Tuanze moja: Tuachie wafungwa wote walio magerezani na walio rumande bila masharti

Kama ulikua rumande kwa kupiga dili kubwa kubwa unaachiwa. Kama ulipiga dili ndogo ndogo unaendelea kula msoto.

Moral of the story: Mwenye nacho huongezewa, asiyenacho atanyang'anywa hata kile kidogo.
Kwahio wezi wa simu rumande ni kama oxygen yao😂😂😂
 
Watanzania wengi ni mahiri sana kwa kuunganisha mambo kivivu bila ushahidi.

Yani mtu anaweza kukuona umevaa nguo nyekundu na nyeupe tu, akakubambika ushabiki wa Simba.

Kumbe wewe mfanyakazi wa ubalozi wa Japan umevaa nguo za rangi ya bendera ya Japan!

Nyani Ngabu
 
Kama Magufuli aliharibu nchi Samia si ndo aitengeneze kwa kuachia huru wafungwa wote!
Ushauri wako ni mzuri ila hautekelezeki,ngoja DPP awatoe wote atakoona wanastahili kutolewa kama ambavyo Biswalo alikuwa anawaweka ndani bila dhamana wale wote aliojisikia kuwaweka ndani
 
Hahahaha hahahaha hii ni sarcasm Mpwa!
 
Ushauri wako ni mzuri ila hautekelezeki,ngoja DPP awatoe wote atakoona wanastahili kutolewa kama ambavyo Biswalo alikuwa anawaweka ndani bila dhamana wale wote aliojisikia kuwaweka ndani
Hamaainishi hivyo, huyu analeta hoja kwa kujeli. haamini kuwa Jey ameshapumzika
 
Halafu there is this thing ya uteuzi.

Sielewi ni kwa nini watu wanaona kuteuliwa na Rais ni big deal.

Sijawahi hata siku moja kuwaza kufanya kazi serikalini.

Much less, sijawahi kabisa hata kuwaza kuwa eti ukikubaliana na Rais kuhusu jambo flani, basi eti unatafuta uteuzi!

Hii nadhani inawaakisi wao [watoaji hizo tuhuma] zaidi. Nadhani wao ndo huona ni big deal kuteuliwa na Rais.

Halafu, kwa mtu aliyeanzisha mada kama hii kupinga baadhi ya kauli za Magufuli, kuitwa ni mkabila, halafu papo hapo kuambiwa natafuta uteuzi, ni matusi kwa watu wenye akili Bomoabomoa Mwanza: Rais Magufuli omba radhi kama....
 
Wanabambikiziwa kesi na nani? Wanaowabambikizia kesi wako wapi? Ni nani hajambikiziwa kesi? Tunajuaje wanaoachiliwa sasa walibambikiziwa kesi? Na je wote waliofungwa kabla ya 2015 walifungwa kihalali...Na wote wanaokamatwa sasa na kufungwa wanafungwa kihalali (hawajabambikiziwa)...tunajuaje? Ngosha hoja yako inachokoza...ni fujo gete!

NB* Namjua jamaa mmoja yuko Keko mwaka wa nane hivi anasubiria kesi...
 
Mimi mtu akianza kuniambia habari za uteuzi ni kama kanichokoza nianze ku lord it over them.

Nawaambia hakuna uteuzi utakaonifaa, hakuna mshahara wa serikali ya Tanzania utakaonifaa. Na mimi siamini katika kutumia nafasi ya kazi kupata rushwa. Na pia siamini katika kufanya kazi ya serikali kama wito wa kizalendo Tanzania.

Nimeanza kutembea corridors za Ikulu tangu nipo tumboni mwa mama yangu.Nimekula ma apple ya Mama Joan Wicken hapo Magogoni. Wakati huo rais ni rais na Ikulu ni Ikulu. Waende kum Google Joan Wicken labda watapata somo la historia.

Sasa leo teuzi za kuteuliwa na kutukanwa, lawama tupu, nani atataka?

