Tuchangiane uzoefu katika malezi: Malezi yako yalikuwaje, unahisi yamekuathiri, ungependa kulea watoto wako kama ulivyolelewa?

Tuchangiane uzoefu katika malezi: Malezi yako yalikuwaje, unahisi yamekuathiri, ungependa kulea watoto wako kama ulivyolelewa?

Tabia ya kurithi ipo ila ngoja nikupe mfano watoto wawili wa baba mlev,mmoja anaweza kuwa Mrefu km baba yake Mmoja sio mrefu.Kwanini hilo linatokea??kama tunarithi kupitia vinasaba??

Wengi wao ni wanaiga matendo ya wazazi wa baada ya kuzaliwa.Ni ukweli kwamba mzazi Ana uwezo wa kumuambukiza feelings mtoto,ukiwa na furaha mtoto akiwa karibu yako atakuwa na furaha bila hata kusema neno,hivo hivo ukiwa na huzuni,malaya,mkorofi, kiburi.Mtoto haitaji kujifunza kiburi Ni akiwa karibu na wewe tu karibu anabeba hisia zako za kiburi na majivuno mda wote..

Hapo tunarud kwenye ile ile point ya mwanzo mtoto Anaangalia matendo yako na hisia zako basiii maneno hana habari nayo..Una mood gani ukiwa mbele yake?ukiwa na hasira unafanyaje?ukiwa na furaha unafanyaje?mwanamke akipita mbele yako unafanyaje?
hahahahahahah mkuu hapo kwenye mwanamke akipita mbele yako hapo

asante kwa ufafanuzi mkuu mi sina mengi ya kusema hapo kwenye kurithi maana najua machache sana kuhusiana na hilo
 
MALEZI NI MAPANA SANA KWA KWELI KUTOKANA NA JAMII NYINGI ZILIZOPO ULIMWENGUNI KUWA TOFAUTI PAMOJA NA HAPA NCHINI KWETU PIA. MALEZI HUAMBATANA NA HISTORIA NA NDIO MSINGI MKUU. HISTORIA NDIO HUFUNUA ANZIKO LA FAMILIA, KOO, KABILA, TAMADUNI, DINI NA SHERIA ZA JAMII NZIMA HUSIKA YA MAHALA FULANI (MF: TAIFA). KWAHIYO LAZIMA TUKUBALIANE KUWA JINSI TUNAVYORITHI NDIO TUNACHOFUATA MARA NYINGI ZAIDI KATIKA SHUGHULI ZETU ZA KIBINADAMU KILA SIKU NA PIA MABADILIKO HUPATIKANA KUTOKANA NA HISTORIA YENYEWE.

KWAHIYO MALEZI NI TUNU YA URITHI AMBAYO MTU HUSIKA ANAJIFUNZA KATIKA FAMILIA ALIYOTOKA, KABILA LAKE, DINI YAKE NA JAMII YAKE KIUJUMLA. MFANO MASWALA YA HASIRA, MAJIGAMBO, UCHAPAJI KAZI, STAREHE, KUJIUA, UKATILI, UNYANYAPAJI NA MENGINE MENGI.

KWA MALEZI HASA YA FAMILIA KUNA CHANGAMOTO NYINGI SANA HASA ULIMWENGU WA LEO, ILA NAPO HISTORIA YA NYUMA KULIKUWA NA CHANGAMOTO ZAKE PIA. KINACHO TOFAUTISHA UWINGI WA CHANGAMOTO NI IDADI YA WATU WA SASA NA ZAMANI, WATU WA SASA NI WENGI ZAIDI WANAKUMBWA NA KADHIA YA MALEZI KULIKO IDADI NDOGO YA WATU WA ZAMANI. UNAWEZA KUFUATILIA TAKWIMU ZA SENSA KUJUA ZAIDI.

MALEZI YA FAMILA HUTAFSIRIWA KWA FAMILIA MOJA MOJA, KWAHIYO HIZI FAMILIA HAZIWEZI KUWA SARE KATIKA HUDUMA, TABIA, UONGOZI WA FAMILIA N.K. KWAHIYO KILA BINADAMU ANAYEZALIWA KWENYE FAMILIA HUSIKA ANAWAJIBU WA KUJIONEA YALIYO SAHIHI NA YASIYO SAHIHI KWENYE MALEZI YAKE ILI KULETA MTAZAMO TOFAUTI PINDI ANAPOANZISHA FAMILIA YAKE BAADAE. JAPO BADO ZIPO CHANGAMOTO ZA UKABILA, UDINI NA MIENENDO YA JAMII INAVYOTAKA PAMOJA NA SHERIA ZILIZOPO KITAIFA KWAHIYO HUTIA UGUMU KWENYE KUBADILISHA MITAZAMO ILIYOPO. MFANO MASWALA YA NDOA, MALEZI YA FAMILIA, ELIMU YA UJANA, HAKI ZA KIJINSIA N.K

