hapo ndugu, marafiki na hata mwajiri na mwisho kabisa Polisi.Mkuu Superbug, hii ni ramli chonganishi!.
Ben Saanane alipotea, hakuna ajuaye sababu, unless kama unaijua sababu, na ukiitwa kusaidia polisi utatoa ushirikiano
vinginevyo...
Hizi pen names humu jf zisitupe kiburi na jeuri ya kupitiliza kwa kusema lolote au kumtuhumu yoyote kwa kumtaja majina bila na ushahidi, tumuhurumie Mkuu Max, anateseka sana kwa ajili yetu, kwenye yale ya ukweli ni acha ateseke, na kusulubiwa, kwa sababu hata Yesu alisulubiwa kwa ajili ya dhambi zetu na ni kwa kupigwa kwake sisi tuliponywa, lakini tuhuma nyingine bila ushahidi ni kuponza tuu watu bure, kama kitu huna ushahidi usituhumu kwa kutaja majina!.
P
Hili ni vizuri kuachia hapa kwasababu whoever who was behind shooting ya Tundu Lissu ni shetani kabisa, the devil in human flesh, mimi siamini tunaye shetani wa aina hii, ila kwa vile sio kila kinachofanywa na serikali lazima kiripotiwe kwenye media hivyo mimi ninaamini 100% chini ya 100% serikali imechunguza, zile CCTV ni nyumba ya Kalemani ila sio CCTV za serikali, naamini hadi Mzee atakuwa ameulizia, na uchunguzi umekwama kutokana na kukosekana mashahidi wawili wakuu ambao ni muhimu sana. Endapo kugetokea fatality kazi ingekuwa well done, by now file lingeisha fungwa, lakini kwasababu mashahidi wapo, wanasubiriwa wahojiwe ndipo uchunguzi uendelee.Narration yako makes a big sense! BUT look: Mr, Pascal, usizidi kunipa mashaka! Mauaji, upoteaji, uteswaji, kesi za 'kipuuzi" wanazokutana nazo watu... Rais fulani hajawahi kuzikemea. Yoooooooooooooooooooooooooooooooooote yaliyotokea kwa Lisu sanasana alichojibu ni kuwa yule jamaa amelitelekeza jimbo! Wadau woooooooooooooooooooooote walisema ruhusu uchunguzi huru toka nje watampata aliyempiga risasi Lisu.. he never commented anything! Watu wamekutuhumu, kujibu tuhuma unafanyaje? Unasema Njoo mchunguze then ukweli utapatikana.
Pascal nambie yaliyotokea kwa Lisu kama angalikuwa hana mkono wake asingeruhusu kuona watu wanapoteza CCTV, wanaondoa walinzi, angelisema nataka kujua leo leo nani aliwaondoa walinzi! He never did that..... Maswali ni mengi yanayomwelemea.. irresisitible inference kuwa anahusika...
Ngoja niachie hapa......
Mkuu Konyola, nimekuleta huku kwasababu umewaombea Corona hawa wasiojulikana.Pascal mimi natamani yafuatayo; kwakuwa sina uwezo na madaraka natamani lile jopo lililokaa na kuona suluhisho la kumdhibiti Tundu Antiphas Mughwai Lissu ni kumtwanga Risasi COVID-19 iwapitie, wale waliotafuta upenyo wa kibabe wa kukwepa kumlipia Lissu gharama za matibabu na akati anastahili hadi mimi na umasikini wangu nikakopa na kutuma Tsh1,000,000/= kama mchango wa dhati ya moyo wangu ili Lissu apatiwe matibabu ya kuokoa uhai wake nasema COVID-19 ikiwa na jina la Yesu ndani yeke pamoja na moto wa maserafi na makerubi ikawapige hao wauaji kama upepo wa kisulisuli.
Wale waliohusika kuua na kufunga miili ya watz kwenye sandarusi na kwenda kuitupa mto Ruvu na wengine kwenye fukwe za bahari nasema COVID-19 popote ulipo kawapitie hawa wasaidizi wa Lucifer watangulie kabisa kule kwenye ziwa la moto.
Haiwezekani ktk nchi hii kuwe na watu wenye mamlaka ya kutoa uhai wa watu halafu tusio na uwezo wa kuwafanya chochote tushindwe hata kumuomba Mungu au shetani kuwasulubisha.
Pamoja na kwamba kisulisuli kilishindwa kuwabeba wanaume wa kuwaoa wale mabinti wa kanisa la mlima wa moto pendine ni kwa sababu ya uzito wao lakini bado nakiamini kisulisuli hakiwezi kushindwa kuwabeba COVID-19 na kwenda kuwafanyia INOCULATION hao niliowataja hapo juu.
Haiwezekani watu watekeleze mauaji ya watz wenzetu halafu bado tuendelee kuwasifia kisa teuzi, wapitie huu uzi hapa ili wajue kuwa hatuwapendi kwa matendo yao.
Kuna hawa wadudu wengine wanaitwa wasiojulikana ikitokea COVID-19 ikawasafisha pamoja na vizazi vyao Pascal huoni kama hii itakuwa ni baraka kutoka kwa Mnyazi Mungu kwa kutupunguzia watu wenye roho mbaya za Black Mamba a.k.a Koboko (Dendroaspis polylepis) au Anaconda a.k.a Water boa or Bull killer kama wataalam wanavyomfaham kwa jina la Eunectes murinus.
Nikipata bahati ya kuipata AK47 ikiwa loaded halafu nikaonyeshwa kwamba huyu ndiye aliyemfyatulia risasi Lissu Pascal otea nini kitatokea? Kama niliyoyasema hapo juu ni uongo na kwamba hao hawahusiki na madhila husika basi namkaribisha ZRAIL nyumbani aje anisalimie na si vinginevyo.