Tuamke, tuwaamshe mizimu wetu, katika nyakati za hatari watusaidie

Tuamke, tuwaamshe mizimu wetu, katika nyakati za hatari watusaidie

Ndio maana jamii hizo zikaamua kuitupilia mbali.
Tumeitupilia mbali.
Unasahau kazi ya msikiti na kanisa, unasahau sanaa na ufundi wa hati, hisabati na kumbu hifadhi vilianzia hapa....kwamba tulikuwa tuna evolve, ndio wakaingilia kati na kuchomeka misumari katika mkufu utuunganishao, ndio Chinua Achebe akakwambia THINGS FALL APART
 
Wangoni na wahehe waliiomba sana mizimu ili iwasaidie vita dhidi ya wajerumani, ikawadanga kuwa watashida,
Kinjeketile Ngwale akadanganywa kuwa risasi ya mjerumani itageuka maji. Risasi haikugeuka maji, Jeshi la Wangoni likaangam
We mbona husemi awali wajerumani walichapwa na mkwawa?? Na hiyo usemayo ni historia changa ya juzi, Africa ilikuwepo tangu enzi na enzi, ni sisi tulianza kwenda Asia na Ulaya, tofauti ni kwamba, wakati sisi tulipeleka mwanga kule, wao ndio walioleta giza huku
 
Hebu ngoja nikuulize swali dogo tu, Bill Gates ndiye mbunifu wa MICROSOFT, sasa hebu niambie wakati anaibuni na kuitengeneza hii program wewe hukuwepo wala hukumwona, umesoma tu kwenye vitabu kuwa Bill Gates ndiyo mwanzilishi wa MICROSOFT na unaamini hivyo na kukubali. Sasa iweje unaamini sana kazi za Wanadamu kwa kusoma tu, lakini hutaki kuamini kazi za MUNGU kwa kusoma pia???

Kwanini unahoji uwepo wa MUNGU wakati kazi alizozifanya zinaonekana ikiwamo wewe mwenyewe ni kazi ya mikono yake, kila kitu unachokula ni kazi ya mikono yake, hewa unayovuta ni kazi ya mikono yake, kila kitu ni kazi ya mikono yake??

Habari za MUNGU umesoma kwenye vitabu, lakini unapinga na kuhoji uwepo wake na kazi za mikono yake unazikataa, mbona umesomo uwepo wa akina Bill Gates na kazi za mikono yao unazitumia lakini haupingi uhalali wao?? Kwanini unapinga uhalali MUNGU?

Mkuu nahisi kama umeenda chaka, mbona sijaona popote mtu akipinga uhalali wa Mungu? Au mimi ndiye niko chaka au sijui kusoma?
 
Nimeifukunyua hii kutoka Maktaba!

HISTORIA YA AFRIKA ILIYOFICHIKA - Na Mwl. Matteo E. Mwita

Kumekuwa na historia iliyopotoshwa kuhusu Bara letu la Afrika, historia hiyo imekuwa ikituelezea sisi waafrika na bara letu kama watu tulikuwa nyuma sana kimaendeleo, watu ambao hatuna chochote cha maana. Bara na watu tuliokuwa tumeghubikwa na kila aina ya ushenzi, kwa muda mrefu tumekuwa tukiaminishwa kuwa bila ya ujio wa wazungu tusingefikia hatua ya kimaendeleo tuliopo leo, chakusikitisha baadhi ya waafrika wamekuwa wakiamini ghiliba hizo kutoka kwa wazungu. Vitabu vingi vya kihishtoria vilivyo ndikwa na wanazuoni wa kimagharibi vimejaribu kulipaka matope bara letu, vimetulaghai kiasi cha sisi kujidharau na kujiona hatukuwa na cha maana. Ila kuna baadhi ya vitabu kama when we ruled: The Ancient and Medieval History of Black civilization na How Europe Undeveloped Africa, vimekuwa na mitazamo tafauti kuhusu bara letu na kujaribu kuonyesha mafanikio ambayo tulikuwa tumeyafikia kama bara kwa karne kadhaa nyuma hata kabla ya ujio wa wageni. Makala haya yanaangazia kwa ufupi mafanikio ya eneo mmoja la Afrika zama hizo.