MALEZI KATIKA FAMILIA NI SWALA LA WAZAZI/ WALEZI NA WATOTO KWA PAMOJA. CHANGAMOTO ZA KIMALEZI NI PANA SANA ILA WANAOUMIA KWA ASILIMIA KUBWA NI WATOTO. MAUMIVU YA WATOTO HAWA YANAWEZWA KUSABABISHA MATUNDA MABAYA SANA KATIKA VIZAZI VIJAVYO.

MFANO WA MAMBO AMBAYO YANAENDEKEZA MALEZI MABOVU KWA MTAZAMO WANGU NI KAMA IFUATAVYO, UKIJUMUISHA JAMBO MOJA WAPO ULILOGUSIA MTOA MADA;
1. KUGAWANA MAJUKUMU YA ULEZI KULINGANISHA KIPATO (KIUCHUMI) KATI YA WAZAZI/WALEZI.
2. KUTOKUWA NA USHIRIKIANO WA WAZAZI KATIKA MAMBO YA KIFAMILIA HADI KUAMBUKIZA WATOTO.
3. KUTOKUWAPA WATOTO HAKI YA KUSIKILIZWA WANAPOKUWA NA HISIA JUU YA MAMBO YAO.
4. WAZAZI/WALEZI KUWA NA UKALI SANA USIOJENGA FIKRA ZA WATOTO VIZURI.
5. WAZAZI/WALEZI KUWA NA UPOLE ULIOVUKA MPAKA KUFANYA WATOTO KUJISAHAU.
6. WAZAZI/WALEZI KUKAA MBALI NA WATOTO, LABDA KIKAZI,KIBIASHARA AU SITOFAHAMU BINAFSI.
7. WAZAZI KUVURUGA NDOA ZAO WENYEWE KWA VITENDO VYA USALITI, UHAWARA N.K
8. WAZAZI KUFARIKI GHAFLA NA KUACHA PENGO KWA WATOTO CHINI YA WALEZI WASIO WAZURI.
9. WAZAZI/WALEZI MATENDO YAO HUAMBUKIZA WATOTO, MF; ULEVI, UZINZI, MAPIGANO N.K
10. WAZAZI/WALEZI KUENDELEZA MILA NA DESTURI ZISIZO KUWA NZURI KWA WAKATI ILIOPO, MF; UKATILI, USHAURI N.K
11.WAZAZI/WALEZI KUSHIKILIA MAMBO FULANI YA KIDINI YASIYO KUWA NA MASHIKO KIMALEZI, MF; UNYANYASAJI, USIKIVU, MSAADA, UPENDO N.K
12. WAZAZI/WALEZI KUTOA UHURU ULIOPITILIZA KWA WATOTO WAO NA KUTOA MIANYA IYAKUJA KUWAPA SHIDA WAO WENYEWE NA JAMII KUWAREKEBISHA. MF; UTANDAWAZI
13. WAZAZI/WALEZI KUTOFANYA KAZI/KUJI SHUGULISHA KWA BIDII NA KUACHIA WATOTO KUKIMBIA HALI DUNI NJE YA JAMII.
14. WAZAZI KUPATA WATOTO WALIKUJA DUNIANI BILA MATARAJIO YAO MAALUMU NAKUWEPO MAMBO YA LAANA AU MIKOSI.
15. WALEZI WALIOKOSA UPENDO WA DHATI KWA WATOTO WALIOACHIWA NA MAREHEMU NDUGU/MARAFIKI ZAO.
16. WAZAZI/WALEZI KIPINDI CHA NYUMA WALIPITIA MALEZI MABOVU NA PIA KUAMBIKIZA HALI HIYO KAMA MATOKEO KWA WATOTO WAO PIA. (MTOTO WA NYOKA, NI NYOKA).

