Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 301,577
- 754,412
Leo ilikuwa mechi ya watani wa jadi SIMBA na Yanga. Maarufu kama Deby ya Kariakoo.
Michezo pia ni siasa.. Lakini pale inapokuwa ni siasa safi bila agenda za siri nyuma yake.. Kinyume chake ni uchuro wenye nuksi mbaya na laana!
Mimi ni mwana SIMBA original kabisa.. Na Nilikuwa na imani kubwa timu yangu itanifuta machozi leo. Lakini kitendo cha kuona tambara jekundu lenye nakshi ya picha ya mwanasiasa kilinikata stimu kabisa na kujua mwanzoni kabisa tutafungwa.
Hayo matambara hayajatengenezwa na pesa za SIMBA.. Kwanini kampeni mpaka huku? Kwanini tusiachwe tufurahie maisha kidogo.
Haki ya nani nilipoona ile picha na ule wekundu nikakumbuka damu nyingi iliyomwagika isiyo na hatia kwasababu tu ya siasa
Haya mahela yote yanayotumika kutengeneza matangazo yote haya kwenye kila tukio nchi nzima yanatoka wapi?
Huyu mwanasiasa kama anadhani anaji brand kapotea njia vibaya mno.. Branding yenye baraka ni kuulinda, kuutunza na kuuhudumia uumbaji wa Mwenyezi Mungu na tunu zake na rasilimali zake zote
Mapambo yakizidi badala ya kupendeza huchukiza. Manukato yakizidi badala ya kuvutia hukarahisha.. Kuna baadhi badala ya kunukia hunuka!
Sasa hivi hakuna kunukia tena bali ni kunuka! Tambara la leo limetunukia harufu mbaya.. Tumetengwa na kukimbiwa na nguvu chanya. ! Badala ya kufungwa tukajifunga.. Tujitenge na hawa wanasiasa na siasa zao..hii ya leo ni warning
Michezo pia ni siasa.. Lakini pale inapokuwa ni siasa safi bila agenda za siri nyuma yake.. Kinyume chake ni uchuro wenye nuksi mbaya na laana!
Mimi ni mwana SIMBA original kabisa.. Na Nilikuwa na imani kubwa timu yangu itanifuta machozi leo. Lakini kitendo cha kuona tambara jekundu lenye nakshi ya picha ya mwanasiasa kilinikata stimu kabisa na kujua mwanzoni kabisa tutafungwa.
Hayo matambara hayajatengenezwa na pesa za SIMBA.. Kwanini kampeni mpaka huku? Kwanini tusiachwe tufurahie maisha kidogo.
Haki ya nani nilipoona ile picha na ule wekundu nikakumbuka damu nyingi iliyomwagika isiyo na hatia kwasababu tu ya siasa
Haya mahela yote yanayotumika kutengeneza matangazo yote haya kwenye kila tukio nchi nzima yanatoka wapi?
Huyu mwanasiasa kama anadhani anaji brand kapotea njia vibaya mno.. Branding yenye baraka ni kuulinda, kuutunza na kuuhudumia uumbaji wa Mwenyezi Mungu na tunu zake na rasilimali zake zote
Mapambo yakizidi badala ya kupendeza huchukiza. Manukato yakizidi badala ya kuvutia hukarahisha.. Kuna baadhi badala ya kunukia hunuka!
Sasa hivi hakuna kunukia tena bali ni kunuka! Tambara la leo limetunukia harufu mbaya.. Tumetengwa na kukimbiwa na nguvu chanya. ! Badala ya kufungwa tukajifunga.. Tujitenge na hawa wanasiasa na siasa zao..hii ya leo ni warning