Je, ulipata kujua kuwa karne ya kumi na nne mji wa Timbuktu uliopo Afrika Magharibi ulikuwa na ukubwa mara tano zaidi ya jiji la London na ulikuwa ni mji tajiri zaidi ulimwenguni? Leo hii London ni kubwa mara 236 kwa Timbuktu. Mji huo hauna chochote kinachoweza kuonesha kuwa ni mji wa kisasa, idadi ya wakazi wake imepungua kwa mara mbili ya idadi ya wakazi karne tano zilizopita, mji umezingirwa na mitaa michafu iliyojaa ombaomba. Timbuktu hauna uwezo tena wakutunza hata makavazi na majengo yake ya asili.

Katika karne ya 14, sehemu tatu tajiri kabisa duniani zilikuwa China, Iraki/Irani na Himaya ya Mali inayopatikana Afrika Magharibi kati ya maeneo hayo matatu, sehemu ambayo ilikuwa huru na inashamiri ni himaya ya Mali. Uchina na eneo lote la mashariki ya kati yalikuwa chini ya utawala wa Genghis Kan. Himaya ya Mali ilikuwa chini ya utawala wa mtu aliyepata kuwa tajiri katika historia ya mwanadamu aliyepata kuishi hapa duniani Mansa Musa I, iliyokuwa inatawala maeneo ambayo kwa leo ni nchi za Mali, Senegal, Gambia, na Guinea. Hadi anafariki mwaka 1331, Mansa Musa alikuwa na utajiri wa dola bilioni 400. Kipindi hicho Mali ikizalisha zaidi ya nusu ya dhahabu na chumvi iliyokuwa inazalishwa duniani.

Mansa Musa alivyokwenda hija Mecca mwaka 1324 alibeba na kugawa dhahabu nyingi kiasi cha kuporomosha bei ya dhahabu duniani kwa miaka kumi mfululizo katika hija hiyo alifuatana na watu 60,000. Alianzisha maktaba ya Timbuktu, maandishi maarufu ya Timbuktu yalioandika kwa upana juu ya maarifa mbalimbali ya ulimwengu huu, yaliandikwa wakati wa utawala wake.

Mashuhuda wa mafanikio na ukuu wa Himaya ya Mali walitoka sehemu mbalimbali za dunia. Sergio Domian msomi na mhandishi wa Italia aliandika yafuatayo kuhusu utawala wa Mali. “kipindi hicho: ndipo ulipoanzia ustarabu wa miji, wakati wa uongozi wake, Mali ilikuwa na miji ipatayo 400 na eneo la Delta lilikuwa ni eneo lenye wakazi wengi sana.” Mji wa Mali wa Timbuktu katika karne ya 14 ulikuwa na idadi ya watu waliofikia 115,000, mara tano ya wakazi wakipindi hicho wa London.
Hivi karibuni National Geographic imeuelezea mji wa Timbuktu kama paris ya zama za kati. kwa utamaduni wake wa uwanazuoni na usomi wanafunzi takribani 25,000 walihitimu masomo ya chuo kikuu katika mji huo. Familia nyingi za kale za Afrika Magharibi zilikuwa na maktaba binafsi. Mji wa Chinguetti na Oudane uliyopo Mauritania una idadi ya vitabu 3,450 vilivyo andikwa kwa mkono enzi ya zama za kati. Inakisiwa kuwepo vitabu zaidi ya 6,000 hivi sasa katika mji wa Walata, baadhi vikiwa na vimeandikwa karne ya 8 AD. Kuna vitabu 11,000 katika makavazi binafsi Niger. Leo hii Timbuktu kuna vitabu zaidi ya 700,000 vilivyo andikwa zama hizo, kwa lugha za Mande, Suqi, Fulani, Timbuctu na Sudani. Maudhui ya vitabu hivyo yanajumuisha hisabati, utabibu, ushairi, sheria na unajimu. Ensaiklopidia ya kwanza duniani iliandikwa Mali katika karne ya 14, kabla ya wazungu kupata hilo wazo karne nne baadaye. Kwa msomi wa Afrika Magharibi wa karne ya 16, vitabu 1,600 vilikuwa ni maktaba ndogo sana kwake. Professor Ahmed Baba wa Timbuktu alinukuliwa akisema alikuwa na maktaba ndogo zaidi ya walizokuwa nazo rafiki zake, yake ilikuwa na vitabu 1600. Imam wa Timbuktu kwa mfano alikuwa na mkusanyiko wa maandiko ya kisayansi yanayo onyesha sayari zinavyo lizunguka jua. Huo ni ushahidi anuwi kuwa wasomi wa Timbuktu walijua vingi zaidi ya wenzao wa kimagharibi.