NB: NINGEPENDA NIISHIE HAPA NA PIA SIKUTAKA KUFAFANUA SANA NADHANI NIMEGUSIA TU MADA, ILA SIJAPONDA WALA KUKATAZA DINI, SHERIA AU TARATIBU ZA MILA FULANI. CHA MSINGI TUWE NA HOFU JUU YA MATOKEO MABAYA YA MALEZI KWA WATOTO, KUWA NA HOFU NJEMA YA MUNGU, KUELEWA VYEMA MILA NA DESTURI NZURI NA MBAYA, KUFAHAMU NA KUHESHIMU SHERIA ZINAZOLINDA HAKI ZA WATOTO.

PEACE & LOVE
Asante sana mkuu BenKaile umetoa ufafanuzi mzuri sana juu ya vitu vinavyoathiri malezi

lakini mkuu back to you,wewe binafsi na utu wako unadhaani unatokana na malezi uliyopewa na wazazi wako au unadhani ni vile tu jinsi ulivyo? unadhani malezi uliyopewa yamekuathiri kwa namna moja ama nyingi eiza hasi au chanya? ungependa kulea watoto wako kama ulivyolelewa?
 
PERSONALLY NISINGEPENDA MALEZI NILIYOPITIA WATOTO WANGU NAO WAPITIE, NA IMANI KWA KILA MTU ITAKUWA VIVYO HIVYO KWANI NYAKATI ZA KIMAISHA ZINATOFAUTIANA. KILA UZAO UNA MAPITO YAKE NA WAJAO MBELENI YAO PIA YAPO MENGINE MAPYA WATAKUMBANA NAYO. KWAHIYO NI KUBOBEA ZAIDI KATIKA MAWASILIANO NA VIZAZI VYETU VIZURI KWANI TAARIFA SAHIHI KATIKA MASWALA SAHIHI NI TIBA KWENYE MDA SAHIHI WA MAMBO YANAVYOKWENDA.

I COULD ENCOURAGE WALE NA MIMI AMBAO BADO HATUJAANZISHA FAMILIA NA WALE AMBAO MATHALANI WAMO NDANI YA FAMILIA ZAO TUWE TUNAFANYA TAFITI ZA MABADILIKO KWENYE ULIMWENGU WETU NA KUAANDA TAARIFA SAHIHI KATIKA KUJENGA JAMII BORA. FAMILIA IKIWA BORA NA JAMII/ULIMWENGU UTAPA SULUHU, KWA SABABU MALEZI NA MIFANO HUANZIA HUMO.
oh asante pia kwa hapa nimekuuliza swali ambalo hapa umetoa majibu yake japo nusu sikuwa nimeona mkuu

ila swali kwako mkuu,kwa nini usingependa kulea watoto wako kama vile ulivyolelewa? ni kwa mantiki kwamba ulilelewa kufuata na nyakati zile?unahisi kuna vitu umekuwa na huvipendi na ni kwa sababu ya malezi au ni nini hasa chanzo?
 
Nachukua strengths ktk malezi yangu ya utoto naachana weakness. Binafsi hii ni kipindi cha kusahihisha makosa na kujenga kizazi bora zaidi cha baadae.
sure sure mkuu umejibu vyema kabisa kuhsua kuacha gaps na kuchukua mazuri

but mami unahisi utu ulionao sasa ni matunda ya malezi uliyoyapata? umewahi kuona jirani au Rafiki au mtu yeyote yule ambaye malezi yamempa utu wa ain Fulani utusimulie kisa hicho ili tuzidi kujifunza hata Zaidi?
 
Mkuu BAK madini yako yana umuhimu sana katika hii mada tafahdali tia neno

nakusubiria hapa hapa
 
  • Kicheko
Reactions: BAK
https://jamii.app/JFUserGuide you baba.... https://jamii.app/JFUserGuide youuuu..mpaka leo unanifanya ni hishi kwa shida tu uka mwacha mama. ukaweka malaya mmoja tena kwenye jasho la. familia na nakupa taharifa kihama chako kinakuja mda si mrefu.....niacheni kwanza maana namengi yakuandika apa maana kurasa azitoshi
 
Mi ninaamini kua asilimia kubwa kwa WaTz tumepitia malezi ya kibabe na nidhamu ya woga ikiwemo na mm mwenyewe "obey the last order ". Ila malez sahihi kwangu ni urafiki na ukaribu baina ya mzazi/mlez na watoto wake. Nimekua nikipokea ushaur ktoka kwa boy of 3 age hasa kw mambo yamhusuyo mwenyewe. Inansaidia sn kubaini mambo yake na mawazo yake yooote. Hop itatupeleka pazur
 
Viroboto , chawa- nguoni na kichwani, kunguni, utitiri, mbu, Vyoote mimi. kuosha vyombo, kuteka maji kisimani! Kutengwa wakati wa sala! yaani......

