Sharamdala
JF-Expert Member
- Aug 14, 2022
- 3,558
- 6,538
Mechi ya Champions league mwaka 2000 Realmadrid vs Valencia ilikuwa binge la mechiNimekuwa shabiki wa soka kwa muda mrefu sana. Kwa muda wa miaka 20 sasa. Nimeangalia mechi nyingi sana na za kutosha, zaidi ya 1000 hadi leo hii.
Toka enzi za goli la dhahabu hadi leo hii ambapo goli la ugenini limefutwa kwenye mashindano ya Ulaya na technolojia ya VAR inatumika.
Nimeangalia fainali 6 za kombe la dunia, toka 2002 hadi 2022. Nimeangalia zaidi ya fainali 14 za Uefa Champions league. Nimeangalia mechi nyingi sana za mashindano tofauti tofauti na zenye matukio ya kusisimua na matokeo ya kustaajabisha....Jaribu kuwaza,,
Nani amesahau kuhusu usiku wa Liverpool dhidi ya Ac Milan 2005?..Je ile comeback ya Barcelona dhidi ya PSG 2017?...vipi kuhusu usiku wa Drogba pale Allianz Arena 2012?....Bila shaka wote tunakumbuka goli la Iniesta lilivyowapa ubingwa Spain mbele ya Uholanzi pale Soccer city kwa madiba....Na vipi kuhusu ile Acrobatic ya Wayne Rooney dhidi ya Man city dakika za kuelekea mwisho kabisa kwenye mechi muhimu ya kuamua bingwa wa EPL 2010/2011...Mungu amlaze pema Cheikh Tiote anayetukumbusha Comeback ya Newcastle dhidi ya Arsenal game ambayo Newcastle wanatoka nyuma kwa bao 4 na kufanya matokeo kuwa 4 kwa 4...vip kuhusu Madrid dhidi ya City UCL mwaka jana?
Hakika kuna mechi nyingi sana ambazo tumezishuhudia na kuzifurahia. Na ambazo zilituacha na kumbukumbu nzuri sana mioyoni mwetu. Lakini pamoja na hayo, kuna mechi moja ambayo kwangu mimi nimeiweka katika kilele cha ubora. Ndiyo, ni Mechi Bora zaidi ya soka ambayo nimewahi kuishuhudia. Unataka kuifahamu?
Usipate tabu, rudisha kumbukumbu zako hadi Jioni ya Tarehe 18.12.2022 pale Qatar...ARGENTINA vs FRANCE....Dakika 120 za dhahabu. Ni mechi kubwa iliyoamuliwa na wachezaji wakubwa katika hatua kubwa ya mshindano makubwa zaidi ya soka duniani.
Kwangu mimi Argentina Vs France ndio mechi yangu bora zaidi ya soka niliyowahi kuishuhudia toka nimeanza kuangalia soka....
Tuambie kwa upande wako, ipi mechi bora kwako!!!
Aisee kumbe huwa tunabishana na wazazi wetuKuna hiyo ya Simba na Stella Abidjan mwaka 1993. Ilikuwa fainali ya ambayo sasa inajulikana kama CAF Confederation Championship. Ndio mechi ilifanya niwe shabiki wa Simba mpaka leo.
Kabisa. Kila asubuhi uwe unanisalimia ndio uende kwenye majukumu yako.Aisee kumbe huwa tunabishana na wazazi wetu
Hizo za 90 uliziona au uliona marudioKwa mpangilio;
1.Bayern Munich vs Man utd UEFA Final 1999.
2.Liverpool vs AC Milan UEFA Final 2005.
3.Spain Vs Nigeria WC 1994 goli la ushindi la Negeria la Sunday Oliseh.
Mkuu mimi kipundi hicho nilikua na jamaa yangu ni shabiki wa Liverpool alinifunga shati kama wanavyofungwa wafungwa wawili asee ilikua na tension kubwa sana.Chelsea walianza lambwa mbili kwanza kipindi cha kwanza, nilikaa na kaka yangu shabiki wa Chelsea alinuna balaa yaani. Nikawa nacheka kama mwehu ndiyo kwanza nikamtia hasira, walivyosawazisha alishangilia kama hamnazo. Isingekuwa sub ya lampard ingeisha 4-2
1994 kombe la Dunia lilichezwa Marekani na mechi zilikuwa zinaanza saa 8:30 usiku. Mnalala kwanza kisha mnaamka mnaangalia mechi. Nikiwa Shinyanga kipindi hicho mechi zinaonyeshwa Bitiama Hotel na Bwalo la Polisi.Hizo za 90 uliziona au uliona marudio
Sawa mkuu1994 kombe la Dunia lilichezwa Marekani na mechi zilikuwa zinaanza saa 8:30 usiku. Mnalala kwanza kisha mnaamka mnaangalia mechi. Nikiwa Shinyanga kipindi hicho mechi zinaonyeshwa Bitiama Hotel na Bwalo la Polisi.
1999 nyumba nyingi zilishanunua TV tukitumia madishi makubwa. Hii niliiangalia nyumbani kwangu sebleni kwenye TV niliyonunua mwenyewe.
Umenielewa Mkuu?
Mimi nimeanza kuangalia live kombe la Dunia 1990 ushindi wa Germany dhidi ya Argentina kwa goli la penati ya Andreas Brehme.
Daah kwamba usijekukimbia ukumbini😁😁😃😅😅Mkuu mimi kipundi hicho nilikua na jamaa yangu ni shabiki wa Liverpool alinifunga shati kama wanavyofungwa wafungwa wawili asee ilikua na tension kubwa sana.
Ulisimuliwa au ulitazama mwenyew. Alisawazisha kwa kona sasa offside itokee wapi.Alafu extra aliingia marcelo upande mmoja di maria upande mwingine marcelo atletico aliita maji mma ila ni kweli walionewa lile goli la ramos la kusawazisha lilikua offside