Katika karne ya kumi na tano, wataalamu wa hisabati wa Timbuktu walikuwa wanajua kuhusu mzunguko wa yasari, kupatwa kwa jua, walijua vitu vilivyowachukua wazungu miaka 150 kuvijua, hadi pale Galileo na Copernicus walipo andika kuhusu dhana hizo.

Mabaharia wa Mali walikanyaga aridhi ya Marekani mwaka 1311 AD, miaka 181 kabla ya Columbus. Msomi mashuhuri wa Misri zama hizo Ibn Fadl Al- Umari alipata kuandika juu ya hilo mwaka 1342, Katika sura ya kumi kwenye kitabu chake ameongelea mashua kubwa mbili zilizotumwa na mtangulizi wa Mansa Musa, mfalme alierithi kiti cha ufalme mwaka 1312. Huyo mfalme hakuandikwa na Al-Umari, ila wasomi wa zama hizi wameweza kumtaja kama Mansa Abubakari II.

Matukio hayo yalikuwa yanatokea wakati Ulaya kama bara ilikuwa imeghubikwa na zama za giza totoro, likishambuliwa na maradhi ya tauni na baa la njaa, wakiuwana wenyewe kwa wenyewe kwa ukabila na udini.

Miji mbalimbali ya kale iliharibiwa na uvamizi wa wageni, mji kama Kilwa uliopata kuwa mji tajiri na mashuhuri katika Pwani ya Afrika Mashariki katika karne ya 11 ulivamiwa na kuharibiwa vibaya na wareno. Wavamizi mbalimbali wa magharibi walivamia na kuharibu miji mbalimbali Afrika na kuharibu kabisa historia ya maendeleo waliokuwa wamejijengea waafrika kipindi hicho. Itoshe kusema hakuna maendeleo wazungu walioleta Afrika zaidi ya uharibifu, wizi na unyonyaji
 
Hadi ugonjwa wa ukimwi, ni kutudhoofisha, madawa ya uzazi wa mpango, kuwa makini sana, tunawekewa sumu
Katika pita pita zangu nimekutana na watu wanaosema wameponywa huu ugonjwa na waganga hawa hawa tunaowadharau....
Tukijitambua hata hospital hatufia kwenye foleni.
 