Binafsi nilijitenga na wenzangu shuleni sababu kaptula ya shule ilichanika matundu makubwa matakoni tena bila chupi ndani,

Manake nilichekwa na watoto wenzangu, na kuonekana kituko, kuchunga ng'ombe mbugani pekupeku siku za likizo, ndo zilikuwa zangu.sikujua viatu.

kujisaidia ni vichakani tu sometimes unaona kabisaaa minyoo juu ya kinyesi chako, sababu ya utoto unaona kawaida. hkn pa kusemea!

Bora niende Shule nitii sheria za shule ili nikae salama kunako kivulini cha drs, na mwalimu kuliko kubaki nyumbani nikalime shamba asubuhi then nikachunge mifugo siku nzima,
ambayo haikuwa na tija kwangu mfano kwa kunywa maziwa , hata kununuliwa shati au kaptula ya kuchungia.

Kusema kweli bila kuficha kila, usiku, ulipokuwa ukiingia Roho inauma sana, juu ya utitiri, chawa na viroboto vitakavyo ning'ata usiku kucha,

Nguo pekee ya kuchungia; Shukrani, ilikuwa ni sweta la kijani lililo sheheni chawa, tena bila vishikizo alinipatia marehemu dada yangu,
nalo lili nasa miiba ya porini kibao, kishikizo pekee kilikuwa mkono wangu wa kushoto. na ule wa kulia nilishika fimbo ya kuswagia mifugo. ngozi ya tumbo ilibadilika ajili ya ukurutu! mchana wadudu hawaumi sana km usiku!

Miaka hiyo Hakuna majira niliyo furahia km Asubuhi ikianza na mchana, jioni ilikuwa simanzi sana. sikutarajia kuijua key board. at the age of 8-9 yrs, nikaanza fanya vibarua kwa kificho ili nipate hela!

But all in all niliona ni sehemu tu ya kawaida kimaisha!

Bahati sana, bila kutegemea, nikafaulu kwenda Sec. huko baba mkuu Akili ndo ilifunguka paaa! nikaona km Ulaya nilivo heshimiwa, na walimu, wanafunzi.

Dawati, kitanda, ni vya peke yako, chakula kizuri nabembelezwa kula kwa mara ya kwanza eti nisigomee chakula! duuu!, mimi huyu! .....mngejua!

Ktk yale maisha yangu. ilikuwa ni kawaida kula ugali mgumu wa mtama, na mboga za majani chukuchuku daily, wali mkavu kwa nadra sana,
but Sec. duuu! Wali nyama Maharagwe, ndizi, mbatata, tena umeungwa vizuri na mafuta, maarufu km wese!.

Na kweli ya Mungu kadri nilivo panda Madarasa mfululizo. Mpaka kupata kazi, nilipendwa na kuheshimiwa sana na wanafunzi pamoja na wafanya kazi wenzangu,

pia jamii za watu niliokutana nao, tena mno! kuliko nilikotoka. mfano nilipoenda semina kwa mara ya kwanza Bagamoyo, sikuamini niliyotendewa seminani! na posho juu!

Hakika ya Mungu sikurudi tena kwa Shangazi yangu hata likizo tu, mpaka amekufa, wala sikumpenda kiviiile japo sikuonyesha chuki! Mpaka leo nikioa mwanamke ana tabia za ki-shangazi yangu, ananikata steam palepale!

Alikuwa hachapii wala kukufokea, but her facial expression spoke thousands of words, she really, and completely abandoned me like no body business, funny enough, and shamelessly, she did it to me, at that early age! very bad!
I dare say she was really evil. she deserve to drove to the pit of Hell!

Mpaka leo sijawahi ishi maisha ya hovyo, yaliyo jaa udhariri, Concealed hope, dharau, kejeli, umaskini, ujinga, Ubaguzi km yale, May God forbid!

MTOTO NI MAMA YAKE MZAZI TU, NDIYO ATAKUWA MTU BORA KATI YA WATU BORA, KINA DADA BEBENI WATOTO WENU WENYEWE,HATA KM HUNA HELA!
WATOTO WANGU NIKIKOSANA NA MAMA YAO. NI BORA WAKAE NA MAMA YAO TU! NITATOA MATUNZO PALE INAPO BIDI!
 
Wale tuliolelewa kama maiti au kama tuliovamia dunia vile tunacomment wapi? Fuc.k my parents. Wengine tuko duniani kuwasindikiza wenzetu shit!
 
