Tuelezane Ukweli Mficha Ugonjwa Kifo Humfichua

Tuelezane Ukweli Mficha Ugonjwa Kifo Humfichua

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Kumekuwapo na wimbi la Mafua yenye kuambatana na homa kali, maumivu ya mwili, kikohozi, kupoteza hamu ya kula, nk yasiyokuwa ya kawaida.

Zaidi sana leo hadi mechi ya wekundu wa Msimbazi na Kagera Sugar kule Kaitaba, imebidi kuahirishwa. Kisa na mkasa ugonjwa huu uliowang'ang'ania ghafla wengi wa wageni waliowasili kutokea Dar.

Taarifa ya ufafanuzi kutokea wizarani kuhusiana na hali hii ni kuwa huu ugonjwa ni wa kawaida. Kwamba hutokea mara kwa mara mwishoni mwa mwaka.

Kwa hakika taarifa hii ya wizara ni mfano wa majibu rahisi kwenye maswali magumu.

Hakuna mwaka wowote zaidi ya huu hali iliwahi kuwa hivi. Mwaka huu tumefikia hadi kufuta mechi wachezaji wanaumwa?!

Dalili za mvua ni mawingu. Mficha u*hi hazai. Pia mficha maradhi kifo humfichua.

Hala hala tusije kulaumiana.

Maisha ya watu ni muhimu zaidi kuliko kitu chochote.
 
Tukiachana na Wizara ya Afya, Waziri Mkuu amesemaje ? Tuchape kazi jamani !
3038576_IMG_20211218_184246.jpg


IMG_20211218_184246.jpg
 
Kama Watu wanapata mafua kwa wingi hivi na hakuna anaefikia hatua ya kulazwa tuseme Alhamdulillah hii ndio Herd Immunity ya Jumla inajijenga na baada ya hapo itapita kama hakuna kitu

Hata 2019 miezi kama hii hali ilikuwa kama hii na ikatusaidia kuvuka salama tulivyovuka
 
Kumekuwapo na wimbi la Mafua yenye kuambatana homa kali, maumivu ya mwili, kikohozi, kupoteza hamu ya kula, nk yasiyokuwa ya kawaida.

Zaidi sana leo hadi mechi ya we kundi wa Msimbazi na Kagera Sugar kule Kaitaba, imebidi kuahirishwa. Kisa na makosa ikiwa ugonjwa huu kwa wengi wa wageni waliowasili kutokea Dar.

Taarifa ya ufafanuzi kutokea wizarani kuhusiana na hali hii ni kwamba huu ugonjwa ni wa kawaida. Kuwa hutokea mara kwa mara mwishoni mwa mwaka.

Kwa hakika taarifa hii ya wizara ni mfano wa majibu rahisi kwenye maswali magumu.

Hakuna mwaka wowote zaidi ya huu hali aliwahi kuwa hivi. Mwaka huu tumefikia kufuta mechi wachezaji wanaumwa!

Dalili za mvua ni mawingu. Mficha u*hi hazai. Pia mficha maradhi kifo humfichua.

Hala hala tusije kulaumiana.

Maisha ya watu ni muhimu zaidi kuliko kitu chochote.
brazaj serikali ya awamu ya sita ni ya uwazi hina maficho ficho kama ya awamu ya sita ndio maana wanavaa barakoa kwenye hili la kesho hawavai halaiki hii vile hii vile....

How do you coat meal sijui mafua mafua seasonal flu wakati kama ni omcron waburst tu watu wachukue tahadhari. Mlisema hamtaki unafiki but what we see is.better off handling ya mafua ya awamu ya tano kuliko haya ya awamu ya sita ya kinafki。

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Kama Watu wanapata mafua kwa wingi hivi na hakuna anaefikia hatua ya kulazwa tuseme Alhamdulillah hii ndio Herd Immunity ya Jumla inajijenga na baada ya hapo itapita kama hakuna kitu

Hata 2019 miezi kama hii hali ilikuwa kama hii na ikatusaidia kuvuka salama tulivyovuka
Herd immunity ilijengwa awamu ya tano na ikaibukia awamu ya sita.

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Tuna tatizo kubwa sana kama nchi. Wanasiasa wamechukua nafasi za wataalam wenye taaluma husika. Hivyo kila kitu kinaenda kisiasa tu. Budget kubwa wamepatiwa wabunge na kulipa Kisogo masuala ya utafiti, hatuna mda nayo kabisa.
 
Kama Watu wanapata mafua kwa wingi hivi na hakuna anaefikia hatua ya kulazwa tuseme Alhamdulillah hii ndio Herd Immunity ya Jumla inajijenga na baada ya hapo itapita kama hakuna kitu

Hata 2019 miezi kama hii hali ilikuwa kama hii na ikatusaidia kuvuka salama tulivyovuka

Really? 2019? COVID-19 iligundulika Wuhan December 2019. TZ tulikuwa nayo tayari?
 
Pitia page ya facebook ya aliekuwa Mkuu wa Wilaya ya Bahi Mh.Betty Mkwasa wakati huo akihoji hali kama inayolalamikiwa sasa hata humu ililetwa


Pengine hujui tarehe ya ugonjwa kugundulika na ugonjwa kuwepo ni vitu viwili tofauti
Really? 2019? COVID-19 iligundulika Wuhan December 2019. TZ tulikuwa nayo tayari?
 
brazaj serikali ya awamu ya sita ni ya uwazi hina maficho ficho kama ya awamu ya sita ndio maana wanavaa barakoa kwenye hili la kesho hawavai halaiki hii vile hii vile....

How do you coat meal sijui mafua mafua seasonal flu wakati kama ni omcron waburst tu watu wachukue tahadhari. Mlisema hamtaki unafiki but what we see is.better off handling ya mafua ya awamu ya tano kuliko haya ya awamu ya sita ya kinafki。

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app

Ndiyo maana wanaitana wahuni.

Zitto anasema yamemkuta. Huko alikokuwa nao mkutanoni hatupeani mrejesho. Ila baba lao anapuyanga tu:

IMG_20211216_215554_004.jpg
 
Back
Top Bottom