Binadamu anapozaliwa tu, anajikuta yupo chini ya utawala wa Mama.
Mama anaamua amnyonyeshe au la, na kama hivyo ni muda gani.
Mama ndiye anayeamua akunyonyeshe hadi ushibe au kabla.
Mama ndiye Malkia na kamwe binadamu huyo mdogo hawezi kujitoa chini ya utawala wa huyo Malkia.
Yeye ataamua binadamu huyu ni muda gani, alale,aamke, ale, aoge, avae nk.
Hapa inapita miaka kadhaa kabla ya kujikuta chini ya utawala wa Malkia na Mfalme Baba.
Hawa watawala watammiliki huyu binadamu kwa kipindi fulani pia.
Katika kipindi hicho binadamu inampasa kufuata sheria zote anazopangiwa na hao ma mjamaa, la sivyo kuna adhabu zitamfika, kama kuchapwa viboko, makofi, kufinywa, kunyimwa chakula, kutishwa na hawezi kujinasua nao.
Binadamu huyu anazidi kukua, Baba na mama wananza kuona kuwa kijana anapata uwezo unaolingana na wao, wanaanza kuogopa kumchapa kama hatafuata wanavyotaka, wanaamua jambo lingine nalo ni kumkabidhi kwa Jamii.
Kijana anakabidhiwa kwa Jamii au taasisi zake.
Anaanza kupelekwa Shule, ili kafunzwe ustaraabu zaidi, hapo akiwakosea wazazi hawamchapi tena, wanamwogopa, watachukua hatua ya kumuonya na ikishindikana wanampeleka Polisi.
Juhudi zote hizo wanataka kijana afuate sheria fulani fulani ambazo zinazunguka ndani ya jamii husika.
Kijana kwakuwa sasa anapaswa kuwaacha wazazi na kwenda Shule, au taasisi nyingine ya kijamii, ambako atakutana na watu wenye mafundisho mengine, wazazi wanaamua kumlinda kwa kumkabidhi kwa taasisi za Ki imani.
Ili kuirutubisha akili yake isimtume kijana kufanya matendo ambayo hayakubaliki na jamii hiyo.
Kijana anapokuwa mtu mzima haraka haraka anakabidhiwa wake wa jinsia nyingine kwa Amri ya Ndoa ili asilale peke yake, asije akalala Bar.
Katika ndoa nako kuna sheria kibao za kuzifuata, kijana analazimika kusaini mkataba wa ndoa, na anaambiwa kabisa hakuna kuvunja ndoa kirahisirahisi. Kwa kujiamlia tu asubuhi unapoamka.
Hapo mke au mume anakuwa sio mpenzi tu, bali Polisi pia.
Polisi wa kumlinda kijana ili asikengeuke
Kijana lazima umsirikishe huyu Mpenzi Polisi katika kila jambo unalo amua kufanya.
Hata ukitaka kuondoka nyumbani lazima umuage huyu Mlinzi wako.
Ni lazima umtii huyu Mpenzi kumbe ni Mlinzi.
Na kwakuwa mko peke yenu lazima na nyinyi wote mlindwe na Mlinzi Mwingine msije mkakengeuka wote wawili ikawa badala ya kulala Nyumbani mjalala Kasino.
Hapa sasa mnakabidhiwa kwa walinzi wawili, Jirani na Serikali.
Mkigombana tu mlinzi wa kwanza anawajia ( jirani) atajaribu kuwa suluhisha mkiwa wabishi anaripoti kwa mlinzi wa tatu, Polisi, Serikali.
Hapo ukiendelea kuwa mbishi Polisi anajua pa kukupeleka, na unaweza ukapotea moja kwa moja kama hutajirekebisha.
Sasa basi
Tunaona kila hatua ya binadamu kuna ulinzi unamfuatilia, upo nyuma yake ambao tunauona kwa macho.
Swali linalobaki huyu mlinzi atalindwa na nani ?
Ili kumfanya asimwonee binadamu anapo taka, yaani mlinzi, mke au mume, mlinzi jirani, mlinzi polisi, mlinzi Serikali, nk.
Ili mlinzi mmoja asimwonee mwenzake hapa ndipo anapojitokeza mlinzi mkuu.
Jamii inampa cheo, cha Uungu, huyo ndiye Mungu, huyo anajulikana kuwa ni Alfa na Omega. Muweza wa yote, Almighty.
Katika kila jamii ukiitembelea ina Mungu wake.
Nenda Uchina, nenda Brazil nenda kokote duniani utamkuta huyo Mungu ambaye jamii inamwogopa na kumheshimu sana sana, na kulazimika kumtii kwa kila anachosema.
Ukikosea kimtii jamii inaweza kukuadhibu, sehemu nyingine unakatwa kichwa kabisa kwa kumkose, au Kumkufuru, huyo Mungu.
Tanaona hadi leo, Serikari ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ikitaka kuanza kutunga sheria zake Bungeni, lazima kwenye ufunguzi wa kikao kuna Kusali uli kupata baraka zake, huyo Mungu.
Ref. Sala ya Bunge.
Iko pia sala ya Taifa, ambayo inajulikana kama Wimbo wa Taifa.
Humo Mungu hutajwa sana, ili aibariki Nchi, Viongozi na Watu wake.
Yaani vyoote hivyo ni vyake, mali yake, yeye ndiye aliyevitengeneza, na hana mshirika.
Leo tunaona Viongozi wa Serikali wakiwa wanawaonea Raia wanaowaongoza, wanakaripiwa vikali na Wafanyakazi wa huyo Mungu, wanaojulikana kama Watumishi wa Mungu.
Wana vyeo kama vile, Shehe, Imamu, Padri, Askofu, Mchungaji nk.
Wanaionya Serikali kwa Nyaraka na Matamko, na kuitisha kuwa wataishitaki kwa Mungu, nayo Serukali inaogopa na kujirekebisha kiasi fulani fulani.
(Hapa nilikuwa nadadavua uhalisia wa kimaisha wa Binadamu)
Binadamu anazungukwa na walinzi kila kona. Kila dakika kila sekunde, walinzi wanaoonekana na wasioonekana.
Uhuru wa wa kifikra utapatikana wapi kwa binadamu ?
maana ukiwa huru kifikra unakuwa huru kimatendo pia.
Toka anazaliwa hadi anakufa Binadamu hayuko huru kuamua au kutenda anachotaka mwenyewe binafsi.
Kwa mfano.
Hapa Tanzania mtu akiamua kutumia madawa ya kulevya anakamatwa, akitaka kupanda Bangi shambani mwake ili aitumie anakatazwa na hata kutishiwa kufungwa na Mlinzi Serikali.
Hapo uhuru uko wapi ?
Bangi navuta mimi wewe
Inakuhusu nini ?
Mbona unaiingilia uhuru wangu mimi binafsi ukichukulia sivuti hadharani bangi yangu ?
Mwenyewe napenda kuvuta huku nikiimba
" Bangi Nibangue nilime hadi kuleee "
Bangi usiyovuta yakuwashiani ?
Kuna uhuru hapo ?
Uhuru gani wa kulazimishwa kutii sheria alizotunga mtu
mwingine ? Au Mungu ?
Maana ya Uhuru ni Kuwa Huru Kifikra na Kimatendo pia.
(To Be Total Free)
Je unaweza kujikomboa kwenye mikono ya hawa walinzi wote nilio wataja ukianzia na Mama mzazi ?
Anafuata, Mke au Mume, Jirani, Serikali, na Mungu ?
Au unataka usimtii mmojawapo kati ya hao walinzi ?
Ndipo ujulikane kuwa uko huru ?
Hit.
Binadamu hawezi kuwa huru,
kwani analazimika kutii sheria alizowekewa na waliomtangulia, la sivyo atakumbana na adhabu kali zinazoweza hata kumtoa uhai wake, kama ataendele kuwa mkaidi.
Hello to Free Men.
Kuwa huru ni kazi sana
 