Wale tuliolelewa kama maiti au kama tuliovamia dunia vile tunacomment wapi? Fuc.k my parents. Wengine tuko duniani kuwasindikiza wenzetu shit!
Duh mkuu sina chakusema zaidi ya Mungu akukumbuke na akumulikie nuru ya uso wake....
 
Ni kweli mtoto umleavyo ndivyo akuavyo...

Nashukuru Mungu wazazi wangu wamenipatia malezi bora sana, ambayo sina cha kujutia...



Cc: mahondaw
 
Mi ninaamini kua asilimia kubwa kwa WaTz tumepitia malezi ya kibabe na nidhamu ya woga ikiwemo na mm mwenyewe "obey the last order ". Ila malez sahihi kwangu ni urafiki na ukaribu baina ya mzazi/mlez na watoto wake. Nimekua nikipokea ushaur ktoka kwa boy of 3 age hasa kw mambo yamhusuyo mwenyewe. Inansaidia sn kubaini mambo yake na mawazo yake yooote. Hop itatupeleka pazu

Mi ninaamini kua asilimia kubwa kwa WaTz tumepitia malezi ya kibabe na nidhamu ya woga ikiwemo na mm mwenyewe "obey the last order ". Ila malez sahihi kwangu ni urafiki na ukaribu baina ya mzazi/mlez na watoto wake. Nimekua nikipokea ushaur ktoka kwa boy of 3 age hasa kw mambo yamhusuyo mwenyewe. Inansaidia sn kubaini mambo yake na mawazo yake yooote. Hop itatupeleka pazur
wow umeongea kitu chenye ukweli mkubwa sana kiongozi,sasa labda utuambie ni kwa jinsi gani ulliweza kuibadilisha akili yako kutoka kwenye malezi uliyopewa mpaka hayo unayowapa watoto wako sasa?maanake tulio wengi tunaathiriwa yaani yale malezi tuliyopewa tunataka kuwapa watoto wetu hayo pia.
 
Wale tuliolelewa kama maiti au kama tuliovamia dunia vile tunacomment wapi? Fuc.k my parents. Wengine tuko duniani kuwasindikiza wenzetu shit!
Dah kiongozi hii ni serious sana aisee,unaweza kushare na sis nini kilitokea? kwa sababu hili ni jambo zito mnoo hasa hapo kwenye ....my parents,ujue bado wao ni wazazi wako na huwezi kulibadili hilo,ndio waliokuleta duniani wangeweza kukuua ikiwa wangetaka lakini hawakufanya hivyo,huoni kama umekasirika mnooo kiongozi?
 
Viroboto , chawa- nguoni na kichwani, kunguni, utitiri, mbu, Vyoote mimi. kuosha vyombo, kuteka maji kisimani! Kutengwa wakati wa sala! yaani......

Binafsi nilijitenga na wenzangu shuleni sababu kaptula ya shule ilichanika matundu makubwa matakoni tena bila chupi ndani,

Manake nilichekwa na watoto wenzangu, na kuonekana kituko, kuchunga ng'ombe mbugani pekupeku siku za likizo, ndo zilikuwa zangu.sikujua viatu.

kujisaidia ni vichakani tu sometimes unaona kabisaaa minyoo juu ya kinyesi chako, sababu ya utoto unaona kawaida. hkn pa kusemea!

Bora niende Shule nitii sheria za shule ili nikae salama kunako kivulini cha drs, na mwalimu kuliko kubaki nyumbani nikalime shamba asubuhi then nikachunge mifugo siku nzima,
ambayo haikuwa na tija kwangu mfano kwa kunywa maziwa , hata kununuliwa shati au kaptula ya kuchungia.

Kusema kweli bila kuficha kila, usiku, ulipokuwa ukiingia Roho inauma sana, juu ya utitiri, chawa na viroboto vitakavyo ning'ata usiku kucha,

Nguo pekee ya kuchungia; Shukrani, ilikuwa ni sweta la kijani lililo sheheni chawa, tena bila vishikizo alinipatia marehemu dada yangu,
nalo lili nasa miiba ya porini kibao, kishikizo pekee kilikuwa mkono wangu wa kushoto. na ule wa kulia nilishika fimbo ya kuswagia mifugo. ngozi ya tumbo ilibadilika ajili ya ukurutu! mchana wadudu hawaumi sana km usiku!