Niende kukaa vikao vya groupthink na kulamba viatu Makonda types kwa kisa gani mtu world citizen na roll na Wall Street crowd?

Mazee nipate teuzi serikali ya Bongo, halafu kwenda likizo yangu mwenyewe Turks and Caicos mpaka niombe kibali? Nani anataka ujinga huo?

Hizi teuzi zinaweza kuonekana deal kwa watu hohehahe au wapumbavu.

Sisi ambao tumeanza kutembea corridor za Ikulu tangu matumboni mwa mama zetu hizi teuzi ndizo tulizozikimbia Tanzania.

Unaweza kupewa uteuzi ukabweteka kuandikwa magazetini, kumbe una limit potential yako kwenye world stage.

Nani anataka ujinga huo?

Hawa watu ambao ukoo mzima hawajapata presidential appointmemnt ndiyo wana matatizo, sisi wengine washua wamepata appointments tangu enzi za Nyerere na Mwinyi huko, bado tushangalie teuzi mpaka leo?

Tumejiongeza world cities tunakula maisha kimataifa, wabaki na teuzi zao za kuchunga paka kivyao.
 
Yeah.. tuachie hadi sabaya. Mnawaachia wahalifu papa msofe masheikh wa ugaidi etc halafu mnawaweka lupango wanamapinduzi sabaya na fitina zinaendelea ali hapi makonda etc wawekwe lupango. Sijui hii ni serikali gani ya chama cha mapinduzi. Nahisi wapinga maendeleo na vibaraka wa ubeberu wanashika usukani kwa sasa.
 
Duuuh!
 
Tunataka nchi hii iendeshwe kama huko ulimwengu wa kwanza.Hakuna mtu kwekwa mahabusu bila dhamana na DPP, kesi zote ziwe na dhamana na Mahakama kuu pekee ndio iwe na uwezo wa kumnyima mtu dhamana pale itakapojiridhisha inahitajika kufanya hivyo.
Ni vigumu haki kutendeka kwa mtindo huu ambao serikali ndio mkamataji na mfunga watu kwa kuzuia dhamana.
Kuna mfungwa aliachiwa kwa msamaha wa Rais Samia sikukuu ya muungano, hajakaa kitaa mwezi kafanya zali tena!

Tuweke process tu ya kuhakiki kesi zilivyoendeshwa na haki itolewe.

Lakini huu msamaha unaotaka utaleta majanga.
 
Kwa nini watu wanakamatwa bila upelelezi wa kutosha kuendesha kesi mahakamani?
Watu ambao hakuna ushahidi wa kesi zao hawapaswi kuwa mahabusu kwa namna yoyote.
 
Sawa mkuu, na dhamana iwe ya haki.

Si unamkamata kapuku kwa kesi ya kuiba kuku, tena ya kubambikiwa, halafu dhamana sh trillioni moja.

Hapo itakuwa bado umemnyima dhamana tu.
 
Huo ushauri wako wa kinafiki peleka kule kweny kaburi la mungu wenu wa chatttle,,

Tunajua hampendi mama aongoze Nchi kwa haki wapuuzi nyinyi,mnataka aongoze Nchi Kama alivyokuwa anaongoza yule dikteta uchwara aliyopotelea mavumbini
 
Hivyo unaamini Tanzania ni EDEN hakuna crime. Kama crime ipo na criminals wapo ubaya wa mwalifu yoyote ukimhoji anasema amesingiziwa kwani huona uhalifu ni haki yao. Hiyo 99% imenishtua kidogo labda uwe umeongea kwa code
 
Kuna wengine wanapenda kukaa jela, tena akitoka anaacha shuka yake anasema atarudi,

Kuwatoa wote itakua wengine hawajatendewa haki yao ya kuishi jela.
 
Wafiwa mnateseka sana!😄 na hii mwanzo tu, mpaka miaka ya mama iishe siyo leo!
Anyway, wazo lako lipo ndani ya Box mojawapo kati ya hayo mabox unayo beba!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…