Nimeifukunyua hii kutoka Maktaba!

HISTORIA YA AFRIKA ILIYOFICHIKA - Na Mwl. Matteo E. Mwita

Kumekuwa na historia iliyopotoshwa kuhusu Bara letu la Afrika, historia hiyo imekuwa ikituelezea sisi waafrika na bara letu kama watu tulikuwa nyuma sana kimaendeleo, watu ambao hatuna chochote cha maana. Bara na watu tuliokuwa tumeghubikwa na kila aina ya ushenzi, kwa muda mrefu tumekuwa tukiaminishwa kuwa bila ya ujio wa wazungu tusingefikia hatua ya kimaendeleo tuliopo leo, chakusikitisha baadhi ya waafrika wamekuwa wakiamini ghiliba hizo kutoka kwa wazungu. Vitabu vingi vya kihishtoria vilivyo ndikwa na wanazuoni wa kimagharibi vimejaribu kulipaka matope bara letu, vimetulaghai kiasi cha sisi kujidharau na kujiona hatukuwa na cha maana. Ila kuna baadhi ya vitabu kama when we ruled: The Ancient and Medieval History of Black civilization na How Europe Undeveloped Africa, vimekuwa na mitazamo tafauti kuhusu bara letu na kujaribu kuonyesha mafanikio ambayo tulikuwa tumeyafikia kama bara kwa karne kadhaa nyuma hata kabla ya ujio wa wageni. Makala haya yanaangazia kwa ufupi mafanikio ya eneo mmoja la Afrika zama hizo.