Miaka hiyo Hakuna majira niliyo furahia km Asubuhi ikianza na mchana, jioni ilikuwa simanzi sana. sikutarajia kuijua key board. at the age of 8-9 yrs, nikaanza fanya vibarua kwa kificho ili nipate hela!

But all in all niliona ni sehemu tu ya kawaida kimaisha!

Bahati sana, bila kutegemea, nikafaulu kwenda Sec. huko baba mkuu Akili ndo ilifunguka paaa! nikaona km Ulaya nilivo heshimiwa, na walimu, wanafunzi.

Dawati, kitanda, ni vya peke yako, chakula kizuri nabembelezwa kula kwa mara ya kwanza eti nisigomee chakula! duuu!, mimi huyu! .....mngejua!

Ktk yale maisha yangu. ilikuwa ni kawaida kula ugali mgumu wa mtama, na mboga za majani chukuchuku daily, wali mkavu kwa nadra sana,
but Sec. duuu! Wali nyama Maharagwe, ndizi, mbatata, tena umeungwa vizuri na mafuta, maarufu km wese!.

Na kweli ya Mungu kadri nilivo panda Madarasa mfululizo. Mpaka kupata kazi, nilipendwa na kuheshimiwa sana na wanafunzi pamoja na wafanya kazi wenzangu,

pia jamii za watu niliokutana nao, tena mno! kuliko nilikotoka. mfano nilipoenda semina kwa mara ya kwanza Bagamoyo, sikuamini niliyotendewa seminani! na posho juu!

Hakika ya Mungu sikurudi tena kwa Shangazi yangu hata likizo tu, mpaka amekufa, wala sikumpenda kiviiile japo sikuonyesha chuki! Mpaka leo nikioa mwanamke ana tabia za ki-shangazi yangu, ananikata steam palepale!

Alikuwa hachapii wala kukufokea, but her facial expression spoke thousands of words, she really, and completely abandoned me like no body business, funny enough, and shamelessly, she did it to me, at that early age! very bad!
I dare say she was really evil. she deserve to drove to the pit of Hell!

Mpaka leo sijawahi ishi maisha ya hovyo, yaliyo jaa udhariri, Concealed hope, dharau, kejeli, umaskini, ujinga, Ubaguzi km yale, May God forbid!

MTOTO NI MAMA YAKE MZAZI TU, NDIYO ATAKUWA MTU BORA KATI YA WATU BORA, KINA DADA BEBENI WATOTO WENU WENYEWE,HATA KM HUNA HELA!
WATOTO WANGU NIKIKOSANA NA MAMA YAO. NI BORA WAKAE NA MAMA YAO TU! NITATOA MATUNZO PALE INAPO BIDI!
Dah umepitia mengi sana na ya kuhuzunisha mkuu,pole mnoooo,lakini hongera pia kwa kuviruka viunzi vyote hivyo na sasa umedhililisha ubora wako,unahisi malezi yale yaliathiri utu wako ambao labda kuna vitu unastruggle navyo mpaka leo,kwa sababu ya malezi uliyoyapitia?
 
Ndio...natamani saana kulea kama nilivolelewa mimi na zaidi (nililelewa vema)

Malezi niliolelewa yamenijenga kua mtu mpole,mcheshi...nisiehukumu watu,na mwelewa na ambaye ninaweza kuishi na kila mtu (mtu wa aina yeyote)
Tunatamani kufahamu zaidi, tudadavulie kwa mifano ya hapa na pale
 
Dah umepitia mengi sana na ya kuhuzunisha mkuu,pole mnoooo,lakini hongera pia kwa kuviruka viunzi vyote hivyo na sasa umedhililisha ubora wako,unahisi malezi yale yaliathiri utu wako ambao labda kuna vitu unastruggle navyo mpaka leo,kwa sababu ya malezi uliyoyapitia?
Akhsante sana Mkuu! ajabu ni kuwa wakt ule wa utoto sikuona Mateso ki viile! nilijionea kawaida tu! kwanza hata sikuwahi kuwaza kuna maisha bora, ya kupata kazi! sikuwahi kufikiri kuna ku pass mitihani huko juu! siku ya kwanza ku-pass vizuri nilikuwa naambiwa tu na watu umefanya vizuri endelea ivo!

nilisoma tu shule! kwa sababu ilikuwa ni mahali tulivu, ile tu kukaa drsani kivulini, nilihusudu mnoo! kuliko juani , nikichunga ng'ombe, ambao hawakunipa faida yeyote!
 
Back
Top Bottom