Je, ulipata kujua kuwa karne ya kumi na nne mji wa Timbuktu uliopo Afrika Magharibi ulikuwa na ukubwa mara tano zaidi ya jiji la London na ulikuwa ni mji tajiri zaidi ulimwenguni? Leo hii London ni kubwa mara 236 kwa Timbuktu. Mji huo hauna chochote kinachoweza kuonesha kuwa ni mji wa kisasa, idadi ya wakazi wake imepungua kwa mara mbili ya idadi ya wakazi karne tano zilizopita, mji umezingirwa na mitaa michafu iliyojaa ombaomba. Timbuktu hauna uwezo tena wakutunza hata makavazi na majengo yake ya asili.

Katika karne ya 14, sehemu tatu tajiri kabisa duniani zilikuwa China, Iraki/Irani na Himaya ya Mali inayopatikana Afrika Magharibi kati ya maeneo hayo matatu, sehemu ambayo ilikuwa huru na inashamiri ni himaya ya Mali. Uchina na eneo lote la mashariki ya kati yalikuwa chini ya utawala wa Genghis Kan. Himaya ya Mali ilikuwa chini ya utawala wa mtu aliyepata kuwa tajiri katika historia ya mwanadamu aliyepata kuishi hapa duniani Mansa Musa I, iliyokuwa inatawala maeneo ambayo kwa leo ni nchi za Mali, Senegal, Gambia, na Guinea. Hadi anafariki mwaka 1331, Mansa Musa alikuwa na utajiri wa dola bilioni 400. Kipindi hicho Mali ikizalisha zaidi ya nusu ya dhahabu na chumvi iliyokuwa inazalishwa duniani.

Mansa Musa alivyokwenda hija Mecca mwaka 1324 alibeba na kugawa dhahabu nyingi kiasi cha kuporomosha bei ya dhahabu duniani kwa miaka kumi mfululizo katika hija hiyo alifuatana na watu 60,000. Alianzisha maktaba ya Timbuktu, maandishi maarufu ya Timbuktu yalioandika kwa upana juu ya maarifa mbalimbali ya ulimwengu huu, yaliandikwa wakati wa utawala wake.

Mashuhuda wa mafanikio na ukuu wa Himaya ya Mali walitoka sehemu mbalimbali za dunia. Sergio Domian msomi na mhandishi wa Italia aliandika yafuatayo kuhusu utawala wa Mali. “kipindi hicho: ndipo ulipoanzia ustarabu wa miji, wakati wa uongozi wake, Mali ilikuwa na miji ipatayo 400 na eneo la Delta lilikuwa ni eneo lenye wakazi wengi sana.” Mji wa Mali wa Timbuktu katika karne ya 14 ulikuwa na idadi ya watu waliofikia 115,000, mara tano ya wakazi wakipindi hicho wa London.
Hivi karibuni National Geographic imeuelezea mji wa Timbuktu kama paris ya zama za kati. kwa utamaduni wake wa uwanazuoni na usomi wanafunzi takribani 25,000 walihitimu masomo ya chuo kikuu katika mji huo. Familia nyingi za kale za Afrika Magharibi zilikuwa na maktaba binafsi. Mji wa Chinguetti na Oudane uliyopo Mauritania una idadi ya vitabu 3,450 vilivyo andikwa kwa mkono enzi ya zama za kati. Inakisiwa kuwepo vitabu zaidi ya 6,000 hivi sasa katika mji wa Walata, baadhi vikiwa na vimeandikwa karne ya 8 AD. Kuna vitabu 11,000 katika makavazi binafsi Niger. Leo hii Timbuktu kuna vitabu zaidi ya 700,000 vilivyo andikwa zama hizo, kwa lugha za Mande, Suqi, Fulani, Timbuctu na Sudani. Maudhui ya vitabu hivyo yanajumuisha hisabati, utabibu, ushairi, sheria na unajimu. Ensaiklopidia ya kwanza duniani iliandikwa Mali katika karne ya 14, kabla ya wazungu kupata hilo wazo karne nne baadaye. Kwa msomi wa Afrika Magharibi wa karne ya 16, vitabu 1,600 vilikuwa ni maktaba ndogo sana kwake. Professor Ahmed Baba wa Timbuktu alinukuliwa akisema alikuwa na maktaba ndogo zaidi ya walizokuwa nazo rafiki zake, yake ilikuwa na vitabu 1600. Imam wa Timbuktu kwa mfano alikuwa na mkusanyiko wa maandiko ya kisayansi yanayo onyesha sayari zinavyo lizunguka jua. Huo ni ushahidi anuwi kuwa wasomi wa Timbuktu walijua vingi zaidi ya wenzao wa kimagharibi.

Katika karne ya kumi na tano, wataalamu wa hisabati wa Timbuktu walikuwa wanajua kuhusu mzunguko wa yasari, kupatwa kwa jua, walijua vitu vilivyowachukua wazungu miaka 150 kuvijua, hadi pale Galileo na Copernicus walipo andika kuhusu dhana hizo.

Mabaharia wa Mali walikanyaga aridhi ya Marekani mwaka 1311 AD, miaka 181 kabla ya Columbus. Msomi mashuhuri wa Misri zama hizo Ibn Fadl Al- Umari alipata kuandika juu ya hilo mwaka 1342, Katika sura ya kumi kwenye kitabu chake ameongelea mashua kubwa mbili zilizotumwa na mtangulizi wa Mansa Musa, mfalme alierithi kiti cha ufalme mwaka 1312. Huyo mfalme hakuandikwa na Al-Umari, ila wasomi wa zama hizi wameweza kumtaja kama Mansa Abubakari II.

Matukio hayo yalikuwa yanatokea wakati Ulaya kama bara ilikuwa imeghubikwa na zama za giza totoro, likishambuliwa na maradhi ya tauni na baa la njaa, wakiuwana wenyewe kwa wenyewe kwa ukabila na udini.

Miji mbalimbali ya kale iliharibiwa na uvamizi wa wageni, mji kama Kilwa uliopata kuwa mji tajiri na mashuhuri katika Pwani ya Afrika Mashariki katika karne ya 11 ulivamiwa na kuharibiwa vibaya na wareno. Wavamizi mbalimbali wa magharibi walivamia na kuharibu miji mbalimbali Afrika na kuharibu kabisa historia ya maendeleo waliokuwa wamejijengea waafrika kipindi hicho. Itoshe kusema hakuna maendeleo wazungu walioleta Afrika zaidi ya uharibifu, wizi na unyonyaji
Ahsante sana.
 
Eti Michael Jackson, yule wal izika 2008, kwanza familia ya Michael Jackson hawakuhudhuria msiba, tunataarifa na ushahidi, ilikunyamaza kimya, familia ya Michael Jackson, walilipwa pesa ndefuuuuuuu
Ni June 2009 sio 2008
 
Jamani bado tu tuingie kazini, tunataka ukombozi.... African Culture mbele kwa mbele.
 
michael time hizo alikuwa in riptide hiyo ilikuwanga first sign of warning, wonder shall never end ile alikuwanga amepanga show yake ya mwisho ili dunia ijue siri aliyoko nayo but bofore They Day dated, they put him down
Mmmh mbona tunaambiwa huyo alikuwa fake sasa?
 
Back
Top Bottom